Nafasi Ya Matangazo

February 25, 2026




Na Heri Shaaban ,Dar es Salaam
Mkuu wa Wilaya ya Ilala Edward Mpogolo, amewasilisha Taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya chama cha Mapinduzi CCM ya Desemba 2025 mpaka FEBRUARY 2026 kwa wajumbe wa Halmashauri Kuu ya ccm wilaya ya Ilala. 


Akiwasilisha taarifa hiyo Mkuu wa Wilaya Edward Mpogolo, amesema Halmashauri hiyo imejipanga kujenga vyumba vya madarasa kwa ajili ya kupokea wanafunzi  65000 ambapo Halmashauri hiyo imeweka fedha nyingi sekta ya Elimu. 

Alisema miradi yote Ilala imekamilika kwa asilimia 89 changamoto ilikuwa katika vyumba vya madarasa kwa sasa wanaenda kuitatua changamoto ndani ya wilaya Ilala. 

"Leo nimewasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani katika taarifa hii tumeelekeza shilingi bilioni 80 kuelekezwa katika miradi mbalimbali ya maendeleo katika fedha  shilingi bilioni  347 zilizotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan ambapo natumia fursa hii kumpongeza Rais kwa kushusha Neema Ilala inaenda kuwa ya kisasa" amesema Mpogolo .

Katika hatua nyingine aliagiza viongozi wa ngazi ya kata kusimamia vikundi vya mikopo ya Serikali ya asilimia kumi ambayo inatolewa ngazi ya Halmashauri wakishirikiana Umoja wanawake UWT Wilaya ya Ilala katika kuratibu vikundi hivyo .

Akizungumzia migogoro ya ardhi ndani ya wilaya Ilala  ameagiza viongozi wa chama na Serikali kushirikiana pamoja katika kutatua changamoto hizo.

Alitumia fursa hiyo kuwapongeza Wajumbe wa Halmashauri Kuu wilaya ya Ilala wakiongozwa na Madiwani na Wabunge kwa kufanya kazi kwa kushirikiana 

Wakati huohuo Mkuu wa Wilaya Edward Mpogolo amesema Wenyeviti wa Serikali za mitaa 159 wa Wilaya ya Ilala hivi karibuni wanatarajia kukabidhiwa Vitamburisho vyao vya kazi  hivyo aliwataka wavute subira taratibu zote zimekamilika 

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Ilala Said Sidde alitumia fursa hiyo kumpongeza mkuu wa Wilaya Edward Mpogolo pamoja na Katibu Tawala Wilaya Charangwa Selemani na Watendaji wote kwa kuleta maendeleo makubwa Ilala. 

Mwenyekiti Side alisema Ilala wana mahusiano mazuri kati ya chama na Serikali katika utendaji wao wa kazi kila jambo wanashirikiana pamoja kujenga Serikali. 


Meya wa Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam Nurudini sheta ameomba Wajumbe wa Halmashauri Kuu wilaya waweze kupatiwa mafunzo kwa ajili ya kuwajengea uwelewa kila mjumbe aweze kufanya kazi kwa Weledi. 
Posted by MROKI On Wednesday, February 25, 2026 No comments






Na Mwandishi Wetu, Dodoma
Serikali kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeyapatia ufumbuzi malalamiko ya muda mrefu ya viwanja mbadala kwa wananchi wa jiji la Dodoma.

Suluhisho hilo linafuatia malalamiko ya takriban wananchi 4000 wa jiji la Dodoma wanaodai viwanja na halmashauri ya jiji la Dodoma kuwapa ahadi bila kutekeleza mpaka sasa.

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 25 Februari 2026 na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo wakati akizungumza na wananchi wenye migogoro ya ardhi katika eneo la Mahomanyika lilopo kata ya Nzuguni jijini Dodoma.

Dkt Akwilapo amesema, eneo la Mahomanyika ni eneo la serikali hivyo lipangwe na kupimwa kwa ajili ya utatuzi wa migogoro ya meneo mbalimbali ya jiji la Dodoma pamoja na matumizi ya serikali.

"Eneo hili lenye mgogoro hapa Mahomanyika ni eneo la serikali hivyo lipangwe na kupimwa kwa ajili ya utatuzi wa migogoro na siyo ya hapa tu na mingine ya jiji la Dodoma na matumizi ya serikali" amesema.

Amesisitiza kuwa katika upangaji wa eneo hilo kipaumbele kiwe kutatua changamoto za wananchi wa jiji la Dodoma ambao kwa muda mrefu wamedai viwanja na jiji kuwaahidi bila ya kuwapatia.

Katika kufanikisha zoezi hilo, zimeundwa timu mbili kwa ajili ya upangaji na upimaji na pamoja na ile ya kushughulika na uhakiki wa wananchi wenye migogoro na kustahili kupatiwa  viwanja mbadala.

"Timu hizi zitaanza kazi mara moja na kazi hiyo itafanyika kwa muda wa siku sitini, miezi miwili kazi iwe imekamilika kila mtu kujua amepata nini na anaenda wapi" amesema.

Akigeukia uuzwaji viwanja 1,037 vilivyoingizwa kwenye mfumo wa TAUSI ili wananchi wapate viwanja vilivyopimwa katika eneo la Mahomanyika, Dkt. Akwilapo amuagiza Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kuendelea na uuzaji viwanja kwa waombaji 352 pekee walioanza kulipa huku wale ambao hawajaanza kulipa maombi yao yasitishwe.

Eneo la Mahomanyika limekuwa na changamoto ya malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa wananchi wakidai ni wamiliki wa asili wa maeneo hayo jambo lililosababisha kuundwa kwa Timu (Timu ya DC) ambayo ilishirikisha wananchi, Vyombo vya Usalama na Wataalam ambapo timu hiyo ilibaini eneo husika ni eneo la Serikali.
Posted by MROKI On Wednesday, February 25, 2026 No comments

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila leo Feb 25,2026 amekutana na Gavana wa Jimbo la Maniema-Congo DRC Mhe Mussa Kabwankubi Moise akiwa ameambatana na ujumbe wake alipomtembelea Ilala Boma Jijini Dar es Salaam.

Katika mazungumzo yao wamekubaliana mashirikiano katika nyanja mbalimbali ikiwemo Uchumi na Masuala ya Kiusalama kati ya Mkoa wa Dar es Salaam na Jimbo la Maniema.

Aidha RC Chalamila amesema Congo na Tanzania ni majirani na ni marafiki wa muda mrefu ndiyo maana katika Mkoa wa Dar es Salaam wakongo ni wengi na wanajishughulisha na shughuli mbalimbali ikiwemo biashara

"Ukiangalia  kupitia Bandari ya Dar es Salaam mzigo unaokwenda Congo kitakwimu ni kiasi kikubwa kwa mwaka hivyo Mkoa unathamini sana wacongo" Alisema Chalamila










Posted by MROKI On Wednesday, February 25, 2026 No comments
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imetoa Tuzo za ubunifu kwa washindi 9 waliotoa mawazo bora zaidi yatakayosaidia kuendelea kuboresha huduma za kodi na kuongeza wigo wa kodi. 

Akikabidhi tuzo hizo, vyeti pamoja na hundi kwa washindi hao Februari 25.2026, Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar ameipongeza TRA kwa kuja na Tuzo hizo ambazo zitaongeza ukaribu na ushirikishwaji wa wananchi katika masuala ya ukusanyaji wa kodi. 

Mshindi wa jumla katika tuzo hizo ni Gabriel Mashenene ambaye amepatiwa hundi ya Sh. Milioni 50, washindi watatu wamepatiwa Sh. Milioni 30 kila mmoja huku washindi 5 wakipatiwa Sh. Milioni 20  kwa kila mmoja.










Posted by MROKI On Wednesday, February 25, 2026 No comments

 Na Mwandishi wetu, Ruvuma
Wapiga Kura 127,632 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura watashiriki katika uchaguzi wa kuchagua Mbunge katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Mkoa wa Ruvuma na Kata ya Shiwinga iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Songwe.
 
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele ameyasema hayo leo Februari 25, 2026 mjini Songea Mkoani Ruvuma wakati akisoma risala maalum kuhusu uchaguzi katika jimbo na kata husika utakao fanyika kesho Februari 26, 2026 na kusema kuwa jumla ya vituo 373 vya Kupigia Kura vitatumika.
 
“Kati yao wapiga kura 120,780 ni wa Jimbo la Peramiho na wapiga kura 6,852 wapo katika kata ya shiwinga na jumla ya vituo 373 vya Kupigia Kura vitatumika, ambapo vituo 354 vipo Jimbo la Peramiho na vituo 19 vipo katika Kata ya Shiwinga Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi,”amesema Jaji Mwambegele.
 
Aidha, amesema kwa uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Peramiho vyama vya siasa 15 vimesimamisha wagombea na  kwa upande wa uchaguzi mdogo wa udiwani katika Kata ya Shiwinga vyama vya siasa nane (08) vimesimamisha  wagombea.
 
“Natumia fursa hii kuvikumbusha Vyama vya Siasa vinavyoshiriki uchaguzi kesho Februari 26, 2026 kuzingatia wajibu wao wa kuweka mawakala katika vituo vyote vya zoezi la kupiga, kuhesabu na kujumlishia kura. Wasimamizi wa uchaguzi katika Jimbo na Kata husika, wamekamilisha taratibu zinazoweka mazingira yanayowawezesha mawakala wa vyama vya siasa kufuatilia mchakato mzima wa uchaguzi,”alisema Jaji Mwambegele.
 
Amesema, mawakala hao, wanawajibika katika kulinda maslahi ya vyama na wagombea wao. Hivyo, wanapaswa kuzingatia Sheria, Kanuni, taratibu za Uchaguzi na maelekezo ya Tume katika utekelezaji wa majukumu yao vituoni.
 
Jaji Mwambegele amesema vituo vitafunguliwa saa 01:00 asubuhi na kufungwa saa 10:00 jioni na kwamba ifikapo muda wa kufunga kituo saa 10:00 kamili jioni, kama wapiga kura bado wapo kwenye mistari, mlinzi wa kituo atasimama nyuma ya mtu wa mwisho na zoezi la upigaji kura litaendelea hadi wapiga kura walio kwenye mstari watakapomalizika.
 
“Baada ya kumaliza kupiga kura, mpiga kura anatakiwa kuondoka eneo la kituo cha kupigia kura; na Mpiga kura awapo kituoni, anatakiwa kufuata maelekezo yote atakayopewa na karani mwongozaji wapiga kura,”amesema Jaji Mwambegele.
 
Kwa mpiga kura ambaye ameandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na taarifa zake zipo katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura lililopo katika kituo husika, lakini amepoteza kadi yake au kadi yake imeharibika, ataruhusiwa kupiga Kura kwa kutumia moja wapo ya vitambulisho cha Taifa NIDA, Leseni ya udereva au Pasi ya kusafiria (Passport).

Posted by MROKI On Wednesday, February 25, 2026 No comments

February 24, 2026

Taswira ya Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Kikombo Mkoani Dodoma mara baada ya kuzinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, tarehe 24 Februari, 2026.
Matukio mbalimbali yakimuonesha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alipozindua rasmi Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Kikombo Mkoani Dodoma tarehe 24 Februari, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Maafisa Askari, Watumishi wa umma na wageni mbalimbali waliohudhuria uzinduzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Kikombo Mkoani Dodoma tarehe 24 Februari, 2026.












 

Posted by MROKI On Tuesday, February 24, 2026 No comments




WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amekagua ujenzi wa Stendi Kuu ya Mabasi yaendayo mikoani unaotekelezwa katika eneo la Bondeni City kwenye Halmashauri ya Jiji la Arusha kwa gharama ya sh. bilioni 14.3.

Akizungumza na wafanyakazi na wananchi waliofika eneo hilo leo (Jumanne, Februari 24, 2026), Waziri Mkuu amesema ameona jinsi stendi iliyopangiliwa na amefurahishwa kuona kwamba wamebakiza eneo la akiba kwa ajili ya ujenzi wowote utakaohitajika kwenye awamu ya pili.

“Nimeona kuna eneo la akiba mmelibakiza. Pia kuna matoleo ya BRT ambayo mmesema ni maandalizi ya kuweka miundombinu ya mabasi yaendayo haraka. Maeneo mengine ya Zanzibar na Dar es Salaam yatakapofanyika mashindano haya ya AFCON, nayo tuwe kwenye standard hizohizo. Tuongee na sekta binafsi ili tupate fedha za mabadiliko ya tabianchi ili hapa Arusha tuwe na mabasi yanayotumia gesi,” amesema.

Amesema yakipatikana mabasi hayo, na stendi ikakamilika, kutakuwa na magari ya kubeba wageni watakaokuwa wamefika kushuhudia michuano ya AFCON.

Naye, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Mbunge wa Arusha, Paul Makonda amesema ziara za Waziri Mkuu zinawapa faraja na matumaini wananchi wengi wakiwemo wa Jiji la Arusha.

“Ziara yako sisi wananchi wa Arusha Mjini inatupa matumaini ya kuelekea nchi ya ahadi ambayo tumeahidi katika Ilani yetu; ujenzi wa uwanja unatokana na kazi njema inayofanywa na Chama cha Mapinduzi, kwa miradi hii hatuacha kumuombea Rais Dkt Samia Suluhu Hassan,” amesema.

“Tunaomba utuwekee alama za nyayo zako kila utakapopita katika hii miradi, iweze kukamilika kwa wakati ili wananchi wa Jiji la Arusha waweze kunufaika nayo. Wafanyabiashara wote watapata nafasi sawa katika stendi hii ili waweze kupata kipato na tunaamini kupitia stendi hii mji wetu wa Arusha utapumua.”

Mapema, Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, John Kayombo alimweleza Waziri Mkuu kuwa mradi huo ambao unatarajiwa kukamilika Mei 30, 2026  hadi sasa umefikia asilimia 49. Alisema mradi huo una lengo la kuboresha miundombinu ya usafiri na usafirishaji, kupunguza msongamano katikati ya Jiji na kuongeza mapato ya Halmashauri ya Jiji hilo.

Alisema itakapokamilika, stendi hiyo itakuwa na jengo kuu la kituo cha mabasi (ghorofa moja) na sehemu mbili za kusubiri abiria, maduka 23 ya biashara, maeneo mawili kwa wauza vyakula, vyoo vya kisasa pande zote mbili na nyumba ya walinzi. Vingine ni  nyumba ya umeme (power house), tanki la maji, vituo vitano vya ukaguzi na ulinzi, vituo 20 vya kukusanyia taka na eneo maalum la dharura.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa soko la Kilombero unaotekelezwa na Halmashauri ya Jiji la Arusha ili kuboresha huduma za biashara na miundombinu ya soko hilo.

Akizungumza na wananchi waliofika sokoni hapo leo (Jumanne, Februari 24, 2026), Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwaeleza mafanikio yaliyofanywa na Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika nyanja mbalimbali.

Amesema Rais Samia ameweza kukwamua miradi mikubwa ya maji ambayo awali ilikaa kwa muda mrefu bila kukamilika kama vile ya Mwanga-Same-Korogwe. Pia amenunua mitambo na vifaa kwenye sekta za maji na afya.

“Zamani tulikuwa na mitambo miwili au mitatu ya kuchimba visima lakini sasa hivi kila mkoa una mitambo yake. Pia kuna mitambo mitano ya kupima maji chini ya ardhi, kila kanda imepata mtambo wake. Na jana tu, nilishuhudia kule kata ya Sinya, wilaya ya Longido wamepata maji chini ya ardhi umbali wa mita 300 (sawa na viwanja vitatu vya mpira). Wamechimba maji na sasa yanaenda hadi Namanga.”

“Kwenye sekta ya afya, Mheshimiwa Rais wetu amenunua vifaa vya kisasa kwenye hospitali zetu. Amenunua mashine 32 za CT-scan sasa hivi kila hospitali za mkoa na rufaa zina vifaa vya kisasa, zamani zilikuwa kwenye hospitali chache sana. Amejenga hospitali mpya za wilaya 119, vituo vya afya 649 na zahanati 2,800.”

Kwa mujibu wa taarifa ya ujenzi wa soko hilo, hadi kukamilika linatarajiwa kugharimu sh. bilioni 9.5 na hadi sasa ujenzi wake umefikia asilimia 43 ambapo kutakuwa na jengo la soko kuu lenye ghorofa mbili zenye vizimba 518, vibanda 70, majengo mawili ya vyoo kila moja likiwa na matundu 19 na vyumba viwili vya kubadilishia nguo. 

Pia, kutakuwa na vyumba vya kulelea watoto, vyumba viwili vya ofisi, vyumba viwili vya kuabudia, maeneo 54 ya maegesho, sehemu saba za kukusanya taka na stendi ya kushusha/kupakia abiria. 
Posted by MROKI On Tuesday, February 24, 2026 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo