Nafasi Ya Matangazo

April 30, 2026

Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa (Mst) Mbarouk Salim Mbarouk akizungumza wakjati akifunga mafunzo ya watendaji wa uchaguzi yaliyofanyika Mkoani Morogoro. Mafunzo hayo yamefungwa leo tarehe 30 Aprili, 2026 na yaliyofanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 28 Aprili, 2026.
Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa (Mst) Mbarouk Salim Mbarouk akizungumza wakjati akifunga mafunzo ya watendaji wa uchaguzi yaliyofanyika Mkoani Morogoro. Mafunzo hayo yamefungwa leo tarehe 30 Aprili, 2026 na yaliyofanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 28 Aprili, 2026.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa rufani Jacobs Mwambegele akiwa katika ufungaji wa mafunzo hayo. 

Na. Mwandishi Wetu, Morogoro
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imetoa wito kwa watendaji wa uchaguzi kuhakikisha wanatumia muda wao kusoma Katiba, sheria za uchaguzi, kanuni na maelekezo ya Tume ili waweze kusimamia uchaguzi kwa weledi.
 
Wito huo umetolewa na Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa (Mst) Mbarouk Salim Mbarouk Mkoani Morogoro leo tarehe 30 Aprili, 2026 wakati akifunga mafunzo ya watendaji wa uchaguzi yaliyofanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 28 Aprili, 2026.
 
Mafunzo hayo ni sehemu ya mchakato wa maandalizi ya uchaguzi mdogo wa ubunge kwenye Jimbo la Ismani Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Mkoani Iringa na Kata 12 za Tanzania Bara unaotarajiwa kufanyika tarehe 01 Juni, 2026.
 
“Natumia nafasi hii kuendelea kuwasisitiza kuhusu umuhimu wa kutenga sehemu ya muda wenu kusoma Katiba, sheria na maelekezo mbalimbali yanayotolewa na Tume ili yawaongoze katika kusimamia uchaguzi utakaokuwa huru na wa haki,” amesema Jaji Mbarouk.
 
Amewataka watendaji hao wa uchaguzi kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na weledi ili kufanikisha uchaguzi huo mdogo ambao unafanyika kujaza nafasi wazi ya mbunge na madiwani.
 
 “Jukumu lililopo mbele yetu ni kubwa na muhimu, linahitaji umakini na kujituma. Ni matazamio ya Tume kwamba, baada ya kupatiwa mafunzo haya, mtatekeleza majukumu yenu kwa ufanisi na weledi mkizingatia ratiba ya utekelezaji ili kufanikisha uchaguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Ismani na Kata 12 za Tanzania Bara unaotarajiwa kufanyika tarehe 01 Juni, 2026,” amesema Jaji Mbarouk.
 
Amesisitiza kuwa ili ufanisi uwepo ni muhimu watendaji hao wazingatie sifa na uwezo wakati wa kuteua na kuajiri watendaji wa vituo vya kupigia kura kwa kuwa hao ndio watakaosimamia zoezi la kupiga kura na kuhesabu kura vituoni.
 
“Kuhusu ajira za watendaji wa vituo, tunayo imani kuwa mtateua na kuajiri watendaji wenye sifa na uwezo wa kufanya kazi hii muhimu kwa kuwa hao ndio watakaosimamia zoezi la kupiga kura na kuhesabu kura vituoni. Kazi ambayo inahitaji umahiri, umakini na weledi katika kuitekeleza.,” amesema Jaji Mbarouk.
 
Amewataka watendaji hao kuhakikisha kuwa mafunzo ya watendaji wa vituo yanafanyika kwa ufanisi na weledi katika tarehe zilizopangwa kwenye ratiba ya utekelezaji wa shughuli za uchaguzi.
 
Ameongeza kuwa mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo ili waweze kufahamu majukumu yao na kuyatekeleza ipasavyo wakati wa uchaguzi.
 
Mafunzo hayo yamewahusisha Waratibu wa Uchaguzi wa Mikoa, Wasimamizi wa Uchaguzi, Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi Ngazi ya Jimbo, Wasimamizi wa Uchaguzi Ngazi ya Kata, Maafisa Uchaguzi, Maafisa Ununuzi na Wahasibu.
 
Kata 12 za Tanzania Bara zitakazofanya uchaguzi wa Udiwani ni Mzimuni iliyopo Manispaa ya Kinondoni; Zongomera, Manispaa ya Kahama; Itilo, Halmashauri ya Mji wa Nzega; Ketare, Halmashauri ya Mji wa Tarime na Nyumbigwa, Halmashauri ya Mji wa Kasulu.
 
Nyingine ni kata ya Kala iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi; Ziba, Halmashauri ya Wilaya Igunga; Kamsisi, Halmashauri ya Wilaya ya Mlele; Nyamugali, Halmashauri ya wilaya ya Buhigwe; Namasakata Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru; Bwongera, Halmashauri ya Wilaya ya Chato na Kibiti Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti.

Sehemu ya watendaji wa uchaguzi katika jimbo la Isimani Mkoani Iringa na Kata 12 za Tanzania bara wakisikiliza hotuba ya kufunga mafunzo ya siku tatu yaliyofanyika mkoani Morogoro kuanzia tarehe 28 hadi 30 Aprili, 2026. 

Sehemu ya watendaji wa uchaguzi katika jimbo la Isimani Mkoani Iringa na Kata 12 za Tanzania bara wakisikiliza hotuba ya kufunga mafunzo ya siku tatu yaliyofanyika mkoani Morogoro kuanzia tarehe 28 hadi 30 Aprili, 2026. 

Sehemu ya watendaji wa uchaguzi katika jimbo la Isimani Mkoani Iringa na Kata 12 za Tanzania bara wakisikiliza hotuba ya kufunga mafunzo ya siku tatu yaliyofanyika mkoani Morogoro kuanzia tarehe 28 hadi 30 Aprili, 2026. 
Posted by MROKI On Thursday, April 30, 2026 No comments

April 29, 2026









Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) leo tarehe 29.04.2026 imezindua awamu ya pili ya kupokea mawazo bunifu kutoka kwa Umma katika kuongeza wigo wa kodi na kuboresha huduma za kodi nchini.

Akizindua awamu hiyo ya pili ya kupokea mawazo bunifu kutoka kwa Umma katika kuongeza wigo wa kodi na kuboresha huduma  jijini Dar es Salaam, Kamishna Mkuu wa TRA Bw. Yusuph Juma Mwenda amesema lengo la kuwashirikisha wananchi kutoa mawazo yao ni kutaka maboresho yanayofanywa na TRA pamoja na ubunifu utokane na wananchi wenyewe.

Amesema TRA ni chombo cha wananchi kinachokusanya kodi kwa wananchi kwaajili ya wananchi hivyo ni hatua muhimu kuwashirikisha kutoa mawazo yao ya ubunifu ikiwa ni awamu ya pili huku awamu ya kwanza ikitajwa kuwaibua wabunifu 9 kati ya 106 waliofika kwenye hatua ya pili kutoka wabunifu 5,681 waliowasilishq mawazo yao.

Kamishna Mkuu Mwenda amesema awamu ya pili ya Tuzo imeboreshwa kwa kiasi kikubwa kwa kuweka Kamati huru itayoratibu kazi zote zitakazotumwa na waombaji ambayo haihusishi watumishi wa TRA huku zawadi zitakazotolewa nazo zikiwa zimeboreshwa.

Amesema mshindi wa kwanza atajipatia Sh. Milioni 50, washindi wawili wa Pili watapata milioni 30 kila mmoja, washindi wa nafasi ya tatu wawili watapata Sh. Milioni 20 kila mmoja huku washindi wengine 15 wakipatiwa Sh. Milioni 10 kila mmoja ambapo washiriki ambao wazo lao litafika hatua ya pili watapatiwa Sh. Laki moja kwa kila mmoja wao.

Kukusu maeneo ya kipaumbele yatakayozingatiwa kwenye bunifu hizo amesema miongoni mwake ni Upanuzi wa wigo wa kodi hususan katika sekta isiyo rasmi, urahisishaji wa ukadiriaji na ulipaji wa kodi kwa wafanyabiashara wadogo, Maboresho ya huduma za Kidijitali, Maboresho ya utatuzi wa migogoro ya kikodi na matumizi ya teknolojia katika usimamizi wa kodi. 

Kamishna Mkuu Mwenda amewahakikishia wote wanaotarajia kuwasilisha mawazo yao ya ubunifu kuwa matarajio yao yatafikiwa hivyo wajitokeze kwa wingi kutuma mawazo bunifu.

Awali akimkaribisha Kamishna Mkuu, Naibu Kamishna Mkuu wa TRA Bw. Mcha Hassan Mcha mawazo bunifu yatakayotolewa yanatarajiwa kuongeza ufanisi katika masuala ya kodi na kutatua baadhi ya changamoto ikizingatiwa kuwa changamoto za kodi zinahitaji ushirikishwaji na matumizi ya teknolojia katika utatuzi wake.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Utafiti na Mipango Dkt. Ephraim Mdee amesema awamu hii  wamefanya Maboresho makubwa kwa vigezo na zawadi zinazotolewa na hiyo ni baada ya kupata uzoefu katika awamu ya kwanza sambamba na maoni ya wadau mbalimbali. 
Posted by MROKI On Wednesday, April 29, 2026 No comments

Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndg. Baraka Leonard, akizungumza na Naibu Katibu wa Bunge la Ghana anayeshughulikia Shughuli za Bunge, Ndg. Camillo Pwamang alipomtembelea leo tarehe 29 Aprili, 2026 ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.

Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndg. Baraka Leonard, akizungumza na Naibu Katibu wa Bunge la Ghana anayeshughulikia Shughuli za Bunge, Ndg. Camillo Pwamang alipomtembelea leo tarehe 29 Aprili, 2026 ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.

Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndg. Baraka Leonard, akisalimiana na Naibu Katibu wa Bunge la Ghana anayeshughulikia Shughuli za Bunge, Ndg. Camillo Pwamang alipomtembelea leo tarehe 29 Aprili, 2026 ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.
Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndg. Baraka Leonard, akionyeshwa alama kuu na muhimu katika historia na utamaduni wa ufalme wa Ashanti kutoka nchini Ghana na Naibu Katibu wa Bunge la Ghana anayeshughulikia Shughuli za Bunge, Ndg. Camillo Pwamang alipomtembelea leo tarehe 29 Aprili, 2026 ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.
Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndg. Baraka Leonard, akionyeshwa alama kuu na muhimu katika historia na utamaduni wa ufalme wa Ashanti kutoka nchini Ghana na Naibu Katibu wa Bunge la Ghana anayeshughulikia Shughuli za Bunge, Ndg. Camillo Pwamang alipomtembelea leo tarehe 29 Aprili, 2026 ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.
Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndg. Baraka Leonard, katika picha ya pamoja na Naibu Katibu wa Bunge la Ghana anayeshughulikia Shughuli za Bunge, Ndg. Camillo Pwamang baada ya mazungumzo yaliyofanyika leo tarehe 29 Aprili, 2026 ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.

Posted by MROKI On Wednesday, April 29, 2026 No comments






MKUU wa Wilaya ya Kiteto Mheshimiwa Remidius Mwema ameongoza zoezi la uchomaji ekari tano za dawa za kulevya aina ya bangi iliyolimwa ndani ya mashamba ya mahindi katika kitongoji cha Kimaraunga, Kijiji cha Mbigiri Kata ya Partimbo.

Mhe DC Mwema amewataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano  kwa Serikali kukabiliana  na ulimaji wa bangi huku akipongeza jitihada za utoaji taarifa zinazosaidia kubaini uwepo wa mashamba hayo. 

Amelitaka jeshi la polisi kuhakikisha linawakamata watuhumiwa wote ikiwa ni pamoja na wamiliki wa mashamba hayo huku akisisitiza wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo ili sheria ichukue mkondo wake.

“Tumeshirikisha wananchi katika zoezi la kuteketeza dawa za kulevya ili kuonyesha kwa vitendo dhamira njema ya Serikali katika mapambano haya na tunatuma ujumbe kwa wananchi wote kuendelea kukabiliana na hali hii, operesheni hizi zitaendelea wakati wote ndani ya Wilaya yetu ,wananchi waendelee kutoa ushirikiano,” amesema Mhe. Mwema.

Katika hatua nyingine Mhe. Mwema amesema 
Serikali imewekeza nguvu kubwa katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya kupitia Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA),vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na jamii kwa ujumla hatua ambayo imeendelea kuleta mafanikio makubwa katika kudhibiti uzalishaji, usafirishaji na matumizi ya dawa hizo hatarishi.

Aidha, Mkuu wa Wilaya amewasihi wananchi kuendelea kutoa taarifa pale wanapohisi au kushuhudia viashiria vya biashara au matumizi ya dawa za kulevya kwa vyombo husika ili kuifanya Wilaya ya Kiteto na nchi ya Tanzania kuwa mahali salama dhidi ya matumizi na biashara ya dawa hizo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Mbigiri  Omari Athumani Goda ameeleza utayari wao kuungana na Serikali katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya huku akitoa ahadi ya kushirikiana na jeshi la polisi kuhakikisha wamiliki wa mashamba hayo wanapatikana mara moja ili taratibu za kisheria ziweze kuchukua mkondo wake.

Hata hivyo, baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Mbigiri, wamepongeza jitihada za Serikali katika kuteketeza kwa moto dawa hizo za kulevya na kuepuka athari katika  jamii ikiwemo kupoteza nguvu kazi ya Taifa hususani kundi kubwa la Vijana.
Posted by MROKI On Wednesday, April 29, 2026 No comments








Fursa mpya za biashara, uwekezaji na ushirikiano wa kimkakati zimefunguliwa kufuatia kusainiwa kwa Hati ya Makubaliano ya Maelewano (MoU) kati ya Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC) na National Export Promotion Council of Belarus.

Hafla hiyo iliyofanyika Aprili 28,2026 Mkoani Dar es Salaam ilishuhudiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo, pamoja, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo (Mb) na Waziri wa Mambo ya Nje wa Belarus, Maxim Ryzhenkov.

Makubaliano hayo yanafungua milango ya ushirikiano katika sekta mbalimbali zenye mchango mkubwa kwa ukuaji wa uchumi, ikiwemo kilimo, viwanda na usindikaji, biashara ya bidhaa na huduma, teknolojia, madini, nishati, vifaa tiba, usafirishaji pamoja na upanuzi wa masoko ya kimataifa kwa bidhaa za Tanzania na Belarus.

Akizungumza katika hafla hiyo, Balozi Kombo alisema ushirikiano huo unaweka msingi imara wa kupanua mahusiano ya kiuchumi yenye manufaa kwa mataifa yote mawili na kuongeza mchango wa sekta binafsi katika maendeleo ya biashara na uwekezaji.

“Makubaliano haya yanaweka msingi imara wa kufungua fursa mpya za ushirikiano wenye manufaa kwa pande zote mbili,” alisema Balozi Kombo.

Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Nje wa Belarus, Maxim Ryzhenkov, alisema Belarus iko tayari kuendeleza ushirikiano wa vitendo utakaozalisha matokeo chanya ya kiuchumi na kibiashara kwa pande zote mbili.

“Tuko tayari kuendeleza ushirikiano wa vitendo utakaoleta matokeo chanya kwa mataifa yetu,” alisema Ryzhenkov.

Akizungumzia umuhimu wa makubaliano hayo kwa sekta binafsi, Rais wa TNCC, Bw. Vicent Minja, alisema MoU hiyo ni daraja muhimu la kufungua biashara na uwekezaji zaidi, akisisitiza utekelezaji madhubuti wa makubaliano hayo ili kuleta matokeo halisi.

“Sasa tunahitaji kuhamisha makubaliano haya kutoka kwenye nyaraka kwenda kwenye utekelezaji wenye matokeo,” alisema Minja.

Kupitia MoU hiyo, Tanzania na Belarus zinatarajiwa kuimarisha ushiriki wa sekta binafsi, kuongeza ubadilishanaji wa teknolojia na maarifa, kuchochea miradi ya pamoja, na kuimarisha diplomasia ya uchumi kupitia masoko mapya na fursa za kimataifa.
Posted by MROKI On Wednesday, April 29, 2026 No comments

April 28, 2026




Na Mwandishi wetu, Addis Ababa, Ethiopia 
Serikali ya Tanzania imesisitiza umuhimu wa matumizi endelevu ya madini muhimu (critical minerals) kama nyenzo kuu ya kuchochea maendeleo ya viwanda na kukuza uchumi Barani Afrika.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, Aprili 28, 2026, wakati wa kongamano la Kikanda lililofanyika Makao Makuu ya Tume ya Umoja wa Mataifa ya Uchumi Afrika (UNECA) jijini Addis Ababa.

Dkt. Kiruswa amesema Afrika ina nafasi ya kimkakati duniani kutokana na utajiri wa madini muhimu yanayotumika katika teknolojia za nishati safi, akitaja madini ya lithiamu, kobalti na nikeli kuwa nguzo muhimu katika uzalishaji wa betri za magari ya umeme na mifumo ya nishati jadidifu. Amesema hali hiyo inaifanya Afrika kuwa mhimili muhimu katika mabadiliko ya uchumi wa dunia kuelekea matumizi ya nishati safi.

Aidha, Dkt. Kiruswa ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Kongamano hilo, ambapo ameeleza dhamira ya Serikali ya Tanzania ya kuhakikisha rasilimali za madini zinasimamiwa kwa manufaa ya wananchi kupitia Sera na Mikakati inayolenga uongezaji thamani wa madini ndani ya nchi, ajira na ukuaji jumuishi wa uchumi.

Awali, Aprili 27, 2026, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Msafiri Mbibo, alisema Afrika ina fursa kubwa ya kunufaika na ongezeko la mahitaji ya madini hayo duniani, lakini akasisitiza umuhimu wa kuhakikisha uwekezaji unaendana na misingi ya uendelevu na uwajibikaji.

Alibainisha changamoto zinazoikabili sekta ya madini kuwa ni pamoja na uchimbaji usio rasmi, uharibifu wa mazingira na ushirikishwaji mdogo wa jamii, akisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya serikali, sekta binafsi na wadau wa maendeleo ili kukabiliana nazo.

Pamoja na Mambo mengine, Mbibo aliongeza kuwa Tanzania itaendelea kuimarisha ushirikiano wa kikanda na kimataifa sambamba na kuhamasisha matumizi ya teknolojia za kisasa katika shughuli za uchimbaji ili kuongeza tija na kupunguza athari kwa mazingira.

Kongamano hilo limewakutanisha mawaziri, wataalamu na wadau wa sekta ya madini kutoka nchi mbalimbali za Afrika na nje ya bara hilo, likilenga kujadili namna bora ya kuhakikisha madini muhimu yanachangia kikamilifu maendeleo ya viwanda na ustawi wa jamii.

Miongoni mwa washiriki mashuhuri ni Hailemariam Desalegn na Habtamu Tegegne, ambao kwa pamoja wamesisitiza umuhimu wa ushirikiano wa kikanda ili Afrika inufaike ipasavyo na rasilimali zake za madini.
Posted by MROKI On Tuesday, April 28, 2026 No comments
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano, Deus Sangu akizungumza wakati wa kilele cha Maadhimisho ya Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) 2026 yaliyofanyika mkoani Njombe Region.
 
Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Anthony Mtaka akizungumza wakati wa kilele cha Maadhimisho ya Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) 2026 yaliyofanyika mkoani Njombe Region.
Viongozi mbalimbali wakifuatilia Maadhimisho ya Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) 2026 yaliyofanyika mkoani Njombe Region.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA), Bi. Khadija Mwenda, akizungumza wakati wa kilele cha Maadhimisho ya OSHA 2026 yaliyofanyika mkoani Njombe Region.
Picha ya pamoja ya viongozi.

Na Mwandishi Wetu, Njombe.
CRDB Bank Plc imeshiriki katika kilele cha Maadhimisho ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) 2026 yanayofanyika Njombe Region, ikionesha dhamira yake ya kuunga mkono juhudi za Serikali pamoja na wadau mbalimbali katika kuboresha mazingira ya kazi na ustawi wa wafanyakazi.

Maadhimisho hayo yanabebwa na kaulimbiu isemayo, “Mazingira Bora ya Kazi Kisaikolojia ni Njia ya Kuimarisha Ustawi wa Wafanyakazi na Kujenga Taasisi Imara.”

Kilele cha maadhimisho hayo kimeongozwa na Deus Sangu, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Ajira na Mahusiano.

Katika maonesho hayo, benki hiyo imekuwa ikiendelea kutoa huduma mbalimbali za kifedha kwa wananchi wa Njombe na maeneo ya jirani, zikiwemo ufunguzi wa akaunti, elimu ya fedha pamoja na huduma za mikopo kwa wajasiriamali wadogo na wa kati.

Wananchi wengi wamejitokeza kutembelea banda la benki hiyo kwa lengo la kujifunza na kunufaika na huduma zinazotolewa, hatua inayotajwa kusaidia kuongeza uelewa kuhusu matumizi sahihi ya huduma za kifedha.

Mbali na huduma hizo, CRDB Bank Plc pia imeendelea kutoa huduma za afya bure kwa wananchi kama sehemu ya mchango wake kwa jamii.

Benki hiyo ni mdhamini mkuu wa maadhimisho hayo muhimu, ambapo ushiriki wake unaakisi dhamira ya kuchochea maendeleo ya kiuchumi sambamba na kulinda afya na usalama wa jamii.

Posted by MROKI On Tuesday, April 28, 2026 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo