Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Asha-Rose Migiro, leo Jumatatu,Machi 9,2026, amefungua rasmi mafunzo maalum ya Uongozi na Utawala Bora kwa viongozi na watendaji waandamizi wa Chama yanayofanyika katika Ukumbi wa Mount Royal, Mkoani Iringa.
March 09, 2026
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Asha-Rose Migiro, leo Jumatatu,Machi 9,2026, amefungua rasmi mafunzo maalum ya Uongozi na Utawala Bora kwa viongozi na watendaji waandamizi wa Chama yanayofanyika katika Ukumbi wa Mount Royal, Mkoani Iringa.
Ameyasema hayo leo Jumapili, Machi 08, 2026 alipozungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Laela A wilayani Sumbawanga, Rukwa. Amesisitiza kuwa watu hawatovumiliwa kwa kuwa wana lengo la kuliingiza Taifa katika njaa.
Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo baada ya Mbunge wa Viti Maalumu, Sylvia Sigula kuishukuru Serikali kwa kuwapatia ruzuku ya pembejeo ila ameiomba Serikali kuwatatulia changamoto ya kuuziwa mbegu zisizokuwa na ubora jambo linalosababisha wakulima kupata hasara kwani kilimo ndio uchumi wa Rukwa.
ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kufanya uchunguzi wa kina kuhusu matumizi ya fedha za miradi ya maendeleo katika baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Rukwa kufuatia taarifa za kuchelewa kwa utekelezaji wa miradi hiyo.
Ametoa agizo hilo leo Jumapili (Machi 8, 2026) wakati akizungumza na mamia ya wananchi wa Laela mkoani Rukwa baada ya kupokea taarifa za utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika eneo hilo.
Dkt. Mwigulu amesema Serikali haitavumilia kuona miradi ya maendeleo ikicheleweshwa wakati fedha zake tayari zimetolewa kwa ajili ya kuwahudumia wananchi.
“Kamanda wa TAKUKURU nifanyie uchunguzi wa kina, senti mpaka senti, yeyote aliyehusika kwenye hii fedha hapa nipe taarifa hiyo ili niweze kufanya maamuzi,” amesema.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameonesha kutoridhishwa na kuchelewa kwa utekelezaji wa baadhi ya miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa shule za sekondari, madarasa pamoja na miundombinu mingine ya elimu katika eneo hilo.
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Kilimo, David Silinde amesema wizara amekuwa ikifanya uchunguzi na kuchukua hatua pale inapobaini kuwepo kwa pembejeo zisizokuwa na ubora na tayari kuna mtu mmoja amekamatwa mkoani humo.
Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Miti Sao Hill, PCO Tebby Yoramu akiwa anamfariji mtoto wa yatima wa kituo cha Caring from Childhood to Youth kilichopo katika kijiji cha Bumilayinga,wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.
Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Miti Sao Hill, PCO Tebby Yoramu akiwa akikabidhi zawadi katika kituo cha watoto yatima cha Caring from Childhood to Youth kilichopo katika kijiji cha Bumilayinga,wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake..jpg)
Na Fredy Mgunda, Mufindi
Ziara hiyo imefanyika ikiwa ni sehemu ya shughuli za kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, ambapo wanawake hao walionyesha upendo na mshikamano kwa watoto hao kwa kutumia muda kuzungumza nao pamoja na walezi wao na kusikiliza changamoto wanazokabiliana nazo.
Akizungumza kwa niaba ya wanawake hao, Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Miti Sao Hill, PCO Tebby Yoramu, alisema licha ya majukumu yao ya kulinda na kuhifadhi rasilimali za misitu, wanatambua pia umuhimu wa kushiriki katika shughuli za kijamii zinazogusa maisha ya watu moja kwa moja.
Alisema vitendo hivyo vinasaidia kuimarisha upendo, mshikamano na ushirikiano ndani ya jamii, huku vikiwapa watoto walioko katika mazingira magumu matumaini na ari ya kuendelea kupambana ili kufikia malengo yao ya maisha.
Kwa upande wake, Meneja wa Kituo cha Caring from Childhood to Youth, Bw. Ponsiano Mfikwa, aliwashukuru wanawake hao kwa kuwatembelea na kuwakumbuka watoto hao, akisema ujio wao umeleta faraja kubwa kwa watoto pamoja na walezi wao.
Alisema msaada huo ni ishara ya moyo wa upendo na unatoa mfano mzuri kwa jamii kuendelea kuwasaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu ili waweze kukua katika malezi bora.
Naye Diwani wa Kata ya Sao Hill ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Mafinga, Mhe. Stephen Msigwa, aliwapongeza wanawake wahifadhi kwa juhudi zao katika kulinda na kuhifadhi rasilimali za misitu pamoja na kushiriki katika shughuli za kijamii.
Ameyasema hayo tarehe 8 Machi 2026, katika Mji wa Laela, Halmashauri ya wilaya ya Sumbawanga wakati wa ziara ya Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba iliyoanza jana mkoani Rukwa.
“Kwa
maelekezo ya Rais, Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan na maelekezo yako, tunaendelea kuhakikisha
inapofika mei 2026 tunawasha umeme kupitia mradi wa TAZA. Hali ya mradi inaenda
vizuri na kama kila kitu kitakwenda kama kilivyo, itakapofika mwezi wa tano
mwaka huu hatimaye Mkoa huu wa Rukwa utanufaika na umeme wa gridi.” Amesema
Mhe.Salome
Ameeleza
kuwa, kwa sasa mkoa wa Rukwa unapata umeme kutoka nchini Zambia kupitia
mashirikiano ya biashara ya umeme katika nchi za Ukanda wa Kusini mwa Afrika (Southern
Africa Power Pool) ambayo yanawezesha nchi wanachama kuuza au kununua umeme pale
kunapokuwa na uhitaji ili kukidhi mahitaji ya wananchi.
Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia, amesema jitihada mbalimbali zinaendelea ili kuweza kufikia asilimia 80 ya wananchi wanaotumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo 2034 ikiwemo ya kusambaza majiko banifu na mitungi ya gesi kwa bei ya ruzuku.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalum), Prof. Palamagamba J. Kabudi, ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa 26 wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jumuiya ya Madola (CFAMM) uliofanyika Machi 8, 2026 jijini London, Uingereza akimwakilisha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.).March 08, 2026
March 07, 2026
Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba akiitika Dua wakati wa mashindano ya kuhifadhi qur’an Tukufu yaliyofanyika katika Kijiji cha Bukulu, Kondoa mkoani Dodoma,Machi 7, 2026
Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba akizungumza na Mbunge wa Kondoa ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji wakati wa mashindano ya kuhifadhi qur’an Tukufu yaliyofanyika katika Kijiji cha Bukulu, Kondoa mkoani Dodoma, Machi 7, 2026.
WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba ametoa majibu ya mgogoro wa ardhi baina ya wakazi wa Wilaya ya Monduli na Jeshi la Wananchi ambao umedumu tangu mwaka 2004 baada ya kumpigia simu Mkuu wa Majeshi nchini na kumweleza kilio cha wanaMonduli.




















































