Nafasi Ya Matangazo

March 04, 2026







Na Eleuteri Mangi, WANMM- Bariadi, Simiyu
Serikali kupitia Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeanzisha Kliniki Maalumu ya Wanawake “Samia Ardhi Kliniki” hatua inayoweka mazingira rafiki kwa wanawake wengi kumiliki ardhi kisheria sambamba na kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi na maendeleo. 

Wanawake wa Mkoa wa Simiyu ambao ni miongoni mwa wanufaika wa kliniki hiyo wameishukuru Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kuwapelekea Samia Ardhi Kliniki inayoendelea kuwahudumia wanawake na kutatua changamoto zinazowakabili katika umiliki wa ardhi katika maeneo mbalimbali nchini.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kliniki hiyo Machi 4, 2026 mjini Bariadi, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anamringi Macha amesema, Kliniki hiyo imekuja muda muafaka kwa kuwa itasaidia wanawake wa mkoa huo kumiliki ardhi. 

Pia Mkuu wa Mkoa Mhe. Macha ametoa wito kwa wanawake katika mkoa huo kujitokeza kwa wingi katika wiki ya Samia Ardhi Kliniki ili kupata elimu, ushauri na huduma mbalimbali za Sekta ya Ardhi ikiwemo kupimiwa maeneo yao na kupata Hati Miliki zao. 

Pamoja na uwepo wa Sera na Sheria zinazolinda haki za wanawake, takwimu zinaonesha kuwa takribani asilimia 28 pekee ya wanawake nchini ndio wenye hati miliki katika maeneo mbalimbali nchini.

Akitoa taarifa ya utendaji kazi wakati wa ufunguzi wa Kliniki hiyo, Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Simiyu Bw. Denis Masami amesema, hadi kufikia tarehe 4 Machi 2026 wametoa jumla ya Hati 198 na kuweka bayana kuwa, kliniki hiyo inayotarajiwa kuhitimishwa Machi 7, 2026 ni sehemu ya kuelekea maadhimisho Siku ya Kimataifa ya Wanawake ambayo huadhimishwa kila mwaka Machi 08.

Ameongeza kuwa, Mkoa wa Simiyu una lengo la kutoa hati 3,000 kwa mwaka 2025/2026 ambapo hadi sasa wametoa jumla ya hati 1,441 sawa na asilimia 48 ya lengo ambapo kati ya hati hizo 403 ni za wanawake sawa na asilimia 28 ya hati zote zilizotolewa katika mkoa huo.

Kwa upande wake Bi. Stela Manyonyi kutoka Wilaya ya Busega mkoani Simiyu ameahidi kuitumia hati aliyoipata katika shughuli za maendeleo kwa kuchukulia mkopo wa kuendeleza biashara zake.

Kaulimbiu ya maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake mwaka huu ya  inahimiza "Haki sawa kwa Wanawake na Wasichana; Msingi Jumuishi kifikia Dira 2050" huku Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi ikisisitiza kuwa “Mwanamke; Haki Yako, Miliki Ardhi Sasa’’.
Posted by MROKI On Wednesday, March 04, 2026 No comments
Makatibu Wakuu wa Vyama Rafiki vya Ukombozi Kusini mwa Afrika, wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, kwenye Kikao cha Bodi ya Wadhamini wa Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere (MJNLS), kilichoketi leo tarehe 4 Machi 2026, Kibaha, mkoani Pwani. 

Wajumbe wengine waliohudhuria kikao hicho ni; Katibu Mkuu wa Chama cha ANC (Afrika Kusini), Fikile Mbalula, Katibu Mkuu wa Chama cha FRELIMO (Msumbiji), Chakil Felizardo Passadas Aboobacar, Katibu Mkuu wa Chama cha ZANU-PF (Zimbabwe), Jacob Francis Nzwindamilimo Mudenda, Chama cha SWAPO (Namibia), kimewakilishwa na Mjumbe wa Kamati Kuu, Dkt. Samuel Abraham Peyavali Mushelenga na Chama cha MPLA (Angola) kimewakilishwa na Mjumbe wa Kamati Kuu, Frederico Toth Jorge De Miranda.






Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, (katikati), akiwa kwenye picha ya pamoja na  Katibu Mkuu wa Chama cha ANC (Afrika Kusini), Fikile Mbalula (kulia pichani) pia Katibu Mkuu wa Chama cha FRELIMO (Msumbiji), Chakil Felizardo Passadas Aboobacar (kushoto pichani), kabla ya kuanza Kikao cha Bodi ya Wadhamini wa Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere (MJNLS), kilichoketi leo tarehe 4 Machi 2026, Kibaha, mkoani Pwani. Wajumbe wa kikao hicho ni Makatibu wa Vyama Rafiki vya Ukombozi Kusini mwa Afrika. Vyama vingine ni SWAPO (Namibia), ZANU - PF (Zimbabwe) na MPLA (Angola).


Posted by MROKI On Wednesday, March 04, 2026 No comments
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Zuhura Yunus akielezea jambo wakati wa hafla ya uzinduzi wa mafunzo ya Uanagenzi awamu ya nane kwa mwaka 2025/2026 yanayofanyika Chuo cha Ufundi Don Bosco Dodoma Machi 3, 2026
Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Ajira na Ukuzaji Ujuzi Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Bi. Alana Nchimbi akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa mafunzo ya Uanagenzi awamu ya nane kwa mwaka 2025/2026 yanayofanyika Chuo cha Ufundi Don Bosco Dodoma Machi 3, 2026






Serikali imesema itaendelea kuratibu na kuimarisha Sera, Sheria na Miongozo inayosimamia programu za Mafunzo ya Uanagenzi na kuhamasisha sekta binafsi kushiriki kikamilifu katika kutoa nafasi za mafunzo kwa vitendo kwa wanagenzi nchini.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano Deus Sangu amesema hayo  leo Machi 03,2026 katika chuo cha ufundi stadi Daon Bosco jijini Dodoma wakati akifungua  Awamu ya Nane ya Mafunzo ya Stadi za Kazi kwa Njia ya Uanagenzi kwa Vijana 5,746 waliodahiliwa katika Vyuo 46 nchini kwa mwaka 2025/26 ambapo utekelezaji wa programu umewezesha jumla ya wanufaika 93,495 hadi kufikia Februari, 2026.

Waziri Sangu amesema mafunzo hayo yanachangia kwa kiasi kikubwa katika kuwapa vijana uzoefu wa kazi kwa nadharia na vitendo, kupunguza pengo la ujuzi kati ya mafunzo ya kitaaluma na mahitaji ya waajiri na kuongezeka kwa ajira kwa vijana kuajiriwa au kujiajiri.

“Hii ni dhamira ya dhati ya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kujenga nguvukazi yenye ushindani na tija kwa maendeleo endelevu ya Taifa.” amesema.

Aidha, amesisitiza kuwa kuelekea Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Tanzania inahitaji nguvukazi yenye ujuzi, weledi na uwezo wa kutumia teknolojia ili kuhimili ushindani wa kikanda na kimataifa, huku Serikali ikiendelea kuboresha sera, sheria na mifumo ya mafunzo kuongeza fursa za ajira kwa vijana.

Awali akitoa salamu za wananchi wa Dodoma, Mkuu wa Mkoa huo Rosemary Senyamule ameipongeza serikali kwa kuendelea kutenga bajeti maalum kwa ajili ya mafunzo ya uanagenzi hatua ambayo inaonyesha wazi kuwa serikali inawekeza katika rasilimali muhimu za taifa hususani Vijana.

Kwa upande wake Naibu Katibu, Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano Zuhura Yunus amesema Serikali kupitia Ofisi hiyo, inatekeleza Mafunzo ya Uanagenzi kupitia Programu ya Taifa ya Kukuza Ujuzi Nchini kuanzia mwaka 2016/17 na dhumuni la programu hiyo ni kukuza ujuzi wa nguvukazi iliyopo katika soko la ajira ili kuongeza tija kwenye uzalishaji wa bidhaa na utoaji wa huduma.

