Nafasi Ya Matangazo
Showing posts with label MICHEZO. Show all posts
Showing posts with label MICHEZO. Show all posts

September 15, 2022

Na Shamimu Nyaki - Dodoma
Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Pauline Gekul ameeleza kuwa ujenzi wa Uwanja wa Mpira wa Miguu jijini Dodoma upo katika hatua ya utekelezaji na tayari Serikali imeshaanza kutenga fedha za ujenzi huo.

Mhe. Gekul ameeleza hayo leo Septemba 13, 2022 Bungeni jijini Dodoma, wakati akijibu swali la Mbunge Mhe. Innocent Edward Kalogeris ( Morogoro Kusini) aliyeuliza ni lini ahadi ya ujenzi wa Uwanja wa mpira Dodoma iliyotolewa na Mfalme wa Moroko itatekelezwa.

Akijibu swali hilo, Mhe. Gekul amesema, mawasiliano kuhusu utekelezaji wa mradi huo baina ya Serikali ya Tanzania na Morocco yanaendelea, huku akieleza kuwa Serikali inaendelea kutafuta fedha kutoka kwa wadau na wabia wa maendeleo.

"Serikali imeshakamilisha upembuzi yakinifu kuhusu ujenzi huo, na mwaka huu wa fedha ujenzi utaanza lakini pia kutakua na kiasi cha  shilingi Bilioni 10 kuboresha viwanja vya michezo vya Arusha, Tanga, Dodoma na Geita" amesema Mhe. Gekul.
Mhe. Waziri wa wizara hiyo, Mohamed Mchengerwa ametoa majibu ya nyongeza katika swali hilo kwa kusisitiza kuwa ujenzi huo utakua wa kisasa na miondombinu bora ambayo inaendana na teknolojia ya viwanja vya sasa Duniani.

Akijibu swali la  nyongeza  la Mhe.Salma Kikwete kuhusu kukamilisha ujenzi wa Uwanja wa Majaliwa Stadium, Mhe. Gekul amesema Serikali inaendelea kuunga mkono jitihada za wadau wanaowekeza katika Sekta ya michezo, ambapo amesema imepunguza kodi katika nyasi bandia pamoja na kutoa ushauri wa kitaalamu kwa wawekazaji wa sekta hiyo.

Mhe.Gekuk ametumia nafasi hiyo kumpongeza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa kwa ujenzi wa Uwanja wa Ruangwa na kueleza kuwa ujenzi huo utakua chachu ya kuongeza vipaji katika Soka, na kupunguza changamoto ya miundombinu ya viwanja nchini.
Posted by MROKI On Thursday, September 15, 2022 No comments

October 13, 2019

 Nahodha wa Mdori Fc Hassan Sharifu akipokea kombe la ubingwa kutoka kwa Spika wa la hifadhi ya jamii ya wanyamapori burungev Marcelo Yeno baada ya kutwaa ubingwa chemchemnCup 2019
 Mratibu miradi ya jamii ya Chemchem association, Walter Pallangyo  akizungumzia michuano hiyo.
 Mashabiki wakifuatilia mtanange wa fainali kati ya Mdori FC na Majengo FC
  ************
Mwandishi wetu, Babati
Babati. Timu ya soka ya Mdori FC, juzi imetwaa ubingwa wa michuano ya chemchem CUP mwaka 2019, iliyokuwa na lengo la kupiga vita ujangili na kuendeleza utalii, baada ya kushinda kwa penati 4-3 dhidi ya timu ya Majengo FC katika mchezo wa fainali uliochezwa uwanja wa Mdori wilayani Babati.

Katika mchezo huo wa fainali, ambao ulikuwa umevuta maelfu ya watu, timu hizo zilitoka sale kwa kufungana goli 1-1 kwa dakika 90 na ndipo bingwa akapatikana kwa mikwaju ya penati, Manyara ndio walikuwa wa kwanza kupata gori dakika ya 57 kupitia kwa Andason Agustin na Mdoro walisawazisha dk 87 kupitia Rajabu Said

Baada ya fainali hiyo, Mdori walikabidhiwa kikombe chenye thamani ya zaidi ya sh 1.5 milioni na fedha taslimu sh 1.7 milioni na Spika wa hifadhi ya jamii ya Burunge, Marceli Yeno ambapo washindi wa pili walipewa zawadi ya fedha taslimu 1.1 milioni na kikombe zawadi zote zilizotolewa na mwekezaji wa Chemchem.

Washindi wa tatu wa michuano hiyo, timu ya Kisangaji ilipewa zawadi wa sh 650,000 na washindi wa nne timu ya Sangaiwe ilipata zawadi ya sh 300,000 na upande wa timu za mpira wa pete mabingwa walikuwa Mdori waliopewa zawadi ya sh 250,000 ,wa pili Mbuyuni 150,000 na timu ya tatu walimu 100,000.

Akizungumza baada ya michuano hiyo, Mratibu wa miradi ya jamii ya taasisi ya Chemchem Association ambayo, imewekeza hoteli na utalii wa picha katika eneo hilo,Walter Pallangyo alisema lengo la taasisi yao kudhamini mashindano hayo ni kuhamaisha vijana kupenda uhifadhi, kupiga vita ujangili na kuendeleza utalii.

"tunaamini Chemchem kama wawekezaji katika eneo hilo, michezo hii inasaidia pia kuwakutanisha vijana na kutambua vipaji vyao na baadhi wamekuwa wakipata fursa ya kuchaguliwa timu za nyingine nchini"alisema

Katibu wa chama cha soka wilaya ya Babati,Ramadhani Mnyoti alipongeza michuano hiyo, kwa kueleza imekuwa ikiibua vijaji lakini pia kusaidia kukuza utalii na kupiga vita ujangili kupitia michezo.

Michuano ya Chemchem CUP ambayo, ilikuwa inashirikisha timu 20 kutoka vijiji vinavyozunguka hifadhi ya jamii ya wanyamapori ya Burunge,lengo lake ni kupiga vita ujangili, kuendeleza uhifadhi na Utalii katika eneo hilo.
Posted by MROKI On Sunday, October 13, 2019 No comments

August 26, 2019

Nahodha wa timu ya Dar es Salaam Corridor akinyanyua kombe juu pamoja na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Standard Charteredb Bank Ajmair Riaz mara baada ya kukabidhiwa na Rais wa TFF Bw. Wallace Karia kushoto kwenye michuano ya fainali za kombe la Standard Chartered Bank Cup 2019 katika viwanja vya JK Park Kidongo Chekundu jijini Dar es Salaam, Jumamosi Agosti 24, 2019
Rais wa TFF Wallace Karia akikabidhi kombe kwa nahodha wa timu ya Dar es Salaam Corridor (katikati) ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Standard Chartered Bank Ajmair Riaz.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Standard Charteredb Bank Ajmair Riaz akinyanyua kombe na nahodha wa timu ya Dar es Salaam Corridor mara baada ya kukabidhiwa.
Wachezaji wa timu ya wa timu ya Dar es Salaam Corridor mara baada ya kukabidhiwa nishani zao kabla ya kukabidhiwa kombe.
Wachezaji wa timu ya wa timu ya Dar es Salaam Corridor wakiwa na kombe lao mara baada ya kukabidhiwa. BOFYA HAPA KUONA ZAIDI
Posted by MROKI On Monday, August 26, 2019 No comments

March 21, 2019

Mkurugenzi Mtendaji wa Arusha United Sports Club Otte Beda Ndaweka
TIMU ya Arusha United Sports Club, inayoshiriki ligi daraja la kwanza imetangaza kujitoa rasmi katika ligi hiyo kwa madai  ya kuchoshwa na vitendo ambavyo si vya kimichezo huku TFF kupitia bodi ya ligi ikishindwa kuchukua hatua stahiki.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha, Mkurugenzi Mtendaji wa timu hiyo Otte Beda Ndaweka amesema kuwa licha ya timu hiyo kuwa katika nafasi nzuri katika kundi B imeona si buasara kuendelea na ligi hiyo kufuatia matukio mbalimbali ikiwemo kufanyiwa vurugu wakati ikicheza na timu kadhaa tangu timu hiyo ianze kushiriki ligi hiyo msimu wa mwaka 2018-2019.
Aidha Ndaweka amesema licha ya timu hiyo kuwa na vibali vya kurekodi michezo yake yote ya ligi kuanzia mchezo wake dhidi ya Dodoma Fc uliofanyika mjini Dodoma bodi hiyo pia imeshindwa kuhakikisha maelekezo,miongozo au vibali vyake vinaheshimiwa na au kuchukua hatua pale ambapo haviheshimiwi.
Timu ya Arusha United ni moja ya timu zinazoshiriki ligi daraja la kwanza Tanzania bara kwa kundi B,kwa sasa ikiwa imekwisha cheza michezo 17 kukusanya jumla ya point 28 huku ikishika nafasi ya tano ambapo timu ya Geita gold FC ikiongoza ligi hiyo ikiwa na point 33.
Posted by MROKI On Thursday, March 21, 2019 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo