February 20, 2026
WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewaagiza watendaji wanaosimamia sekta ya elimu kuanzia sasa waanze kujenga shule zitakazokidhi mahitaji ya mtaala mpya wa elimu ifikapo mwaka 2028.
February 19, 2026
Na.Sophia Kingimali.Akizungumza leo Februari 19,2026 jijini Dar es salaam wakati wa makabidhiano ya gari hilo, Dkt. Semesi amesema mradi huo ulioanza mwaka 2020 na unaotarajiwa kukamilika Juni mwaka huu,
"Mradi huu umewezesha upatikanaji wa miundombinu muhimu ikiwemo maabara hiyo inayotoa majibu ya papo kwa papo (real time) wakati wa ukaguzi wa mazingira,hivyo kifaa hicho kitapima viwango vya kelele, mitetemo, ubora wa maji, hali ya hewa, udongo pamoja na metali nzito kama zebaki, hivyo kurahisisha utoaji wa maamuzi ya haraka dhidi ya vitendo vya uchafuzi wa mazingira",Amesema Dkt Semesi.
Aidha Dkt. Semesi, ameongeza kuwa matumizi ya maabara hayo yatapunguza gharama na muda uliokuwa ukitumika kusafirisha sampuli kwenda maabara nyingine zilizoidhinishwa, ambapo gharama ya kipimo kimoja ilikuwa inaweza kufikia kati ya Sh milioni 5 hadi 10 kulingana na aina ya sampuli amesema kwa sasa NEMC itaweza kufanya uchunguzi ndani ya muda mfupi na kuchukua hatua stahiki mara moja, hali itakayoongeza ufanisi katika kulinda mazingira.
Aidha, amesema baraza lina kanda 13 nchini na matarajio ni kupata angalau magari 12 zaidi ya maabara tembezi ili kuimarisha huduma katika mikoa yote na kuhakikisha ukaguzi unafanyika kwa haraka na kwa ufanisi zaidi.
Kwa upande wake Mratibu wa Mradi huo, Paul Kalokola, amesema maabara hiyo pia ina vifaa vya kisasa ikiwemo droni kwa ajili ya kufikia maeneo magumu na yaliyofichika, hatua itakayowezesha upimaji wa kisayansi kufanyika popote nchini na kusaidia maamuzi yanayotegemea ushahidi wa kitaalamu.
Naye Meneja wa Programu za Mazingira na Hali ya Hewa kutoka Ubalozi wa Sweden, Stephen Mwakifwamba, amesema jumla ya mradi huo ulikuwa na thamani ya dola milioni tatu za Marekani na ulijumuisha pia uboreshaji wa sheria na kanuni za mazingira pamoja na kuzitafsiri kwa Kiswahili ili ziweze kueleweka kwa wananchi hivyo ameishauri NEMC kuhakikisha vifaa hivyo vinatunzwa na kufanyiwa matengenezo ya mara kwa mara ili viweze kudumu na kutoa huduma kwa muda mrefu.
Serikali ya Sweden imeahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania katika kuimarisha uhifadhi wa mazingira kwa maendeleo endelevu na ustawi wa wananchi.
Maabara hiyo imenunuliwa kupitia mradi wa miaka mitatu uliofadhiliwa na Serikali ya Sweden kupitia Shirika la Maendeleo la Sweden (Sida), uliolenga kujenga uwezo wa taasisi za serikali na binafsi katika kusimamia mazingira.






















































