Jaji Mwambegele ameyasema
hayo wakati akitembelea mafunzo ya siku moja kwa Makarani hao waogozaji katika
Jimbo la Isimani yaliyofanyika katika Shule Sekondari Ufundi Ifunda mkoani
Iringa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Uchaguzi huo utakaofanyika Jumatatu ya
Juni 1, 2026.
Jaji Mwambegele pia
amewasisistiza watendaji hao kuishi
kwenye viapo vyao wakati wa utekelezaji majukumu yao ya Uchaguzi ili kujiepusha
na upendeleo wa aina yoyote.
Kwa upande wake mwenyekiti wa Mafunzo
hayo ya Makarani Waongozaji Wapiga Kura Vituoni Bw. Baraka Matonya amemuhakikishia
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kwamba watafuata sheria, kanuni,
miongozo na maelekezo ya Tume wakati wote wa Utekelezaji wa majukumu yao ya Uchaguzi
.
Naye Msimamizi wa Uchaguzi
wa Jimbo la Isimani,Bi. Caroline Otieno amesema maandalizi ya uchaguzi huo Mdogo wa Jimbo hilo, yamekamilika kwa
asilimia 100 ambapo vifaa vyote vimepokelewa.
Uchaguzi huo utafanyika
sambamba na uchaguzi mdogo katika kata 12 za Tanzania Bara ambazo ni Mzimuni
iliyopo Manispaa ya Kinondoni; Zongomera, Manispaa ya Kahama; Itilo,
Halmashauri ya Mji wa Nzega; Ketare, Halmashauri ya Mji wa Tarime na Nyumbigwa,
Halmashauri ya Mji wa Kasulu.
Nyingine ni kata ya Kala
iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi; Ziba, Halmashauri ya Wilaya Igunga;
Kamsisi, Halmashauri ya Wilaya ya Mlele; Nyamugali, Halmashauri ya wilaya ya
Buhigwe; Namasakata Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru; Bwongera, Halmashauri ya
Wilaya ya Chato na Kibiti Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti.















































