Mwandishi Wetu, TJNCDF
Shirikisho la Vyama vya
Magonjwa Yasiyo ya Kuambukiza Tanzania (TANCDA) linaeleza kuwa karibu kila mtu
anakabiliwa na tatizo la msongo wa mawazo.
Kinachosababisha hali hiyo,
TANCDA inaeleza kuwa ni hali ya jumla ya maisha. Mazingira na mifumo ya maisha
ambayo jamii inaishi yanachagiza binadamu kujikuta anapata msongo wa mawazo.
Kuna mambo mengi yanayoweza
kumsababishia mtu kuwa na msongo, na hapa TANCDA inayaelezea kwa mfumo wa
maswali.
Katika maswali hayo ukiona
miongoni yanakuhusu, unapaswa kuchukua tahadhari ili tatizo la msongo wa mawazo
lisikusababishie madhara.
Siyo rahisi mtu kujua madhara
anayopata kama yanatokana na msongo wa mawazo yanayomkabili kwa sababu hiyo
TANCDA inashauri jamii kuchukua tahadhari.
Miongoni mwa maswali mtu
anayoweza kujiuliza ni: Je, hatuwi na wasiwasi kuwa watu wanachunguza ngua tunazovaa?
Je, hatushikwi na hofu pale
tunapovuka barabara kuwa tunaweza kugongwa na magari? Je, hatuwi na wasiwasi
pale tunaposhindwa kumaliza kazi zetu kwa wakati? BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI MAKALA HAYA.























