March 25, 2026
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Ado Shaibu, amebainisha maeneo kadhaa yanayohitaji marekebisho ili kuendana na matakwa ya kisheria na ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Kuhusu mradi wa ujenzi wa majengo ya Idara ya Afya, Kamati imemuelekeza Afisa Masuuli kuhakikisha kiasi cha shilingi 527,049,323 kilichotolewa kama malipo ya awali kwa mkandarasi kinarejeshwa. Aidha, Kamati imetaka kuwepo kwa uthibitisho wa mapokezi ya fedha hizo kwa CAG kila robo mwaka kwa ajili ya uhakiki.
Vilevile, Ofisi ya Rais - TAMISEMI imeombwa kupitia upya taratibu zilizotumika katika malipo ya shilingi 1,125,678,889 na kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria kwa watumishi waliohusika na ukiukwaji wa kanuni za manunuzi.
Katika mradi wa Soko Kuu la Mwanza, Kamati imesisitiza umuhimu wa kukamilisha miundombinu ya msingi kama mifumo ya maji nje ya soko na ufungaji wa kamera za usalama (CCTV). Maelekezo hayo yanalenga kuimarisha ufanisi na usalama wa soko hilo kwa manufaa ya wafanyabiashara.
Pia, uongozi wa Jiji umepewa hadi tarehe 30 Mei, 2026 kurekebisha mapungufu yote yaliyoonekana kwenye mradi wa jengo la makazi ya Mkurugenzi ili kuhakikisha thamani ya fedha inaonekana.
Naibu Waziri wa TAMISEMI (Elimu), Mhe. Reuben Kagilwa, amepokea maelekezo hayo na kusema kuwa Wizara itahakikisha yanafanyiwa kazi kwa wakati.
Kwa upande wake, Meya wa Jiji la Mwanza, Mhe. Sima Constantine Sima, ameishukuru Kamati kwa ushauri wake wa kitaalamu na kuahidi kuwa Jiji litashirikiana kikamilifu kufikia malengo yaliyokusudiwa.
March 24, 2026
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Asha-Rose Migiro, anaondoka nchini leo kuelekea Beijing, Jamhuri ya Watu wa China, kwa ziara ya kikazi ya siku sita kufuatia mwaliko wa Chama cha Kikomunisti cha China.
Ziara hiyo inalenga kuendeleza na kuimarisha uhusiano wa kihistoria na ushirikiano wa karibu uliopo kati ya Chama Cha Mapinduzi na Chama cha Kikomunisti cha China.
Ziara hii inafanyika katika kipindi ambacho mwaka 2026 umetangazwa rasmi kuwa mwaka wa kukuza uhusiano na maelewano ya kijamii na kitamaduni kati ya China na Afrika. Hivyo, mwaka huu unatoa fursa adhimu ya kuimarisha urafiki, kubadilishana uzoefu na kujenga uelewano wa pamoja kati ya vyama hivi viwili.
Katika ziara hiyo, Katibu Mkuu ataambatana na ujumbe wa watu watano.
Akiwa nchini humo, yeye pamoja na ujumbe wake watafanya mazungumzo na viongozi wa juu wa Chama cha Kikomunisti cha China.
Tanzania imeingia hatua muhimu ya kuimarisha biashara na Marekani baada ya Serikali na Kampuni ya Panda Hill Tanzania Limited kusaini mkataba wa makubaliano ya kuendeleza Mradi wa Niobium wa Panda Hill, hatua inayolenga kuifanya Mbeya kuwa kitovu cha uzalishaji na usindikaji wa madini mkakati.
Akizungumza katika hafla hiyo, Waziri wa Madini Mheshimiwa Anthony Mavunde amesema mradi huo ni wa uzalishaji wa madini adimu ambayo hayapatikani kila mahali duniani, na kwamba Tanzania inalenga kuchukua nafasi ya kipekee katika soko la kimataifa la niobium kupitia mradi huo. Amesema soko la dunia kwa sasa linatawaliwa na wazalishaji wachache wakubwa, na Panda Hill itaiweka Tanzania kwenye ramani ya wazalishaji wakuu duniani.
Mheshimiwa Mavunde ameeleza kuwa mzalishaji mkubwa duniani yupo Brazil na huzalisha takriban asilimia 80 ya mahitaji ya dunia, mzalishaji wa pili naye yupo Brazil na huzalisha takriban asilimia 11, huku Canada ikichangia takriban asilimia 6. Kupitia Panda Hill, amesema Tanzania inalenga kuwa mzalishaji wa nne duniani kwa kuchangia takriban asilimia 4 ya mahitaji ya dunia, na uzalishaji unaolengwa kufikia takriban tani 100,000 kwa mwaka.
Katika kusisitiza mwelekeo wa Serikali, Waziri Mavunde amesema dira ya maendeleo ya 2025-2050 na maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan yanalenga kuhakikisha madini yanaongezewa thamani hapa hapa nchini ili manufaa yawe makubwa kwa wananchi. Amesema Tanzania inaenda zaidi ya uchimbaji wa kawaida kwa kujenga uwezo wa ndani wa kuchakata na kuzalisha bidhaa za viwandani zenye thamani kubwa.
Mradi huo unahusisha niobium, madini ya kimkakati inayotumika kuongeza uimara wa chuma na kutengeneza aloi za utendaji wa juu zinazohitajika kwenye miundombinu mikubwa, miundombinu na matumizi ya teknolojia za kisasa. Pia, Waziri Mavunde ametaja matumizi katika maeneo ya kisasa kama yanayohusiana na magari ya umeme na injini za ndege, akieleza kuwa hii inaongeza uzito wa mradi katika uchumi wa kisasa wa viwanda.
Kwa upande wa mwekezaji, Pierre Joubert, ambaye ni Meneja Mkuu wa Panda Hill Tanzania Limited, amesema kampuni inaingia kwenye hatua mpya ya utekelezaji kwa kushirikiana na Serikali kama mshirika rasmi, baada ya kipindi kirefu cha majadiliano na maandalizi. Ameeleza kuwa mradi ulikuwa karibu kuanza ujenzi mwaka 2017 kabla ya mabadiliko ya sheria, na tangu wakati huo kampuni imekuwa ikifanya kazi kwa karibu na Serikali kuhitimisha makubaliano ya msingi ya kuusukuma mradi mbele.
Joubert amesema hatua zinazofuata ni kuendelea na taratibu za kupata Leseni Maalum ya Uchimbaji Madini, kusasisha taarifa za upembuzi yakinifu ili kuakisi gharama za sasa za uwekezaji na uendeshaji, kuingiza matumizi ya umeme wa gridi kwenye mpango wa uendeshaji, pamoja na kufanya tathmini ya masoko ya ferroniobium ili kuhakikisha bidhaa inaingia kwa ushindani kwenye soko la dunia, ikiwemo soko la Marekani.
Kwa mujibu wa taarifa za kampuni hiyo, mradi unahusisha ujenzi wa mgodi wa niobium pamoja na kituo cha uchenjuaji na kiwanda cha kuzalisha ferroniobium, bidhaa yenye thamani iliyoongezwa inayohitajika na viwanda vya chuma na uzalishaji wa viwandani. Kampuni imeeleza kuwa bidhaa hiyo inalengwa kuuzwa kwenye masoko ya Afrika, Asia, Ulaya na Marekani, na hivyo kuifanya Tanzania kuwa mshiriki wa moja kwa moja katika minyororo ya ugavi ya viwanda ya thamani ya juu.
Kipengele kinachoifanya Panda Hill kuwa ya kipekee, kwa mujibu wa taarifa za kampuni, ni ujenzi wa kiwanda cha ferroniobium ambacho kitakuwa cha pekee barani Afrika na kitakuwa cha nne kujengwa duniani katika kipindi cha miaka 40 iliyopita. Hili linaipa Tanzania nafasi ya kuingia kwenye kundi dogo la nchi zenye uwezo wa kuzalisha bidhaa hiyo kwa kiwango cha viwandani.
Kwa biashara za ndani na wazabuni wa Tanzania, amesema mradi umebeba fursa kubwa ya muda mrefu. Panda Hill imeeleza kuwa katika maisha ya mradi, thamani ya manunuzi ya ndani inakadiriwa kufikia Dola za Marekani bilioni 1.77, huku asilimia 70 ya manunuzi ya bidhaa na huduma ikilengwa kufanyika ndani ya nchi wakati wa uzalishaji. Hii, kwa maelezo ya wadau, inamaanisha mikataba ya muda mrefu kwa kampuni za Kitanzania katika maeneo ya ujenzi, usafirishaji, matengenezo, huduma za kiufundi, ulinzi, chakula na huduma nyingine muhimu za uendeshaji.
Kuhusu ajira, Waziri Mavunde amesema mradi unatarajiwa kuajiri zaidi ya 1,600 kusaidia ujenzi na kutoa ajira za kudumu takriban 600, huku jumla ya watu watakaonufaika moja kwa moja na wasio wa moja kwa moja ikitarajiwa kufikia takriban 7,000.
Mradi uko katika eneo la Gereza la Kilimo la Songwe, na Waziri Mavunde ameeleza kuwa takriban ekari 5,434 za eneo la mradi zipo ndani ya eneo la gereza hilo. Aliongeza kuwa mpango wa utekelezaji unahusisha ujenzi wa gereza jipya la kisasa, akieleza kuwa linalenga kuwa miongoni mwa magereza ya kisasa zaidi katika Afrika Mashariki na Kati.
Pia, Waziri Mavunde amesisitiza kuwa kurejesha kwa jamii ni sharti, akisema uwajibikaji wa mwekezaji kwa jamii na miradi ya kijamii ni sehemu ya lazima ya uendeshaji wa mradi, sambamba na mapato ya Serikali kupitia kodi, tozo na ushuru mbalimbali.
Kwa upande wa ushiriki wa Serikali, imeelezwa kuwa, Tanzania itakuwa na umiliki wa hisa asilimia 16 kupitia mfumo wa Hisa huru zisizohafifishwa (free carried interest), unaolenga kuimarisha ushiriki wa Taifa katika maamuzi ya kimkakati na faida za mradi. Katika hatua ya utiaji saini, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Samwel Maneno amesaini Framework Agreement kwa niaba ya Serikali, huku Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali pamoja na Msajili wa Hazina Nehemiah Mchechu wakisaini mkataba wa wana hisa (Shareholder Agreement) na wawekezaji, kukamilisha muundo wa ushiriki wa Serikali na mfumo wa usimamizi wa mradi.
Waziri wa Nishati na Madini wa Malawi, Mhe. Dkt. Jean Mathanga (katikati) akimsikiliza Meneja wa Mafuta wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Yona Malago (kushoto) akifafanua kuhusu namna flowmeters zinavyosaidia kujua kiasi cha mafuta ya petroli kilichoingia,wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua miundombinu ya mafuta kwenye Kituo cha Kurasini Oil Jet (KOJ-1), kilichopo katika Bandari ya Dar es Salaam leo Machi 24,2026 jijini Dar es Salaam.. Wengine pichani ni ujumbe ulioambatana na Waziri kutoka nchini Malawi pamoja na na baadhi ya watumishi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA).
Muonekano wa meli ya mafuta ya petroli ikipakua mafuta katika Kituo cha Kurasini Oil Jet (KOJ-1), kilichopo kwenye Bandari ya Dar es Salaam leo Machi 24,2026 jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nishati na Madini wa Malawi, Mhe. Dkt. Jean Mathanga (katikati) akiwa ameongozana na Mwakilishi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA), Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Petroli PBPA, Mhandisi Bruno Tarimo (kushoto) kukagua miundombinu ya mafuta kwenye Kituo cha Kurasini Oil Jet (KOJ-1), kilichopo katika Bandari ya Dar es Salaam leo Machi 24,2026 jijini Dar es Salaam. Wengine pichani ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini wa Malawi, Mhandisi Emmanuel Matapa na ujumbe ulioambatana na Waziri kutoka nchini Malawi na baadhi ya watumishi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA).
Muonekano wa meli ya mafuta ya petroli ikipakua mafuta katika Kituo cha Kurasini Oil Jet (KOJ-1), kilichopo kwenye Bandari ya Dar es Salaam leo Machi 24,2026 jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nishati na Madini wa Malawi, Mhe. Dkt. Jean Mathanga (katikati) akiwa ameongozana na Mwakilishi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA), Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Petroli PBPA, Mhandisi Bruno Tarimo (kushoto) kukagua miundombinu ya mafuta kwenye Kituo cha Kurasini Oil Jet (KOJ-1), kilichopo katika Bandari ya Dar es Salaam leo Machi 24,2026 jijini Dar es Salaam. Wengine pichani ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini wa Malawi, Mhandisi Emmanuel Matapa na ujumbe ulioambatana na Waziri kutoka nchini Malawi na baadhi ya watumishi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA).
Mwakilishi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA), Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Petroli PBPA, Mhandisi Bruno Tarimo akifafanua kuhusu Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja unavyofanya kazi wakati wa ziara ya kikazi ya aziri wa Nishati na Madini wa Malawi, Mhe. Dkt. Jean Mathanga (kushoto kwake) iliyofanyika katika Kituo cha Kurasini Oil Jet (KOJ-1), kilichopo katika Bandari ya Dar es Salaam leo Machi 24,2026 jijini Dar es Salaam. Wengine pichani ni ujumbe ulioambatana na Waziri kutoka nchini Malawi pamoja na na baadhi ya watumishi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA).
****************
Na Mwandishi Wetu, Dar es SalaamSerikali kupitia Bandari ya Dar es Salaam imeendelea kuwa nguzo muhimu ya upatikanaji wa mafuta kwa nchi jirani ya Malawi, hatua inayochochea shughuli za kiuchumi na kuboresha maisha ya wananchi wa nchi hizo mbili.
Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua miundombinu ya mafuta katika Kituo cha Kurasini Oil Jet (KOJ-1), kilichopo katika Bandari ya Dar es Salaam leo Machi 24, 2026, Waziri wa Nishati na Madini wa Malawi, Mhe. Dkt. Jean Mathanga, aliishukuru Serikali ya Tanzania kwa mchango wake mkubwa katika kuwezesha mtiririko wa mafuta kwenda nchini Malawi.
Alisema kuwa kutokana na Malawi kutokuwa na bandari, nchi hiyo inategemea kwa kiasi kikubwa miundombinu ya nchi jirani, hususan Tanzania, katika kuhakikisha upatikanaji wa mafuta unaendelea kuwa wa uhakika.
Alibainisha kuwa ziara hiyo imelenga kujionea kwa vitendo namna mafuta yanavyopokelewa na kusimamiwa bandarini ili kuboresha mipango ya ununuzi na usambazaji wa mafuta nchini Malawi.
Kwa upande wake, Mwakilishi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA), ambaye ni Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Petroli PBPA, Mhandisi Bruno Tarimo, alifafanua kuwa sehemu kubwa ya mafuta yanayoingia Malawi hupitia Tanzania kupitia Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (BPS), huku wakati mwingine nchi hiyo ikiagiza moja kwa moja kutoka kwa wazabuni wake.
Sekta ya madini nchini imeendelea kuonesha mwelekeo chanya wa ukuaji wa uchumi nchini, baada ya kuchangia asilimia 12.7 ya Pato la Taifa katika kipindi cha Julai hadi Septemba 2025.
Hayo yameelezwa leo Machi 24, 2026 na Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Eng. Yahya Samamba, wakati akifungua Baraza la Pili la Wafanyakazi wa Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2025/2026, lililofanyika katika ukumbi wa Midland Hotel, jijini Dodoma.
Katika hatua nyingine, Eng. Samamba amesema kuwa thamani ya mauzo ya mazao ya madini nje ya nchi kwa mwaka 2025 imefikia dola za Marekani milioni 4,119 sawa na zaidi ya shilingi trilioni 10.3 za kitanzania.
Amebainisha kuwa mafanikio hayo yametokana na juhudi za Serikali katika kuimarisha usimamizi wa biashara ya madini, hususan kupitia uanzishwaji na uboreshaji wa masoko ya madini pamoja na mikakati madhubuti ya kudhibiti utoroshaji wa madini.
Akizungumza katika kikao hicho, Mwakilishi wa Afisa Kazi Mkoa wa Dodoma, Eunice Mmary, amesema Ofisi ya Kamishna wa Kazi inajivunia ushirikiano na mafanikio ya Wizara ya Madini katika kuzingatia masuala ya haki na ustawi wa wafanyakazi.
Kwa upande wake, Mwakilishi wa TUGHE Taifa, Happiness Kitarima, ameipongeza Wizara ya Madini kwa kuwa miongoni mwa taasisi zinazotekeleza kwa vitendo misingi na kanuni za chama hicho, ikiwemo kulinda maslahi ya watumishi na kuimarisha mahusiano kazini.
Kwa ujumla, takwimu hizo zinaashiria kuimarika kwa mchango wa sekta ya madini katika uchumi wa taifa, sambamba na kuongezeka kwa mapato ya fedha za kigeni na kudhibiti mianya ya upotevu wa rasilimali. Sekta ya Madini inaendelea kuwa miongoni mwa mihimili muhimu katika ajenda ya maendeleo ya uchumi wa viwanda na uwekezaji nchini.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akizungumza wakati akifungua Mkutano wa Tatu wa Wanawake katika Sekta ya Fedha (Women in Finance Conference 2026), ulioandaliwa na Chama cha Wanawake katika Sekta ya Fedha Tanzania (Tanzania Women in Finance Association - TAWiFA), katika Jengo la Papu Tower, jijini Arusha, ambapo aliwapongeza wanawake katika kuchangia ukuaji wa uchumi wa nchi na katika kuchangia maendeleo nchini katika sekta mbalimbali.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (kulia), akipokea tuzo maaalum kutoka kwa Mlezi wa Chama cha Wanawake katika Sekta ya Fedha Tanzania (Tanzania Women in Finance Association - TAWiFA) ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais -Ikulu Zanzibar, Mhe. Dkt. Saada Mkuya Salum, kama Ishara ya kutambua mchango wake kwa Chama hicho, wakati alipofika kufungua Mkutano wa Tatu wa Wanawake katika Sekta ya Fedha (Women in Finance Conference 2026), katika Jengo la Papu Tower, jijini Arusha.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (katikati), akionesha tuzo maaalum aliyopewa na Chama cha Wanawake katika Sekta ya Fedha Tanzania (Tanzania Women in Finance Association - TAWiFA), kama Ishara ya kutambua mchango wake kwa chama hicho, wakati alipofika kufungua Mkutano wa Tatu wa Wanawake katika Sekta ya Fedha (Women in Finance Conference 2026), katika Jengo la Papu Tower, jijini Arusha. Wengine katika picha ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais -Ikulu Zanzibar ambaye pia ni mlezi wa chama hicho, Mhe. Dkt. Saada Mkuya Salum (kushoto) na Rais wa Chama hicho, Bi. Fikky Ntomola.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb)(Kulia), akimkabidhi Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), Bi. Sauda Msemo, tuzo ya shukran kwa kudhamini Mkutano wa Tatu wa Wanawake katika Sekta ya Fedha (Women in Finance Conference 2026), ulioandaliwa na Chama cha Wanawake katika Sekta ya Fedha Tanzania (Tanzania Women in Finance Association - TAWiFA), katika Jengo la Papu Tower, jijini Arusha.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb)(Kulia), akimkabidhi Kamishna wa Bima Tanzania, Dkt. Baghayo Saqware, tuzo ya shukran kwa kudhamini Mkutano wa Tatu wa Wanawake katika Sekta ya Fedha (Women in Finance Conference 2026), ulioandaliwa na Chama cha Wanawake katika Sekta ya Fedha Tanzania (Tanzania Women in Finance Association - TAWiFA), katika Jengo la Papu Tower, jijini Arusha.
Na. Joseph Mahumi, WF, Arusha
Serikali imeahidi kuendelea kuimarisha juhudi za uwezeshaji wa wanawake kiuchumi kupitia sekta ya fedha, ikitambua kuwa eneo hilo ni nguzo muhimu katika kukuza uchumi jumuishi na endelevu nchini.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), wakati akifungua Mkutano wa Tatu wa Wanawake katika Sekta ya Fedha (Women in Finance Conference 2026), ulioandaliwa na Chama cha Wanawake katika Sekta ya Fedha Tanzania (Tanzania Women in Finance Association- TAWiFA), katika Jengo la Papu Tower, jijini Arusha.
Akizungumza katika hafla hiyo Mhe. Balozi Omar alisema kuwa, wanawake wana nafasi kubwa katika maendeleo ya uchumi wa Taifa, na Tafiti za mapato na matumizi ya kaya (HBS) zinaonesha kuwa wanawake wanashiriki kikamilifu kwa uwekezaji, biashara na kuchangia nguvukazi katika sekta mbalimbali za Uchumi ikiwemo kuendesha zaidi ya asilimia 50 ya biashara ndogo na za kati nchini, hali inayoonesha wazi mchango wao katika uzalishaji wa ajira na ukuaji wa uchumi wa ndani.
“Wanawake ni mhimili mkuu wa uzalishaji hususan katika sekta ya kilimo na biashara. Hivyo, kuwawezesha kupitia sekta ya fedha ni hatua muhimu katika kujenga uchumi imara,” alisema Mhe. Balozi Omar.
Mhe. Balozi alisema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imechukua hatua mbalimbali kuimarisha ujumuishaji wa kifedha, kuboresha mazingira ya biashara na kuanzisha mifuko ya uwezeshaji kwa wanawake na vijana ambapo kati ya mwaka 2022 na 2025, zaidi ya wanawake milioni 1.3 wamenufaika na mikopo yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 748 kupitia mifuko hiyo, hatua iliyosaidia kuanzisha na kukuza biashara zao.
Aliongeza kuwa, sekta ya fedha ina nafasi ya kipekee katika kukuza shughuli za wanawake kiuchumi kupitia huduma za benki, bima, masoko ya mitaji na mifumo ya kidijitali, ambayo imeongeza upatikanaji wa huduma za kifedha nchini.
“Zaidi ya asilimia 60 ya watumiaji wa mikopo ya kidijitali ni wanawake, jambo hili linaloonesha namna wanavyonufaika na maendeleo ya teknolojia ya fedha katika kukuza biashara zao” aliongeza Balozi Omar.
Mhe. Balozi Omar, aliipongeza TAWiFA kwa mchango wake katika kuwainua wanawake kiuchumi, akibainisha kuwa zaidi ya wanawake 800 katika maeneo ya Dodoma na Zanzibar pamoja na 200 mkoani Arusha wamepata mafunzo ya elimu ya fedha kupitia programu mbalimbali za chama hicho.
Aidha alitoa wito TAWiFA na wadau wengine kuimarisha juhudi za kuwajengea uwezo wanawake katika masuala ya elimu ya fedha ili waweze kutumia ipasavyo huduma za kifedha, kama ambavyo kaulimbiu ya mkutano huo ikisisitiza umuhimu wa uwekezaji katika kuwawezesha wanawake kama njia ya kujenga ustawi wa jamii na kukuza uchumi wa Taifa.
Alitamatisha hotuba yake kwa kuzitaka taasisi za fedha kubuni bidhaa na huduma zinazozingatia mahitaji ya wanawake katika makundi mbalimbali, hususan maeneo ya vijijini, ili kuongeza ushiriki wao katika uchumi rasmi.
Naye, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais -Ikulu Zanzibar ambaye pia ni mlezi wa chama hicho, Mhe. Dkt. Saada Mkuya Salum, alitoa rai kwa wadau wote ikiwemo taasisi za fedha, watunga sera na washirika wa maendeleo, kuendelea kushirikiana katika kuweka mazingira wezeshi ambayo yatawezesha wanawake kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya uchumi.
Alisema kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa uoande wake, imechukua hatua kadhaa za kuwawezesha wanawake kiuchumi na katika sekta ya fedha kwa ujumla kwa kuanzisha program mbalimbali ikiemo kutoa mikopo na kuwajengea miundombinu ya masoko.
Kwa Upande wake Rais wa Chama cha Wanawake katika Sekta ya Fedha Tanzania-TAWiFA), Bi. Fikira Ntomola, alisema kuwa uwezeshaji wa wanawake katika sekta ya fedha si suala la hiari bali ni mkakati wa msingi wa kukuza uchumi wa taifa na kuwa uwepo wa viongozi wa juu serikalini unaonesha dhamira ya dhati ya Serikali kuifanya ajenda hiyo kuwa kipaumbele cha kitaifa.
Bi. Ntomola alibainisha kuwa TAWiFA imeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuwawezesha wanawake, ikiwemo kutoa mafunzo ya elimu ya fedha kwa zaidi ya wanawake wajasiriamali 800 kutoka Dodoma na Zanzibar, pamoja na zaidi ya 200 mkoani Arusha na kuanzisha programu ya uanagenzi inayolenga kuandaa viongozi wanawake wa baadaye katika sekta ya fedha, ambapo tayari kundi la kwanza la washiriki limeanza kunufaika.
Aliongeza kuwa hivi sasa pia wameanzisha Mfumo wa Uanachama wa TAWiFA utakaosaidia kujenga kanzidata ya kitaifa ya wanawake waliopo katika sekta ya fedha ili kurahisisha upatikanaji wao katika fursa za uongozi na maamuzi.
“Wadau wote tunapaswa kushirikiana ili kuondoa vikwazo vinavyokwamisha maendeleo ya wanawake, kwa kuwa tunapowawezesha wanawake katika sekta ya fedha hatupanui tu wigo wa usawa, bali tunaimarisha uchumi mzima wa Taifa na mkutano huu uwe chachu ya mabadiliko kwa kuchochea hatua za vitendo zitakazofungua milango zaidi ya fursa kwa wanawake nchini” alisema Bi. Ntomola.
Naye Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania – BOT, Bi. Sauda Msemo, alisema Ujumuishwaji wa wanawake katika ngazi za maamuzi unatoa fursa ya mabadiliko, Unarekebisha pengo la kimuundo (bridges structural inequities), na huonyesha ufanisi wa soko, na kushughulikia vikwazo vilivyopo upande wa watumiaji wa huduma kwa usahihi na umakini (addresses demand-side constraints with precision and empathy).
Bi. Msemo aliongeza kuwa Benki Kuu ilitoa maelekezo kuhakikisha kuwa walau theluthi moja ya viongozi kwenye menejimenti na bodi ni wanawake na kutoa muda wa miezi 36 kukamilisha utekelezaji wake kikamilifu ambapo hadi sasa, muelekeo unaridhisha.
Alisema kuwa hivi sasa kuna ongezeko la benki na taasisi za fedha zenye theluthi moja au zaidi ya viongozi wanawake kwenye bodi, huku ikishuhudia uandaaji wa mpango wa urithishaji wa madaraka (succession planning) kupitia programu mbalimbali za uongozi, kimalezi na ushauri (Leadership development programs, Mentorship and coaching) ili kuhakikisha uendelevu wa juhudi za ujumuishwaji wa viongozi wanawake.
“Juhudi hizi sio tu zinasaidia kuziba pengo la uongozi kijinsia, bali pia huhakikisha kuwa mitazamo ya kijinsia inazingatiwa katika muundo wa bidhaa, utawala, na ufanyaji maamuzi wa kimkakati, unaoathiri moja kwa moja matokeo ya ujumuishaji wa kifedha” alisema Bi. Msemo.
Meza Kuu ikiongozwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (Katikati aliyeketi), wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanachama wa Chama cha Wanawake katika Sekta ya Fedha Tanzania (Tanzania Women in Finance Association - TAWiFA), baada ya hafla ya kufungua Mkutano wa Tatu wa Wanawake katika Sekta ya Fedha (Women in Finance Conference 2026), ulioandaliwa na Chama hicho, katika Jengo la Papu Tower, jijini Arusha.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,WF, Arusha)
Serikali kupitia Tume ya Madini imeendelea kusisitiza umuhimu wa utekelezaji madhubuti wa sheria na kanuni katika sekta ya madini, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuhakikisha rasilimali za taifa zinawanufaisha Watanzania na kulinda maslahi mapana ya nchi.
Akizungumza jijini Dodoma katika kikao kazi kilichowakutanisha wawakilishi wa mawakili kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Ofisi ya Mwasheria Mkuu wa Serikali pamoja na viongozi kutoka Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) na taasisi ya Breakthrough Attorneys, Mkurugenzi wa Ukaguzi na Biashara ya Madini, CPA Venance Kasiki, amesema wanasheria na kampuni za sheria ni wadau muhimu katika kuimarisha ufuataji wa sheria na utatuzi wa migogoro katika sekta hiyo.
Amesema uwepo wa ushauri bora wa kisheria unachangia kuongeza ufanisi wa shughuli za uchimbaji, hususan kwa wamiliki wa leseni, wakandarasi na watoa huduma migodini, hivyo kuchochea ukuaji endelevu wa sekta ya madini.
CPA Kasiki amefafanua kuwa kikao hicho kimeandaliwa mahsusi kujenga uelewa wa pamoja kuhusu utekelezaji wa Kanuni ya 13A ya Kanuni za Ushirikishwaji wa Watanzania katika nyanja ya huduma za kisheria, akisisitiza umuhimu wa wadau hao kuzingatia weledi, uadilifu, uwazi na gharama nafuu katika utoaji wa huduma zao.
“Ni muhimu kwa kampuni za sheria na wanasheria binafsi kuhakikisha wanatoa huduma zenye viwango vya juu vya taaluma, zitakazochochea uwekezaji na kulinda maslahi ya Taifa,” amesema CPA Kasiki.
Aidha, amewataka wanasheria wa ndani kujenga uwezo wa kitaaluma ili waweze kushindana katika miradi mikubwa ya kimkakati, hususan katika kukabiliana na changamoto ya kuoanisha mikataba ya kimataifa na sheria za ndani.
Kwa upande mwingine, maboresho ya Sheria ya Madini, Sura ya 123 pamoja na kanuni zake, yameendelea kuweka mkazo katika kuongeza ushiriki wa Watanzania kupitia utoaji wa kipaumbele kwa bidhaa na huduma za ndani, ikiwemo huduma za kisheria.
Amesema utekelezaji wa Kanuni za Ushirikishwaji wa Watanzania za mwaka 2018 umeleta mafanikio makubwa, yakiwemo ongezeko la ajira, kukuza matumizi ya bidhaa na huduma za ndani, uhamishaji wa teknolojia pamoja na kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu nafasi yao katika sekta ya madini.
CPA Kasiki amebainisha kuwa wanasheria wana jukumu la msingi katika kuhakikisha mafanikio hayo yanaendelea kudumishwa, ikiwa ni pamoja na kutoa ushauri wa kisheria, kusimamia mikataba ya ubia, kuhakikisha kipaumbele kinatolewa kwa Watanzania katika ajira na huduma, pamoja na kushiriki kikamilifu katika utatuzi wa migogoro.
Kikao kazi hicho kimejadili kwa kina uwezo, mchango na mafanikio ya kampuni za sheria zinazomilikiwa kwa asilimia 100 na Watanzania, pamoja na kubaini changamoto zilizopo na kupendekeza mikakati ya kuboresha ushiriki wao katika sekta ya madini.

March 21, 2026
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza
na Waumini wa Dini ya Kiislamu, Viongozi, Wageni mbalimbali na Watanzania kwenye
Baraza la Eid El Fitr Kitaifa lililofanyika katika Kituo cha Mikutano cha
Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Machi, 2026.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza
na Waumini wa Dini ya Kiislamu, Viongozi, Wageni mbalimbali na Watanzania kwenye
Baraza la Eid El Fitr Kitaifa lililofanyika katika Kituo cha Mikutano cha
Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Machi, 2026.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza
na Waumini wa Dini ya Kiislamu, Viongozi, Wageni mbalimbali na Watanzania kwenye
Baraza la Eid El Fitr Kitaifa lililofanyika katika Kituo cha Mikutano cha
Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Machi, 2026.
Viongozi mbalimbali pamoja na Waumini wa Dini ya Kiislamu wakiwa kwenye Baraza la Eid El Fitr Kitaifa lililofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Machi, 2026.
Sheikh
Mkuu na Mufti wa Tanzania Dkt. Abubakar Zubeir Bin Ally akizungumza kwenye
Baraza la Eid El Fitr Kitaifa lililofanyika katika Kituo cha Mikutano cha
Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Machi, 2026.
Viongozi mbalimbali pamoja na Waumini wa Dini ya Kiislamu wakiwa kwenye Baraza la Eid El Fitr Kitaifa lililofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Machi, 2026. Viongozi mbalimbali pamoja na Waumini wa Dini ya Kiislamu wakiwa kwenye Baraza la Eid El Fitr Kitaifa lililofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Machi, 2026.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiteta jambo
na Mwenyekiti wa Taifa wa Jumuiya ya Wanawake wa Kiislam Tanzania (JUWAKITA)
Mama Shamim Khan mara baada ya kuwasili katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa
cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kushiriki kwenye
Baraza la Eid El Fitr tarehe 21 Machi, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amehutubia Baraza la Eid el-Fitr lililofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.Rais Dkt. Samia amewataka wananchi kuendelea kudumisha amani, mshikamano na heshima miongoni mwa Watanzania, akisema misingi hiyo ndiyo nguzo ya maendeleo ya Taifa, na kuongeza kuwa amani iliyopo nchini ni matokeo ya mshikamano wa wananchi na uongozi imara uliojengeka katika msingi wa kuheshimiana bila kujali tofauti za kidini au kijamii.
Aidha, amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kulinda uhuru wa kuabudu kwa mujibu wa Katiba, huku akionya dhidi ya matumizi mabaya ya uhuru huo yanayoweza kuvuruga mshikamano wa Taifa au kuchochea migawanyiko katika jamii.
Katika hatua nyingine, amepongeza mchango wa viongozi wa dini nchini katika kujenga maadili na kuhimiza mshikamano wa kijamii, akieleza kuwa wamekuwa nguzo muhimu ya kuimarisha utulivu na maadili ya jamii.
Rais Dkt. Samia pia ameitaka jamii kuepuka vitendo, kauli au mienendo inayoweza kuchochea mgawanyiko au kuvuruga umoja wa kitaifa, huku akikemea matumizi mabaya ya uhuru wa kuabudu yanayoweza kuchochea chuki, uhasama au kuvuruga amani ya nchi.
“Tofauti zetu kiimani zijengewe daraja la kuimarisha udugu wa Watanzania na umoja wa Taifa letu,” amesema Rais Dkt. Samia na kuongeza kuwa Serikali itaendelea kulinda uhuru wa kuabudu kwa mujibu wa Katiba, huku akisisitiza umuhimu wa uhuru huo kuendana na uwajibikaji ili kuepusha matumizi mabaya yanayoweza kuhatarisha amani na mshikamano wa Taifa.
Akirejea mafunzo ya kipindi cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, Rais Dkt. Samia amesema kipindi hicho kimejenga misingi ya huruma, uvumilivu na kusaidiana, na kutoa wito wa kuyaendeleza mema hayo hata baada ya kipindi cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Kwa upande wake, Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Dkt. Abubakary Zubery Ally, amesema jamii inapaswa kujenga utamaduni wa kuheshimiana na kushirikiana bila kujali tofauti za imani, akibainisha kuwa mshikamano wa kidini na kitaifa ni nguzo muhimu ya kudumisha amani.
Halikadhalika, ameonya dhidi ya fikra au vitendo vinavyoweza kuleta mpasuko katika jamii, akisisitiza kuwa hakuna nafasi ya migawanyiko katika Taifa lenye historia ya kuishi kwa umoja na amani.
Naye, Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), Alhaj Nuhu Jabir Mruma, amesema amani na utulivu wa nchi si jukumu la Serikali pekee, bali ni wajibu wa kila Mtanzania.
Ameongeza kuwa ni jukumu la kila mmoja kuchangia kwa vitendo katika kujenga jamii yenye maadili, heshima na uzalendo, akibainisha kuwa msingi wa jamii bora huanzia katika mwenendo wa mtu mmoja mmoja.

Viongozi mbalimbali pamoja na Waumini wa Dini ya Kiislamu wakiwa kwenye Baraza la Eid El Fitr Kitaifa lililofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Machi, 2026.
Viongozi mbalimbali pamoja na Waumini wa Dini ya Kiislamu wakiwa kwenye Baraza la Eid El Fitr Kitaifa lililofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Machi, 2026.
Viongozi mbalimbali pamoja na Waumini wa Dini ya Kiislamu wakiwa kwenye Baraza la Eid El Fitr Kitaifa lililofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Machi, 2026.
Viongozi mbalimbali pamoja na Waumini wa Dini ya Kiislamu wakiwa kwenye Baraza la Eid El Fitr Kitaifa lililofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Machi, 2026.
Subscribe to:
Comments (Atom)













.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)












.jpg)


.jpg)














.jpeg)


.jpeg)






.jpeg)









