WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Februari 6, 2026 ameahirisha Mkutano wa Pili wa Bunge la 13 jijini Dodoma na kutumia fursa hiyo kuwaasa Watanzania wote kuwa na matumizi chanya ya mitandao ya kijamii na kuifanya kuwa nyenzo muhimu ya kujielimisha, kuendeleza biashara na kueneza ujumbe wa mshikamano.
February 06, 2026
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Februari 6, 2026 ameahirisha Mkutano wa Pili wa Bunge la 13 jijini Dodoma na kutumia fursa hiyo kuwaasa Watanzania wote kuwa na matumizi chanya ya mitandao ya kijamii na kuifanya kuwa nyenzo muhimu ya kujielimisha, kuendeleza biashara na kueneza ujumbe wa mshikamano.
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema kuwa ahadi za Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan zimeendelea kutekelezwa kikamilifu ikiwemo ya kugharimia kwa asilimia 100 matibabu ya vipimo vya kibingwa kwa magonjwa sugu yasiyoambukiza kama saratani, figo, moyo, sukari, mifupa na mishipa ya fahamu.
WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema mipango inayoandaliwa na Serikali inalenga kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha usafiri na usafirishaji wa bidhaa, viwanda na biashara katika ukanda wa Afrika.
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group imetoa huduma za upimaji na matibabu ya magonjwa mbalimbali kwa watu 138,699 kwa mwaka 2025.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Hospitali ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Dkt. Tulizo Shemu alisema watu wazima 124,959 na watoto 13,740 walipatiwa matibabu mwaka 2025 huku wagonjwa 4,144 kulazwa katika hospitali hiyo kwaajili ya matibabu.
Dkt. Shemu alisema ukilinganisha na mwaka 2024 Hospitali hiyo ilitoa huduma kwa wagonjwa 133,756 kati yao watu wazima walikuwa 109,931 na watoto 23,825 hivyo kuwa na ongezeko la wagonjwa 4,943 huku idadi ya watoto ikipungua na idadi ya watu wazima ikiongezeka.
“Huduma nyingine zilikuwa ni kliniki ya mfumo wa mkojo, kliniki ya magonjwa ya tumbo na ini, kliniki ya magonjwa ya figo, upasuaji mkubwa na mdogo, huduma za fiziotherapia (mazoezi tiba) na huduma za maabara”, alisema Dkt. Shemu.
Aidha Dkt. Shemu alisema kwa mwaka 2025 JKCI Hospitali ya Dar Group ilitoa huduma mpya ambazo hapo awali zilikuwa hazitolewi ikiwemo kuangalia shinikizo la damu kwa masaa 24 (ambulatory blood pressure monitoring), matibabu ya kuangalia umeme wa moyo kwa masaa 24 (ECG Halter Monitoring) na kipimo cha kuchunguza mishipa ya damu ya moyo na mfumo wa umeme wa moyo katika hali ya mazoezi kwa kutumia mashine ya treadmill (Treadmill stress test).
Kwa upande mwingine Dkt. Shemu alisema watu 251 walifanyiwa uchunguzi na matibabu ya magonjwa mbalimbali yakiwemo magonjwa ya moyo, ngiri, vidonda sugu, matatizo ya mifupa na mgongo pamoja na tiba ya kinywa na meno kupitia huduma za tiba mkoba zijulikanazo kwa jina la Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach Services zilizofanyika katika viwanja vya Mbagala wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam.
“Kupitia kambi hiyo jumla ya watu 198 walikutwa na magonjwa mbalimbali na hivyo kupewa rufaa ya kufika JKCI Hospitali ya Dar Group kwaajili ya vipimo zaidi na kuanzishiwa matibabu”, alisema Dkt. Shemu.
Dkt. Shemu alisema mwaka 2025 JKCI Hospitali ya Dar Group ilifanya upasuaji kwa wagonjwa 1,874 ikiwemo upasuaji wa mfumo wa mkojo, upasuaji wa mifupa, Upasuaji wa uzazi, Upasuaji wa pua, masikio na koo, Upasuaji wa matatizo mbalimbali ya wanawake na upasuaji wa jumla.
Upande wa ajira Dkt. Shemu alisema Serikali kupitia Tume ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa mwaka 2025 ilitoa ajira mpya kwa wafanyakazi 149 katika kada mbalimbali zikiwemo za afya, utawala, uhasibu, ugavi, ICT, na nyinginezo.
SERIKALI imewahimiza wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuwekeza katika viwanda vya uchenjuaji na uchakataji wa madini ya dhahabu mkoani Geita ili kuongeza thamani ya madini, kuimarisha ajira, kulinda mazingira na kukuza mapato ya Taifa.
Wito huo umetolewa na Mjiolojia kutoka Ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Geita, John Maganga, wakati wa ziara ya kutembelea masoko ya madini mkoani humo, ambapo amesema Geita ina fursa kubwa ya uwekezaji kutokana na uzalishaji mkubwa wa dhahabu unaofanywa na wachimbaji wadogo na wa kati.
Amesema licha ya uzalishaji huo, bado kuna upungufu wa viwanda vya uchenjuaji na uchakataji wa dhahabu, hali inayosababisha madini mengi kuuzwa yakiwa ghafi bila kuongeza thamani, jambo linalonyima wananchi na Serikali mapato makubwa.
“Ni wakati sasa kwa wawekezaji kuchangamkia fursa zilizopo Geita kwa kujenga viwanda vya uchenjuaji na uchakataji wa dhahabu, hatua itakayopunguza matumizi ya zebaki, kulinda afya za wananchi na mazingira, pamoja na kuongeza mapato ya Serikali,” amesema.
Ameeleza kuwa uanzishwaji wa viwanda hivyo utaenda sambamba na uwepo wa masoko rasmi ya madini, ambayo yameimarisha uwazi, usalama na ufanisi katika biashara ya dhahabu, na kudhibiti vitendo vya magendo vilivyokuwa vikisababisha upotevu wa mapato ya Serikali.
Ameongeza kuwa masoko ya dhahabu yamekuwa kichocheo cha ukuaji wa uchumi wa mkoa wa Geita kwa kuongeza ajira, biashara na mzunguko wa fedha, huku wachimbaji wakinufaika kwa kuuza madini yao kwa bei ya soko na kwa mifumo rasmi ya Serikali.
Kwa upande wake, Afisa Mthaminishaji wa Madini, Peter Jamhuri, amesema mifumo ya kidigitali inayotumika katika masoko ya madini imeongeza uwazi na ufanisi kwa kuwezesha ukusanyaji wa takwimu sahihi za mauzo, jambo linalosaidia wafanyabiashara kupata mikopo kutoka taasisi za fedha.
Amesema mifumo hiyo imeimarisha uwazi na kuondoa magendo, huku akimpongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kusimamia sera na mifumo bora inayochochea maendeleo ya sekta ya madini na uchumi wa Taifa kwa ujumla.
Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, imesaini Hati ya Makubaliano (MoU) na Benki ya CRDB kupitia CRDB Bank Foundation kwa ajili ya uendeshaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Vijana, hatua inayolenga kuimarisha uwezeshaji wa vijana kiuchumi, kijamii na kitaaluma nchini.February 05, 2026
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amekabidhi hundi ya shilingi bilioni 200 kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana, Joel Nanauka ikiwa ni utekelezaji wa vitendo wa ahadi ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoitoa wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, ya kutenga na kutoa mitaji kwa ajili ya kuwawezesha vijana na wanawake.
Pia, Waziri Mkuu amesema uwezeshaji wananchi kiuchumi ni mhimili wa kukuza uzalishaji, biashara, uwekezaji na ustawi wa maisha ya wananchi, hasa vijana na wanawake ambapo amezitaka wizara, taasisi na mamlaka za kisekta zinazoendelea kutekeleza mpango huo kuhakikisha fedha hizo zinawafikia walengwa wote na program zilizokusudiwa na kutoa tija tarajiwa.
“Utoaji wa Hundi ya Shilingi Bilioni 200 unaonesha kwa vitendo kwamba Serikali ya Awamu ya Sita inatekeleza ahadi zake kwa vitendo, si kwa maneno. Tukio hili linaweka msingi mpya wa kuimarisha ushiriki wa vijana na wanawake katika uchumi wa Taifa na kuharakisha safari ya Tanzania kuelekea uchumi jumuishi na endelevu.”
Amekabidhi hundi hiyo leo Alhamisi, Februari 5, 2026 katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma, ambapo pamoja na mambo mengine amesisitiza kuwa mafanikio hayo hayatapimwa kwa kiasi cha fedha kilichotolewa, bali kwa mabadiliko halisi ya maisha ya wananchi, hususan vijana na wanawake.
“Wizara, Taasisi na Mamlaka zote zinazoshiriki katika utekelezaji wa uwezeshaji kiuchumi lazima zibadilishe mtazamo kutoka katika kutoa fedha kwenda katika kusimamia matokeo na kwamba kila taasisi ijiwekee malengo yanayopimika, viashiria vya utendaji na ratiba za utekelezaji, ili kuhakikisha mitaji hiyo inazalisha ajira, kipato na biashara endelevu.”
Waziri Mkuu amesisitiza kwamba uwezeshaji huo usiwe zoezi la kawaida la kiofisi bali uwe chombo cha mageuzi ya kiuchumi, hivyo utekelezaji wa Shilingi Bilioni 200 lazima uendeshwe kwa uwazi na uwajibikaji. “Taarifa za maendeleo zitolewe mara kwa mara, na hatua zichukuliwe dhidi ya matumizi mabaya. Serikali haitasita kuchukua hatua kwa yeyote atakayekiuka dhamira ya uwezeshaji huu.”
Kadhalika, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema katika kipindi kifupi cha Novemba 2024 hadi Januari 2025, Serikali kupitia mifuko na programu za kuwawezesha wananchi kuichumi imetoa mikopo na dhamana zenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 66.9 kwa wanufaika zaidi ya 13,000, wakiwemo vijana na wanawake katika sekta mbalimbali.
Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu); William Lukuvi amemshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwa kinara katika kukuza uwezeshaji kiuchumi pamoja na jitihada mbalimbali anazofanya katika kuhakikisha vijana na wanawake wanashiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi ikiwa ni pamoja na kuwawezesha mitaji.
Waziri Lukuvi amesema hata hivyo, changamoto ya upatikanaji wa mitaji ikiwemo mikopo, vifaa, mashine na mitambo bado imekuwa kikwazo kikubwa cha ukuaji wa shughuli za kiuchumi zinazotekelezwa na vijana na wanawake. ”Kutokana na changamoto hiyo, Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongeza fedha shilingi bilioni 200 kwa ajili ya kuwawezesha vijana na wanawake.
Amesema uwezeshaji huo wa shilingi bilioni 200 ni uthibitisho wa maono na dhamira aliyonayo Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inayolenga kupanua wigo wa upatikanaji wa mitaji ya gharama nafuu kwa vijana na wanawake ili waweze kuwa shindani kitaifa, kikanda na kimataifa.
Kamishna wa Idara ya Usimamizi wa Bajeti, Bw. Meshack Anyingisye (kushoto) na Kamishna Msaidizi wa Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Omary Khama, wakifuatilia kikao kati ya Waziri wa Fedha, Mhe Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) na Kiongozi wa Timu ya Wataalamu kutoka Taasisi ya kimataifa inayojihusisha na tathmini ya nchi kukopesheka katika masoko ya mitaji ya kimataifa (Sovereign Credit Rating) Moody’s Investor Service (Moody’s), Bw. John Walsh (hawapo pichani), Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.Na. Peter Haule. na Jordan Mbwambo, WF, Dodoma
Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amesema kuwa mageuzi ya uchumi yataendelea kuwa ajenda ya muda mrefu yakilenga si tu kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi bali kuhakikisha ukuaji huo unachangia katika upatikanaji wa ajira na ustawi wa wananachi kwa ujumla.
Amebainisha hayo wakati wa kikao na Timu ya Wataalamu kutoka Taasisi ya kimataifa inayojihusisha na tathmini ya nchi kukopesheka katika masoko ya mitaji ya kimataifa ya Moody’s Investor Service ikiongozwa na Bw. John Walsh, kilichofanyika Ofisi za Treasury Square, jijini Dodoma.
Mhe. Balozi Omar alisema kuwa uchumi wa nchi umeendelea kuimarika licha ya matukio kadhaa yaliyokwaza ustawi wa uchumi wa dunia ukiwemo uviko 19 ambapo katika kipindi cha mwaka jana uchumi ulikua kwa asilimia 5.4 na unatarajiwa kukua zaidi mwaka huu wa fedha 2025/26 hadi kufikia asilimia 6.
Aidha, alibainisha kuwa mahitaji ya uwekezaji yanaendelea kuwa makubwa hususani kwenye miundombinu ya kimkakati kama Bandari, Viwanja vya Ndege, Reli na mtandao wa Barabara ili kuchochea maendeleo.
Alieleza kuwa nchi inaendelea kuwekeza katika ujenzi wa miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo Reli iendayo Kasi -SGR, Bwawa la uzalishaji wa umeme la Julius Nyerere na uimarishaji wa sekta nyingine za kijamii na kiuchumi hatua itakayochochea zaidi ukuaji na uimara wa uchumi wa nchi na maendeleo ya jamii.
Akizungumzia Mfumuko wa bei amesema kuwa, hali imeendelea kuwa tulivu ambapo kiwango cha mfumuko wa bei kimeendelea kubaki chini ya asilimia tano kwa miaka kadhaa, kikiwa kati ya asilimia 2.9 na 3.4.
Kwa upande wake Kiongozi wa Timu ya Wataalamu kutoka Taasisi ya kimataifa inayojihusisha na tathmini ya nchi kukopesheka katika masoko ya mitaji ya kimataifa Moody’s, Bw. John Walsh, alisema kuwa uamuzi wa kupandisha hadhi ya uwezo wa nchi kukopesheka na kuipa alama B1 yenye mtazamo thabiti ulitokana na uthabiti wa kiuchumi na kifedha ambao nchi imeuonesha licha ya changamoto za uchumi za dunia katika miaka ya karibuni.
Alisema kuwa Tanzania iliendelea kurekodi ukuaji thabiti wa uchumi licha ya athari za janga la UVIKO-19, mfumuko wa bei wa kimataifa na kupanda kwa viwango vya riba duniani.
“Uamuzi wa kupandisha hadhi kwa kiwango cha B1 ulitokana na uthabiti wa sera za uchumi jumla na mageuzi ya Serikali yanayotekelezwa chini ya Mpango wa Shirika la Fedha la Kimatafa (IMF), unaokaribia kukamilika”, alisema Bw. Walsh.
Alisema kuwa Serikali imepiga hatua muhimu katika kushughulikia changamoto za muda mrefu, ikiwemo ukusanyaji mdogo wa mapato ya ndani na mapungufu ya utekelezaji wa sera, hivyo Tathmini ya sasa inalenga kufuatilia mafanikio, changamoto zilizopo, na mwelekeo wa mageuzi katika kipindi cha miaka miwili iliyopita.
Aidha alieleza kuwa tathmini hiyo inalenga kupata taswira ya kina ya hali ya sasa ya uchumi wa Tanzania, mafanikio yaliyopatikana, pamoja na hatua zinazochukuliwa kuhakikisha ukuaji endelevu na uthabiti wa kifedha kwa muda mrefu.
Matokeo ya mapitio ya hivi karibuni ya Kampuni za Moody’s na Fitch ziliipa Tanzania daraja la B1 (stable outlook) na B+ (stable outlook), mtawalia ambayo yanaonesha kwamba Tanzania ni nchi salama kwa wawekezaji.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania, Bw. Philip Besiimire, akizungumza jambo wakati wa kikao cha Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani) na Kampuni hiyo kilichofanyika katika Ofisi ya Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma, ambapo walijadiliana masuala mbalimbali ya kukuza sekta ya mawasiliano na masuala ya kidigitali katika maendeleo ya Uchumi wa jamii, ambacho kilifanyika katika Ofisi ya Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akiongoza kikao chake na Uongozi wa Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania, ulioongozwa na Mwenyekiti wa Bodi wa Kampuni hiyo Bw. David Tarimo (hayupo pichani), ambapo walijadiliana masuala mbalimbali ya kukuza sekta ya mawasiliano na masuala ya kidigitali katika maendeleo ya Uchumi wa jamii, ambacho kilichofanyika katika Ofisi ya Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania, Bw. David Tarimo (Kulia) akizungumza jambo wakati wa kikao cha Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani) na Kampuni hiyo kilichofanyika katika Ofisi ya Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma, ambapo walijadiliana masuala mbalimbali ya kukuza sekta ya mawasiliano na masuala ya kidigitali katika maendeleo ya uchumi wa jamii, ambacho kilifanyika katika Ofisi ya Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma. Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania, Bw. Philip Besiimire.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (Katikati), Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb) (wa tatu kushoto), Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania, Bw. David Tarimo (wa tatu kulia), Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania, Bw. Philip Besiimire (wa pili kushoto), Mkurugenzi wa Masuala ya Nje wa Vodacom Tanzania, Bi. Zuweina Farah (kushoto) na maafisa wengine waandamizi wa kampuni hiyo, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kikao chao kilichojadili masuala mbalimbali ya kukuza sekta ya mawasiliano na masuala ya kidigitali katika maendeleo ya uchumi wa jamii, ambacho kilifanyika katika Ofisi ya Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.





































.jpg)



.jpg)



