Nafasi Ya Matangazo

June 05, 2026





Na Mwandishi Wetu, Dodoma
WIZARA ya Madini imevuka lengo la ukusanyaji wa Maduhuli ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 baada ya kukusanya Sh trilioni 1.27 hadi Juni 5, 2026, dhidi ya lengo la Sh trilioni 1.2, huku ikitarajia kufikia Sh trilioni 1.3 ifikapo  Juni 30, 2026.

Kutokana na mafanikio hayo, watumishi wa Wizara hiyo na taasisi zake wametakiwa kuondokana na uzembe, kuongeza bidii na kufanya kazi kwa weledi ili kufikia lengo jipya la ukusanyaji wa Sh trilioni 1.4 lililowekwa kwa mwaka wa fedha 2026/2027.

Akizungumza katika kikao cha watumishi wote wa Wizara ya Madini na taasisi zake ambazo ni GST, TEITI, Tume ya Madini, STAMICO na TGC, Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Eng. Yahya Samamba, amesema mafanikio yaliyopatikana yanapaswa kuwa chachu ya kuongeza juhudi katika usimamizi wa Sekta ya Madini kwa kuzingatia Sera, miongozo, kanuni na Sheria zilizowekwa.

Amesema watumishi wanapaswa kutambua kuwa wanapowahudumia wananchi wanatekeleza wajibu wenye thamani kubwa kwa taifa, hivyo wanapaswa kuwahudumia watu wote kwa usawa bila kujali itikadi, dini wala uraia wao.

“Wachache tuliokabidhiwa jukumu la kuhudumia sekta ya madini tunapaswa kuhakikisha watu wote wanahudumiwa kwa haki na uzalendo mkubwa ili kuendelea kujenga taifa letu,” amesema.

Amesema watumishi ndiyo injini ya Serikali katika sekta ya madini na kwamba mchango wao una nafasi muhimu katika kukuza uchumi wa nchi kupitia usimamizi bora wa rasilimali madini.

“Wito wangu ni kufanya kazi kwa bidii, weledi na kusimamia sera, miongozo, kanuni na sheria zilizowekwa ili sekta hii iendelee kutoa mchango mkubwa kwa maendeleo ya taifa,” amesema.

Katibu Mkuu huyo amesema watumishi wanapaswa kujiepusha na vitendo vya rushwa, uvivu na uzembe ambavyo vinaweza kuharibu imani ya wananchi kwa wizara, taasisi zake na Serikali kwa ujumla.

“Tusiharibu imani ya wananchi kwa rushwa, uvivu na uzembe. Mtu mmoja anayepokea rushwa anaweza kuchafua kazi za watumishi wengi waadilifu. Tufanye kazi kwa uzalendo mkubwa ili kuhakikisha hakuna mtu au wachache miongoni mwetu wanaochafua taswira ya wizara, taasisi zetu na Serikali kwa ujumla,” amesema.

Amesema watumishi wanapaswa kuchagua kuwa mwangaza badala ya kuwa kivuli na kuendelea kuimarisha ushirikiano baina ya wizara na taasisi zake kwa kuwa wote ni timu moja yenye malengo yanayofanana.

“Kazi ya mwenzako ikichelewa, mafanikio yako pia yanachelewa. GST ikichelewa kutekeleza majukumu yake, Tume ya Madini nayo itaathirika. Tusaidiane kwa pamoja kufikia malengo yetu,” amesema.

Katika salamu za Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, watumishi wamepongezwa kwa kuvuka lengo la ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Aidha, imeelezwa kuwa kwa mwaka wa fedha 2026/2027, Wizara ya Madini kupitia Tume ya Madini imepangiwa kukusanya Sh trilioni 1.4, lengo ambalo linahitaji watumishi kuongeza uwajibikaji, uadilifu na weledi katika utekelezaji wa majukumu yao.
Posted by MROKI On Friday, June 05, 2026 No comments











Na, mwandishi wetu – Mwanza
SERIKALI imezindua rasmi Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura cha Mkoa wa Mwanza, hatua inayolenga kuimarisha uratibu wa shughuli za usimamizi wa maafa na majanga katika mkoa huo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo leo tarehe 05 Juni, 2026, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mheshimiwa Said Mtanda, amesema kituo hicho ni nyenzo muhimu katika kufuatilia na kudhibiti matukio ya dharura kwa ufanisi zaidi. 

Amesema kupitia kituo hicho, mkoa unaweza kufuatilia matukio ya dharura kwa karibu, kukusanya na kuchambua taarifa kwa wakati pamoja na kuimarisha mawasiliano kati ya wadau mbalimbali wa usimamizi wa maafa.

“Kupitia kituo hiki, taarifa muhimu zinafika kwa mamlaka husika kwa haraka ili kuwezesha maamuzi stahiki kufanyika kwa wakati,” anasema Mhe.Mtanda.

Ameongeza kuwa kituo hicho kinaunganishwa moja kwa moja na Kituo cha Taifa cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura, hatua inayorahisisha mtiririko wa taarifa na kuimarisha uratibu wa shughuli za kukabiliana na maafa kati ya ngazi ya mkoa na taifa.

Kwa mujibu wa Mhe. Mtanda, hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za serikali kujenga mfumo jumuishi wa usimamizi wa maafa wenye uwezo wa kutoa mwitikio wa haraka na wenye ufanisi katika kukabiliana na majanga.

Aidha, amewataka watumishi na viongozi kutumia mafunzo wanayopata kujenga uelewa, kubadilishana uzoefu na kuimarisha mshikamano wa kiutendaji ili kuboresha zaidi usimamizi wa maafa katika Mkoa wa Mwanza.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Brigedia Jenerali Hosea Ndagala, amesema kituo hicho kina umuhimu mkubwa kwa mkoa wa Mwanza na taifa kwa ujumla.

Amesema kituo hicho kinakuwa kitovu cha ukusanyaji, uchambuzi na usambazaji wa taarifa za matukio ya dharura na maafa, ambapo kinaunganishwa moja kwa moja na Kituo cha Taifa cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura, hivyo kuwezesha upatikanaji wa taarifa kwa wakati na kufanya maamuzi ya haraka na sahihi.

“Kupitia kituo hiki, Serikali inaweza kufuatilia vihatarishi mbalimbali, kutoa tahadhari za mapema, kuratibu rasilimali za kukabiliana na maafa na kuimarisha mawasiliano kati ya wadau wote wanaohusika na usimamizi wa maafa,”alisema.

Ameongeza kuwa, “Huu ni uwekezaji muhimu katika kuimarisha utayari wa mkoa na taifa kwa ujumla. Sambamba na hilo, timu ya mkoa ya kukabiliana na dharura tunayoizindua leo ndiyo nguzo kuu ya kukabiliana na matukio ya maafa kwa wakati.”

Vilevile amesema uzinduzi wa kituo hicho unakuja katika wakati muafaka ambapo serikali inaendelea kujiandaa na kuimarisha mifumo ya tahadhari ya mapema kufuatia taarifa kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania kuhusu uwezekano wa kutokea kwa hali mbaya ya hewa, ikiwemo athari zinazoweza kusababishwa na El Niño.
Posted by MROKI On Friday, June 05, 2026 No comments

Dodoma
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ametembelea banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika kilele cha Maonesho ya Siku ya Mazingira Duniani 2026 yanayofanyika jijini Dodoma. 

Mhe. Balozi Dkt. Nchimbi ametembelea banda la REA leo Juni 5, 2026 ambapo ameelezwa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Wakala maeneo ya Vijijini na Mkurugenzi wa Nishati Jadidifu na Teknolojia Mbadala Mha. Advera Mwijage.

Halikadhalika, Mha. Mwijage amemueleza Mhe. Balozi Dkt. Nchimbi kuwa, kupitia miradi inayotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imesaidia kupunguza athari za uharibifu na uchafuzi wa mazingira.

Maonesho ya mwaka huu yamepambwa na kauli mbiu isemayo: Dira 2050: Tuwajibike Kukijanisha Tanzania
Posted by MROKI On Friday, June 05, 2026 No comments
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb), akijibu swali la Mbunge wa Ilemela, Mhe. Tinnar Andrew Chenge, aliyetaka kujua, kigezo kinachotumiwa na Serikali katika kutoza Kodi ya Majengo kupitia Mfumo wa Mita za Luku, bungeni jijini Dodoma.
*************
Na. Jordan Mbwambo, WF, Dodoma
Serikali imefafanua vigezo vinavyotumika katika utozaji wa Kodi ya Majengo (Property Tax) kupitia Mfumo wa Mita za Umeme za LUKU, hatua inayolenga kurahisisha ukusanyaji wa kodi na kuongeza ufanisi katika usimamizi wa mapato ya ndani.

Hayo yameelezwa bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Tinnar Andrew Chenge, aliyetaka kujua kigezo kinachotumiwa na Serikali katika kutoza Kodi ya Majengo kupitia Mfumo wa Mita za LUKU.

“Kwa sasa Serikali inatumia viwango mfuto katika kutoza kodi ya majengo kupitia mita za umeme za LUKU. Vigezo vinavyotumika kutoza kodi ya majengo kupitia LUKU ni nyumba ya kawaida ambayo inatozwa shilingi 18,000 kwa mwaka au shilingi 1,500 kwa mwezi na nyumba ya ghorofa ambayo inatozwa shilingi 90,000 kwa kila sakafu kwa mwaka au shilingi 7,500 kwa kila sakafu kwa mwezi,” alisema Mhe. Luswetula.

Aidha, alisema kuwa nyumba za nyasi, udongo, majengo ya huduma za jamii, ibada pamoja na nyumba zinazoishi wazee wenye umri wa miaka 60 na kuendelea hazitozwi Kodi ya Majengo isipokuwa pale majengo hayo yanapotumika kwa shughuli za biashara.

Mhe. Luswetula alisema kuwa utaratibu huo unalenga kuhakikisha mfumo wa utozaji kodi unaendelea kuwa rahisi, wenye ufanisi na unaozingatia makundi maalum yanayostahili msamaha kwa mujibu wa sheria.
Posted by MROKI On Friday, June 05, 2026 No comments
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akisikiliza maelezo kutoka kwa Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Manyinga ya Mvomero, Morogoro, Jackline Eliabi kuhusu utumiaji wa taka katika kutengeneza bidhaa mbadala, wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete mkoani Dodoma, leo tarehe 05 Juni 2026.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akisikiliza maelezo kutoka kwa Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Manyinga ya Mvomero, Morogoro, Jackline Eliabi kuhusu utumiaji wa taka katika kutengeneza bidhaa mbadala, wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete mkoani Dodoma, leo tarehe 05 Juni 2026.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akisikiliza maelezo kutoka kwa Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Dumila Juu ya mkoani Morogoro, Alhad Yusuph kuhusu matumizi ya michezo katika kuhamasisha utunzaji mazingira, wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete mkoani Dodoma, leo tarehe 05 Juni 2026.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akitembelea na kukagua mabanda mbalimbali ya maonesho kuhusu shughuli za uhifadhi mazingira, wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete mkoani Dodoma, leo tarehe 05 Juni 2026.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akitembelea na kukagua mabanda mbalimbali ya maonesho kuhusu shughuli za uhifadhi mazingira, wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete mkoani Dodoma, leo tarehe 05 Juni 2026.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akitembelea na kukagua mabanda mbalimbali ya maonesho kuhusu shughuli za uhifadhi mazingira, wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete mkoani Dodoma, leo tarehe 05 Juni 2026.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akiwa na viongozi mbalimbali wakiwa katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete wakishiriki Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani tarehe 05 Juni 2026.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akiwasili katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete Mkoani Dodoma kushiriki Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, leo tarehe 05 Juni 2026.

Posted by MROKI On Friday, June 05, 2026 No comments
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Asha-Rose Migiro, leo Ijumaa Juni 5,2026 amefanya mazungumzo na Mheshimiwa Marianne Young, Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, katika Makao Makuu ya CCM, Dodoma.

Mazungumzo hayo yalihusu maeneo ya ushirikiano wa maendeleo kati ya Tanzania na Uingereza, kwa kuzingatia vipaumbele vilivyobainishwa katika Ilani ya CCM ya Uchaguzi ya mwaka 2025–2030, Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 pamoja na Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs).

Viongozi hao walijadili fursa za kuendeleza ushirikiano kwenye maendeleo ya kijamii na kiuchumi, hususan katika kuwawezesha vijana na wanawake kupitia elimu, ujuzi, ubunifu na uwekezaji.

CCM inaendelea kuthamini ushirikiano wa kimataifa unaochangia maendeleo endelevu na ustawi wa wananchi wa Tanzania.







Posted by MROKI On Friday, June 05, 2026 No comments



Namtumbo, Ruvuma-
Mradi wa Urani wa Mto Mkuju uliopo Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma unatarajiwa kuifanya Tanzania kuwa miongoni mwa wazalishaji wakubwa wa madini ya urani duniani, huku ukikadiriwa kuchangia takribani asilimia 4 ya uzalishaji wa urani duniani mara utakapofikia hatua ya uzalishaji.

Akizungumza kuhusu maendeleo ya mradi huo mapema wiki hii, Meneja wa Mradi wa Mto Mkuju, Beria Vorster, alisema maandalizi ya utekelezaji wa mradi yanaendelea kwa kasi na kwamba mradi huo una umuhimu mkubwa katika kukidhi mahitaji ya nishati safi duniani.

“Mradi wa Mto Mkuju ni miongoni mwa miradi mikubwa ya urani barani Afrika. Uzalishaji utakapoanza, unatarajiwa kuchangia takribani asilimia 4 ya uzalishaji wa urani duniani, jambo ambalo litaiweka Tanzania katika nafasi muhimu kwenye soko la kimataifa la madini hayo,” alisema Vorster.

Kwa mujibu wa Shirika la World Nuclear Association (WNA), mwaka 2024 uzalishaji wa urani duniani uliongozwa na Kazakhstan kwa asilimia 39, ikifuatiwa na Canada kwa asilimia 24 na Namibia kwa asilimia 12. Uzbekistan ilichangia takribani asilimia 7, huku Urusi ikichangia kati ya asilimia 4 hadi 5 ya uzalishaji wa dunia. Hivyo, makadirio ya Mradi wa Mto Mkuju kuchangia asilimia 4 ya uzalishaji wa urani duniani yanaweza kuiweka Tanzania miongoni mwa nchi 10 zinazoongoza kwa uzalishaji wa urani duniani mara mradi huo utakapoanza uzalishaji wa kibiashara.

Alifafanua kuwa urani itakayozalishwa nchini Tanzania haitahusishwa kwa namna yoyote na utengenezaji wa silaha za nyuklia, bali itatumika kuzalisha nishati safi inayotumika katika vituo vya kuzalisha umeme wa nyuklia duniani.

Vorster alisema Tanzania ni mwanachama wa Mkataba wa Kuzuia Uenezaji wa Silaha za Nyuklia (Treaty on the Non-Proliferation of Nuclear Weapons - NPT), hali inayoweka misingi madhubuti ya kuhakikisha matumizi ya madini ya urani yanazingatia malengo ya amani na maendeleo endelevu.

“Urani kutoka Tanzania itatumika katika uzalishaji wa nishati safi na salama. Serikali ya Tanzania pamoja na taasisi za kimataifa zina mifumo madhubuti ya usimamizi na ufuatiliaji kuhakikisha madini haya yanatumika kwa madhumuni yaliyokusudiwa pekee,” alisisitiza Vorster.

Aliongeza kuwa katika kipindi ambacho dunia inaelekea kwenye matumizi ya nishati zenye kiwango kidogo cha uzalishaji wa hewa ukaa, nishati ya nyuklia imeendelea kupewa kipaumbele kama sehemu ya suluhisho la changamoto za mabadiliko ya tabianchi na mahitaji ya umeme yanayoongezeka.

Akizungumzia manufaa ya mradi huo kwa wananchi, Meneja wa Mradi wa Mto Mkuju, Beria Vorster, alisema mradi unatarajiwa kuzalisha zaidi ya ajira 1,000 za moja kwa moja pindi utakapoanza shughuli zake za uzalishaji kwa kiwango kamili, sambamba na maelfu ya ajira zisizo za moja kwa moja kupitia utoaji wa huduma kwenye mradi.

Alisema Kampuni imeanza mapema kuandaa rasilimali watu kutoka maeneo yanayouzunguka mradi ili kuhakikisha wananchi wa eneo husika wanakuwa sehemu ya mafanikio ya mradi huo.

“Tayari vijana 100 kutoka vijiji vinavyozunguka mradi wameshapatiwa mafunzo ya uendeshaji wa mitambo mbalimbali inayotumika katika shughuli za uchimbaji na usindikaji wa madini. Kati yao, vijana 10 tayari wameajiriwa na mradi, na programu hii itaendelea ili kuandaa wataalamu zaidi watakaohitajika wakati wa utekelezaji kamili wa mradi,” alisema Vorster.

Aliongeza kuwa mkakati huo unalenga kuongeza ushiriki wa Watanzania katika shughuli za mradi na kuhakikisha ujuzi na teknolojia vinahamishiwa kwa wananchi wa maeneo husika.

Kwa upande wake, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Ruvuma, Eng. Alphonce Bikulamchi, alisema pamoja na ajira za moja kwa moja, mradi huo utafungua mamia ya fursa nyingine katika sekta za usafirishaji, huduma za chakula, biashara, ujenzi, malazi na huduma nyingine zinazohusiana na shughuli za uchimbaji madini.

“Mradi huu ni kichocheo kikubwa cha maendeleo ya Mkoa wa Ruvuma. Mbali na mapato yatakayopatikana kwa Serikali, wananchi watanufaika kupitia ajira, ongezeko la shughuli za kiuchumi na ukuaji wa biashara zinazozunguka mradi,” alisema Eng. Bikulamchi.

Kwa kuzingatia ukubwa wa akiba zake, mchango wake katika uzalishaji wa urani duniani, pamoja na fursa za ajira na uwekezaji zitakazozalishwa, Mradi wa Mto Mkuju unatajwa kuwa miongoni mwa miradi ya kimkakati inayoweza kuibadilisha Tanzania kuwa kitovu muhimu cha uzalishaji wa madini ya urani kwa matumizi ya nishati safi duniani.
Posted by MROKI On Friday, June 05, 2026 No comments
Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba, akisalimia na Mbunge wa Isimani, Emmanuela Mtatifikolo Bungeni jijini Dodoma, Juni 5, 2026. Kulia ni Mbunge wa Iringa mjini Fadhili Ngajilo (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akizungumza na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza Johari, Bungeni jijini Dodoma, Juni 5, 2026. 

Posted by MROKI On Friday, June 05, 2026 No comments

June 04, 2026

 
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mheshimiwa Said Mtanda akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Kamati za Usimamizi wa Maafa kwa mkoa wake, yaliyoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu leo tarehe 4 Juni, 2026. (Picha na OWM)
Baadhi ya wajumbe wa Kamati za Usimamizi wa Maafa kwa mkoa wa Mwanza, wakifuatilia mada zilizowasilishwa wakati wa mafunzo ya Kamati hizo yaliyoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu tarehe 4 Juni, 2026.
Baadhi ya wajumbe wa Kamati za Usimamizi wa Maafa kwa mkoa wa Mwanza, wakifuatilia mada zilizowasilishwa wakati wa mafunzo ya Kamati hizo yaliyoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu tarehe 4 Juni, 2026.
Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Mwanza Bw. Henry Mwaijega akizungumza jambo wakati wa mafunzo ya Kamati za Usimamizi wa Maafa kwa ngazi ya mkoa yaliyoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu
Baadhi ya wajumbe wa Kamati za Usimamizi wa Maafa kwa mkoa wa Mwanza, wakifuatilia mada zilizowasilishwa wakati wa mafunzo ya Kamati hizo yaliyoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu tarehe 4 Juni, 2026.
Mratibu wa Maafa kutoka Idara ya Usimamizi wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) Bi. Numpe Mwambenja akiwasilisha mada kuhusu Nyenzo za Usimamizi wa Maafa wakati wa mafunzo ya Kamati za Usimamizi wa Maafa kwa mkoa wa Mwanza.Mafunzo yamefanyika tarehe 4 Juni, 2026.
Mratibu wa Maafa kutoka Idara ya Usimamizi wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) Bi. Dorothy Pantaleo akiwasilisha mada kuhusu Mfumo wa Usimamizi wa Maafa wakati wa mafunzo ya Kamati za Usimamizi wa Maafa kwa mkoa wa Mwanza.Mafunzo hayo yaliyoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu
Mratibu wa Maafa kutoka Idara ya Usimamizi wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) Bi. Wilfrida Ngowi akiwasilisha mada kuhusu Dhana ya Usimamizi wa Maafa wakati wa mafunzo ya Kamati za Usimamizi wa Maafa mkoa wa Mwanza, yaliyoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu.Mafunzo yamefanyika tarehe 4 Juni, 2026.

Na, mwandishi wetu - Mwanza
Mkoa wa Mwanza umetajwa kuwa Kinara kwa kuratibu na kusimamia ipasavyo shughuli za kukabiliana na maafa, majanga na mawasiliano ya dharura kutokana na hatua mbalimbali za kuimarisha mifumo ya utayari na mwitikio wa dharura.

Sifa hizo zimetolewa Juni 4, 2026 na wataalamu wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakati wa mafunzo ya Kamati za Usimamizi wa Maafa yanayofanyika mkoani Mwanza kwa siku mbili yakilenga kuongeza uwezo wa kukabiliana na majanga.

Akifungua mafunzo hayo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mheshimiwa Said Mtanda amesema maafa yameendelea kuwa tishio kubwa duniani kutokana na athari zake kwa maisha ya watu, uchumi na maendeleo ya jamii.

Ametaja baadhi ya majanga yanayoikabili Tanzania kuwa ni mafuriko, ukame, maporomoko ya ardhi, matetemeko ya ardhi, mioto ya misitu na magonjwa ya mlipuko.

Kutokana na kuongezeka kwa matukio hayo Mhe. Mtanda amezitaka Wilaya zote Mkoani humo kuwa na mipango kazi na mifumo imara ya usimamizi wa maafa ili kuhakikisha maandalizi, mwitikio wa haraka na urejeshaji wa hali unafanyika kwa ufanisi.

Aliongezea kuwa, Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu imeendelea kuimarisha usimamizi wa maafa kwa kutumia Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Maafa ya mwaka 2024 pamoja na Sheria ya Usimamizi wa Maafa Na. 6 ya mwaka 2022.

Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa mafunzo hayo yatawajengea uwezo viongozi na wataalamu katika utekelezaji wa sera, sheria na miongozo ya usimamizi wa maafa katika maeneo yao.

Aidha, ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa msaada kwa waathirika wa mafuriko Wilayani Kwimba, uliojumuisha tani tisa za mahindi, mablanketi, ndoo na vifaa vya wanafunzi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Usimamizi wa Maafa eneo la utafiti kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Bw. Vanvaco Luvanda amesema mafunzo hayo ya siku mbili yanaendelea kutolewa nchini kote kwa lengo la kuongeza utayari na uwezo wa kitaalamu wa kukabiliana na maafa yanapotokea.

Alifafanua kuwa, uwepo wa mafunzo hayo yamekuja kwa wakati muafaka ambapo uzoefu unaonesha kuwa athari za maafa zinaendelea kuongezeka kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo mabadiliko ya tabianchi, ongezeko la shughuli za kibinadamu na changamoto nyingine zinazoweza kusababisha maafa.
Posted by MROKI On Thursday, June 04, 2026 No comments



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akitunukiwa Shahada ya Udaktari wa Heshima (Honoris Causa) na Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi- (RUDN University) kutoka kwa Mkuu wa Chuo hicho Profesa Oleg Yastrebov kwenye hafla iliyofanyika Chuoni hapo Moscow nchini Urusi, tarehe 04 Juni, 2026. Rais Mhe. Dkt. Samia ametunukiwa Shahada hiyo ya Uzamivu kutokana na mchango wake katika Mageuzi ya sekta ya Elimu, juhudi zake za kuimarisha Diplomasia ya Tanzania, pamoja na mchango wake katika kuimarisha hadhi ya Tanzania Kimataifa ikiwemo kupitia sekta ya Utalii.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akihutubia viongozi wa Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi- (RUDN University), Wanafunzi wa Chuo hicho, wageni mbalimbali baada ya kutunukiwa Shahada ya Udaktari wa Heshima (Honoris Causa) kwenye hafla iliyofanyika chuoni hapo Moscow nchini Urusi, tarehe 04 Juni, 2026. 










Viongozi wa Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi- (RUDN University), Wanafunzi wa Chuo hicho pamoja na wageni mbalimbali wakiwa kwenye hafla ya Kutunukiwa Shahada ya Udaktari wa Heshima (Honoris Causa) kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Chuoni hapo Moscow nchini Urusi tarehe 04 Juni, 2026. 


Posted by MROKI On Thursday, June 04, 2026 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo