Nafasi Ya Matangazo

June 18, 2026

Waziri wa Inchi Ofisiya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete ameipongeza Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) kwa kusimamia kwa ufanisi utekelezaji wa miradi ya maendeleo pamoja na kutoa elimu kwa wananchi.


Kikwete ametoa pongezi hizo leo Juni 17/2026 Jijini Dodoma alipotembelea banda la TEA katika maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Jijini hapa.

Katika maonesho hayo Kikwete alikuwa mgeni rasmi wa maonesho hayo ambapo alipata fursa ya kutembelea mabanda ya taasisi mbali mbali za hapa nchini.

Akitoa maelezo kuhusu huduma zinazotolewa na TEA Afisa uhusiano na mawasiliano wa Mamlaka hiyo Eliafile Solla amesema taasisi hiyo inatumia maonesho hayo kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu yake, huduma mbalimbali zinazotolewa pamoja na miradi mbalimbali inayotelekezwa kwa fedha za mfuko wa Elimu wa Taifa.

Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026 yalianza Juni 16 na ynatarajiankumalizika Juni 23 mwaka huu.
Posted by MROKI On Thursday, June 18, 2026 No comments




Na, Mwandishi wetu - Dodoma
Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Bi. Stella Mwaiswaga pamoja na Watumishi wengine kutoka Ofisi hiyo wameshiriki ufunguzi wa Maonesho ya Wiki ya Utumishi tarehe 17 Juni, 2026 katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma.
 
Maonesho ya Wiki ya Utumishi ni moja ya matukio katika kalenda ya Umoja wa Afrika (AU) ambapo nchi wanachama huadhimisha kwa kaulimbiu moja na kufanya maonesho ya kazi mbalimbali kuhusu masuala ya Utumishi wa Umma ambapo hufanyika kila mwaka kuanzia tarehe 16 hadi 23 Juni.
 
Kwa mwaka huu Maadhimisho hayo yamebeba kaulimbiu isemayo; “Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi wa Huduma Endelevu”.
 
SAmbamba na hilo Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu inashiriki maonesho hayo huku ikitoa elimu mbalimbali kwa umma kuhusiana na shughuli za Wakala Serikali wa uchapishaji Tanzania, elimu kuhusu masuala ya Menejimenti ya Maafa, Watu wenye Ulemavu, Ufuatiliaji na Tathimini pamoja na Masuala ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi.



Posted by MROKI On Thursday, June 18, 2026 No comments
Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi, akiwa katika mazungumzo na Bw. Lorenzo Guadagno wa Sekretarieti ya Santiago Network pamoja na ujumbe ulioambatana nao, pembeni mwa mkutano wa SB64 mjini Bonn, Ujerumani.
Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Richard Muyungi (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mtaalamu wa Ushirikishwaji wa Wanachama wa Sekretarieti ya Santiago Network, Bw. Lorenzo Guadagno baada ya mazungumzo yaliyolenga kuimarisha ushirikiano na kuhakikisha Ofisi ya Kanda ya Santiago Network kwa Afrika iliyopo Dar es Salaam inatekeleza majukumu yake kwa ufanisi na kufikia malengo yaliyowekwa.
*************
Wadau wa mazingira kutoka Taasisi ya Hanns R. Neumann Stiftung (HRNS) ya Ujerumani wameonesha nia ya kuwekeza na kushirikiana na Tanzania katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo endelevu ikiwemo uhifadhi wa mazingira, nishati safi, biashara ya kaboni, maendeleo ya vijana na kilimo.

Nia hiyo imebainishwa katika mazungumzo kati ya Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi na Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini wa HRNS, Bw. Olaf Tschimpke, yaliyolenga kutafuta maeneo mapya ya ushirikiano kati ya taasisi hiyo na Serikali ya Tanzania.

Kikao hicho kimefanyika pembezoni mwa Mkutano wa 64 wa Wataalam wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (SB64) unaofanyika Bonn, Ujerumani.

Akizungumza katika kikao hicho, Dkt. Muyungi aliwasilisha vipaumbele vya Taifa vilivyomo katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ikiwemo maendeleo ya masoko ya kaboni, nishati jadidifu, uchumi wa buluu, nishati safi ya kupikia na ushiriki wa vijana katika uhifadhi wa mazingira.

Aidha, Dkt. Muyungi alieleza umuhimu wa kupata wadau wa kusaidia kuendesha Kituo cha Vijana cha Afrika cha Majadiliano ya Mabadiliko ya Tabianchi kilichopo Dar es Salaam.

Kwa upande wake, Bw. Tschimpke alisema HRNS ina uzoefu wa kusaidia wakulima wadogo wa kahawa, kulinda mazingira na kuwawezesha vijana katika nchi mbalimbali za Afrika, ikiwemo Tanzania, Uganda na Ethiopia.

Maeneo yaliyotajwa kuwa na fursa za ushirikiano ni pamoja na kusaidia wakulima wadogo wa kahawa, kuanzisha Muungano wa Kudhibiti Uchafuzi wa Plastiki nchini, kuendeleza masoko ya kaboni, uwekezaji katika nishati ya jua, programu za michezo kwa vijana, mafunzo ya mazingira na ujasiriamali kwa vijana pamoja na uwekezaji katika teknolojia za usafiri wa umeme (e-mobility).

Pia, pande hizo mbili zimekubaliana kuendelea na mazungumzo kupitia kikao cha ufuatiliaji kitakachofanyika mwezi Julai mjini Bonn, Ujerumani, pamoja na kuandaa Hati ya Makubaliano (MoU) itakayobainisha maeneo ya ushirikiano na utekelezaji wake.

Vilevile, imekubaliwa kuandaliwa kwa mkutano wa wadau utakaowakutanisha washirika wa HRNS na Serikali ya Tanzania nchini Tanzania ili kujadili kwa kina fursa za ushirikiano, uwekezaji na utekelezaji wa maeneo yaliyobainishwa kuwa na maslahi ya pamoja.

Katika hatua nyingine, Dkt. Muyungi, amekutana na Mwakilishi wa Sekretarieti ya Santiago Network, Bw. Lorenzo Guadagno kwa lengo la Lengo kuu la mazungumzo hayo kuimarisha ushirikiano kati ya Ofisi ya Makamu wa Rais na Santiago Network, pamoja na kujadili namna ya kuhakikisha kuwa Ofisi ya Kanda ya Santiago Network kwa Afrika iliyopo Dar es Salaam.

Tanzania, inatekeleza majukumu yake kwa ufanisi na kufikia malengo yaliyokusudiwa katika kusaidia nchi za Afrika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi, hususan Hasara na Uharibifu (Loss and Damage).

Dkt. Muyungi alisisitiza dhamira ya Serikali ya Tanzania ya kuendelea kushirikiana na Santiago Network ili kuhakikisha kuwa ofisi hiyo ya kikanda inakuwa kitovu muhimu cha uratibu, ujenzi wa uwezo, kubadilishana uzoefu na utoaji wa msaada wa kiufundi kwa nchi za Afrika. Alieleza kuwa Tanzania iko tayari kutoa ushirikiano unaohitajika ili kuwezesha utekelezaji wa majukumu ya ofisi hiyo kwa manufaa ya bara la Afrika.

Kwa upande wake, Bw. Guadagno alieleza dhamira ya Sekretarieti ya Santiago Network ya kuimarisha ushirikiano na Tanzania na wadau wengine wa kikanda ili kuhakikisha kuwa huduma na msaada wa kiufundi unaotolewa kupitia ofisi ya Dar es Salaam unawafikia walengwa kwa wakati na kwa ufanisi, sambamba na malengo ya Santiago Network ya kusaidia nchi zinazoendelea kukabiliana na changamoto za hasara na uharibifu unaotokana na mabadiliko ya tabianchi.

Pande zote mbili zilikubaliana kuendelea kuimarisha mawasiliano na ushirikiano wa karibu ili kuhakikisha kuwa Ofisi ya Kanda ya Santiago Network kwa Afrika inakuwa chombo madhubuti cha kusaidia nchi za bara hilo katika kujenga ustahimilivu na kuimarisha uwezo wa kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
 
Posted by MROKI On Thursday, June 18, 2026 No comments

June 17, 2026

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kupitia Idara ya Mambo ya Ndani (INAD), leo Juni 17, 2026 imeandaa Kongamano la Maadili lililowakutanisha viongozi wa dini mbalimbali kujadili nafasi ya maadili katika kuimarisha ukusanyaji wa kodi na kujenga utamaduni wa ulipaji kodi kwa hiari. 

Kongamano hilo ni sehemu ya maandalizi ya Maadhimisho ya Miaka 30 ya TRA yatakayofanyika Julai 1, 2026.

Akifungua kongamano hilo kwa niaba ya Kamishna Mkuu wa TRA, Naibu Kamishna wa TRA, Bw. Mcha Hassan Mcha, amesema kuwa katika kipindi cha miaka 30 tangu kuanzishwa kwa TRA, taasisi hiyo imepiga hatua kubwa katika kuimarisha mifumo ya ukusanyaji wa mapato, huku maadili yakiendelea kuwa nguzo muhimu katika utekelezaji wa majukumu yake.

Bw. Mcha amesema TRA inaendelea kuwekeza katika mifumo na mikakati mbalimbali ya kuimarisha maadili kwa watumishi wake na walipakodi ili kujenga uaminifu, uwajibikaji na kuongeza kiwango cha ulipaji kodi kwa hiari.

“Maadili hujenga imani, na imani hujenga ulipaji wa kodi kwa hiari,” alisema Bw. Mcha.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano Tanzania (JMAT), Sheikh Alhad Mussa Salum, ameipongeza TRA kwa kuandaa kongamano hilo na kueleza kuwa maadili ni msingi muhimu wa maendeleo ya jamii na taifa. Amesema mafundisho ya dini yanasisitiza uadilifu, uwajibikaji na kufanya mema, huku ulipaji wa kodi ukiwa sehemu ya wajibu unaochangia ustawi wa wananchi na maendeleo ya nchi.

Naye Mkuu wa Evangelical Fellowship Church Tanzania, Askofu Charles Asher Howard, amesema maandiko matakatifu yanaelekeza waumini kutimiza wajibu wao kwa mamlaka halali, ikiwemo kulipa kodi. Amebainisha kuwa maendeleo ya Tanzania yanategemea mchango wa kila mwananchi, hivyo ulipaji wa kodi ni jukumu la pamoja linalopaswa kutekelezwa kwa uaminifu na uzalendo.

Viongozi hao wa dini wamepongeza hatua ya TRA ya kuwashirikisha katika mijadala ya maadili na ukusanyaji wa mapato, wakisisitiza kuwa ushirikiano kati ya taasisi za umma na viongozi wa dini una nafasi muhimu katika kuhamasisha wananchi kulipa kodi kwa hiari na kujenga taifa lenye uwajibikaji, uadilifu na maendeleo endelevu.
Posted by MROKI On Wednesday, June 17, 2026 No comments

 

Posted by MROKI On Wednesday, June 17, 2026 No comments



Dodoma 
Wadau wa Sekta ya Madini wamehimizwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia shughuli za madini ili kuhakikisha rasilimali hizo zinaendelea kuchangia maendeleo ya taifa na kunufaisha wananchi.

Mwanasheria wa Tume ya Madini, Janeth Kanyasu, amesema hayo kwenye Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park mkoani Dodoma, ambapo Tume inaendelea kutoa elimu kwa wananchi na wadau mbalimbali kuhusu masuala ya Sekta ya Madini.

Amesema elimu hiyo inahusu Sheria ya Madini Sura ya 123 na kanuni zake, ikijumuisha utoaji wa leseni mbalimbali, biashara ya madini, uwekezaji, shughuli za uchimbaji na usimamizi wa mazingira ili kuhakikisha rasilimali za madini zinatumika kwa tija na kwa kuzingatia matakwa ya sheria.

“Kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa ni msingi wa kuhakikisha Sekta ya Madini inaendeshwa kwa uwazi, uadilifu na kuendelea kutoa manufaa kwa taifa na wananchi,” amesema Kanyasu.

Amesema pia wananchi wanaelimishwa kuhusu ushiriki wa Serikali katika shughuli za madini, ushirikishwaji wa Watanzania katika sekta hiyo kupitia sera ya Ushiriki wa Watanzania katika Sekta ya Madini pamoja na utekelezaji wa miradi ya uwajibikaji kwa jamii (CSR) inayotekelezwa na kampuni za madini.

Kwa mujibu wa Kanyasu, Tume ya Madini inaendelea kutoa ufafanuzi kuhusu ulipaji wa mirabaha na tozo mbalimbali zinazotakiwa kisheria, ikiwemo Service Levy, HIV Levy, mrabaha wa madini ya ujenzi wa asilimia tatu, madini ya metali asilimia sita na ada ya ukaguzi ya asilimia moja.

Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka huu yanaongozwa na kaulimbiu isemayo, “Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu,” na yanatarajiwa kuhitimishwa Juni 23, 2026.

Posted by MROKI On Wednesday, June 17, 2026 No comments
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa akifanya mazungumzo na watendaji wa Benki ya NMB kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na kuweka mikakati ya pamoja ya hifadhi ya mazingira endelevu, kikao kilichofanyika jijini Dodoma Juni 16, 2026.

Mkuu wa Biashara ya Serikali NMB Bi. Vicky Bishubo (Kushoto) akizungumza wakati wa kikao na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa chenye lengo la kuimarisha ushirikiano na kuweka mikakati ya pamoja ya hifadhi ya mazingira endelevu, kikao kilichofanyika jijini Dodoma Juni 16, 2026.
****************
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa amewaomba wadau wa maendeleo kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali za kupanda miti ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Amesema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na watendaji wa Benki ya NMB kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na kuweka mikakati ya pamoja ya hifadhi ya mazingira endelevu, kikao kimefanyika jijini Dodoma Juni 16, 2026.

Mhe. Kwagilwa alisema kuwa katika kufikia lengo la upandaji wa miti takriban bilioni mbili lililowekwa kupitia Dira 2050 zinahitajika nguvu za pamoja kati ya Serikali na wadau na kuendelea kuhamasisha jamii kupanda miti kwenye maeneo yao.

Alisema ni lazima kuunganisha nguvu za pamoja kushirikiana ili kuifanya nchi kuwa ya kijani kwani hata katika kaulimbiu iliyotumika kwenye Siku ya Mazingira Duniani mwaka huu inasema ‘Dira 2050; Tuwajibike kukijanisha Tanzania’ ambayo inasisitiza umuhimu wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
 
“Karibu nusu ya eneo la nchi yetu ni misitu, tunaongelea hekta takriban milioni 48 na hata tungeweza kuwa zaidi ya hapo lakini bado tunakata sana misitu, na ukitembea huioni miti pamoja na kufanyika kampeni nyingi, natamani tupande miti zaidi,” alisisitiza.

Aidha, Mhe. Kwagilwa alipendekeza kuwepo na vitalu vya miche katika kata zote 3950 zilizopo nchini ambayo ikisambazwa na kupandwa hatua hiyo itasaidia kustawisha miti mingi zaidi na kupunguza changamoto ya upotevu wa miti 370,000 inayopotea kila mwaka.
 
Pamoja na hayo alisema kwenye Sheria mpya ya Mazingira itakuwa ni vyema ikaweka sharti la kumtaka mtu mwenye kumiliki eneo kubwa ni lazima apande miti badala ya kuliacha likawa wazi bila kutumika.
 
Kuhusu kaboni ya buluu aliipongeza Beki ya NMB kwa kuanza kutekeleza miradi hiyo katika ukanda wa pwani ambapo aliwaomba wakutane na wataalamu wa Kituo cha Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC) chini ya Ofisi ya Makamau wa Rais kwa ajili kubadilishana uzoefu na kufanikisha jambo hilo.
 
Kwa upande wake Mkuu wa Biashara ya Serikali NMB Bi. Vicky Bishubo alisema pamoja na masuala mbalimbali, Benki hiyo imejikita katika shughuli za mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
 
Alisema katika kuunga mkono juhudi hizo, mwaka 2024 walizindua kampeni ya upandaji wa miti nchi nzima kwa kushirikiana na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), halmashauri kupitia shule za Tazania Bara na Zanzibar na taasisi zikiwemo Magereza na Jeshi la Wananchi kwa kupanda miti milioni mbili.
 
Bi. Vicky alisema asilimia 80 ya miti iliyopandwa ilistawi hivyo wanafunzi waliofanya vizuri katika ustawishaji wa miti walipata zawadi kama motisha na kuongeza kuwa lengo ni kupanda miti milioni 10 ifikapo mwaka 2030.
 
Naye Meneja Mkuu wa NMB Foundation Bw. Nelson Karumuna alisema katika uchumi wa buluu, taasisi hiyo inatekeleza mradi wa kuwajengea uwezo wakulima wa mwani katika eneo la pwani ili waongeze kipato na kutunza maeneo ya bahari.
 
Aliongeza kuwa taasisi hiyo inashiriki kikamilifu katika kupunguza hewa ya ukaa ambapo inatarajia kuzindua mradi wa vyombo vya moto (magari) vinavyotumia umeme badala ya mafuta.
Wataalamu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais wakiwa katika kikao cha Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa na watendaji kutoka benki ya NMB chenye lengo la kuimarisha ushirikiano na kuweka mikakati ya pamoja ya hifadhi ya mazingira endelevu, kikao kilichofanyika jijini Dodoma Juni 16, 2026.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa akiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa Benki ya NMB mara baada ya kufanya mazungumzo katika kikao chenye lengo la kuimarisha ushirikiano na kuweka mikakati ya pamoja ya hifadhi ya mazingira endelevu, kikao kilichofanyika jijini Dodoma Juni 16, 2026.



Posted by MROKI On Wednesday, June 17, 2026 No comments
Na Mwandishi wetu, Dodoma
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa na Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mary Chatanda, amesema katika zama hizi za kutafuta fursa za kiuchumi duniani, sera ya kutofungamana upande wowote, inafaa zaidi kutumiwa.

Chatanda ameyasema hayo Juni 16, Jijini Dodoma, alipokuwa akitoa maoni yake kutokana na mwelekeo wa serikali ya Awamu ya Sita, chini ya uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kuifungua nchi kimataifa na mkakati wa kuhimiza diplomasia ya kiuchumi.

"Hii ya kusema mimi rafiki yangu huyu, yule adui yangu, sio nzuri, hii ya kusema nampenda huyu namchukia yule, kisa ana ugomvi na nchi mshirika wako haifai. Tanzania chini ya Rais Dk. Samia tumejitanabaisha kuwa hatufungamani na upande wowote.
Kutofungamana pande wowote kutatupa uwanja mpana wa kushirikiana na mataifa mengi duniani na kufaidi fursa mbalimbali za kiuchumi zitakazoweza kuleta tija kwa wananchi na Taifa letu," amesema Chatanda.

Sambamba na hilo, Chatanda amesema wakati mwingine nchi inanunua ugomvi usiowahusu kisa tu mataifa mawili yamegombana na hivyo nchi kumchukia nchi aliyegombama na rafiki mshirika wake.

"Tanzania tumekataa kujiingizia katika ugomvi usiotuhusu, sisi tunakwenda na yeyote ilimradi tunaona ana dhamira ya dhati ya kushirikiana na sisi katika kuchochea maendeleo. Ndiyo maana binafsi, nasimamia na Rais wetu kwa msimamo huu wa kutofungamana upande wowote," amesisitiza Chatanda.

Aidha, Chatanda amesema tunahitaji kushirikiana na mataifa mengi duniani na kila Taifa lina upekee wake katika nyanja mbalimbali kama kilimo, nishati, teknolojia, madini, elimu, afya, hivyo Tanzania inajiweka pazuri katika kuwa na washirika wengi wa maendeleo.

Ikumbukwe kuwa, Rais Dk. Samia alipokuwa ziarani nchini Urusi, katika mahojiano yake na mwandishi wa habari, aliulizwa Tanzania inawezaje kuhusiana na mataifa tofauti katika kipindi ambacho mazingira ya uchumi wa dunia yamebadikika.

Akijibu swali hilo, Rais Dk. Samia amesema "Tanzania inafuata misingi ya kutofungamana na upande wowote. Kwahiyo, adui wa rafiki yetu si adui wetu, na rafiki wa adui yetu si adui wetu".

Kimsingi, Tanzania inaendelea kusimamia sera ya diplomasia ya kiuchumi yenye mkazo wa kushirikiana na mataifa mengine ulimwenguni huku mashirikiano hayo yakiwa na wajibu wa kuleta manufaa kijamii na kiuchumi kwa pande zote.
Posted by MROKI On Wednesday, June 17, 2026 No comments
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limehimiza ushirikiano wa karibu kati ya serikali, sekta binafsi, taasisi mbalimbali na wananchi katika juhudi za kulinda na kuhifadhi mazingira nchini. 

Hatua hiyo inalenga kuhakikisha rasilimali za asili zinaendelea kutumika kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho huku zikihifadhiwa kwa uendelevu.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kaimu Meneja wa Kitengo cha Mawasiliano wa NEMC, Martha Kawishe, amesema kuwa mafanikio ya uhifadhi wa mazingira yanategemea ushiriki wa wadau wote. 

Amesema changamoto za mazingira, ikiwemo uchafuzi wa mazingira, utupaji holela wa taka na shughuli zinazoweza kuharibu ikolojia, zinahitaji juhudi za pamoja ili kudhibitiwa kwa ufanisi.

Kawishe amesisitiza umuhimu wa wananchi kutoa taarifa kwa mamlaka husika wanapobaini vitendo au shughuli zinazohatarisha mazingira katika maeneo yao. 

Amesema ushirikiano huo utasaidia mamlaka kuchukua hatua kwa wakati na kuzuia madhara yanayoweza kuathiri afya za wananchi, uchumi na mazingira kwa ujumla. 

Aidha, NEMC itaendelea kutoa elimu kwa umma na kuimarisha ushirikiano na wadau mbalimbali ili kuongeza ufanisi katika usimamizi na uhifadhi wa mazingira nchini.

Katika hatua nyingine, Kawishe amesema NEMC imekuwa ikipokea taarifa kuhusu baadhi ya watu wasio waaminifu wanaojitambulisha kwa uongo kuwa wakaguzi wa mazingira kutoka NEMC kwa lengo la kuwalaghai wananchi, wafanyabiashara na wawekezaji. 

Amesema watu hao wamekuwa wakijaribu kutumia jina la taasisi hiyo kufanya ukaguzi usio rasmi au kudai fedha kinyume na taratibu zilizowekwa.

Kutokana na hali hiyo, amewashauri wananchi, wafanyabiashara na wawekezaji kuwa makini wanapokutana na watu wanaodai kuwa maafisa wa NEMC. 

Amesema kabla ya kuruhusu ukaguzi wowote, ni muhimu kuomba kuonyeshwa kitambulisho cha kazi, kitambulisho maalumu cha ukaguzi wa mazingira pamoja na nyaraka rasmi zinazompa mhusika mamlaka ya kufanya ukaguzi huo. 

NEMC imeeleza kuwa tahadhari hiyo itasaidia kudhibiti vitendo vya udanganyifu na kulinda maslahi ya wananchi pamoja na wawekezaji nchini.

Posted by MROKI On Wednesday, June 17, 2026 No comments
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa kitengo cha Uhusiano kwa Umma na Nyaraka wa kampuni ya magazeti ya Serikali (TSN), Bi. Nadhifa Omar ambayo iko chini ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, mara baada ya kutembelea na kupata huduma katika banda hilo jijini Dodoma katika viwanja vya Chinangali ambapo maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026 yanafanyika, Juni 17, 2026.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa kitengo cha Uhusiano kwa Umma na Nyaraka wa Kampuni ya magazeti ya Serikali (TSN), Bi. Nadhifa Omar ambayo iko chini ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, mara baada ya kutembelea na kupata huduma katika banda hilo jijini Dodoma katika viwanja vya Chinangali ambapo maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026 yanafanyika, Juni 17, 2026.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akipewa maelezo ya shughuli na huduma zinazotolewa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na taasisi zake kutoka kwa Mkurugenzi Msaidizi wa rasilimali watu wa wizara hiyo, Bw. Gideon Malabeja, jijini Dodoma katika viwanja vya Chinangali ambapo maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026 yanafanyika, Juni 17, 2026.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akipewa maelezo ya shughuli na huduma zinazotolewa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na taasisi zake kutoka kwa Mkurugenzi Msaidizi wa rasilimali watu wa wizara hiyo, Bw. Gideon Malabeja, jijini Dodoma katika viwanja vya Chinangali ambapo maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026 yanafanyika, Juni 17, 2026.
Posted by MROKI On Wednesday, June 17, 2026 No comments




Na. Ssgt Mawazo Mtondo - Dodoma.
Mkuu wa Sehemu ya Usimamizi wa Maadili na Ushughulikiaji wa Malalamiko (Mrejesho) wa Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Adolphina Ngoso, Mkuu wa Kitengo cha Utumishi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Naibu Kamishna wa Zimamoto na Uokoaji (DCP) Fatma Ngenya na Mkuu wa Kitengo cha Mafunzo  Idara ya Uhamiaji, Naibu Kamishna wa Uhamiaji (DCI) Bahati Mwaifuge kwa nyakati tofauti, leo Juni 17, 2026 wametembelea Banda la Maonesho la Jeshi la Magereza lililopo katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.

Viongozi hao walifanya ziara hiyo katika Maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026 yanayoendelea kufanyika Jijini Dodoma, ambapo walipata fursa ya kujionea huduma mbalimbali, shughuli za urekebishaji wa wafungwa, pamoja na kazi za uzalishaji mali zinazotekelezwa na Jeshi la Magereza kupitia Programu mbalimbali za urekebishaji.

Kwa nyakati tofauti, wageni hao walipokelewa na Mkuu na Msemaji wa Jeshi la Magereza katika Maonesho ya Mwaka huu, Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Elmas L.Mgimwa, ambaye aliwaeleza majukumu ya Jeshi la Magereza katika Usalama, mchango wake katika utoaji wa huduma za urekebishaji na mageuzi yaliyopo sasa katika utekelezaji wa majukumu yake yanayochsngia kwa kiasi kikubwa maendeleo nch kijamii na kiuchumi.
Posted by MROKI On Wednesday, June 17, 2026 No comments


Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uwekezaji Mfuko wa Mabadiliko ya Tabianchi (GCF) Dkt. Achala Abeysinghe Juni 16, 2026 jijini Bonn, Ujerumani.
 
Kikao hicho cha pande mbili baina ya Jamhuri ya Muungano waTanzania na GCF kimfanyika kando ya Mkutano wa 64 wa Kamati za Utekelezaji na Sayansi na Ushauri chini ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi (SB64) ukiendelea. 

Madhumuni ya kikao hicho ni kukuza mashirikiano yaliyopo kati ya JMT na Taasisi hiyo hasa katika kuiwezesha Tanzania kupata msaada wa kifedha na utalaamu wa kiufundi katika kuisadia nchi kupata fedha za kupambana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Katika mkutano huo, Dkt. Muyungi alieleza kuwa Tanzania ikiwa moja ya nchi nufaika na fedha kutoka mfuko huo za utekelezaji miradi ya maendeleo ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. 

Hivyo, kutokana na fursa ilizopo Tanzaia imeweza kuwasilisha maombi ya kuipatia Ithibati Wizara ya Fedha ili kuweza kupata fedha moja kwa moja kutoka katika mfuko huo. 

Hadi sasa JMT inataasisi moja ambayo ni CRDB iliyopewa ithibati ili kuweza kunufaika moja kwa moja na fedha zinazotolewa na mfuko huo za kuhimili athari za abadiliko ya tabiachi. 

Mkutano huo ulihudhuriwa na wataalamu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Wizara ya Fedha na Taasisi za Kifedha za nchini ikiwemo Benki ya TIB, Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) na Bneki ya NBC.

 
Posted by MROKI On Wednesday, June 17, 2026 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo