June 20, 2026
June 19, 2026
Akizungumza Juni 19, 2026, katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma, Afisa Mkaguzi wa Migodi wa Tume ya Madini, Rose Mika, amesema ukaguzi wa mara kwa mara unaofanyika katika migodi mikubwa, ya kati na midogo unalenga kuhakikisha shughuli za uchimbaji zinaendeshwa kwa kuzingatia Sheria ya Madini pamoja na Kanuni za Usalama, Afya na Utunzaji wa Mazingira za mwaka 2010.
Amesema ukaguzi huo husaidia kubaini mapema changamoto zinazoweza kuhatarisha usalama wa wafanyakazi na wananchi wanaoishi jirani na maeneo ya migodi, hivyo kuwezesha hatua stahiki kuchukuliwa kabla ya kutokea kwa madhara.
Rose amesema Tume ya Madini pia inaendelea kusimamia utekelezaji wa mipango ya usimamizi wa mazingira, ikiwemo kudhibiti uchafuzi wa maji, hewa na ardhi pamoja na kuhakikisha taka zinazotokana na shughuli za uchimbaji zinahifadhiwa na kushughulikiwa kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa.
Aidha, amesema Tume inafuatilia utekelezaji wa mipango ya kufunga migodi (Mine Closure Plans) ili kuhakikisha maeneo yaliyokwishafanyiwa uchimbaji yanarejeshwa katika hali salama na yenye tija baada ya shughuli hizo kukamilika.
Kwa mujibu wa Rose, hatua hiyo ni muhimu katika kuhakikisha ukuaji wa sekta ya madini unaenda sambamba na uhifadhi wa mazingira na ustawi wa jamii zinazozunguka maeneo ya migodi.
Mbali na ukaguzi wa migodi, Tume ya Madini inaendelea kusimamia matumizi ya baruti katika shughuli za uchimbaji, ikiwemo utengenezaji, uingizaji, usafirishaji na biashara yake kwa mujibu wa sheria na kanuni zilizopo.
Katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, Tume ya Madini inaendelea kutoa elimu kwa wananchi na wadau kuhusu fursa mbalimbali zilizopo katika sekta hiyo na kuwahamasisha kushiriki katika shughuli za utafiti, uchimbaji, uchenjuaji, biashara ya madini pamoja na utoaji wa huduma kwenye migodi ya madini kwa kuzingatia matakwa ya sheria, ili kuchangia ukuaji wa uchumi wa Taifa.
Na Oscar NkemboMsimamizi wa Dawati la Ukaguzi wa Kemikali wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Ofisi ya Kanda ya Kati, Suitbert Sinduhije amesema Mamlaka imedhibiti Kemikali ya Sulphur iliyomwagika eneo la Mikumi na amewataka Madereva kuzingatia mafunzo wanayopata huku akiwasihi Wananchi kutoa taarifa kwa Mamlaka pindi ajali za Kemikali zinapotokea.
Sinduhije amesema hayo Juni 18, 2026 baada ya kukamilisha zoezi la kuiondoa Kemikali iliyomwagika ikiwa inasafirishwa kwa njia ya barabara ambapo alisema.
“Tumepata Taarifa kuhusu Kemikali hii iliyomwagika tumefika kwaajili ya kudhibiti na hali ni shwari athari ndogo ndogo zilizosababishwa na vumbi la Kemikali hiyo ni kusikia muwasho mwishili na usoni ambapo kunywa maji mengi na kuosha eneo lililofikiwa na Kemikali inamuweka mwananchi salama kabisa, nawasihi Madereva kuzingatia mafunzo ambayo Mkemia Mkuu amewapa, pia nawaomba wananchi waendelee kutupa taarifa pindi matukio haya yanapotokea ili yakabiliwe kwa wakati bila madhara kwa wananchi” alisema Sinduhije.
Aggrey Kinzilizi na Yusta Komba ni wakazi wa Mikumi wanaofanya Biashara kando ya Barabara wamesema wamesikia muwasho sehemu zao za mwili baada ya vumbi la Kemikali hiyo kuwafikia.
“Magari yanapopita yanatibua ile Kemikali inakuja huku kiukweli ni kuwashwa mwanzo mwisho, Mkemia amefika akatueleza tunawe kwa maji mengi kwa sasa hamna tena ule muwasho, tunaomba hawa wanaosafirisha Kemikali wasiwe peke yao Mkemia wa Serikali awe anawafuatilia kwa nyuma ili changamoto hizi zisitukute” walisema wakazi hao wa Mikumi.
June 18, 2026
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
Na Mwandishi WetuMkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Ramadhan Kailima, amepongeza ufanisi na uwazi wa Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja unaosimamiwa na Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja, akieleza kuwa mfumo huo umechangia kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya Serikali na kuhakikisha upatikanaji wa mafuta nchini.
Bw. Kailima alitoa pongezi hizo Juni 18, 2026 alipotembelea banda la PBPA katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.
Akizungumza baada ya kupata maelezo kuhusu utekelezaji wa mfumo huo, alisema kuwa umejengwa katika misingi ya uwazi na ushindani, jambo linalosaidia kupunguza gharama za uagizaji wa mafuta na kuongeza ufanisi katika usimamizi wa sekta hiyo muhimu kwa uchumi wa nchi.
Akitoa ufafanuzi kwa mgeni huyo, Mkaguzi wa Mafuta wa PBPA, Bw. Issa Mwitazy, alisema kuwa katika mfumo wa uagizaji mafuta kwa pamoja, ushindani hujikita katika gharama za usafirishaji wa mafuta (Premium).
Alieleza kuwa wazabuni hushindanishwa kwa kuwasilisha bei za usafirishaji wa bidhaa za petroli, dizeli na mafuta ya taa, ambapo mzabuni mwenye gharama nafuu zaidi hupatiwa zabuni husika.
“Utaratibu huu umetuwezesha kuhakikisha upatikanaji wa mafuta ya kutosha nchini wakati wote na wakati huohuo kuipa Serikali taarifa sahihi za kiasi cha mafuta na hivyo kuwezesha ukusanyaji wa mapato yatokanayo na biashara ya mafuta,” alisema.
Aliongeza kuwa mikataba ya uagizaji wa mafuta husainiwa mapema kabla ya bidhaa kuwasili nchini, jambo linaloiwezesha Serikali kufanya makadirio sahihi ya mapato yatokanayo na sekta hiyo.
Kwa mujibu wa Mwitazy, mafanikio ya mfumo huo yameifanya PBPA kuwa kitovu cha huduma za uagizaji mafuta kwa nchi kadhaa za ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, zikiwemo Malawi, Rwanda, Zambia na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambazo huleta mahitaji yao kupitia mfumo wa uagizaji wa mafuta kwa pamoja.
Ziara ya Bw. Kailima katika banda la PBPA ni sehemu ya shughuli za Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayolenga kuonesha mafanikio, huduma na ubunifu unaotekelezwa na taasisi za umma katika kuwahudumia wananchi na kuchangia maendeleo ya taifa.

Afisa Mwandamizi wa Idara ya Usimamizi wa Sera za Ununuzi wa Umma, Wizara ya Fedha, Bi. Anne Swila, akitoa elimu kwa wananchi kuhusu Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Mnyororo wa Ugavi ya Mwaka 2025, walipotembelea Banda la Maonesho la Wizara ya Fedha, katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026, yenye Kaulimbiu ya “Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu”, yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.
Msimamizi wa Fedha Mkuu, Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Wizara ya Fedha, Bi. Grace Samwel, akitoa elimu kwa mwananchi kuhusuusimamizi wa fedha binafsi, walipotembelea Banda la Maonesho la Wizara ya Fedha, katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026, yenye Kaulimbiu ya “Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu”, yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.Mchumi Mkuu wa Idara ya Ubia Kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi, Wizara ya Fedha, Bi. Josephina Buhili, na Mchumi Daraja la Kwanza wa Idara ya Ubia Kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi, Bi. Anastazia Amandi, wakitoa elimu kwa wananchi kuhusu, majukumu, mipango na malengo pia miradi mbalimbali iliyotekelezwa na Idara hiyo, walipotembelea Banda la Maonesho la Wizara ya Fedha, katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026, yenye Kaulimbiu ya “Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu”, yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.
Mchumi Mwandamizi wa Idara ya Bajeti, Wizara ya Fedha, Bi. Consolatha Komba, akifafanua kwa wananchi kuhusu, vipaumbele na utekelezaji wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2026/27, walipotembelea Banda la Maonesho la Wizara ya Fedha, katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026, yenye Kaulimbiu ya “Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu”, yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.
Maafisa wa Wizara ya Fedha wakiendelea kutoa elimu kwa wananchi waliotembelea Banda la Wizara ya Fedha, kuhusu majukumu yanayotekelezwa na wizara, wakati wananchi hao walipotembelea Banda la Wizara ya Fedha, katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, yenye kauli mbiu ‘Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Maendeleo Endelevu’, yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali, jijini Dodoma.Serikali imeanza kutumia Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Mnyororo wa Ugavi ya Mwaka 2025, hatua inayolenga kufungamanisha na kuboresha usimamizi wa shughuli za Mnyororo wa Ugavi nchini ili kuongeza ufanisi, matumizi bora ya rasilimali na kupata thamani halisi ya fedha za umma.
Hayo yalibainishwa na Afisa Mwandamizi wa Idara ya Usimamizi wa Sera za Ununuzi wa Umma, Wizara ya Fedha, Bi. Anne Swila, wakati akitoa elimu kwa wananchi waliotembelea Banda la Maonesho la Wizara ya Fedha, katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026, yenye Kaulimbiu ya “Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu”, yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.
Alisema kuwa Sera hiyo inalenga maeneo sita makuu, yakiwemo Ununuzi wa Umma, Ugomboaji na Uondoshaji wa Mizigo ya Serikali, Upokeaji na Urejeshaji, Utunzaji na Uhifadhi, Usambazaji, pamoja na uhifadhi wa Mazingira na Utawala Bora.
‘‘Kwa miaka mingi tumekuwa na sheria nzuri za ununuzi, lakini hazikuwa zimeunganishwa kwa msingi mmoja wa kisera, Sera hii sasa inakwenda kuziba pengo hilo na kuhakikisha kila shilingi ya umma inatumika kwa thamani yake halisi, kwa kuhakikisha mikakati ya utekelezaji inajumuisha kuimarisha udhibiti wa bei, uchaguzi wa wazabuni, na kuendeleza Kada ya Ununuzi na Ugavi Serikalini " alieleza Bi. Swila.
Alisisitiza kuwa ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wa Sera hii itaongeza ushindani na kuwapa fursa wazabuni wazawa, sekta binafsi na makundi maalum ya kijamii, hatua itakayowezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika uchumi na kuchochea ukuaji wa ajira.
Bi. Swila alisema Sera hiyo pia inatarajiwa kuimarisha matumizi ya mifumo ya kielektroniki na rasilimali za ndani, kuvutia uwekezaji katika miundombinu ya uhifadhi na usambazaji, na hivyo kuifanya sekta ya mnyororo wa ugavi kuwa kichocheo muhimu cha maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
‘‘Miongoni mwa mafanikio yanayotarajiwa ni kuongezeka kwa ufanisi, udhibiti bora wa gharama, kuimarika kwa ubora wa huduma kwa wananchi, ongezeko la ajira, uzingatiaji wa uhifadhi wa mazingira, na kuwa na mfumo jumuishi wa ufuatiliaji na tathmini utakaohakikisha utekelezaji wa sera unaleta tija iliyokusudiwa’’, alifafanua Bi Swila.
Aidha, alisema kuwa Sera hiyo itawezesha kuwepo kwa mfumo jumuishi wa ufuatiliaji na tathmini, hatua itakayoifanya sekta ya mnyororo wa ugavi kuwa kichocheo muhimu cha maendeleo ya kiuchumi na kijamii na kuchangia kupunguza umasikini nchini.
Sera hiyo inatarajiwa kutekelezwa kwa kipindi cha miaka 10 kuanzia mwaka 2026 hadi 2036 na tathmini ya utekelezaji itafanyika kila baada ya miaka mitano ya utekelezaji.

Tume ya Madini imesema kuanzishwa kwa masoko ya madini na vituo vya ununuzi wa madini nchini kumeongeza uwazi katika biashara ya madini na kusaidia kudhibiti utoroshaji wa rasilimali hiyo, hatua iliyochangia kuongezeka kwa mapato ya Serikali.
Dodoma – “Sasa najua ni nini ninapaswa kuangalia ninapojaza mafuta, kununua sukari au hata ninaponunua gesi ya kupikia.” Ni kauli ya Bw. Bilson Vedastus, mmoja wa wananchi waliotembelea banda la Wakala wa Vipimo (WMA) katika Maonesho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea Viwanja vya Chinangali Park, Dodoma.
















.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)












.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)


.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)