Naye, Mkuu wa Chuo cha Don Bosco Dodoma, Mhandisi Dkt. Justine Mulebya, ameshukuru Serikali kwa kukipatia chuo hicho wanafunzi 650 na ameiomba kuwawezesha vifaa wahitimu wa mafunzo ya uanagenzi ili kuwawezesha kujiajiri na kuajiri vijana wengine wakihitimu mafunzo yao.
Posted by MROKI On Wednesday, March 04, 2026 No comments

March 03, 2026




Na Mwandishi wetu, Dodoma
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amekutana na Mkurugenzi wa Go Plant Tanzania Bw. Emmanuel Likida kwa lengo la kujadili namna ya kushirikiana katika maandalizi ya Mjadala (Debate) wa Clean Cooking Solutions utakaowahusisha wanafunzi wa shule za Sekondari katika Halmashauri za Mkoa wa Dodoma. 

Katika kikao hicho, pande zote mbili zimejadili umuhimu wa kuwajengea vijana uelewa wa mapema kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia, athari za matumizi ya nishati zisizo safi kwa afya na mazingira, pamoja na fursa zilizopo katika ubunifu na ujasiriamali wa suluhisho za upishi safi.

Mjadala huo unatarajiwa kuwa jukwaa la kielimu na kimkakati la kukuza uelewa, kuchochea fikra bunifu, na kuibua mabalozi vijana wa Nishati Safi katika jamii.

Kikao hicho kimefanyika leo Machi 03,2026 katika Ofisi za Wizara ya Nishati zilizopo Mtumba, jijini Dodoma.
Posted by MROKI On Tuesday, March 03, 2026 No comments




Na Mwandishi wetu, Bagamoyo
Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Mhe. Subira Mgalu leo Machi 03, 2026 amekabidhi magari mapya kwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani kwa lengo la kuimarisha huduma kwa wateja na kuongeza ufanisi wa utendaji kazi katika kuwahudumia Wateja wilayani Bagamoyo.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika Ofisi ya TANESCO Bagamoyo, Mhe. Mgalu amesema kuwa hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za Serikali kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya umeme kwa wakati, kwa ubora na kwa uhakika zaidi.

“Magari haya yatawezesha mafundi na wahandisi wa TANESCO kuwafikia wananchi kwa haraka pale panapotokea hitilafu au changamoto za umeme. Tunataka kuona muda wa kushughulikia matatizo unapungua na huduma inaboreshwa,” amesema Mhe. Mgalu.

Amesisitiza kuwa, hivi sasa TANESCO imeimarika katika utoaji wa huduma ikiwa ni pamoja na kutoka katika kutengeneza hasara na linajiendesha bila kupata ruzuku kutoka Serikalini.

Aidha, amesema baada ya kukamilika bwawa la Julius Nyerere linalozalisha megawati 2115 na kupelekea Nchi kuwa na uwezo wa takribani wa megawati 4,000 huku mahitaji yakiwa takribani megawati 2,000 hivyo kuitaka TANESCO kuongeza kasi ya kuwaunganishia wateja.

Mkurugenzi wa TANESCO Kanda ya Mashariki,Mha. Kenneth Boymanda amesema  TANESCO inatekeleza miradi mingi ya maendeleo Wilaya ya Bagamoyo ikiwemo ya umeme Vijijini hivyo upatikanaji wa magari hayo kutarahisisha utekelezaji wa miradi hiyo.

“Bagamoyo tunao mpango mkubwa wa kuhakikisha kila nyumba inafikishiwa nishati ya  umeme nak ama Nchi mpaka mwaka 2030 kuunganisha nyumba milioni nane na laki tatu na nyumba Milioni Moja na Laki Saba kwa mwaka”, amesema Mha. Boymanda

Ameongeza kuwa, majukumu hayo yanahitaji uwepo wa vitendea kazi na kusisitiza kuwa TANESCO itafanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha malengo yaliyowekwa na Serikali kupitia mpango wa mission 300.

Serikali imeendelea kuweka mkazo katika kuboresha miundombinu ya umemme kama msingi wa maendeleo ya viwanda, biashara na ustawi wa jamii.

 Hatua ya TANESCO kununua magari hayo ni sehemu ya juhudi za kuimarisha huduma kwa wateja  na kuongeza ubora wa huduma kwa wananchi.
Posted by MROKI On Tuesday, March 03, 2026 No comments

 





Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi imesogeza karibu huduma za Sekta ya Ardhi kwa wanawake nchini nchini kupitia Kliniki ya Ardhi Maalumu "Samia Ardhi Kliniki"

Mkoa wa Simiyu ni miongoni mwa mikoa ambayo Kliniki hiyo inaendeshwa ambapo inatarajiwa kuzinduliwa rasmi Machi 4, 2026 na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anamringi Macha katika Viwanja vya Sabasaba vilivyopo katika mji wa Bariadi.

Katika kufanikisha Kliniki hiyo, Wizara na Ofisi ya Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Simiyu inashirikiana na team ya wataalamu wa Sheria kutoka Mama Samia Legal Aid kutoa huduma za Sekta ya Ardhi ikiwemo upimaji wa ardhi, utoaji wa Hati Miliki, uhamishaji wa umiliki, uthamini wa ardhi, kusikiliza changamoto mbalimbbali za sekta ya ardhi na kutoa ushauri wa kitaalamu kuhusu matumizi bora ya ardhi.

Kliniki hiyo inalenga kutoa huduma za ardhi kwa wanawake nchi nzima kuelekea Siku wa Kimataifa ya Wanawake kuanzia tarehe 2 hadi 7 Machi 2026 ikiongozwa na Kaulimbiu "Haki sawa kwa Wanawake na Wasichana; Msingi Jumuishi kifikia Dira 2050"
Posted by MROKI On Tuesday, March 03, 2026 No comments

March 02, 2026


WAZIRI MKUU Dkt Mwigulu Nchemba amepokea kero na hoja mbalimbali 305 kutoka kwa wananchi wa Wilaya ya Mbulu akiwa kwenye mkutano wa hadhara ambao ni wa mwisho katika ziara ya kikazi ya siku tatu ya Mkoa wa Manyara.

Akizungumza na wananchi na viongozi mbalimbali leo jioni (Jumatatu, Machi 2, 2026) katika uwanja wa mpira wa Mbulu Mjini, Waziri Mkuu amesema anataka kuona utaratibu wa kulundika kero za wananchi unaisha mara moja. 

“Kila mtu aliyeko ofisini anapaswa ajishughulishe na mambo yanayowahusu wananchi. Ninaandaa utaratibu, kila mwisho wa mwezi kila mtu atapaswa kutoa taarifa ametatua kero ipi na ipi imeshindikana kuanzia kijiji na mtaa, kata, tarafa, wilaya hadi mkoa. Tutafuatilia utekelezaji wake,” amesema. 

Dkt. Mwiguliu amesisitiza kuwa hilo siyo la suala la ziara tu bali anataka wananchi wakifika kwenye ofisi za viongozi wapewe vitabu vya wageni na waandike hoja zao ili iwe rahisi kufuatilia utekelezaji wake.

Amesema kuwa mambo ya kupuuza na kuzoea shida za wananchi siyo makusudi ya kuanzishwa kwa ofisi za umma. “Tunataka watumishi wajihusishe na matatizo ya wananchi. Tulianzisha ofisi siyo kwa ajili ya kugawana madaraka, bali watafute ufumbuzi wa matatizo ya wananchi. Tunataka mambo ambayo yanaweza kufika ukomo yaishe,” amesisitiza.

Akiwa njiani kuelekea Mbulu mjini, Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba alikagua ujenzi wa barabara ya km 25 kutoka Mbulu hadi Garbabi ambayo ni sehemu ya barabara kuu inayojengwa kwa kiwango cha lami kutoka Karatu – Mbulu – Haydom – Sibiti River – Lalago – Maswa yenye urefu wa km 389.

Utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 41.7 ambapo sh. bilioni 36.3 zitatumika kukamilisha ujenzi. Hadi sasa, sh. bilioni 12.5 tayari zimeshalipwa.

Mradi huo unaotekelezwa na Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) unalenga kuboresha mawasiliano ya barabara, kuimarisha usafirishaji wa watu na bidhaa, na kuchochea ukuaji wa uchumi katika maeneo husika.

Mapema, Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga alisema kwa mara ya kwanza wameandika historia ya kushika namba mbili kitaifa kwenye matokeo ya kidato cha nne ya mwaka jana. “Hii ni historia, haijapata kutokea,” alisema. 

“Huu si muujiza bali ni majibu ya jitihada za Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwekeza katika elimu kwa kujenga shule za msingi na sekondari, madarasa mapya na mabweni ili kupunguza umbali kwa watoto hasa wanaotoka kwenye jamii za wafugaji,” alisema.
Posted by MROKI On Monday, March 02, 2026 No comments







WAZIRI MKUU Dkt Mwigulu Nchemba amewaomba Wabunge wa Mbulu na uongozi wa wilaya hiyo waendelee kutoa elimu kwa wananchi juu ya kuendeleza amani na kuishi kindugu.

Ametoa wito huo leo (Jumatatu, Machi 2, 2026) wakati akizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye hospitali ya Lutheran ya Haydom, wilayani Mbulu, mkoani Manyara mara baada ya kukagua ujenzi wa jengo la afya ya mama na mtoto.

“Nimepata taarifa ya kuwepo kwa mizozo kule Yaeda Chini. Waheshimiwa Wabunge wa majimbo haya mawili na viongozi wa Halmashauri kaeni na wananchi muwaelimishe kuwa ardhi haiongezeki. Kaeni na wananchi muwaeleze kuwa suluhisho ni kupanga matumizi bora ya ardhi.”

“Endeleeni kuwaelimisha wananchi kuwa hata wakipigana ardhi haiongezeki. Hata mkiwaondoa kabila fulani, bado ardhi haiongezeki kwa sababu watu wanaendelea kuzaa.”

Akizungumzia kuhusu ujenzi wa jengo hilo, Waziri Mkuu amesifu kazi nzuri iliyofanywa na akamshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya hospitali zinazoendeshwa na taasisi za dini ili kuboresha utoaji huduma kwenye hospitali hizo. 

“Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan alielekeza taasisi zinazotoa huduma kwa jamii (charitable organisations) zipewe nafuu ya kikodi. Hii ni kwa sababu hizi taasisi hazifanyi biashara na serikali inatambua mchango mkubwa unaofanywa na hizo taasisi,” amesema. 

Akitoa maelezo kuhusu fedha zinazotolewa na serikali kwenye hospitali hiyo, Naibu Waziri – OWM-TAMISEMI (Elimu), Reuben Kwagilwa alisema kumekuwa na ushirikiano wa mrefua ambapo kila mwezi, Serikali imekuwa ikilipa sh. milioni 188 kwa ajili ya watumishi 128 wa hospitali hiyo.

“Serikali pia imekuwa ikitoa ruzuku ya sh. milioni 545 kila mwaka ambazo hupitia MSD kwa ajili ya ununuzi wa dawa na vifaa tiba. Vilevile, imekuwa ikitoa sh. milioni 57 kila mwaka kwa ajili ya uendeshaji wa hospitali,” amesema.

Mapema, Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Mbulu, Askofu John Nade alimweleza Waziri Mkuu kwamba wanashukuru kwa ushirikiano uliopo baina ya Serikali na kanisa kwenye utoaji wa huduma za jamii.

Alisema mbali na hospitali, wana Taasisi ya Afya ya Haydom ambayo inatoa mafunzo kwenye kozi tano ambazo ni Radiolojia, Famasia, Afisa Tabibu, Maabara na Uuguzi.

Akitoa taarifa ya ujenzi wa mradi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Haydom, Dkt. Paschal Mdoe alisema ujenzi wa jengo hilo umegharimu sh. bilioni 6.3 ambazo zimetokana na vyanzo vya ndani na marafiki wa Haydom Norway.

Alisema hospitali hiyo ya Kanisa imekuwa mdau mkubwa na wa muda mrefu katika sekta ya afya, ikitoa huduma za rufaa na kibingwa kwa wananchi wa Mkoa wa Manyara na mikoa jirani, pamoja na kushirikiana na Serikali katika kuboresha huduma za afya ya jamii.
Posted by MROKI On Monday, March 02, 2026 No comments
Na Mwandishi wetu, Kilimanjaro
MKAKATI wa uongezaji thamani katika Sekta ya Madini umeanza kuzaa matunda mkoani Kilimanjaro, baada ya kampuni ya Mega Copper Co Ltd kujikita katika uongezaji wa kiwango cha ubora wa madini ya shaba kutoka asilimia moja hadi kufikia kati ya asilimia 20 na 25.

Akizungumza katika kijiji cha Kiruru, wilayani Mwanga, Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Ally Ng’anzo, amesema maboresho hayo yameongeza ushindani wa kampuni katika soko la kimataifa, huku China ikiwa soko kuu la sasa la mauzo ya madini hayo.

Amesema pamoja na kampuni kufikia hatua hiyo ya uongezaji thamani ili kuzalisha makinikia ya shaba, matarajio yao ni kufanya uwekezaji zaidi kwa kufunga mitambo maalum ya uongezaji thamani, ili kufikia ubora wa hadi asilimia 99. Hatua hiyo inatarajiwa kuongeza thamani ya bidhaa hiyo, kupanua wigo wa masoko na kuimarisha upatikanaji wa malighafi ya kutengeneza bidhaa za shaba kwa viwanda vya ndani.

Kwa mujibu wa Ng’anzo, kampuni hiyo ina wafanyakazi 65, wakiwemo 20 wa kiwandani na 45 wa migodini, hali inayochangia ajira kwa vijana wa Mwanga na maeneo ya jirani, sambamba na kukuza uchumi wa jamii inayozunguka mgodi huo.

Kwa upande wake, Kaimu Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhandisi Abel Madaha, amesema mgodi huo unaomilikiwa kwa asilimia 100 na Watanzania umeendelea kuwa chanzo muhimu cha mapato, ukichangia  zaidi ya Shilingi milioni 500 katika kipindi cha miaka miwili iliyopita kupitia tozo ya mrabaha pekee.

Amesisitiza kuwa mgodi huo ni mfano halisi wa utekelezaji wa sera ya Serikali ya kuhimiza uongezaji thamani wa madini kabla ya kusafirishwa nje ya nchi, hatua inayolenga kuongeza mapato ya taifa, ajira na uhamishaji wa teknolojia.

Mhandisi Madaha amewahimiza wawekezaji wengine kutumia fursa zilizopo mkoani humo, akieleza kuwa Kilimanjaro ina rasilimali za madini ya metali na viwandani ambazo bado hazijaendelezwa kikamilifu.

“Ofisi ya Madini itaendelea kutoa ushirikiano kwa wawekezaji wote ili kuhakikisha Sekta ya Madini inakua kwa kasi na kuchangia ipasavyo maendeleo ya mkoa na taifa kwa ujumla,” amesema.



Posted by MROKI On Monday, March 02, 2026 No comments
Mwanasheria Mkuu na Waziri wa Katiba wa Ghana Dominic Akuritinga Ayine akipokea Tuzo kwa niaba ya Rais John Mahama wa Ghana
Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete akikabidhi Tuzo kwa Waziri Mkuu wa Lesotho, Samuel Matekane
Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia  wakati wa Hafla hiyo ya kukabidhi Tuzo kwa Viongozi Bora wa Mwaka wa Afrika kwa Mwaka 2026.
********
Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amekabidhi Tuzo za Viongozi Bora barani Afrika kwa Mwaka 2026 katika Hafla iliyofanyika Accra, Ghana tarehe 28 Februari 2026.

Tuzo hizo zinatolewa na Jarida la Africa Leadership Magazine linaloandaliwa na Taasisi ya Uongozi Afrika (Africa Leadership Organisation) ambayo Rais Mstaafu Dkt. Kikwete ni Mwenyekiti wa Bodi yake ya Ushauri.

