April 17, 2026
Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Utalii, Biashara na Kilimo ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, wakiwa katika ziara ya mafunzo, Kituo cha vipimo Misugusugu, mkoani Pwani, Aprili 16, 2026.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo, Bw. Alban Kihulla akifafanua jambo kwa Wajumbe wa Kamati ya Utalii, Biashara na Kilimo ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, wakati wa ziara yao ya mafunzo katika Kituo cha Vipimo Misugusugu, mkoani Pwani, Aprili 16, 2026.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA), Bw. Alban Kihulla akiwaeleza Wajumbe wa Kamati ya Utalii, Biashara na Kilimo ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, namna Wakala hiyo inavyohakiki dira za maji, wakati wa ziara yao ya mafunzo katika Kituo cha Vipimo Misugusugu, mkoani Pwani, Aprili 16. 2026.
Wajumbe wa Kamati ya Utalii, Biashara na Kilimo ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, wakiwa katika ziara ya mafunzo, Kituo cha vipimo Misugusugu, mkoani Pwani, Aprili 16, 2026.
Wajumbe wa Kamati ya Utalii, Biashara na Kilimo ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, wakiwa katika ziara ya mafunzo, Kituo cha vipimo Misugusugu, mkoani Pwani, Aprili 16, 2026.
Wajumbe wa Kamati ya Utalii, Biashara na Kilimo ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, wakiwa katika ziara ya mafunzo, Kituo cha vipimo Misugusugu, mkoani Pwani, Aprili 16, 2026.
Kamati ya Utalii, Biashara na Kilimo ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, imekiri kuvutiwa na utendaji kazi wa Wakala wa Vipimo (WMA) Tanzania Bara na kuahidi kuweka mikakati ya makusudi itakayoisaidia Mamlaka inayosimamia vipimo nchini humo (ZAWEMA) kutekeleza majukumu yake kwa kiwango hicho au zaidi.
Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo Aprili 16, 2026 baada ya ziara ya mafunzo katika Kituo cha Vipimo Misugusugu, mkoani Pwani, Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Dkt. Mohammed Ali Suleiman, amesema Wakala wa Vipimo upande wa Tanzania Bara wamepiga hatua kubwa kiutendaji hivyo kuna kila sababu ya Zanzibar kufuata mfano huo.
“Tumeona wenzetu wamefanya kazi kubwa na wana vipimo vya kisasa ambavyo vinawawezesha kuhakiki mathalani kiwango cha maji anachotumia mteja ndicho anacholipia, halikadhalika kwenye umeme pamoja na vipimo vingine.”
Mhe. Dkt. Suleiman ameongeza kuwa, Kamati yake itaishauri Wizara ya Biashara ambayo ndiyo inayoisimamia Mamlaka ya Vipimo Zanzibar, kuweka mikakati ya makusudi ili kuiwezesha kutekeleza majukumu yake kikamilifu kwa manufaa ya wananchi.
Amesema wataishauri Serikali kuhakikisha ZAWEMA, ambayo ndiyo Mamlaka ya Vipimo kwa upande wa Zanzibar, kwanza inakuwa Mamlaka huru lakini pia ipate mitambo ya kisasa ya uhakiki vipimo na pia ishirikiane kwa ukaribu na WMA ili iweze kutekeleza majukumu yote kwa ufanisi.
“Ukiangalia, Kituo hiki cha Misugusugu kinaipatia Serikali ya Tanzania mapato makubwa sana. Ni muhimu Serikali yetu iwezeshe ZAWEMA kufanya kazi kwa karibu na WMA ili kupata mafanikio kama hapa,” amesisitiza Mhe. Dkt. Suleiman.
Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa WMA, Bw. Alban Kihulla, amesema anaamini kwamba, kupitia ziara hiyo ya mafunzo kwa Kamati kutoka Baraza la Wawakilishi, jukumu la uhakiki na ukaguzi wa vipimo linaenda kuwa bora zaidi kwa pande zote mbili; Zanzibar na Tanzania Bara.
“Niwahakikishie tu kwamba tutaendelea kushirikiana na wenzetu wa Zanzibar ili kuhakikisha Mtoa Huduma analindwa lakini pia Mpokeaji Huduma analindwa.”
Akidadavua zaidi kuhusu ushirikiano uliopo kati ya WMA na ZAWEMA, Mtendaji Mkuu amesema Taasisi hizo mbili zilikwishasaini Hati ya Ushirikiano (MoU) kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo kushiriki kwenye mikutano ya kikanda na kimataifa pamoja na katika kaguzi za vipimo hususan katika bidhaa zilizofungashwa.
Amesema kuwa, WMA wakiwa ndiyo wenyeji katika ziara hiyo, wamewaonesha wageni wao utendaji kazi katika maeneo mbalimbali ikiwemo uhakiki wa tenki za kusafirishia mafuta, uhakiki wa mita za umeme pamoja na uhakiki wa dira za maji.
Wakala wa Vipimo Tanzania imekuwa ikipokea wageni mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi kwa lengo la kuja kujifunza kuhusu majukumu ya uhakiki wa vipimo.
Aidha, kwa sasa, Wakala wa Vipimo Tanzania ndiye Mwenyekiti wa Jukwaa la Kikanda linaloratibu masuala ya kivipimo (legal metrology) kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADCMEL).
April 16, 2026
Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa - Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI), Ndg. Rabia Abdalla Hamid, amefanya Kikao kazi na Kansela wa Chama Cha Kikomunisti (CPC), Ubalozi wa China nchini Tanzania Ndg. Xu Sujiang leo tarehe 16.04.2026, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam.Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Jumatano, Aprili 15, 2026, akimpongeza na kumshukuru Mkurugenzi Mkuu wa Viwanja vya Ndege (TAA) Bw. Abdul Mombokaleo kwa kujitolea computer zenye thamani ya shilingi milioni 170 kama mchango wake yeye na Alumni wengine kwa kuboresha elimu ya Sayansi katika shule hiyo.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Jumatano, Aprili 15, 2026, akupewa maelezo juu ya mradi wa jengo la maabara ya TEHAMA ambayo ni ‘Smart Class’ alipokuwa Mgeni rasmi katika Mahafali ya 59 ya Shule ya Sekondari Kibaha (KSS) kama mgeni rasmi, katika hafla iliyofanyika shuleni hapo, Tumbi, Kibaha Mji, mkoani Pwani.Sehemu ya wahitimu wa kidato cha sita katika Mahafali ya 59 ya Shule ya Sekondari Kibaha (K katika hafla iliyofanyika shuleni hapo, Tumbi, Kibaha Mji, mkoani Pwani.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Jumatano, Aprili 15, 2026, akiwatambulisha baadhi ya Alumni walio katika kamati ya mradi wa ujenzi wa jengo la maabara ya TEHAMA ambayo ni ‘Smart Class’ katika Mahafali ya 59 ya Shule ya Sekondari Kibaha (KSS) kama mgeni rasmi, katika hafla iliyofanyika shuleni hapo, Tumbi, Kibaha Mji, mkoani Pwani. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Viwanja vya Ndege (TAA) Bw. Abdul Mombokaleo, akifuatiwa na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO Nchini Prof. Hamisi Malebo.
(Picha na Habari na Issa Michuzi)
Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Jumatano, Aprili 15, 2026, akikagua na kupewa maelezo juu ya maabara ya TEHAMA ambayoni ‘Smart Class” na Mkuu wa Shule hiyo alipokuwa Mgeni rasmi katika n Mahafali ya 59 ya Shule ya Sekondari Kibaha (KSS) kama mgeni rasmi, katika hafla iliyofanyika shuleni hapo, Tumbi, Kibaha Mji, mkoani Pwani.Akiwa katika mahafali hayo, Dkt. Kikwete amezindua harambee ya kuchangia ujenzi wa jengo la ghorofa la maabara ya TEHAMA na masomo mengine, ambalo linatarajiwa kugharimu shilingi bilioni 3.
Amesema ujenzi huo ni muhimu katika kuendeleza ubunifu na uwezo wa wanafunzi katika masomo ya sayansi, teknolojia, uhandisi na hisabati (STEM).
Aidha, Dkt. Kikwete amekubali kuwa mlezi wa kamati ya kukusanya michango kwa ajili ya mradi huo mkubwa ambao kwa sasa umefikia hatua ya msingi.
Pia, Rais Mstaafu ameishukuru jumuiya ya wanafunzi wa zamani (alumni) wa shule hiyo, wakiuongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Bw. Abdul Mombokaleo, kwa kuchangia kompyuta zenye thamani ya Shilingi Milioni 170 kwa ajili ya “Darasa Janja” (Smart Class) lililoanzishwa shuleni hapo.
Darasa hilo litakuwa ni kituo cha mafunzo kwa wanafunzi wa shule hiyo na shule nyingine zitakazounganishwa kupitia mfumo wa mtandao, ambapo mwalimu anaweza kufundisha madarasa yaliyoko nje ya Kibaha kwa wakati mmoja kwa njia ya kidigitali.
Katika ziara yake, Dkt. Kikwete alipata fursa ya kutembelea na kukagua Darasa Janja hilo, akipokea maelezo kutoka kwa Mkuu wa Shule kuhusu namna teknolojia hiyo inavyotumika kuboresha mbinu za ufundishaji na ujifunzaji shuleni hapo.
Shule ya Sekondari Kibaha, inayomilikiwa na Shirika la Elimu Kibaha na kusimamiwa na Kurugenzi ya Hud uma za Elimu, ilianzishwa mwaka 1965 kupitia ushirikiano kati ya Serikali ya Tanganyika ya wakati huo na nchi za Nordic – Denmark, Finland, Norway, na Sweden. Wakati inaanzishwa, shule ilikuwa na wanafunzi 110 wa Kidato cha Kwanza na 60 wa Kidato cha Tano.
Kwa sasa, shule hiyo ya bweni kwa wavulana ina uwezo wa kuchukua zaidi ya wanafunzi 800 na imeendelea kuwa miongoni mwa taasisi kongwe na zenye heshima kubwa katika sekta ya elimu nchini.
Dkt. Kikwete ni miongoni mwa alumni mashuhuri wa Shule ya Sekondari Kibaha, alikosoma zaidi ya miaka 60 iliyopita. Wengine waliopitia shule hiyo ni pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mkurugenzi Mkuu wa ATCL Bw. Peter Ulanga, Balozi Lazaro Nyalandu, Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO Nchini Prof. Hamisi Malebo, Mkurugenzi Mkuu wa Viwanja vya Ndege Bw. Abdul Mombokaleo, na Mwenyekiti Mstaafu wa CHADEMA Mhe. Freeman Mbowe, miongoni mwa wengine wengi.
Aidha, kwa kutambua mchango mkubwa wa alumni wake, Shule ya Sekondari Kibaha inaendelea kuimarisha ushirikiano na wadau wa elimu ili kuhakikisha inaendelea kuwa kinara katika utoaji wa elimu ya ubora nchini.
April 15, 2026
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Asha-Rose Migiro, leo tarehe 15 Aprili 2026 amefanya mazungumzo na Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Malawi, Mhe. Lazarus Chakwera, katika Ofisi za CCM Lumumba, jijini Dar es Salaam.



.jpg)
.jpg)
.jpeg)

.jpeg)







































