June 17, 2026
Wadau wa Sekta ya Madini wamehimizwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia shughuli za madini ili kuhakikisha rasilimali hizo zinaendelea kuchangia maendeleo ya taifa na kunufaisha wananchi.
Mwanasheria wa Tume ya Madini, Janeth Kanyasu, amesema hayo kwenye Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park mkoani Dodoma, ambapo Tume inaendelea kutoa elimu kwa wananchi na wadau mbalimbali kuhusu masuala ya Sekta ya Madini.
Amesema elimu hiyo inahusu Sheria ya Madini Sura ya 123 na kanuni zake, ikijumuisha utoaji wa leseni mbalimbali, biashara ya madini, uwekezaji, shughuli za uchimbaji na usimamizi wa mazingira ili kuhakikisha rasilimali za madini zinatumika kwa tija na kwa kuzingatia matakwa ya sheria.
“Kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa ni msingi wa kuhakikisha Sekta ya Madini inaendeshwa kwa uwazi, uadilifu na kuendelea kutoa manufaa kwa taifa na wananchi,” amesema Kanyasu.
Amesema pia wananchi wanaelimishwa kuhusu ushiriki wa Serikali katika shughuli za madini, ushirikishwaji wa Watanzania katika sekta hiyo kupitia sera ya Ushiriki wa Watanzania katika Sekta ya Madini pamoja na utekelezaji wa miradi ya uwajibikaji kwa jamii (CSR) inayotekelezwa na kampuni za madini.
Kwa mujibu wa Kanyasu, Tume ya Madini inaendelea kutoa ufafanuzi kuhusu ulipaji wa mirabaha na tozo mbalimbali zinazotakiwa kisheria, ikiwemo Service Levy, HIV Levy, mrabaha wa madini ya ujenzi wa asilimia tatu, madini ya metali asilimia sita na ada ya ukaguzi ya asilimia moja.
Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka huu yanaongozwa na kaulimbiu isemayo, “Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu,” na yanatarajiwa kuhitimishwa Juni 23, 2026.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu
wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa akifanya mazungumzo na
watendaji wa Benki ya NMB kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na kuweka
mikakati ya pamoja ya hifadhi ya mazingira endelevu, kikao kilichofanyika
jijini Dodoma Juni 16, 2026.
Mkuu wa Biashara ya Serikali NMB Bi. Vicky Bishubo (Kushoto)
akizungumza wakati wa kikao na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais
(Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa chenye lengo la kuimarisha
ushirikiano na kuweka mikakati ya pamoja ya hifadhi ya mazingira endelevu,
kikao kilichofanyika jijini Dodoma Juni 16, 2026.
****************
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu
wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa amewaomba wadau wa
maendeleo kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali za kupanda miti ili
kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.Amesema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na watendaji wa Benki ya NMB kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na kuweka mikakati ya pamoja ya hifadhi ya mazingira endelevu, kikao kimefanyika jijini Dodoma Juni 16, 2026.
Mhe. Kwagilwa alisema kuwa katika kufikia lengo la upandaji wa miti takriban bilioni mbili lililowekwa kupitia Dira 2050 zinahitajika nguvu za pamoja kati ya Serikali na wadau na kuendelea kuhamasisha jamii kupanda miti kwenye maeneo yao.
Alisema ni lazima kuunganisha nguvu za pamoja kushirikiana ili kuifanya nchi kuwa ya kijani kwani hata katika kaulimbiu iliyotumika kwenye Siku ya Mazingira Duniani mwaka huu inasema ‘Dira 2050; Tuwajibike kukijanisha Tanzania’ ambayo inasisitiza umuhimu wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
.jpg)
Wataalamu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais wakiwa katika
kikao cha Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira)
Mhe. Reuben Kwagilwa na watendaji kutoka benki ya NMB chenye lengo la
kuimarisha ushirikiano na kuweka mikakati ya pamoja ya hifadhi ya mazingira
endelevu, kikao kilichofanyika jijini Dodoma Juni 16, 2026.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu
wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa akiwa katika picha ya
pamoja na watendaji wa Benki ya NMB mara baada ya kufanya mazungumzo katika
kikao chenye lengo la kuimarisha ushirikiano na kuweka mikakati ya pamoja ya
hifadhi ya mazingira endelevu, kikao kilichofanyika jijini Dodoma Juni 16,
2026.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa na Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mary Chatanda, amesema katika zama hizi za kutafuta fursa za kiuchumi duniani, sera ya kutofungamana upande wowote, inafaa zaidi kutumiwa.
Chatanda ameyasema hayo Juni 16, Jijini Dodoma, alipokuwa akitoa maoni yake kutokana na mwelekeo wa serikali ya Awamu ya Sita, chini ya uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kuifungua nchi kimataifa na mkakati wa kuhimiza diplomasia ya kiuchumi.
"Hii ya kusema mimi rafiki yangu huyu, yule adui yangu, sio nzuri, hii ya kusema nampenda huyu namchukia yule, kisa ana ugomvi na nchi mshirika wako haifai. Tanzania chini ya Rais Dk. Samia tumejitanabaisha kuwa hatufungamani na upande wowote.
Kutofungamana pande wowote kutatupa uwanja mpana wa kushirikiana na mataifa mengi duniani na kufaidi fursa mbalimbali za kiuchumi zitakazoweza kuleta tija kwa wananchi na Taifa letu," amesema Chatanda.
Sambamba na hilo, Chatanda amesema wakati mwingine nchi inanunua ugomvi usiowahusu kisa tu mataifa mawili yamegombana na hivyo nchi kumchukia nchi aliyegombama na rafiki mshirika wake.
"Tanzania tumekataa kujiingizia katika ugomvi usiotuhusu, sisi tunakwenda na yeyote ilimradi tunaona ana dhamira ya dhati ya kushirikiana na sisi katika kuchochea maendeleo. Ndiyo maana binafsi, nasimamia na Rais wetu kwa msimamo huu wa kutofungamana upande wowote," amesisitiza Chatanda.
Aidha, Chatanda amesema tunahitaji kushirikiana na mataifa mengi duniani na kila Taifa lina upekee wake katika nyanja mbalimbali kama kilimo, nishati, teknolojia, madini, elimu, afya, hivyo Tanzania inajiweka pazuri katika kuwa na washirika wengi wa maendeleo.
Ikumbukwe kuwa, Rais Dk. Samia alipokuwa ziarani nchini Urusi, katika mahojiano yake na mwandishi wa habari, aliulizwa Tanzania inawezaje kuhusiana na mataifa tofauti katika kipindi ambacho mazingira ya uchumi wa dunia yamebadikika.
Akijibu swali hilo, Rais Dk. Samia amesema "Tanzania inafuata misingi ya kutofungamana na upande wowote. Kwahiyo, adui wa rafiki yetu si adui wetu, na rafiki wa adui yetu si adui wetu".
Kimsingi, Tanzania inaendelea kusimamia sera ya diplomasia ya kiuchumi yenye mkazo wa kushirikiana na mataifa mengine ulimwenguni huku mashirikiano hayo yakiwa na wajibu wa kuleta manufaa kijamii na kiuchumi kwa pande zote.
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limehimiza ushirikiano wa karibu kati ya serikali, sekta binafsi, taasisi mbalimbali na wananchi katika juhudi za kulinda na kuhifadhi mazingira nchini.
Hatua hiyo inalenga kuhakikisha rasilimali za asili zinaendelea kutumika kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho huku zikihifadhiwa kwa uendelevu.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kaimu Meneja wa Kitengo cha Mawasiliano wa NEMC, Martha Kawishe, amesema kuwa mafanikio ya uhifadhi wa mazingira yanategemea ushiriki wa wadau wote.
Amesema changamoto za mazingira, ikiwemo uchafuzi wa mazingira, utupaji holela wa taka na shughuli zinazoweza kuharibu ikolojia, zinahitaji juhudi za pamoja ili kudhibitiwa kwa ufanisi.
Kawishe amesisitiza umuhimu wa wananchi kutoa taarifa kwa mamlaka husika wanapobaini vitendo au shughuli zinazohatarisha mazingira katika maeneo yao.
Amesema ushirikiano huo utasaidia mamlaka kuchukua hatua kwa wakati na kuzuia madhara yanayoweza kuathiri afya za wananchi, uchumi na mazingira kwa ujumla.
Aidha, NEMC itaendelea kutoa elimu kwa umma na kuimarisha ushirikiano na wadau mbalimbali ili kuongeza ufanisi katika usimamizi na uhifadhi wa mazingira nchini.
Katika hatua nyingine, Kawishe amesema NEMC imekuwa ikipokea taarifa kuhusu baadhi ya watu wasio waaminifu wanaojitambulisha kwa uongo kuwa wakaguzi wa mazingira kutoka NEMC kwa lengo la kuwalaghai wananchi, wafanyabiashara na wawekezaji.
Amesema watu hao wamekuwa wakijaribu kutumia jina la taasisi hiyo kufanya ukaguzi usio rasmi au kudai fedha kinyume na taratibu zilizowekwa.
Kutokana na hali hiyo, amewashauri wananchi, wafanyabiashara na wawekezaji kuwa makini wanapokutana na watu wanaodai kuwa maafisa wa NEMC.
Amesema kabla ya kuruhusu ukaguzi wowote, ni muhimu kuomba kuonyeshwa kitambulisho cha kazi, kitambulisho maalumu cha ukaguzi wa mazingira pamoja na nyaraka rasmi zinazompa mhusika mamlaka ya kufanya ukaguzi huo.
NEMC imeeleza kuwa tahadhari hiyo itasaidia kudhibiti vitendo vya udanganyifu na kulinda maslahi ya wananchi pamoja na wawekezaji nchini.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa kitengo cha Uhusiano kwa Umma na Nyaraka wa kampuni ya magazeti ya Serikali (TSN), Bi. Nadhifa Omar ambayo iko chini ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, mara baada ya kutembelea na kupata huduma katika banda hilo jijini Dodoma katika viwanja vya Chinangali ambapo maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026 yanafanyika, Juni 17, 2026.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa kitengo cha Uhusiano kwa Umma na Nyaraka wa Kampuni ya magazeti ya Serikali (TSN), Bi. Nadhifa Omar ambayo iko chini ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, mara baada ya kutembelea na kupata huduma katika banda hilo jijini Dodoma katika viwanja vya Chinangali ambapo maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026 yanafanyika, Juni 17, 2026.Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akipewa maelezo ya shughuli na huduma zinazotolewa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na taasisi zake kutoka kwa Mkurugenzi Msaidizi wa rasilimali watu wa wizara hiyo, Bw. Gideon Malabeja, jijini Dodoma katika viwanja vya Chinangali ambapo maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026 yanafanyika, Juni 17, 2026.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akipewa maelezo ya shughuli na huduma zinazotolewa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na taasisi zake kutoka kwa Mkurugenzi Msaidizi wa rasilimali watu wa wizara hiyo, Bw. Gideon Malabeja, jijini Dodoma katika viwanja vya Chinangali ambapo maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026 yanafanyika, Juni 17, 2026.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa kitengo cha Uhusiano kwa Umma na Nyaraka wa Kampuni ya magazeti ya Serikali (TSN), Bi. Nadhifa Omar ambayo iko chini ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, mara baada ya kutembelea na kupata huduma katika banda hilo jijini Dodoma katika viwanja vya Chinangali ambapo maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026 yanafanyika, Juni 17, 2026.Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akipewa maelezo ya shughuli na huduma zinazotolewa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na taasisi zake kutoka kwa Mkurugenzi Msaidizi wa rasilimali watu wa wizara hiyo, Bw. Gideon Malabeja, jijini Dodoma katika viwanja vya Chinangali ambapo maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026 yanafanyika, Juni 17, 2026.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akipewa maelezo ya shughuli na huduma zinazotolewa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na taasisi zake kutoka kwa Mkurugenzi Msaidizi wa rasilimali watu wa wizara hiyo, Bw. Gideon Malabeja, jijini Dodoma katika viwanja vya Chinangali ambapo maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026 yanafanyika, Juni 17, 2026.
Na. Ssgt Mawazo Mtondo - Dodoma.
Mkuu wa Sehemu ya Usimamizi wa Maadili na Ushughulikiaji wa Malalamiko (Mrejesho) wa Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Adolphina Ngoso, Mkuu wa Kitengo cha Utumishi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Naibu Kamishna wa Zimamoto na Uokoaji (DCP) Fatma Ngenya na Mkuu wa Kitengo cha Mafunzo Idara ya Uhamiaji, Naibu Kamishna wa Uhamiaji (DCI) Bahati Mwaifuge kwa nyakati tofauti, leo Juni 17, 2026 wametembelea Banda la Maonesho la Jeshi la Magereza lililopo katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.
Viongozi hao walifanya ziara hiyo katika Maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026 yanayoendelea kufanyika Jijini Dodoma, ambapo walipata fursa ya kujionea huduma mbalimbali, shughuli za urekebishaji wa wafungwa, pamoja na kazi za uzalishaji mali zinazotekelezwa na Jeshi la Magereza kupitia Programu mbalimbali za urekebishaji.
Kwa nyakati tofauti, wageni hao walipokelewa na Mkuu na Msemaji wa Jeshi la Magereza katika Maonesho ya Mwaka huu, Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Elmas L.Mgimwa, ambaye aliwaeleza majukumu ya Jeshi la Magereza katika Usalama, mchango wake katika utoaji wa huduma za urekebishaji na mageuzi yaliyopo sasa katika utekelezaji wa majukumu yake yanayochsngia kwa kiasi kikubwa maendeleo nch kijamii na kiuchumi.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uwekezaji Mfuko wa Mabadiliko ya Tabianchi (GCF) Dkt. Achala Abeysinghe Juni 16, 2026 jijini Bonn, Ujerumani.
Madhumuni ya kikao hicho ni kukuza mashirikiano yaliyopo kati ya JMT na Taasisi hiyo hasa katika kuiwezesha Tanzania kupata msaada wa kifedha na utalaamu wa kiufundi katika kuisadia nchi kupata fedha za kupambana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
Katika mkutano huo, Dkt. Muyungi alieleza kuwa Tanzania ikiwa moja ya nchi nufaika na fedha kutoka mfuko huo za utekelezaji miradi ya maendeleo ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
Hivyo, kutokana na fursa ilizopo Tanzaia imeweza kuwasilisha maombi ya kuipatia Ithibati Wizara ya Fedha ili kuweza kupata fedha moja kwa moja kutoka katika mfuko huo.
Hadi sasa JMT inataasisi moja ambayo ni CRDB iliyopewa ithibati ili kuweza kunufaika moja kwa moja na fedha zinazotolewa na mfuko huo za kuhimili athari za abadiliko ya tabiachi.
Mkutano huo ulihudhuriwa na wataalamu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Wizara ya Fedha na Taasisi za Kifedha za nchini ikiwemo Benki ya TIB, Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) na Bneki ya NBC.
Mwenyekiti wa Timu ya Watalaamu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu na Msaidizi wa Aziri Mkuu Mahusiano, Asasi za Kiraia na Mashirika yasiyo ya Kiserikali, Tryphone Mkorokoti (wa pili kushoto) akiongoza kikao cha maridhiano cha kujadili mgogoro wa fidia kati ya Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni na Kampuni ya Tanganyika Leisure Limited kwenye Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni, Juni 16, 2026. Wengine kutoka kushoto ni Mthamini wa manispaa hiyo Alphonce Chuwa, Mkurugenzi wa Kampuni ya Tanganyika Leisure, Evetha Massawe, Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Erasto Kiwele na Msaidizi wa Waziri Mkuu Masuala ya Ardhi, Senso Magesa. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Wananchi mbalimbali wakifika katika banda la Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kupata huduma na elimu kuhusu shughuli zinazofanywa na wizara hiyo kwenye Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026, jijini Dodoma katika viwanja vya Chinangali, Juni 16, 2026.
Na Adelina Johnbosco - MAELEZO
Wananchi wamehimizwa kushiriki kikamilifu katika maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma hususan katika banda la Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ili kuelimika kuhusu huduma muhimu zinazotolewa na Wizara, Taasisi na Mashirika yake.
Mkurugenzi Msaidizi wa rasilimali watu wa Wizara, Bw. Gideon Malabeja ametoa rai hiyo katika viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma yanakofanyika maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026.
"Wizara yetu ina sekta nne ambazo ni sekta ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo. Kila sekta ina huduma zake, mfano, sekta ya habari kuna Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari ( JAB) inayoshughulikia masuala ya maadili na weledi kwa waandishi wa habari, Shirika la Magazeti ya Serikali (TSN) na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC)" amesema Bw. Malabeja
Amesema TBC inatoa taarifa za habari, vipindi na matangazo mbalimbali kwa ajili ya kuuhabarisha umma ambapo TBC inatangaza mbashara michuano ya Kombe la Dunia inayoendelea nchini Marekani, Mexico na Canada.
Ametaja taasisi zingine zinazotoa huduma chini ya Wizara hiyo kwamba ni Bodi ya Filamu Tanzania, Chuo cha Michezo Malya, Baraza la Michezo la Taifa, Ofisi ya Hakimiliki Tanzania (COSOTA), Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA), Mfuko wa Maendeleo ya Utamaduni, na Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSuBa).
Maonesho hayo yameanza Juni 16, 2026 ambapo ufunguzi wake rasmi ni Juni 17, 2026 na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Mhe. Ridhiwani Kikwete na Utawala Bora.
Wananchi mbalimbali wakifika katika banda la Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kupata huduma na elimu kuhusu shughuli zinazofanywa na wizara hiyo kwenye Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026, jijini Dodoma katika viwanja vya Chinangali, Juni 16, 2026.
Wananchi mbalimbali wakifika katika banda la Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kupata huduma na elimu kuhusu shughuli zinazofanywa na wizara hiyo kwenye Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026, jijini Dodoma katika viwanja vya Chinangali, Juni 16, 2026.
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais
Menejmenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Juma Mkomi akizungumza na
Maafisa kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) alipotembelea banda la
Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyoanza leo
jijini Dodoma.
Afisa Utafiti wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Makrina Komba akimpima uwiano wa urefu kwa uzito Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejmenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Juma Mkomi alipotembelea banda la Taasisi hiyo lililopo katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Daud Gwilenza akimsikiliza mwananchi aliyetembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.
************
Na Mwandishi Maalumu - DodomaTaasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) yafikisha Kampeni ya Jua Namba Zako kwa wananchi wa Mkoa wa Dodoma na Mikoa ya jirani kupitia maonesho ya wiki ya utumishi wa umma yaliyoanza leo katika Viwanja vya Chinangali Park vilivyopo jijini Dodoma.
Katika maonesho hayo wataalamu wa JKCI wanatoa elimu ya umuhimu wa kupima na kufahamu shinikizo la juu la damu, mapigo ya moyo, wingi wa sukari kwenye damu, uwiano wa uzito kwa urefu pamoja na wingi wa mafuta kwenye damu.
Sambamba na elimu hiyo wananchi wanaotembelea katika banda la JKCI wanapata fursa ya kuyafahamu magonjwa ya moyo, namna ya kujikinga na magonjwa yaho lakini pia kufanyiwa uchunguzi wa afya kwa kupimwa vipimo vya moyo, shinikizo la damu, sukari kwenye damu pamoja na uwiano wa urefu kwa uzito.
Tanzania na Canada zimekubaliana kuimarisha ushirikiano katika utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya utafiti wa kina wa madini, hatua inayotarajiwa kuongeza upatikanaji wa taarifa sahihi za kijiolojia, kuhamasisha uwekezaji na kuendeleza Sekta ya Madini nchini.
Hayo yameelezwa leo Juni 16, 2026 jijini Dodoma na Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, wakati wa kikao chake na Balozi wa Canada nchini Tanzania, Mhe. Emily Burns, kilicholenga kujadili namna ya kuendeleza ushirikiano kati ya nchi hizo mbili katika eneo la utafiti wa madini.
Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Mavunde amesema Tanzania hivi sasa inajipanga kuondokana na uchimbaji wa kubahatisha na badala yake kuwa na uchimbaji unaoongozwa na taarifa muhimu za kijiolojia,huku akisisitiza kuwa mkakati uliopo ni kuongeza eneo lililofanyiwa utafiti wa kina kutoka asilimia 16 ya sasa hadi asilimia 50 ifikapo mwaka 2030.
Ameongeza kuwa Tanzania na Canada zimekuwa na uhusiano wa muda mrefu na kwamba ameridhishwa na dhamira iliyooneshwa na Serikali ya Canada ya kushirikiana na Tanzania katika miradi ya kimkakati ya utafiti wa kina wa madini.
Aidha, amesema tafiti za kina zitasaidia kuondoa changamoto ya uchimbaji wa kubahatisha ambayo imekuwa ikiwasababishia wachimbaji wadogo kupoteza muda, mitaji na rasilimali nyingine kutokana na kufanya shughuli za uchimbaji katika maeneo yasiyokuwa na taarifa za kutosha za kijiolojia.
Mhe. Mavunde ameielekeza Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) kuainisha maeneo ya kimkakati yatakayopewa kipaumbele katika utekelezaji wa ushirikiano huo, huku akisisitiza kuwa Serikali ipo tayari kutoa ushirikiano wote unaohitajika ili kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwa ufanisi.
Kwa upande wake, Balozi wa Canada nchini Tanzania, Mhe. Emily Burns, amesema Serikali ya Canada imevutiwa na maono ya *Mining Vision 2030* pamoja na kaulimbiu ya *“Madini ni Maisha na Utajiri”*, na kueleza kuwa nchi hiyo ipo tayari kuendelea kushirikiana na Tanzania katika miradi mbalimbali ya kimkakati ikiwemo utafiti wa kina wa madini kwa kutumia teknolojia ya uchunguzi wa angani kupitia ndege maalum.
Naye Mtendaji Mkuu wa GST, Mhandisi Ally Samaje, amesema ushirikiano huo unatarajiwa kuanza kwa kufanya tafiti za kina katika Block Na. 1 iliyopo Kanda ya Ziwa na Block Na. 5 iliyopo Kaskazini Mashariki mwa Tanzania, maeneo ambayo ni miongoni mwa vipaumbele vya taasisi hiyo katika mwaka wa fedha ujao.
Amesema utekelezaji wa miradi hiyo utaongeza upatikanaji wa taarifa sahihi za kijiolojia, kuimarisha uwekezaji na kuchochea ukuaji endelevu wa Sekta ya Madini, sambamba na kuiwezesha Tanzania kufikia lengo la kuongeza eneo la utafiti wa kina kutoka asilimia 16 ya sasa hadi asilimia 50 ifikapo mwaka 2030.
Subscribe to:
Posts (Atom)



_page-0001.jpg)
_page-0002.jpg)
.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)


.jpeg)







.jpeg)


