Mshindi wa Jumla wa Tuzo hizo ni Rais John Dramani Mahama wa Ghana, ambaye ametunukiwa Tuzo ya Mwafrika wa Mwaka kwa Mwaka 2026 kwa kutambua mchango wake katika kukuza demokrasia na uchumi nchini Ghana pamoja na kuwa kinara katika kuimarisha utengamano wa kikanda kupitia Eneo Huru la Biashara Afrika (AfCFTA).

Akihutubia kabla ya kukabidhi Tuzo hiyo ya mshindi wa jumla, Rais Mstaafu Dkt. Kikwete ameeleza kuwa "kila kizazi za uongozi hukutana na changamoto za kipekee za wakati wake na hivyo hulazimika kubuni njia za kipekee za kuzitatua". Akaongeza kuwa "kipimo mojawapo cha mafanikio katika uongozi ni kuweza kukuza kipato cha mtu mmoja mmoja na kuboresha hali ya jumla ya kimaisha kwa watu unaowaongoza kutoka hali ya chini kwenda hali ya juu zaidi".

Mbali na Rais Mahama, miongoni mwa watu mashuhuri waliiopata Tuzo hizo ni pamoja na Waziri Mkuu wa Ufalme wa Lesotho, Samuel Matekane aliyepata tuzo kwa kutambua mchango wake katika kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na Sekta Binafsi nchini Lesotho pamoja na Mkuu wa Majeshi wa Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba aliyepata tuzo kwa kutambua mchango wake katika kuliimarisha jeshi la Uganda na kukuza diplomasia ya kijeshi katika ukanda wa maziwa makuu.

Rais wa Namibia Netumbo Nandi-Ndaitwah alipata Tuzo ya Kiongozi Bora wa Kisiasa Afrika huku Makamu wa Rais wa Angola Esperança da Costa, Makamu wa Rais wa Angola akioata Tuzo ya Kiongozi Bora Mwanamke barani Afrika.

Tuzo ya Rais Mahama ilipokelewa kwa niaba yake na Mwanasheria Mkuu wa Ghana, ambaye pia ni Waziri wa Sheria wa Ghana, Dominic Akuritinga Ayine wakati tuzo ya Jenerali Kainerugaba ilipokelewa na Msemaji wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Uganda, Kanali Chris Magezi.

Kila mwaka Jarida la Africa Leadership Magazine huratibu mchakato wa wazi unaojumuisha kupokea mapendekezo ya viongozi mbalimbali wenye sifa ambao hupigiwa kura kwa njia ya mtandao ili kupata washindi. 

Viongozi wa tasnia mbalimbali zikiwemo uongozi wa kisiasa, diplomasia, biashara na uwekezaji, ujasiriamali, habari, ulinzi na usalama, nk., wanaoshinda hupokea Tuzo hizo kwa kutambua mchango wao katika kusimamia vizuri tasnia zao pamoja na kulea na kuwaandaa vijana wanaowaongoza ili kuja kuwa viongozi bora wa baadaye.

Katika hafla hiyo, jumla ya Tuzo 36 zilitolewa.

Jarida la Africa Leadership Magazine linaloandaliwa na Taasisi ya Uongozi Afrika (Africa Leadership Organisation) ambayo Rais Mstaafu Dkt. Kikwete ni Mwenyekiti wa Bodi yake ya Ushauri.

Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete akisalimiana na mwigizaji maarufu wa kimataifa wa Ghana Bw. Moses Nyarko aliyeshiriki katika Hafla hiyo ya utoaji wa Tuzo kwa Viongozi Bora barani Afrika kwa Mwaka 2026.
Kanali Chris Magezi, Msemaji wa Jeshi la Wananchi la Uganda akipokea Tuzo kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi wa Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba
Posted by MROKI On Monday, March 02, 2026 No comments

March 01, 2026

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo tarehe 1 Machi, 2026 akiweka jiwe la msingi la uzinduzi wa stendi ya mabasi iitwayo Dkt. Samia Suluhu Hassan iliyopo Kateshi mkoani Manyara. Mradi huo umegharimu kiasi cha Shilingi Bilion 5.69 hadi kukamilika kwake. 
 
Muonekano mradi wa stendi ya mabasi iitwayo Dkt. Samia Suluhu Hassan iliyopo Kateshi mkoani Manyara ambayo imezinduliwa leo tarehe 1 Machi, 2026. Mradi huo umegharimu kiasi cha Shilingi Bilion 5.69 hadi kukamilika kwake.


WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amezindua Stendi ya Mabasi ya Dkt. Samia Suluhu Hassan iliyopo Katesh, wilayani Hanang, mkoani Manyara ambayo imejengwa kwa gharama ya sh. bilioni 5.69.

Stendi hiyo ambayo ujenzi wake umekamilika na imeanza kutumika, imelenga kuboresha utoaji huduma za usafiri na usafirishaji. Miundombinu iliyopo ni pamoja na jengo kuu la kituo cha mabasi, maduka 116, maeneo ya wauza vyakula, vyoo matundu 21, vituo saba vya kukusanyia taka na vituo viwili vya ukaguzi na ulinzi. Hakuna kituo cha polisi. 

Akizungumza na wakazi wa Hanang waliofika kushuhudia uzinduzi huo leo (Jumapili, Machi Mosi, 2026), Waziri Mkuu amesema ameridhishwa na ujenzi wa stendi hiyo ambao ni sehemu ya miradi ya kimkakati ya kuboresha miundombinu ya usafiri na kuongeza mapato ya ndani.

Dkt. Mwigulu ametumia fursa hiyo kumwagiza Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya awasiliane na Waziri wa Ujenzi na Mtendaji Mkuu wa TANROADS ili watafute fedha za kuitengeneza barabara ya Katesh – Babati kutokana na uchakavu ilionao.

Amesema barabara za wilayani za mkoa wa Manyara ziangaliwe na kujengwa haraka kwani mkoa wa Manyara ni miongoni mwa mikoa ambayo haina barabara za lami za wilaya. “Ukiondoa barabara kuu ya Arusha - Dodoma na hii ya Babati – Singida kupitia Katesh, hawana barabara nyingine.”

Kuhusu tabia ya kuwanyang'anya wajasiriamali zana zao za kazi, Waziri Mkuu amekemea tabia hiyo na kuwataka watendaji wanaofanya hivyo waache mara moja. “Acheni watu wafanye kazi, bakuli, sahani, bajaji au pikipiki ni vitendea kazi vyao. Msikamate vitendea kazi vyao,” amesisitiza.

“Tusichukue bidhaa za watu, tusitupe bidhaa za watu hiyo ni mitaji yao. Tuna kazi kubwa ya kutekeleza Dira 2050, tunahitaji fedha nyingi kutekeleza miradi iliyopo. Msichukue bidhaa zao, kama kuna jambo tuongee nao, tuwaeleweshe,” amesisitiza.


Kuhusu kesi zilizoko mahakamani au zilizotolewa maamuzi na mahakama, Waziri Mkuu amewataka wananchi wafuate taratibu za kisheria kwa vile Serikali ni mhimili mwingine na unaheshimu maamuzi yanayotolewa na na mhimili wa mahakama. Amesema maamuzi ya kimahakama hayabatilishwi na matamko ya viongozi kama Makamu wa Rais, Waziri Mkuu au Mkuu wa Mkoa.

“Jambo likishaenda mahakamani Mkuu wa Mkoa wala Waziri Mkuu hawawezi kuweka neno hapo. Sisi ni lazima tuheshimu utaratibu wa kisheria. Kama mwananchi hajaridhika na maamuzi ya awali, ipo njia. Ipo milango ya kufuata, lakini sisi hatuwezi kuingilia maamuzi ya mhimili wa sheria,” amesisitiza.

Waziri Mkuu ambaye amekuwa akisikiliza kero za wananchi kwenye mikutano yake ya hadhara, leo kwenye mkutano huo amepokea hoja nyingi zilizohusu kesi za madai na mirathi, migogoro ya ardhi, familia kudhulumiana na mipaka ya mashamba.
Posted by MROKI On Sunday, March 01, 2026 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo