Nafasi Ya Matangazo

June 17, 2026



Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uwekezaji Mfuko wa Mabadiliko ya Tabianchi (GCF) Dkt. Achala Abeysinghe Juni 16, 2026 jijini Bonn, Ujerumani.
 
Kikao hicho cha pande mbili baina ya Jamhuri ya Muungano waTanzania na GCF kimfanyika kando ya Mkutano wa 64 wa Kamati za Utekelezaji na Sayansi na Ushauri chini ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi (SB64) ukiendelea. 

Madhumuni ya kikao hicho ni kukuza mashirikiano yaliyopo kati ya JMT na Taasisi hiyo hasa katika kuiwezesha Tanzania kupata msaada wa kifedha na utalaamu wa kiufundi katika kuisadia nchi kupata fedha za kupambana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Katika mkutano huo, Dkt. Muyungi alieleza kuwa Tanzania ikiwa moja ya nchi nufaika na fedha kutoka mfuko huo za utekelezaji miradi ya maendeleo ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. 

Hivyo, kutokana na fursa ilizopo Tanzaia imeweza kuwasilisha maombi ya kuipatia Ithibati Wizara ya Fedha ili kuweza kupata fedha moja kwa moja kutoka katika mfuko huo. 

Hadi sasa JMT inataasisi moja ambayo ni CRDB iliyopewa ithibati ili kuweza kunufaika moja kwa moja na fedha zinazotolewa na mfuko huo za kuhimili athari za abadiliko ya tabiachi. 

Mkutano huo ulihudhuriwa na wataalamu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Wizara ya Fedha na Taasisi za Kifedha za nchini ikiwemo Benki ya TIB, Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) na Bneki ya NBC.

 
Posted by MROKI On Wednesday, June 17, 2026 No comments
Mwenyekiti wa Timu ya Watalaamu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu na Msaidizi wa Aziri Mkuu Mahusiano, Asasi za Kiraia na Mashirika yasiyo ya Kiserikali, Tryphone Mkorokoti (wa pili kushoto) akiongoza kikao cha maridhiano cha kujadili mgogoro wa fidia kati ya Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni  na Kampuni  ya Tanganyika Leisure Limited kwenye Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni, Juni 16, 2026. Wengine kutoka kushoto ni Mthamini wa manispaa hiyo Alphonce Chuwa,  Mkurugenzi wa Kampuni ya Tanganyika Leisure, Evetha Massawe, Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Erasto Kiwele na Msaidizi wa  Waziri Mkuu Masuala ya Ardhi, Senso Magesa. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Posted by MROKI On Wednesday, June 17, 2026 No comments

 


Posted by MROKI On Wednesday, June 17, 2026 No comments

Wananchi mbalimbali wakifika katika banda la Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kupata huduma na elimu kuhusu shughuli zinazofanywa na wizara hiyo kwenye Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026, jijini Dodoma   katika viwanja vya Chinangali, Juni 16, 2026.

Na Adelina Johnbosco - MAELEZO 
Wananchi wamehimizwa kushiriki kikamilifu katika maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma hususan katika banda la Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ili kuelimika kuhusu huduma muhimu zinazotolewa na Wizara, Taasisi na Mashirika yake. 

Mkurugenzi Msaidizi wa rasilimali watu wa Wizara, Bw. Gideon Malabeja ametoa rai hiyo katika viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma yanakofanyika maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026.

"Wizara yetu ina sekta nne ambazo ni sekta ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo. Kila sekta ina huduma zake, mfano, sekta ya habari kuna Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari ( JAB) inayoshughulikia masuala ya maadili na weledi kwa waandishi wa habari, Shirika la Magazeti ya Serikali (TSN) na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC)" amesema Bw. Malabeja

Amesema  TBC inatoa taarifa za habari, vipindi na matangazo mbalimbali kwa ajili ya kuuhabarisha umma ambapo TBC inatangaza mbashara michuano ya Kombe la Dunia inayoendelea nchini Marekani, Mexico na Canada.

Ametaja taasisi zingine zinazotoa huduma chini ya Wizara hiyo kwamba ni Bodi ya Filamu Tanzania, Chuo cha  Michezo Malya, Baraza la Michezo la Taifa, Ofisi ya Hakimiliki Tanzania (COSOTA), Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA), Mfuko wa Maendeleo ya Utamaduni, na Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSuBa).

Maonesho hayo yameanza  Juni 16, 2026 ambapo ufunguzi wake rasmi ni Juni 17, 2026 na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Mhe. Ridhiwani Kikwete na Utawala Bora.
Wananchi mbalimbali wakifika katika banda la Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kupata huduma na elimu kuhusu shughuli zinazofanywa na wizara hiyo kwenye Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026, jijini Dodoma   katika viwanja vya Chinangali, Juni 16, 2026.


Wananchi mbalimbali wakifika katika banda la Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kupata huduma na elimu kuhusu shughuli zinazofanywa na wizara hiyo kwenye Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026, jijini Dodoma   katika viwanja vya Chinangali, Juni 16, 2026.

Wananchi mbalimbali wakifika katika banda la Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kupata huduma na elimu kuhusu shughuli zinazofanywa na wizara hiyo kwenye Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026, jijini Dodoma   katika viwanja vya Chinangali, Juni 16, 2026.

Posted by MROKI On Wednesday, June 17, 2026 No comments
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejmenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Juma Mkomi akizungumza na Maafisa kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyoanza leo jijini Dodoma.
Afisa Utafiti wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Makrina Komba akimpima uwiano wa urefu kwa uzito Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejmenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Juma Mkomi alipotembelea banda la Taasisi hiyo lililopo katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.
Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Daud Gwilenza akimsikiliza mwananchi aliyetembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.
************
Na Mwandishi Maalumu - Dodoma
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) yafikisha Kampeni ya Jua Namba Zako kwa wananchi wa Mkoa wa Dodoma na Mikoa ya jirani kupitia maonesho ya wiki ya utumishi wa umma yaliyoanza leo katika Viwanja vya Chinangali Park vilivyopo jijini Dodoma.

Katika maonesho hayo wataalamu wa JKCI wanatoa elimu ya umuhimu wa kupima na kufahamu shinikizo la juu la damu, mapigo ya moyo, wingi wa sukari kwenye damu, uwiano wa uzito kwa urefu pamoja na wingi wa mafuta kwenye damu.

Sambamba na elimu hiyo wananchi wanaotembelea katika banda la JKCI wanapata fursa ya kuyafahamu magonjwa ya moyo, namna ya kujikinga na magonjwa yaho lakini pia  kufanyiwa uchunguzi wa afya kwa kupimwa vipimo vya moyo, shinikizo la damu, sukari kwenye damu pamoja na uwiano wa urefu kwa uzito.
Posted by MROKI On Wednesday, June 17, 2026 No comments









Dodoma
Tanzania na Canada zimekubaliana kuimarisha ushirikiano katika utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya utafiti wa kina wa madini, hatua inayotarajiwa kuongeza upatikanaji wa taarifa sahihi za kijiolojia, kuhamasisha uwekezaji na kuendeleza Sekta ya Madini nchini.

Hayo yameelezwa leo Juni 16, 2026 jijini Dodoma na Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, wakati wa kikao chake na Balozi wa Canada nchini Tanzania, Mhe. Emily Burns, kilicholenga kujadili namna ya kuendeleza ushirikiano kati ya nchi hizo mbili katika eneo la utafiti wa madini.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Mavunde amesema Tanzania hivi sasa inajipanga kuondokana na uchimbaji wa kubahatisha na badala yake kuwa na uchimbaji unaoongozwa na taarifa muhimu za kijiolojia,huku akisisitiza kuwa  mkakati uliopo ni kuongeza eneo lililofanyiwa utafiti wa kina kutoka asilimia 16 ya sasa hadi asilimia 50 ifikapo mwaka 2030.

Ameongeza kuwa Tanzania na Canada zimekuwa na uhusiano wa muda mrefu na kwamba ameridhishwa na dhamira iliyooneshwa na Serikali ya Canada ya kushirikiana na Tanzania katika miradi ya kimkakati ya utafiti wa kina wa madini.

Aidha, amesema tafiti za kina zitasaidia kuondoa changamoto ya uchimbaji wa kubahatisha ambayo imekuwa ikiwasababishia wachimbaji wadogo kupoteza muda, mitaji na rasilimali nyingine kutokana na kufanya shughuli za uchimbaji katika maeneo yasiyokuwa na taarifa za kutosha za kijiolojia.

Mhe. Mavunde ameielekeza Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) kuainisha maeneo ya kimkakati yatakayopewa kipaumbele katika utekelezaji wa ushirikiano huo, huku akisisitiza kuwa Serikali ipo tayari kutoa ushirikiano wote unaohitajika ili kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwa ufanisi.

Kwa upande wake, Balozi wa Canada nchini Tanzania, Mhe. Emily Burns, amesema Serikali ya Canada imevutiwa na maono ya *Mining Vision 2030* pamoja na kaulimbiu ya *“Madini ni Maisha na Utajiri”*, na kueleza kuwa nchi hiyo ipo tayari kuendelea kushirikiana na Tanzania katika miradi mbalimbali ya kimkakati ikiwemo utafiti wa kina wa madini kwa kutumia teknolojia ya uchunguzi wa angani kupitia ndege maalum.

Naye Mtendaji Mkuu wa GST, Mhandisi Ally Samaje, amesema ushirikiano huo unatarajiwa kuanza kwa kufanya tafiti za kina katika Block Na. 1 iliyopo Kanda ya Ziwa na Block Na. 5 iliyopo Kaskazini Mashariki mwa Tanzania, maeneo ambayo ni miongoni mwa vipaumbele vya taasisi hiyo katika mwaka wa fedha ujao.

Amesema utekelezaji wa miradi hiyo utaongeza upatikanaji wa taarifa sahihi za kijiolojia, kuimarisha uwekezaji na kuchochea ukuaji endelevu wa Sekta ya Madini, sambamba na kuiwezesha Tanzania kufikia lengo la kuongeza eneo la utafiti wa kina kutoka asilimia 16 ya sasa hadi asilimia 50 ifikapo mwaka 2030.
Posted by MROKI On Wednesday, June 17, 2026 No comments

June 16, 2026






Wadau mbalimbali waliotembelea Banda la Wakala wa Vipimo (WMA) katika siku ya kwanza ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, Juni 16, 2026 wamekiri kuvutiwa na elimu inayotolewa na timu ya wataalamu kuhusu matumizi sahihi ya vipimo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Nadhifa Nyoni kutoka Mamlaka ya Maji (TANGA UWASA), Rose Mmary (JWTZ) na Janeth Matara, mwananchi mkazi wa Dodoma, wamepongeza kazi zinazofanywa na WMA na kukiri kuwa elimu waliyoipata kutoka kwa wataalamu imewaongezea uelewa kuhusu vipimo.

Kwa upande wake, Abbas Kayanda, mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma, pamoja na kupongeza kazi nzuri inayofanywa na WMA, ameshauri kuongeza nguvu katika utoaji elimu ya vipimo ili kuwapatia uelewa wananchi wengi zaidi hususan walioko vijijini.

Ufunguzi rasmi wa Maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka 2026 yaliyoanza leo, Juni 16 katika uwanja wa Chinangali Dodoma, yatahitimishwa Juni 23.

Kaulimbiu ya mwaka huu ni "Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Maendeleo Endelevu."
Posted by MROKI On Tuesday, June 16, 2026 No comments

Dodoma
Tume ya Madini imeanza kutoa elimu kwa wananchi kuhusu sekta ya madini katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali za kuimarisha uelewa wa wananchi kuhusu rasilimali madini na fursa zinazotokana na sekta hiyo.

Maonesho hayo yaliyoanza leo Juni 16, 2026 yanatarajiwa kuhitimishwa Juni 23, 2026, yakikutanisha taasisi mbalimbali za umma kwa lengo la kuonesha huduma wanazotoa kwa wananchi chini ya kaulimbiu isemayo, “Kuchochea Uwajibikaji kwa Huduma Endelevu.”

Kupitia banda lake, Tume ya Madini inatoa elimu kuhusu aina mbalimbali za madini yanayopatikana nchini, mchango wa sekta hiyo katika kukuza uchumi wa taifa, pamoja na fursa za uwekezaji, ajira na ushiriki wa wananchi katika shughuli za uchimbaji na biashara ya madini.

Aidha, wananchi wanaotembelea banda la Tume wanapata fursa ya kufahamu huduma mbalimbali zinazotolewa na taasisi  kwa wadau wa sekta ya madini, sambamba na kupata ufafanuzi kuhusu taratibu na miongozo inayosimamia shughuli za madini nchini.

Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanatarajiwa kuzinduliwa rasmi kesho Juni 17, 2026 na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete.

Wananchi wamehimizwa kutembelea mabanda mbalimbali ili kujionea huduma zinazotolewa na taasisi za umma na kupata elimu itakayowawezesha kunufaika na fursa zilizopo katika sekta mbalimbali za maendeleo, ikiwemo sekta ya madini.





Posted by MROKI On Tuesday, June 16, 2026 No comments

Dodoma
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu, Bw. Renatus Msangira kutoka Wakala wa  Nishati Vijijini (REA), leo Juni 16, 2026 amewaongoza watumishi wa REA katika kuwaeleza wadau kuhusiana na miradi mbalimbali inayotekelezwa, hatua iliyofikiwa na mipango iliyopo kwa wannachi wanaotembelea banda la REA katika Maadhimisho ya  Kitaifa ya Wiki ya Utumishi kwa Umma 2026 yaliyoanza leo jijini Dodoma. 

Maadhimisho ya mwaka huu yamepambwa na kaulimbiu inayosema "Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu"




Posted by MROKI On Tuesday, June 16, 2026 No comments
Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imeanza  kutoa elimu na huduma za Sekta za Wizara hiyo katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo yameanza  leo  Juni 16, 2026 katika eneo la Chinangali Park jijini Dodoma

Miongoni mwa huduma zinazotolewa ni usajili wa wasanii na vikundi vya Sanaa, Udahili wa Wanafunzi kwenye chuo cha Maendeleo ya michezo Malya, kudahili Wanafunzi kwenye chuo cha Utamaduni na Sanaa Bagamoyo (TaSUBa) kusajili Waandishi wa Habari kupitia Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari.

Vile vile, Baraza la Michezo la Taifa linatoa elimu na kusajili vyama mbalimbali vya michezo.

Aidha, Michezo ya kitamaduni kama vile bao, drafti na karata ni michezo ambayo ni kivutio kikubwa katika banda hilo.

Ndani ya Banda hilo la Wizara ya Habari zipo taasisi zake zote ikiwa ni pamona na Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC), Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN), Baraza la michezo la Taifa (BMT), Bodi ya Filamu Tanzania (TFB), Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA), Ofisi ya Hakimiliki Tanzania (COSOTA),Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) 










Posted by MROKI On Tuesday, June 16, 2026 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo