April 16, 2026
Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Jumatano, Aprili 15, 2026, akimpongeza na kumshukuru Mkurugenzi Mkuu wa Viwanja vya Ndege (TAA) Bw. Abdul Mombokaleo kwa kujitolea computer zenye thamani ya shilingi milioni 170 kama mchango wake yeye na Alumni wengine kwa kuboresha elimu ya Sayansi katika shule hiyo.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Jumatano, Aprili 15, 2026, akupewa maelezo juu ya mradi wa jengo la maabara ya TEHAMA ambayo ni ‘Smart Class’ alipokuwa Mgeni rasmi katika Mahafali ya 59 ya Shule ya Sekondari Kibaha (KSS) kama mgeni rasmi, katika hafla iliyofanyika shuleni hapo, Tumbi, Kibaha Mji, mkoani Pwani.Sehemu ya wahitimu wa kidato cha sita katika Mahafali ya 59 ya Shule ya Sekondari Kibaha (K katika hafla iliyofanyika shuleni hapo, Tumbi, Kibaha Mji, mkoani Pwani.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Jumatano, Aprili 15, 2026, akiwatambulisha baadhi ya Alumni walio katika kamati ya mradi wa ujenzi wa jengo la maabara ya TEHAMA ambayo ni ‘Smart Class’ katika Mahafali ya 59 ya Shule ya Sekondari Kibaha (KSS) kama mgeni rasmi, katika hafla iliyofanyika shuleni hapo, Tumbi, Kibaha Mji, mkoani Pwani. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Viwanja vya Ndege (TAA) Bw. Abdul Mombokaleo, akifuatiwa na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO Nchini Prof. Hamisi Malebo.
(Picha na Habari na Issa Michuzi)
Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Jumatano, Aprili 15, 2026, akikagua na kupewa maelezo juu ya maabara ya TEHAMA ambayoni ‘Smart Class” na Mkuu wa Shule hiyo alipokuwa Mgeni rasmi katika n Mahafali ya 59 ya Shule ya Sekondari Kibaha (KSS) kama mgeni rasmi, katika hafla iliyofanyika shuleni hapo, Tumbi, Kibaha Mji, mkoani Pwani.Akiwa katika mahafali hayo, Dkt. Kikwete amezindua harambee ya kuchangia ujenzi wa jengo la ghorofa la maabara ya TEHAMA na masomo mengine, ambalo linatarajiwa kugharimu shilingi bilioni 3.
Amesema ujenzi huo ni muhimu katika kuendeleza ubunifu na uwezo wa wanafunzi katika masomo ya sayansi, teknolojia, uhandisi na hisabati (STEM).
Aidha, Dkt. Kikwete amekubali kuwa mlezi wa kamati ya kukusanya michango kwa ajili ya mradi huo mkubwa ambao kwa sasa umefikia hatua ya msingi.
Pia, Rais Mstaafu ameishukuru jumuiya ya wanafunzi wa zamani (alumni) wa shule hiyo, wakiuongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Bw. Abdul Mombokaleo, kwa kuchangia kompyuta zenye thamani ya Shilingi Milioni 170 kwa ajili ya “Darasa Janja” (Smart Class) lililoanzishwa shuleni hapo.
Darasa hilo litakuwa ni kituo cha mafunzo kwa wanafunzi wa shule hiyo na shule nyingine zitakazounganishwa kupitia mfumo wa mtandao, ambapo mwalimu anaweza kufundisha madarasa yaliyoko nje ya Kibaha kwa wakati mmoja kwa njia ya kidigitali.
Katika ziara yake, Dkt. Kikwete alipata fursa ya kutembelea na kukagua Darasa Janja hilo, akipokea maelezo kutoka kwa Mkuu wa Shule kuhusu namna teknolojia hiyo inavyotumika kuboresha mbinu za ufundishaji na ujifunzaji shuleni hapo.
Shule ya Sekondari Kibaha, inayomilikiwa na Shirika la Elimu Kibaha na kusimamiwa na Kurugenzi ya Hud uma za Elimu, ilianzishwa mwaka 1965 kupitia ushirikiano kati ya Serikali ya Tanganyika ya wakati huo na nchi za Nordic – Denmark, Finland, Norway, na Sweden. Wakati inaanzishwa, shule ilikuwa na wanafunzi 110 wa Kidato cha Kwanza na 60 wa Kidato cha Tano.
Kwa sasa, shule hiyo ya bweni kwa wavulana ina uwezo wa kuchukua zaidi ya wanafunzi 800 na imeendelea kuwa miongoni mwa taasisi kongwe na zenye heshima kubwa katika sekta ya elimu nchini.
Dkt. Kikwete ni miongoni mwa alumni mashuhuri wa Shule ya Sekondari Kibaha, alikosoma zaidi ya miaka 60 iliyopita. Wengine waliopitia shule hiyo ni pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mkurugenzi Mkuu wa ATCL Bw. Peter Ulanga, Balozi Lazaro Nyalandu, Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO Nchini Prof. Hamisi Malebo, Mkurugenzi Mkuu wa Viwanja vya Ndege Bw. Abdul Mombokaleo, na Mwenyekiti Mstaafu wa CHADEMA Mhe. Freeman Mbowe, miongoni mwa wengine wengi.
Aidha, kwa kutambua mchango mkubwa wa alumni wake, Shule ya Sekondari Kibaha inaendelea kuimarisha ushirikiano na wadau wa elimu ili kuhakikisha inaendelea kuwa kinara katika utoaji wa elimu ya ubora nchini.
April 15, 2026
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Asha-Rose Migiro, leo tarehe 15 Aprili 2026 amefanya mazungumzo na Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Malawi, Mhe. Lazarus Chakwera, katika Ofisi za CCM Lumumba, jijini Dar es Salaam.
April 14, 2026
Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu ameyasema hayo jana jioni Aprili 13, 2026 jijini Dodoma katika Hafla ya Maandalizi ya Mei Mosi, 2026 ambayo Kitaifa inafanyika mkoani Njombe.
Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema Serikali inaendelea kuwaenzi wafanyakazi nchini kutokana na umuhimu wao mkubwa kwa Taifa.
Katika hafla hiyo ya awali, kiashi cha shilingi bilioni 1.105 kimekusanywa ambapo Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu alisema fedha hizo zitausaidia mkoa mwenyeji kukamilisha shughuli za maandalizi kwa ajili ya tukio hilo.
Mheshimiwa Waziri Mkuu aliongeza kwa kulipongeza Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA) kwa ubunifu wa kuhakikisha maadhimisho ya Mei Mosi yanaacha alama katika mkoa mwenyeji.
“Wenzetu TUCTA wamekuja na ubunifu kwamba shughuli za Mei Mosi zinaacha alama katika mkoa husika kwa kutekeleza miradi mbalimbali kama walivyofanya katika maadhimisho ya mwaka 2025 mkoani Singida kwa kujenga uwanja wa Bombadia mkoani humo, uwanja ambao sasa umekuwa na manufaa makubwa kwa Wanasingida, na Njombe nako wamejiandaa kuacha alama kubwa.” Alisema Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba.
Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mheshimiwa Deus Clement Sangu alisema maandalizi ya maonesho ya Mei Mosi mwaka huu yanaendelea vizuri akisisitiza kuwa kwa siku zilizosalia, maandalizi yote yatakamilika ndani ya wakati.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mheshimiwa Anthony Mtaka alisema maadhimisho hayo ni fursa kubwa si tu kwa kwa mkoa wa Njombe, bali kwa mikoa yote ya kanda ya Nyanda za Juu Kusini kwani ugeni wa watu wasiopungua elfu tano unatarajiwa kushiriki sherehe za Mei Mosi Kitaifa mkoani humo.
Naye Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini Nyamhokya alishukuru na kupongeza kuimarika ushirikiano kati ya Serikali na Vyama vya Wafanyakazi, akisema ushirikiano huo umechangia kuwepo kwa utulivu miongoni mwa wafanyakazi nchini.
April 13, 2026
April 12, 2026
April 11, 2026
Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi INEC ambaye pia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume, Ndg. Ramadhani Kailima akizungumza katika kikao hicho cha Baraza.
Watumishi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia katiba, sheria, kanuni na taratibu na kuepuka lugha zozote za uchochezi zinazoweza kuleta uvunjifu wa amani na kuhatarisha maisha ya Watanzania.
Dkt. Kilabuko amesema, taasisi ina malengo yake, upo uwezakano wa kuepusha migogoro ya ndani na nje ya taasisi inayoweza kuathiri utekelezaji wa majukumu ya Tume kwa ufanisi.
Katibu wa Baraza aliyemaliza muda wake, Ndg. Livini Avith akizungumza.
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi INEC wakifuatilia agenda mbalimbali katika mkutano huo.
Mwenyekiti wa TUGHE tawi la INEC, Ndg. Juvenile Kaiza akizungumza.Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi INEC wakifuatilia agenda mbalimbali katika mkutano huo.


































