Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, ameanza ziara rasmi ya kikazi mkoani Geita kwa lengo la kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo, kuhamasisha shughuli za kiuchumi na kufuatilia utekelezaji wa maagizo ya Serikali yanayolenga kuboresha maisha ya wananchi.
Mhe. Mavunde, ambaye pia ni Mlezi wa shughuli za maendeleo mkoani Geita, anatarajiwa kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya kimkakati inayotekelezwa katika halmashauri na wilaya za mkoa huo, sambamba na kuzungumza na wananchi kuhusu fursa za maendeleo na mchango wa sekta ya madini katika kukuza uchumi wa Taifa.
Katika siku ya kwanza ya ziara hiyo, Waziri Mavunde amekagua mradi mkubwa wa maji wenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 40, unaotarajiwa kunufaisha zaidi ya wananchi 185,000 kwa kuwapatia huduma ya maji safi na salama. Ameeleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuwekeza katika miradi ya maji ili kuboresha afya, ustawi wa jamii na kuongeza tija katika shughuli za uzalishaji.
Akizungumza baada ya kukagua mradi huo, Mhe. Mavunde amesema upatikanaji wa maji ni msingi muhimu wa maendeleo ya kijamii na kiuchumi, huku akiwataka wakandarasi kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyokidhi thamani ya fedha za umma.
Katika kuendelea kuhamasisha maendeleo ya sekta ya madini, Waziri Mavunde pia ametembelea mradi wa vijana wa ujenzi wa kiwanda cha kuchenjua madini, akisisitiza kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki yatakayowawezesha vijana kushiriki kikamilifu katika shughuli za uchimbaji na uongezaji thamani wa madini.
Amesema uwekezaji katika viwanda vya uchakataji na uchenjuaji wa madini utaongeza thamani ya rasilimali za madini nchini, kufungua ajira kwa vijana na kuongeza mchango wa sekta hiyo katika ukuaji wa uchumi wa Taifa.
Aidha, Waziri Mavunde ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa Daraja la Rwantaba, mradi unaotarajiwa kuboresha miundombinu ya usafiri na usafirishaji, kurahisisha shughuli za biashara, kuunganisha maeneo ya uzalishaji na masoko pamoja na kuchochea maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi wa Mkoa wa Geita.
Mkuu wa Mkoa wa Geita Mh. Martin Shigela amesema utekelezaji wa shughuli za maendeleo mkoani Geita unajibu changamoto za wa wananchi kivitendo na kwamba serikali ya mkoa imejipanga kuhakikisha miradi yote ya maendeleo inakamilika kwa wakati.





















.jpg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)





















.jpg)
.jpeg)
.jpg)
.jpg)


