Nafasi Ya Matangazo

February 05, 2026

Dar es Salaam — Kampuni ya Mati Super Brands Ltd kupitia kinywaji chake cha kifahari cha Tanzanite Royal Gin imezindua rasmi kampeni maalum ya msimu wa Siku ya Wapendanao (Valentine’s Day) ijulikanayo kama “Tanzanite Royal Gin – Royal Love Challenge 2026”, yenye lengo la kuimarisha uhusiano na wateja pamoja na kusherehekea mapenzi kwa njia ya kipekee.

Akizungumza kuhusu kampeni hiyo, Izack Piganio, Meneja wa Chapa Mati Super Brands, alisema, "Royal Love Challenge ni njia yetu ya kuwapa wateja uzoefu wa kipekee wa kusherehekea Valentine’s Day, huku tukijenga uhusiano wa karibu na wapenzi na wanandoa kupitia chapa ya Tanzanite Royal Gin. Tunataka mapenzi yashehereke kwa hadhi ya kifalme, na washiriki washindwe kwa ubunifu na upendo wao."
Shindano hili la mtandaoni litafanyika kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram, likiwalenga wapenzi, couples na wanandoa. Washiriki wanatakiwa kupiga picha wakionyesha upendo wao pamoja na chupa halisi ya Tanzanite Royal Gin, kisha kuipakia kwenye akaunti zao za Instagram. Ili kushiriki kikamilifu, washiriki wanapaswa kutag ukurasa rasmi wa @TanzaniteRoyalGin, kutumia hashtag #RoyalLoveChallenge, na kufanya collaboration na ukurasa wa kampeni.

Kwa upande wake, Meneja wa hoteli ya Asmorain, Amina Mrutu, alisema: "Tunakufariji kuwa sehemu ya kampeni hii ya Royal Love Challenge. Tunatarajia mshindi atapata zawadi za kipekee zenye mchanganyiko wa mapenzi na burudani, ikiwemo usiku mmoja katika hoteli yetu, chakula cha jioni cha kimapenzi na safari ya kupumzika Hifadhi ya Taifa ya Tarangire."
Mshindi wa Royal Love Challenge 2026 atatangazwa Februari 12, 2026, huku zawadi zote zikitolewa rasmi Februari 14, siku ya Valentine’s Day. Kampeni hii inatarajiwa kuleta burudani, ushindani chanya, na kuendeleza utamaduni wa kusherehekea mapenzi kwa hadhi ya kifalme.
Posted by MROKI On Thursday, February 05, 2026 No comments

Waziri wa Fedha, Mhe Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) akieleza kuhusu maeneo ya uwekezaji wakati wa mkutano na  Kiongozi wa Timu ya Wataalamu kutoka Taasisi ya kimataifa inayojihusisha na tathmini ya nchi kukopesheka katika masoko ya mitaji ya kimataifa ya Moody’s Investor Service, ikiongozwa na  Bw. John Walsh (hayupo pichani), kilichofanyika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha, Mhe Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) akiongoza Kikao na  Timu ya Wataalamu kutoka Taasisi ya kimataifa inayojihusisha na tathmini ya nchi kukopesheka katika masoko ya mitaji ya kimataifa  ikiongozwa na  Bw. John Walsh (wa kwanza kulia), kilichofanyika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.
Kiongozi wa Timu ya Wataalamu kutoka Taasisi ya kimataifa inayojihusisha na tathmini ya nchi kukopesheka katika masoko ya mitaji ya kimataifa (Sovereign Credit Rating) Moody’s Investor Service, Bw. John Walsh,  akielezea  kuhusu ujio wa Timu yake nchini ili kufanya tathimini mpya ya uwezo wa Tanzania kukopesheka katika Soko la Kimataifa la mitaji, wakati wa kikao na Waziri wa Fedha, Mhe Balozi Khamis Mussa Omar (Mb),  kilichofanyika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.
Kiongozi wa Timu ya Wataalamu kutoka Taasisi ya kimataifa inayojihusisha na tathmini ya nchi kukopesheka katika masoko ya mitaji ya kimataifa (Sovereign Credit Rating) Moody’s Investor Service, Bw. John Walsh,  akielezea  kuhusu ujio wa Timu yake nchini ili kufanya tathimini mpya ya uwezo wa Tanzania kukopesheka katika Soko la Kimataifa la mitaji, wakati wa kikao na Waziri wa Fedha, Mhe Balozi Khamis Mussa Omar (Mb),  kilichofanyika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.
Timu ya Wataalamu wa Wizara ya Fedha wakifuatilia maelezo ya Waziri wa Fedha, Mhe Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), wakati wa Kikao na   Timu ya Wataalamu kutoka Taasisi ya kimataifa inayojihusisha na tathmini ya nchi kukopesheka katika masoko ya mitaji ya kimataifa (Sovereign Credit Rating) Moody’s Investor Service (Moody’s) ikiongozwa na Bw. John Walsh (hawapo pichani), kilichofanyika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.
Timu ya Wataalamu kutoka Taasisi ya kimataifa inayojihusisha na tathmini ya nchi kukopesheka katika masoko ya mitaji ya kimataifa (Sovereign Credit Rating) Moody’s Investor Service (Moody’s) ikiongozwa na Bw. John Walsh (kulia), wakisikiliza maelezo ya Waziri wa Fedha, Mhe Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.
Kamishna wa Idara ya Usimamizi wa Bajeti, Bw. Meshack Anyingisye (kushoto) na Kamishna Msaidizi wa Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Omary Khama, wakifuatilia kikao kati ya Waziri wa Fedha, Mhe Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) na Kiongozi wa Timu ya Wataalamu kutoka Taasisi ya kimataifa inayojihusisha na tathmini ya nchi kukopesheka katika masoko ya mitaji ya kimataifa (Sovereign Credit Rating) Moody’s Investor Service (Moody’s), Bw. John Walsh (hawapo pichani), Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.

***************

Na. Peter Haule. na Jordan Mbwambo, WF, Dodoma

Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amesema kuwa mageuzi ya uchumi yataendelea kuwa ajenda ya muda mrefu yakilenga si tu kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi bali kuhakikisha ukuaji huo unachangia katika upatikanaji wa ajira na ustawi wa wananachi kwa ujumla.

Amebainisha hayo wakati wa kikao na Timu ya Wataalamu kutoka Taasisi ya kimataifa inayojihusisha na tathmini ya nchi kukopesheka katika masoko ya mitaji ya kimataifa ya Moody’s Investor Service ikiongozwa na  Bw. John Walsh, kilichofanyika Ofisi za Treasury Square, jijini Dodoma.

 

Mhe. Balozi Omar alisema kuwa uchumi wa nchi umeendelea kuimarika licha ya matukio kadhaa yaliyokwaza ustawi wa uchumi wa dunia ukiwemo uviko 19 ambapo katika kipindi cha mwaka jana uchumi ulikua kwa asilimia 5.4 na unatarajiwa kukua zaidi mwaka huu wa fedha 2025/26 hadi kufikia asilimia 6.

 

Aidha, alibainisha kuwa mahitaji ya uwekezaji yanaendelea kuwa makubwa hususani kwenye miundombinu ya kimkakati kama Bandari, Viwanja vya Ndege, Reli na mtandao wa Barabara ili kuchochea maendeleo.

 

Alieleza kuwa nchi inaendelea kuwekeza katika ujenzi wa miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo Reli iendayo Kasi -SGR, Bwawa la uzalishaji wa umeme la Julius Nyerere na uimarishaji wa sekta nyingine za kijamii na kiuchumi hatua itakayochochea zaidi ukuaji na uimara wa uchumi wa nchi na maendeleo ya jamii.

 

Akizungumzia Mfumuko wa bei amesema kuwa, hali imeendelea kuwa tulivu ambapo kiwango cha mfumuko wa bei kimeendelea kubaki chini ya asilimia tano kwa miaka kadhaa, kikiwa kati ya asilimia 2.9 na 3.4.

 

Kwa upande wake Kiongozi wa Timu ya Wataalamu kutoka Taasisi ya kimataifa inayojihusisha na tathmini ya nchi kukopesheka katika masoko ya mitaji ya kimataifa Moody’s,  Bw. John Walsh, alisema kuwa uamuzi wa kupandisha hadhi ya uwezo wa nchi kukopesheka na kuipa alama B1 yenye mtazamo thabiti ulitokana na uthabiti wa kiuchumi na kifedha ambao nchi imeuonesha licha ya changamoto za uchumi za dunia katika miaka ya karibuni.


Alisema kuwa Tanzania iliendelea kurekodi ukuaji thabiti wa uchumi licha ya athari za janga la UVIKO-19, mfumuko wa bei wa kimataifa na kupanda kwa viwango vya riba duniani.


“Uamuzi wa kupandisha hadhi kwa kiwango cha B1 ulitokana na uthabiti wa sera za uchumi jumla na mageuzi ya Serikali yanayotekelezwa chini ya Mpango wa Shirika la Fedha la Kimatafa (IMF), unaokaribia kukamilika”, alisema Bw. Walsh.


Alisema kuwa Serikali imepiga hatua muhimu katika kushughulikia changamoto za muda mrefu, ikiwemo ukusanyaji mdogo wa mapato ya ndani na mapungufu ya utekelezaji wa sera, hivyo Tathmini ya sasa inalenga kufuatilia mafanikio, changamoto zilizopo, na mwelekeo wa mageuzi katika kipindi cha miaka miwili iliyopita.


Aidha alieleza kuwa tathmini hiyo inalenga kupata taswira ya kina ya hali ya sasa ya uchumi wa Tanzania, mafanikio yaliyopatikana, pamoja na hatua zinazochukuliwa kuhakikisha ukuaji endelevu na uthabiti wa kifedha kwa muda mrefu.

Matokeo ya mapitio ya hivi karibuni ya Kampuni za Moody’s na Fitch ziliipa Tanzania daraja la B1 (stable outlook) na B+ (stable outlook), mtawalia ambayo yanaonesha kwamba Tanzania ni nchi salama kwa wawekezaji.

Posted by MROKI On Thursday, February 05, 2026 No comments
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akizungumza jambo wakati wa Kikao chake na Uongozi wa Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania, ulioongozwa na Mwenyekiti wa Bodi wa Kampuni hiyo Bw. David Tarimo (hayupo pichani), ambapo walijadiliana masuala mbalimbali ya kukuza sekta ya mawasiliano na masuala ya kidigitali katika maendeleo ya uchumi wa jamii, ambacho kilifanyika katika Ofisi ya Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania, Bw. Philip Besiimire, akizungumza jambo wakati wa kikao cha Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani) na Kampuni hiyo kilichofanyika katika Ofisi ya Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma, ambapo walijadiliana masuala mbalimbali ya kukuza sekta ya mawasiliano na masuala ya kidigitali katika maendeleo ya Uchumi wa jamii, ambacho kilifanyika katika Ofisi ya Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akiongoza kikao chake na Uongozi wa Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania, ulioongozwa na Mwenyekiti wa Bodi wa Kampuni hiyo Bw. David Tarimo (hayupo pichani), ambapo walijadiliana masuala mbalimbali ya kukuza sekta ya mawasiliano na masuala ya kidigitali katika maendeleo ya Uchumi wa jamii, ambacho kilichofanyika katika Ofisi ya Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania, Bw. David Tarimo (Kulia) akizungumza jambo wakati wa kikao cha Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani) na Kampuni hiyo kilichofanyika katika Ofisi ya Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma, ambapo walijadiliana masuala mbalimbali ya kukuza sekta ya mawasiliano na masuala ya kidigitali katika maendeleo ya uchumi wa jamii, ambacho kilifanyika katika Ofisi ya Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma. Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania, Bw. Philip Besiimire.
**************
Na Benny Mwaipaja, Dodoma
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amesema kuwa Serikali inatambua mchango mkubwa wa sekta ya mawasiliano katika kukuza uchumi jumuishi wa nchi kupitia mageuzi makubwa ya uchumi wa kidigitali, ulipaji kodi na uboreshaji wa huduma za jamii.

Mhe. Balozi Omar amesema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na Uongozi wa Kampuni ya Simu ya Vodacom ikiongozwa na Mwenyekiti wake wa Bodi, Bw. David Tarimo, katika Ofisi za Hazina-Treasury Square, Jijini Dodoma.

Aliishauri sekta ya mawasiliano nchini itumie fursa ya utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2050 iliyozinduliwa hivi karibuni, kuchangia zaidi maendeleo ya nchi Kupitia matumizi ya teknolojia ambayo itachangia kuongeza ukwasi kwa makundi mbalimbali wakiwemo vijana.

Mhe. Balozi Omar aliahidi kuwa Serikali kwa uopande wake itaendelea kuboresha na kuweka mazingira bora ya uwekezaji ili kuchochea na kukuza mchango wa sekta ya mawasiliano nchini katika kuboresha maisha ya wananchi na kuwawezesha wawekezaji kupata faida.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa VODACOM, Bw. David Tarimo, aliishukuru Serikali kwa kuweka mazingira mazuri ya ufanyaji biashara kwa wawekezaji hali iliyoifanya sekta ya mawasiliano kuchangia kodi ya zaidi ya shilingi trilioni 1.1 katika mwaka wa fedha 2024/2025, huku Vodacom ikichangia zaidi ya shilingi bilioni 621 hadi ilipofikia mwezi Machi, 2025.

Aidha, Bw. Tarimo alieleza kuwa tangu Kampuni yake izinduliwe imewekeza zaidi ya shilingi trilioni 4.5 kwa ajili ya Kujenga miundombinu ya mawasiliano na na mwaka jana 2025 imesaidia jamii zaidi ya shilingi bilioni 3.7 kwa kufadhili miradi mbalimbali ikiwemo sekta za afya, elimu, mazingira na kuwawezesha vijana kiuchumi.

Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), Kaimu Kamishna wa Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Bi. Dionisia Mjema, Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania, Bw. Philip Besiimire, Mkurugenzi wa Masuala ya Nje wa Vodacom Tanzania, Bi. Zuweina Farah, na maafisa wengine waandamizi wa Wizara ya Fedha na Vodacom.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb)(kulia), akiagana na Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania, Bw. David Tarimo, baada ya Kikao chake na uongozi wa Kampuni hiyo, kilichojadili masuala mbalimbali ya kukuza sekta ya mawasiliano na masuala ya kidigitali katika maendeleo ya uchumi wa jamii, ambacho kilifanyika katika Ofisi ya Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (Katikati), Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb) (wa tatu kushoto), Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania, Bw. David Tarimo (wa tatu kulia), Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania, Bw. Philip Besiimire (wa pili kushoto), Mkurugenzi wa Masuala ya Nje wa Vodacom Tanzania, Bi. Zuweina Farah (kushoto) na maafisa wengine waandamizi wa kampuni hiyo, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kikao chao kilichojadili masuala mbalimbali ya kukuza sekta ya mawasiliano na masuala ya kidigitali katika maendeleo ya uchumi wa jamii, ambacho kilifanyika katika Ofisi ya Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.

Posted by MROKI On Thursday, February 05, 2026 No comments


Na Mwandishi wetu, Geita
Masoko ya Madini Katoro na Geita pamoja na vituo vya ununuzi wa madini vinaendelea kuwa chachu ya ukuaji wa uchumi wa wananchi wa Mkoa wa Geita, baada ya kuongeza fursa za ajira, biashara na mzunguko wa fedha katika jamii zinazozunguka maeneo ya shughuli za madini.

Akizungumza kuhusu mchango wa masoko hayo, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Geita, Mjiolojia Samwel Shoo, amesema uwepo wa masoko ya madini na vituo vya ununuzi  wa madini umeimarisha biashara halali ya madini kwa kuweka mfumo wa bei elekezi unaolenga kulinda maslahi ya wachimbaji wadogo na kuongeza uwazi katika biashara ya madini.

Amesema kupitia masoko hayo na vituo vya ununuzi wa madini, wachimbaji wadogo wameweza kuuza madini yao kwa bei nzuri, hali iliyoongeza kipato chao na kuwapa uwezo wa kuboresha maisha yao, ikiwemo kugharamia huduma za kijamii kama elimu, afya na makazi bora.

Mjiolojia Shoo ameongeza kuwa ongezeko la shughuli za masoko ya madini limevutia wafanyabiashara, wasafirishaji na watoa huduma mbalimbali, hatua iliyochochea ukuaji wa biashara ndogondogo, kuongeza ajira kwa vijana na wanawake, pamoja na kuimarisha uchumi wa maeneo yanayozunguka masoko hayo.

Ameeleza kuwa kwa ujumla, Masoko ya Madini Katoro na Geita pamoja na vituo vya ununuzi wa madini yamechangia kuongeza mapato ya Serikali, kuimarisha usimamizi wa sekta ya madini na kuhimiza maendeleo endelevu ya kiuchumi na kijamii katika Mkoa wa Geita.




Posted by MROKI On Thursday, February 05, 2026 No comments

February 04, 2026

Baada ya ufanisi mkubwa wa biashara kwa mwaka 2025 uliochangia kupata faida ya zaidi ya shilingi trilioni 1.04, Benki ya CRDB leo imezindua kampeni yake ya mwaka 2026 inayoitwa ‘Benki Kimpango Wako’ inayolenga kuboresha huduma kwa wateja kwa kupunguza muda wa kukamilisha muamala na kumruhusu mteja kujihudumia vile atakavyo, kwa muda wake akiwa mahali popote duniani.

Kampeni hiyo imezinduliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela ambaye amewashukuru wateja, wawekezaji, wabia wa kimkakati pamoja na wadau wote kwa ujumla kwa imani waliyonayo kwa benki hiyo kubwa zaidi nchini.

“Mwaka jana tumepata faida kubwa kutokana na ushirikiano mkubwa tulioupata kutoka kwa wateja binafsi, wajasiriamali, taasisi, mashirika na serikali pamoja na wabia wetu. Ninyi ndiyo sababu ya uwepo wa Benki ya CRDB. Kila akaunti mliyofungua, mkopo mliouchukua, kila muamala mlioufanya, na kila mradi mlioutekeleza kupitia Benki ya CRDB vilitupa nguvu na ari ya kujituma zaidi. Ninaamini na kuomba ushirikiano huu uendelea mwaka huu pia,” amesihi Nsekela.

Mwaka 2025, Benki ya CRDB imepata faida ya shilingi trilioni 1.04 kabla ya Kodi sawa na ukuaji wa asilimia 33, huku faida baada ya kodi ikifika shilingi bilioni 725 likiwa ni ongezeko la asilimia 31 ikilinganishwa na mwaka 2024. Mizania yake nayo imeongezeka na kufika shilingi trilioni 22.2 sawa na ukuaji wa asilimia 33 na ndani ya kipindi hicho imetoa mikopo kiasi cha shilingi trilioni 13.7 sawa na ukuaji wa asilimia 32.6.
Ukuaji huo, Nsekela amesema unamaanisha uwezo mkubwa zaidi wa kufadhili miradi ya maendeleo, kusaidia kukuza mitaji ya biashara ndogo, za kati na kubwa, kuongeza uzalishaji, kutoa ajira mpya, na kuwawezesha vijana, wanawake na wajasiriamali kutimiza malengo yao ya kiuchumi.

Mafanikio haya yana akisi ushirikiano wa wadau wetu wote. Tutaendelea kutekeleza azma yetu ya kuboresha maisha ya watu wetu na uchumi wa Taifa letu pamoja na masoko mengine ambako benki yetu inatoa huduma. Sisi ni Benki Inayomsikiliza Mteja na kwa kufanya hivyo tunapata syluhisho la kila changamoto ya mteja,” amesema Nsekela.
Kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia, kuongezeka kwa ushindani wa kibiashara na upangaji wa mikakati binafsi ya kiuchumi na maendeleo, Nsekela amesema wateja wanahitaji huduma za fedha ambazo ni rahisi, za haraka, na zinazoendana na mikakati waliyonayo ndio maana Benki ya CRDB imekuja na kampeni ya Benki Kimpango Wake ikikusudia na kuahidi kutoa kipaumbele kwa wateja na wadau wengine ambao ni sehemu ya mafanikio yake ya kibiashara.

Jitihada hizi za kuboresha na kuimarisha huduma kwa wateja na wadau wengine wa Benki ya CRDB, Nsekela amesema zilizanza mwaka jana pale walipofanya maboresho ya mfumo mkuu wa uendeshaji (core banking system) yakilenga kuiweka benki katika viwango vya kimataifa vya utoaji huduma na mapema mwaka huu wakazindua ofisi ya uwakilishi Dubai.
“Maboresho yetu ya mfumo mkuu wa uendeshaji wa yalilenga kubadilisha namna Benki inavyofanya kazi na jinsi mteja anavyopata huduma. Leo tunazindua kampeni tunayoiita Benki Kimpango Wako. Tunawahakikishia Watanzania na wateja wetu wengine popote duniani kuwa Benki yetu ya CRDB ni mbia wa uhakika na wa kutumainiwa katika upatikanaji wa huduma za fedha. Mwaka 2026 tunawaahidi huduma bora na za uhakika zaidi,” amesema Nsekela.

Uzinduzi wa kampeni ya Benki Kimpango Wako umefanyika katika kipindi muhimu kwa historia ya taifa wakati serikali ikianza utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inayoelekeza kuwa uchumi wa Tanzania unapaswa kuwa jumuishi, wenye huduma za fedha zilizowafikia wananchi wengi zaidi, na taasisi za fedha kuwa nguzo ya ukuaji wa uchumi, ubunifu na ustawi wa jamii.
Ili kupata huduma za uhakika, wateja wanaweza kuhudumiwa katika tawi lolote la Benki ya CRDB iwe hapa Tanzania, nchini Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) au katika ofisi ya uwakilishi iliyopo Dubai au kupitia majukwaa tofauti ikiwamo Simbanking, huduma kwa njia ya intaneti au kwa CRDB Wakala. Huduma hizi zinapatikana pia hata kwa wale wanaofuata misingi ya dini kwani huhudumiwa kupitia dirisha la CRDB Al Barakah.

“Benki ya CRDB ni daraja la fursa kwa wananchi wote. Kampeni ya Benki Kimpango Wako inamkumbusha kila mdau kwamba Benki ya CRDB ni mshirika wa kutumainiwa katika safari ya maendeleo kwa mpango wa mteja katika muda wake,” amesisitiza Nsekela.
Posted by MROKI On Wednesday, February 04, 2026 No comments
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Festo Dugange akijibu maswali bungeni wakati wa Kikao cha Saba cha Mkutano wa Pili wa Bunge jijini Dodoma leo Februari 04, 2026.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni (kulia) akizungumza na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Festo Dugange wakati wa kipindi cha maswali na majibu katika Kikao cha Saba cha Mkutano wa Pili wa Bunge jijini Dodoma leo Februari 04, 2026. Mbele ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Hamis Mwinjuma.
*******************
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesema katika kipindi cha mwaka 2020 hadi 2025 jumla ya miradi kumi ya kuhifadhji mazingira na kuhimili mabadiliko ya tabianchi yenye thamani ya takribani shilingi bilioni 97.6 imetekelezwa na kukamilika Zanzibar.
 
Hayo yamebainishwa bungeni jijini Dodoma leo Februari 04, 2026 na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Festo Dugange wakati akijibu swali la Mbunge wa Mtambwe Mhe. Rashid Habib Ali aliyetaka kufahamu Zanzibar inanufaikaje na fedha za mazingira zinazotolewa na wafadhili.
 
Mhe. Dkt. Dugange ameliarifu Bunge kuwa utekelezaji wa miradi ya mazingira umeleta manufaa kwa jamii kwa kuongeza kipato kupitia shughuli mbadala hivyo kuongeza uwezo wa jamii katika uhifadhi wa mazingira na kuhimili mabadiliko ya tabianchi
 
Akiendelea kujibu swali la mbunge huyo alifafanua kuwa utekelezaji wa miradi hiyo umechangia katika ukuaji wa uchumi kwa maendeleo endelevu na ustawi wa jamii kwa ujumla.
 
Mhe. Dkt. Dugange alisema Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa ikipokea fedha kutoka kwenye Mifuko ya Kimataifa ya Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi na wafadhili mbalimbali wakiwemo Mfuko wa Mazingira wa Dunia (GEF), Mfuko wa Mabadiliko ya tabianchi (GCF), Benki ya Dunia (WB) na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB).
 
Aidha, alibainisha kuwa fedha zinazopatikana zimekuwa zikitumika kutekeleza miradi mbalimbali ya hifadhi ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi kwa Tanzania Bara na Zanzibar.
 
Hivyo, alisema Serikali imeendelea kuandaa miradi kwa ajili ya kutafuta fedha kupitia vyanzo mbalimbali ambapo hadi sasa jumla ya miradi mitatu yenye thamani ya takribani shilingi bilioni 62.6 ipo kwenye hatua za awali za maandalizi.
 
Katika hatua nyingine, Naibu Waziri alisema fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya mazingira zinagawanywa kwa kuzingatia uwiano wa uhjtaji wa pande zote mbili za Muungano.
 
Alisema mkakati wa Serikali ni kuboresha maeneo yaliyoathiriwa na mabadiliko ya tabianchi hususan ya kwenye fukwe za bahari ambako maji huingia kwenye makazi ya wananchi na kuleta madhara.
 
Mhe. Dkt. Dugange alisema hayo wakati akijibu swali la nyongeza la Mhe. Ali aliyeuliza ni upi mgawanyo wa utekelezaji wa miradi Tanzania Bara na Zanzibar.
Posted by MROKI On Wednesday, February 04, 2026 No comments

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akizungumza na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji, Bungeni jijini Dodoma, Februari 4, 2026. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akizungumza na Mbunge wa Bariadi Vijijini, Masanja Kadogosa, kwenye viwanja vya Bunge jijini Dodoma, Februari 4, 2026. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
Posted by MROKI On Wednesday, February 04, 2026 No comments
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Rais wa Angola ambaye pia Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) Mhe. João Lourenço,
Rais wa Jamhuri ya Ghana Mhe. John Mahama wa pili kutoka (kushoto), Waziri Mkuu wa Msumbiji Mhe. Maria Benvinda Levy wa kwanza (kushoto), Mwanzilishi Mwenza na Mwenyekiti Mtendaji wa GAIS na Rais Mstaafu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina pamoja na Mwanzilishi na Mwenyekiti Mtendaji wa APCO Worldwide, Bi. Margery Kraus wa kwanza (kulia) mara baada ya uzinduzi rasmi wa Jukwaa la Uwekezaji barani Afrika (GAIS), uliofanyika Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu tarehe 03 Februari, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akihutubia katika uzinduzi wa Jukwaa la Uwekezaji barani Afrika (GAIS), Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu tarehe 03 Februari, 2026.
Posted by MROKI On Wednesday, February 04, 2026 No comments
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Makamu wa Rais wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na Mtawala wa Dubai, Sheikh Mohammed bin Rashid Al Maktoum, kando ya Mkutano wa Dunia (WGS2026) hapa, Dubai, tarehe 04 Februari, 2026.
  


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi ya kitabu kutoka kwa Makamu wa Rais wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na Mtawala wa Dubai, Sheikh Mohammed bin Rashid Al Maktoum, mara baada ya mazungumzo kati yao, kando ya Mkutano wa Dunia (WGS2026) hapa, Dubai, tarehe 04 Februari, 2026.  

Posted by MROKI On Wednesday, February 04, 2026 No comments

Tume ya Ushindani (FCC) imeweka mikakati mbalimbali ya kuimarisha utoaji wa huduma bora kwa wananchi kwa wakati, kupitia matumizi ya mifumo ya kisasa katika utekelezaji wa majukumu yake.

Akizungumza wakati wa kikao kazi na watumishi wa Tume hiyo kwa lengo la kupanga mikakati ya utekelezaji wa majukumu, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, amesema hatua hizo zinalenga kuongeza ufanisi wa huduma na kuwahudumia wananchi kwa viwango vya juu vya ubora.

Amesema FCC inaendelea kutekeleza dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuhakikisha mazingira ya biashara nchini yanaboreshwa na kuwashirikisha wafanyabiashara kupitia mifumo rafiki na yenye ufanisi.

Ngasongwa amesema kuwa katika kipindi cha siku 100 za uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, FCC imekuwa ikichukua hatua mbalimbali za kusogeza huduma karibu na wananchi, ikiwemo kuanzisha Ofisi ya FCC Mkoa wa Tanga na Mipakani ili kuongeza wigo wa utoaji huduma na kuwafikia wananchi wengi zaidi, hususan wale waliopo maeneo ya pembezoni mwa nchi. 

Ameongeza kuwa FCC imeendelea kudumisha cheti hicho cha ubora kutokana na jitihada zake katika utoaji wa huduma kwa wananchi na wadau wa biashara kwa weledi na uwazi.

“Tuko hapa kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi kwa viwango vya ubora vinavyotambulika kimataifa, niwapongeze kwa kuendelea kushikilia Cheti cha Ithibati ya Ubora ISO 9001:2015,” amesema Ngasongwa.

Vilevile watumishi walipata nafasi ya kupitishwa na kujadili tathmini ya rasimu ya Mpango Mkakati Mpya wa Tume wa miaka mitano (Strategic Plan) 2026/27-2030/31 unaoakisi utekelezaji wa Dira ya Taifa ya 2050. 

FCC ina utamaduni shirikishi katika kujadili mambo yahusuyo taasisi, ambapo watumishi wote kupitia ngazi mbalimbali hushirikishwa kwa ustawi wa taasisi. 

Kikao hicho kimefanyika Februari 02,2026 katika ukumbi wa Hoteli ya Tiffany Diamond, Jijini Dar es Salaam.
Bw. Shalua Magandi, Mkurugenzi wa Huduma Saidizi akichangia mada wakati wa kikao kazi na watumishi wa Tume, kilichofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Tiffany Diamond, Jijini Dar es Salaam Februari 02,2026.Mwenyekiti wa Tughe Tawi la FCC, Bw. Emmanuel Ndyetabula akifuatilia kikao kazi cha Kaimu Mkurugenzi Mkuu na watumishi wa Tume, kilichofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Tiffany Diamond, Jijini Dar es Salaam Februari 02,2026.


Sehemu ya watumishi.




Picha za pamoja.

Posted by MROKI On Wednesday, February 04, 2026 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo