Nafasi Ya Matangazo

March 20, 2026



Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Pwani imekamata magendo ya bidhaa katika Wilaya ya Bagamoyo ikiwemo viroba 50 vya mchele, madumu 10 ya mafuta ya kula na sabuni box 25 Aina ya Malaika.

Magendo hayo yalikamatwa kufuatia operesheni ya udhibiti wa bidhaa zinazoingizwa au kusafirishwa bila kufuata taratibu za kisheria za forodha.

Bidhaa hizo zilizokamatwa zimehifadhiwa katika yadi ya TRA Bagamoyo kwa ajili ya kuendelea na taratibu za kiforodha na hatua nyingine za kisheria.

Mamlaka ya Mapato Tanzania imeendelea kutoa wito kwa wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla kufuata sheria na taratibu za kodi na forodha ili kuepuka hasara na adhabu zinazoweza kujitokeza.
Posted by MROKI On Friday, March 20, 2026 No comments
Sehemu ya wanafunzi wa wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata elimu kuhusiana na  masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa  ,ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.
******************
KATIKA harakati za kuimarisha uelewa wa haki za walaji nchini, Tume ya Ushindani (FCC) leo Machi 19, 2026 imetoa elimu kwa wanachuo wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha kuhusu masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji, ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Elimu hiyo ilitolewa na FCC kwa lengo la kuwajengea uelewa wanachuo kuhusu haki zao wanapokuwa wanatumia bidhaa na huduma mbalimbali. Wanachuo walipata nafasi ya kujifunza mambo muhimu ambayo mara nyingi huyapuuzia katika maisha yao ya kila siku.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo,Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi FCC Bi.Magdalena Hall,amewaeleza wanachuo kuwa wengi wao huingia katika mikataba bila kusoma masharti yake, hali inayoweza kusababisha hasara au kunyimwa haki zao bila wao kutambua.

Amefafanua kuwa mikataba mingi hasa ya huduma za simu, mikopo na manunuzi ya mtandaoni huwa na vifungu vinavyohitaji umakini mkubwa kabla ya kukubaliwa. Hivyo aliwataka wanachuo kujenga utamaduni wa kusoma na kuelewa kila wanachosaini.

Aidha, amesema  kuwa mlaji ana haki ya kupata bidhaa bora, taarifa sahihi na huduma stahiki. Pale haki hizo zinapokiukwa, mlaji anatakiwa kuchukua hatua za kisheria au kuripoti kwa mamlaka husika.

"FCC imesisitiza kuwa elimu hii ni endelevu na inalenga kuwafikia makundi mbalimbali ya jamii ili kujenga taifa lenye walaji wenye uelewa na uwezo wa kufanya maamuzi sahihi."amesema Bi.Hall.

Kwa ujumla, mafunzo hayo yamewajengea wanachuo uelewa mkubwa na kuwahamasisha kuwa mabalozi wa haki za walaji, huku yakichangia mafanikio ya maadhimisho ya Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.
Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi FCC Bi.Magdalena Hall,akitoa elimu kuhusu masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha ,ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.
Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi FCC Bi.Magdalena Hall,akitoa elimu kuhusu masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha ,ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.
Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi FCC Bi.Magdalena Hall,akitoa elimu kuhusu masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha ,ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.
Sehemu ya wanafunzi wa wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata elimu kuhusiana na  masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa  ,ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.
Sehemu ya wanafunzi wa wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata elimu kuhusiana na  masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa  ,ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.
Sehemu ya wanafunzi wa wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata elimu kuhusiana na  masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa  ,ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.
 
Wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha wakiuliza maswali mbalimbali kuhusu namna ya kutofautisha mikataba halisi na feki  mara baada ya kupatiwa elimu na FCC  ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani. 
 
Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi FCC Bi.Magdalena Hall,akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha mara baada ya kuwapatia elimu kuhusu masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.
 
Posted by MROKI On Friday, March 20, 2026 No comments
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewasihi Viongozi wa Dini kuendelea kuwekeza katika kufundisha maadili mema kwa kizazi cha sasa ili kuwa na Taifa zuri baadaye.
 
Makamu wa Rais amesema hayo wakati aliposhiriki Futari iliyoandaliwa na Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT) iliyohusisha Viongozi wa Dini na Wadau wa Amani nchini, iliyofanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 19 Machi 2026. Amesema ni vema kutoa kipaumbele cha pekee katika eneo la maadili kwa kuwa kuharibika kwa malezi ya sasa ni kuharibu kizazi kijacho.
 
Amesema kumekua na changamoto katika maadili na makuzi ya watoto, hivyo Viongozi wa Dini watakapoweka kipaumbele katika kufundisha maadili kwa waumini watakuwa wametoa mchango mkubwa kwa jamii na Taifa kwa ujumla.
 
Makamu wa Rais, ameipongeza Jumuiya ya Maridhiano na Amani (JMAT) kwa kazi kubwa waliyofanya ya kuimarisha mahusiano ya dini mbalimbali hapa nchini. Amesema Serikali inatambua na kuthamini kazi inayofanya Jumuiya hiyo ikiwa ni pamoja na kuelimisha wajibu wa viongozi wa dini na wajibu waumini katika kutambua nafasi zao kuleta amani nchini.
 
Makamu wa Rais amesema Tanzania inajivunia kuwa nchi ambayo wananchi wake wana ushirikiano bila kujali dini zao, hivyo ni muhimu kuendelea kusimamia ushirikiano huo.
 
Aidha, amesema ni muhimu kuimarisha mambo yote yaliyofanywa kipindi cha toba yaani Mwezi Mtukufu wa Ramadhan na kwaresma na kuyaendeleza.
 
Futari hiyo imehudhuriwa na Viongozi wa dini mbalimbali, Mabalozi wanaowakilisha nchi zao Tanzania, Wakuu wa Taasisi mbalimbali, Wasanii,  pamoja na wadau wa amani nchini.











Posted by MROKI On Friday, March 20, 2026 No comments

Na Mwandishi Wetu, Lushoto
Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa kushirikiana na Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Mhe. Zephania Sumaye, jana Machi 19, 2026 wameongoza zoezi la upandaji miti katika kijiji cha Kileti, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Misitu Duniani pamoja na kuimarisha uhifadhi shirikishi wa misitu.
 
Akizungumza katika tukio hilo, Mkuu wa Wilaya alimpongeza Kamisna wa Uhifadhi TFS, Pro. Dos Santos Silayo kwa kuendeleza ushirikiano na jamii zinazozunguka misitu, akieleza kuwa hatua hiyo inachangia kurejesha manufaa kwa wananchi na kuongeza ulinzi wa rasilimali hizo muhimu.
 
“Ni jambo la kujivunia kuona wananchi wananufaika moja kwa moja na rasilimali za misitu. Ushirikiano huu utasaidia kuhakikisha misitu inalindwa na kuendelezwa kwa manufaa ya sasa na vizazi vijavyo,” alisema.
 
Alisisitiza umuhimu wa kuweka mipaka ya wazi ya mashamba na maeneo ya misitu kwa kupanda miti, akibainisha kuwa hatua hiyo itasaidia kudhibiti uharibifu wa misitu na kuboresha matumizi bora ya ardhi katika maeneo ya milimani ya Lushoto.
 
Kwa upande wake, Mhifadhi Mkuu wa Shamba la miti Shume, Christopher Yakuti, alifananisha umuhimu wa misitu na maisha ya binadamu, akieleza kuwa uwepo wa misitu ni sawa na uhusiano wa samaki na maji.
 
“Misitu inapotea, maisha pia yanakuwa hatarini. Ni wajibu wetu sote kushirikiana kulinda maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya uhifadhi,” alisema.
 
Naye Kaimu Mhifadhi wa Hifadhi ya Mazingira Asilia Magamba, Mhifadhi Mwandamizi Grace Kabuche, alisema maadhimisho hayo yameambatana na hatua mbili muhimu; kusaidia jamii zinazozunguka hifadhi pamoja na kuhamasisha upandaji miti kwa lengo la uhifadhi endelevu.
 
Alieleza kuwa zaidi ya miti 2,000 imepandwa katika kijiji cha Kileti, huku TFS ikikabidhi mifuko 280 ya saruji kwa vijiji na taasisi za elimu ili kusaidia miradi ya maendeleo, ikiwemo ujenzi wa zahanati na vyoo vya shule.
 
Kabuche aliongeza kuwa vijiji vinavyozunguka hifadhi hiyo vimeunda kamati maalum za uhifadhi zinazoshiriki katika doria na ulinzi wa misitu, hatua inayosaidia kuimarisha usimamizi shirikishi wa rasilimali hizo.
 
Zoezi hilo linaendelea kuwa sehemu ya juhudi za kitaifa za kuhamasisha jamii kushiriki katika uhifadhi wa misitu na kutekeleza ajenda ya maendeleo endelevu kupitia matumizi bora ya rasilimali za asili.









Posted by MROKI On Friday, March 20, 2026 No comments




Wananchi, wanafunzi na walimu wa Kata ya Busonzo, Kijiji cha Idoselo wilayani Bukombe, wamepanda miche 200 ya miti ya matunda katika Shule Shikizi ya Mererani ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Misitu Duniani mwaka 2026.

Zoezi hilo lililofanyika Machi 19, limehusisha ushiriki mkubwa wa wananchi waliojitokeza kwa wingi kuonesha dhamira ya kulinda na kuhifadhi rasilimali za misitu kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Akizungumza katika tukio hilo, Diwani wa Kata ya Busonzo, Mhe. John Malikioli, aliwahimiza wananchi kuhakikisha wanaitunza miti hiyo ili iweze kukua na kuleta manufaa ya kiuchumi na kimazingira.

“Kupanda miti ni hatua ya kwanza, lakini kuitunza ni wajibu wa kila mmoja wetu,” alisisitiza.

Kwa upande wake, Meneja wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Emilian Fabian, aliwataka wananchi kubadili mtazamo hasi dhidi ya wahifadhi na badala yake kushirikiana nao katika kulinda rasilimali za misitu.

Alisema wahifadhi wapo kwa ajili ya kuhakikisha mazingira yanatunzwa na siyo kuwa kikwazo kwa wananchi.

Naye Afisa Misitu, Bi. Bahati Kamwana, akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, alitoa wito kwa wananchi kuendeleza juhudi za utunzaji wa misitu ili kuhakikisha Wilaya ya Bukombe inakuwa ya kijani na yenye mazingira rafiki kwa maendeleo endelevu.

Katika hatua nyingine, imeelezwa kuwa Wilaya ya Bukombe imeendelea kufanya vizuri katika kampeni ya upandaji miti, ambapo zaidi ya miche 500,000 imepandwa katika msimu huu, hatua inayochangia uhifadhi wa mazingira na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Maadhimisho ya Siku ya Misitu Duniani hutoa fursa kwa jamii kukumbushwa umuhimu wa misitu katika kukuza uchumi, kulinda mazingira na kuboresha maisha ya binadamu, huku wananchi wakihimizwa kuendelea kushiriki kikamilifu katika upandaji na utunzaji wa miti.
Posted by MROKI On Friday, March 20, 2026 No comments
Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Laurent Luswetula (Mb) (wa pili kulia), akiwaongoza Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Devotha Minja, kukagua mradi wa ujenzi wa Jengo la Ofisi za Wizara ya Fedha Mtumba, jijini Dodoma lililokamilika kwa asilimia 98.
Msimamizi wa Mradi wa Jengo la Ofisi za Wizara ya Fedha Mtumba, jijini Dodoma, Mhandisi Japhet Mkwamira, akitoa maelezo ya jengo la Ofisi za Wizara ya Fedha kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), ilipofika kukagua mradi huo uliokamilika kwa asilimia 98.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Mhe. Devotha Minja, akiongoza Mkutano wa Majumuisho baada ya kukagua mradi wa ujenzi wa Jengo la Ofisi za Wizara ya Fedha Mtumba, jijini Dodoma lililokamilika kwa asilimia 98, kulia ni Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Laurent Luswetula (Mb) na kushoto ni Katibu wa Kamati hiyo, Bw. Eric Maseke.
Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Laurent Luswetula (Mb) akiteta jambo na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Mhe. Devotha Minja, baada ya kukagua mradi wa ujenzi wa Jengo la Ofisi za Wizara ya Fedha Mtumba, jijini Dodoma.
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) na Mbunge wa Moshi Vijijini, Mhe. Moris Makoi, akiuliza jambo, wakati Kamati hiyo ilipokagua mradi wa ujenzi wa Jengo la Ofisi za Wizara ya Fedha Mtumba, jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Wizara ya Fedha, Bw. Lusius Mwenda akitoa maelezo kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Mhe. Devotha Minja (kushoto), wakati Kamati hiyo ilipokagua mradi wa ujenzi wa Jengo la Ofisi za Wizara ya Fedha Mtumba, jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Laurent Luswetula (Mb) (kulia) akisikiliza maelezo ya Mhasibu Mkuu Fungu 50 CPA. Nuru Mbekenga Abdallahmed (wa pili kulia) baada ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kukagua mradi wa ujenzi wa Jengo la Ofisi za Wizara ya Fedha Mtumba, jijini Dodoma.
Baadhi ya Wakurugenzi wa Idara na Vitengo vya Wizara ya Fedha na wajumbe wengine wakifuatilia maelezo ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Mhe. Devotha Minja, wakati Kamati hiyo ilipokagua mradi wa ujenzi wa Jengo la Ofisi za Wizara ya Fedha Mtumba, jijini Dodoma.
Muonekano wa Jengo jipya la Ofisi za Wizara ya Fedha Mtumba, jijini Dodoma lililokamilika kwa asilimia 98 ambalo limeanza kutumika kwa baadhi ya Idara na Vitengo vya Wizara hiyo.
***************
 Na. Josephine Majura na Peter Haule, WF, Dodoma
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Mhe. Devotha Minja, ameipongeza Wizara ya Fedha kwa kutekeleza Mradi wa Jengo jipya la Ofisi ya Wizara lililopo Mji wa Serikali Mtumba, kwa ufanisi, kwa kuwa mradi huo hauna maswali mengi ikilinganishwa na miradi mingine waliyoitembelea.
 
“Kazi ni nzuri, mmefanya kazi kubwa na taarifa zinazohitajika ziwasilishwe ili tuweza kuishauri vema Serikali”, alisema Mhe. Minja.
 
Aidha Mhe. Minja kwa niaba ya Kamati ameahidi kutoa ushirikiano katika maeneo mbalimbali yanayoihusu Wizara ya Fedha kwa Maendeleo ya Wananchi.
 
Akizungumza na Ujumbe wa Kamati hiyo ya Kudumu ya Bunge ya PAC, Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Laurent Luswetula (Mb) alimshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa jengo la hilo lenye mvuto wa kipekee katika eneo hilo likiwa na urefu wa ghorofa tisa.
 
Mhe. Luswetula alisema kuwa jengo hilo lililofikia hatua ya asilimia 98 katika utekelezaji wake, anaimani watumishi wa Wizara ya Fedha wataongeza morali ya kazi kutokana na mazingira bora ya kazi katika jengo hilo lenye hadhi kubwa.
 
“Kwa mazingira haya majukumu ya Wizara ya Fedha yataenda vizuri ikiwa ni pamoja na utatuzi wa changamoto za wananchi wote kwa ujumla”, alisema Mhe. Luswetula.
 
Mhe. Luswetula alimhakikishia Mwenyekiti wa Kamati ya PAC kufanyia kazi ushauri na mapendekezo yote yaliyotolewa ikiwemo kuwasilisha taarifa za jengo hilo kwa ujumla wake.
 
Kamati ya Kudumu ya PAC imetembelea mradi wa Jengo hilo na kukagua Ofisi mbalimbali zikiwemo za Viongozi na Watumishi wa Wizara, Mifumo ya Fedha, usalama wa jengo, masuala ya Afya, kumbi za Mikutano na maeneo mengine.
 
Mwisho.
 
CAPTIONS
 
1.

 
4.

 
7.

 
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Fedha)
Posted by MROKI On Friday, March 20, 2026 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo