Nafasi Ya Matangazo

February 27, 2026

By Christopher Makwaia
On August noon in forty-four, beneath Tanganyika’s sky,
In Mwazye’s quiet parish land, a child began to cry.

The sixth of nine, yet heaven-marked before the world could see, A shepherd chosen long before he bent his first small knee.
 
His sister saw the spark in him and made a solemn vow, To guard his dream with sacrifice, though trials pressed her brow.

Her youth she gave, her wages too, his schooling to defend, So he might serve the Lord of Life until his journey’s end.
 
Through Karema’s halls and Kaengesa’s rising gleam,
Through Kipalapala’s sacred books and nights of ceaseless stream,
His mind grew luminous, his spirit ardent, his purpose living beam,
A leader formed by discipline, by prayer, by sacred theme.
 
Ordained a priest in seventy-one, still humble, still afraid,
Yet faithful to the call of God, whatever price was paid.
In Rome he drank from ancient wells of moral truth and grace,
Then hastened home to serve his land, not seek a higher place.
 
A bishop young in Nachingwea, in Tunduru he stood, To build where little yet was formed, to plant where none yet could.

Though fear would knock upon his heart whenever roles were new,
His answer was obedience, God’s will he would pursue.
 
In Dar he rose to guide the flock where giants once had been,
A Cardinal in scarlet red, yet simple still within.
He asked, “Why beg for distant grain when ours can fill the bowl?”
And taught the Church to stand upright in dignity of soul.
 
From twenty parishes he dreamed of one hundred in their place,
They doubted such a vision vast could ever run that race.
But when he laid the crozier down and passed the charge along,
One hundred eighteen stood in faith, his vision proved them wrong.
 
For death to him was not defeat, nor darkness, nor despair,
But simply door to promised glory beyond all earthly care.
The pilgrim laid his labors down where saints and angels sing,
And entered joy no mortal tongue could fully name or bring.
 
Though on 19 February he left this earthly state,
On 28 February, in solemn farewell we congregate.
Not stripped of honor, nor lost to sight,
But clothed in dignity, in hallowed rite.
 
A priest for decades he faithfully stood,
A guide in truth, in strength, in good.
A bishop, archbishop, cardinal upright,
A conscience steady in nation’s sight.
 
Eternal rest, O Lord, bestow,
Let endless light upon him glow.
May he who led with faithful hand
Now dwell within God’s promised land.
 
And when the final trumpet rings,
And time surrenders all its kings,
May the shepherd, his flock, and the Church above,
Rejoice in resurrected love.
 
His spirit whispers still,
Through every heart he touched, through every faithful will.
Though tears may fall, his love will never fade,
A shepherd, father, guide, forever ours to aid.

Thank you.

Written by Christopher Makwaia
Tel: +255 789 242 396

The writer, is a University of West London graduate (formerly Thames Valley University) and an expert in Management, Leadership, International Business, Foreign Affairs, Global Marketing, Diplomacy, International Relations, Conflict Resolution, Negotiations, Security, Arms Control, Political Scientist, and a self-taught Computer Programmer and Web Developer.
Posted by MROKI On Friday, February 27, 2026 No comments





🔴DC atoa siku tatu watoto wa bweni warejeshwe makwao

ZIARA ya Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba jijini Arusha imewazindua watendaji na kujikuta wakibaini ujenzi wa shule ya ghorofa usio na vibali na watoto kulazwa katika bweni wakati ujenzi ukiendelea kwenye ghorofa hizo.

Hayo yamebainika leo (Ijumaa, Februari 27, 2026) wakati Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Joseph Mkude na Kamati ya Usalama ya Wilaya walipofanya ziara kwenye shule ya Nariva Hill na kufanya ukaguzi katika madarasa, mabweni, jikoni na eneo wanalojenga ghorofa juu ya bweni lililokuwa linatumika.

Katika ziara hiyo shuleni hapo ambayo ilikuwa ni utekelezaji wa maagizo ya Waziri Mkuu, viongozi hao walibaini kuwepo kwa msongamano wa wanafunzi wa kike wanaolala katika bweni la muda ilhali hawana vyoo wala mabafu kwenye ghorofa yao. Pia walibaini baadhi ya watoto wanalala wawiliwawili kwenye kitanda kimoja.

“Yale mabweni sikuona standards za Wizara ya Elimu, kuanzia leo natoa muda wa siku tatu tu kwa sababu hawa watoto wana kwao; kwa hiyo wazazi wao lazima wajulishwe. Natoa siku tatu mabweni haya yawe yamefungwa. Tumepewa tahadhari ya magonjwa ya kipindupindu na mfumo wa hewa, hali iliyopo mabwenini haipo sawa, yafungwe warudi kusoma shule ya kutwa,” amesema Mkuu huyo wa Wilaya.

Pia amesitisha ujenzi unaoendelea shuleni hapo kwa kuwa hawana vibali vya ujenzi licha ya kuwa walishapewa stop order tangu Oktoba 13, 2025 lakini wakakaidi na kuendelea na ujenzi. “Stop order ilitolewa tangu mwezi wa Oktoba na haikuzingatiwa. Kwa hiyo, kuanzia leo, ianze kutekelezwa hadi vibali kamili vitakapotolewa,” amesema.

Vilevile amemwagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Jiji la Arusha na Mkaguzi wa Elimu wafuatilie barua halisi zilizoruhusu usajili wa shule hiyo ikiwemo nakala za vibali vya kuruhusu kulaza watoto shuleni.

 “Walete nakala za vibali kutoka wizara ya elimu na haraka viwasilishwe kwenye ofisi ya TAKUKURU ya Wilaya ili wafanye uchunguzi zaidi,” amesisitiza.

Mkuu huyo wa Wilaya amesema hali ya jikoni shuleni hapo ni chafu, hakuna bwalo na watoto waliopo shuleni ni zaidi 1,700. Amewataka wamiliki wa shule hiyo wazingatie viwango vya wizara ya elimu vya ujenzi wa jiko.

Kuhusu maji yanayotumiwa na wanafunzi, Mkude amesema eneo la maji ya kunywa ni finyu na watoto wanapokezana vikombe vya kunywea maji kutoka kwenye tenki. 

Amewataka waweke mifumo ya mabomba kama ilivyoelekezwa na wizara ya elimu ambapo mabomba mengi huwekwa kwa pamoja na watoto wanaweza kunywa bila kupanga foleni.

Mapema, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Javelin Gaspar alisema shule hiyo ambayo ilianzishwa mwaka 2016, ina wanafunzi 1,726 wanaosoma kuanzia shule ya awali hadi darasa la saba. “Shule ina madarasa 55, walimu 42, mabweni mawili ambapo wanafunzi wanaolala shuleni ni 162.

Alipoulizwa kuhusu uwepo wa vibali vya ujenzi, mmiliki wa shule hiyo, Emmanuel Saanya na mshauri wa ujenzi wa shule hiyo, Emmanuel Rajab walikiri kutokuwa na vibali vya ujenzi.

Mkuu wa Wilaya hiyo alimwagiza Kamanda wa Polisi wa Wilaya, Georgina Matagi aende nao polisi wakatoe maelezo yao leo hii hii. 
Posted by MROKI On Friday, February 27, 2026 No comments



🔴Ni baada ya kueleza kero yake kwa Waziri Mkuu

JITIHADA za Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba kusikiliza kero za wananchi zimezaa matunda ambapo mkazi wa Kata ya Baraa jijini Arusha, Bi. Agnes Simon Laizer alilipwa fidia ya sh. milioni 7 na mmiliki wa shule ya Nariva Hill (jirani yake) ambaye alikuwa ameharibu jiko na ukuta kutokana na ujenzi wa ghorofa unaoendelea.

Bi. Agnes alikabidhiwa fedha hizo taslimu jana (Alhamisi, Februari 26, 2026) mbele ya mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Polycarp Nkuyumba, Diwani wa Kata hiyo, Mtendaji wa Kata na Mtaa, pamoja na Maafisa wa Wilaya waliokuwa wameambatana na timu ya Wasaidizi wa Waziri Mkuu waliokuwa wakisikiliza kero za wananchi kama alivyoelekeza Waziri Mkuu.

Februari 24, mwaka huu, Bi. Agnes Laizer aliwasilisha kero yake mbele ya Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo linapojengwa soko jipya la Kilombero wakati akiwa kwenye ziara ya siku tatu mkoani Arusha. Bi. Agnes alisema ameathirika kiafya kutokana na ujenzi wa ghorofa kwenye shule ya msingi ya Nariva ikiwemo kuharibiwa ukuta na kubomolewa jiko lake.

Alisema vumbi, zege, vipande vya matofali na mbao vinafika katika eneo lake (kwa kuwa hajaweka neti ya kuzuia), sehemu ya ghorofa imezidi katika eneo lake na bomba lake la maji ya kunywa lililochimbuliwa wakati ujenzi ukianza, bado halijafukiwa.

Februari 25, 2026 Bi. Agnes alifika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha ambako timu ya wataalamu wa Mkoa na Jiji walikutana na kusikiliza kero za wananchi na wakaamua kumuita mmiliki wa shule ya Nariva Hill, Bw. Emmanuel Saanya ambaye alikubali kulipa fidia kwa mama huyo.

Timu iliyofika nyumbani kwa Bi. Agnes Laizer ilishuhudia ujenzi wa ghorofa ukiendelea bila kuwepo kwa nyavu za kuzuia hatari (safety nets), mabomba ya maji yaliyokatika na jiko lililokuwa limebomoka, likiwa limeshakarabatiwa.

Akitoa shukrani baada ya kukabidhiwa fedha hizo, Bi. Agnes alisema anashukuru kwa kulipwa fidia hiyo ambayo ataitumia kukarabati nyumba yake. Alimshukuru Rais Dkt.  Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mawakili wanaotoa msaada wa kisheria ambao kwa sehemu kubwa walishiriki kutatua mgogoro huo.
Posted by MROKI On Friday, February 27, 2026 No comments
Mkuu wa wilaya ya Arusha, Joseph Mkude akikabidhi sh. milioni 1.8 kwa Flora Mbeve aliyeomba msaada kwa Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba wa kulipiwa deni la kikoba. 
Mwenyekiti wa kikundincha Jikomboe,  Laurent Mwita Marwa akisaini mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Arusha kukiri kupokea rejesho la sh. milioni 1.8 kutoka kwa Bi. Flora Mbeve.

🔴Akabidhiwa sh. milioni 1.8 kulipa deni la kikoba

MKAZI wa Arusha, Bi. Florah Mbeve amekabidhiwa sh. milioni 1.8 ili akalipe deni analodaiwa kwenye kikoba ambazo alikopa na kumpa mumewe kisha akatelekezwa na mwanaume huyo kwa madai kuwa anazaa watoto wa kike tu.

Februari 24, mwaka huu, Bi. Florah aliwasilisha kero yake mbele ya Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo linapojengwa soko jipya la Kilombero wakati akiwa kwenye ziara ya siku tatu mkoani Arusha. Alisema alikuwa anauza vipande vya matikiti ili apate fedha za kujikimu na wanawe wanne na kiasi apeleke kwenye rejesho. 

Bi. Florah alikabidhiwa fedha hizo taslimu jana (Alhamisi, Februari 26, 2026) na Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Joseph Mkude kwa niaba ya Waziri Mkuu ambaye aliahidi kumsaidia mama huyo.

Akimkabidhi fedha hizo ofisini kwake mbele ya Mwenyekiti wa kikundi cha Jikomboe, Bw. Laurent Mwita Marwa, Mkuu huyo wa Wilaya ya Arusha alisema kuwa amemkabidhi kiasi hicho cha fedha kutoka kwa Waziri Mkuu kama ambavyo aliahidi kwamba atampatia fedha hiyo ili kumuondolea adha na usumbufu alioupata kutokana na deni hilo analodaiwa kwenye kikoba.

Akizungumza baada ya kupokea fedha hizo, Bw. Marwa alishukuru kupewa rejesho la mama huyo kwa mkupuo kwa sababu tangu mama huyo alipojifungua, alikuwa hana chanzo cha uhakika cha fedha cha kuweza kurejesha mkopo wake.

Akitoa shukrani baada ya kukabidhiwa fedha hizo, Bi. Florah alisema amefurahi sana na akamshukuru Waziri Mkuu kwa msaada huo wa fedha alioupata kwa kuwa fedha hiyo amekuwa akidaiwa kwa muda mrefu na akashindwa kurejesha baada ya mumewe kumtelekeza yeye na watoto wake.

“Ninamshukuru sana Waziri Mkuu, ninamshukuru Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan kwa kutujali wananchi wake. Fedha nilizopewa zimenisaidia kulipa deni kwenye kikoba, deni ambalo mume wangu aliniachia na kunitelekeza na watoto, kwa sasa nina amani, nina tumaini la kuishi,” alisema Bi. Florah. 
Posted by MROKI On Friday, February 27, 2026 No comments

February 26, 2026





Na Mwandishi wetu, Manyara
MGODI wa Itracom Fertilizer Limited unaojihusisha na uchimbaji na uchakataji wa madini ya phosphate uliopo  katika eneo la Vilima Vitatu, Wilayani Babati mkoani Manyara, umechangia Shilingi Bilioni 1.29 katika mapato ya Serikali tangu kuanza kwa shughuli zake mwaka 2023.

Hayo yamebainishwa na Mjiolojia, Waziri Mkupe, akizungumza kwa niaba ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Manyara, Godfrey Nyanda, ambapo amesema mapato hayo yametokana na mrabaha na ada ya ukaguzi wa madini.

Amesema tangu kuanza kwa uzalishaji, mgodi huo umezalisha jumla ya tani 69,929 za madini ya phosphate zenye thamani ya Shilingi Bilioni 36.99, ambazo zimeuzwa katika soko la ndani na nje ya nchi, hususan Nala mkoani Dodoma na nchini Burundi.

Kwa mujibu wa Mkupe, mchango huo umeimarisha ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali na kuchochea maendeleo ya jamii inayozunguka mgodi kupitia utekelezaji wa miradi ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSR).

Ameeleza kuwa tangu kuanza kwa shughuli zake, mgodi huo umechangia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa Shule ya Msingi Vilima Vitatu, nyumba za walimu, na upo katika hatua za awali za ujenzi wa bweni la shule ya sekondari ya wasichana.

Akifafanua kuhusu mauzo ya ndani, amesema kuanzia Desemba 16, 2023 hadi Februari 24, 2026, jumla ya tani 22,686 zenye thamani ya Shilingi bilioni 9.07 ziliuzwa kwenda Nala, Dodoma. Katika mauzo hayo, Serikali ilikusanya Shilingi milioni 90.74 kama mrabaha na kiasi kama hicho kama ada ya ukaguzi.

Kuhusu mauzo ya nje, amesema vibali 13 vilitolewa kwa ajili ya kusafirisha tani 47,243 za madini ya phosphate kwenda Burundi zenye thamani ya Shilingi Bilioni 27.92. Katika kipindi cha Septemba 4, 2024 hadi Februari 24, 2026, Serikali ilikusanya Shilingi milioni 837.64 kama mrabaha na Shilingi milioni 279.21 kama ada ya ukaguzi.

“Mgodi wa Itracom Fertilizer Limited umeendelea kudhihirisha kuwa sekta ya madini ya phosphate ni kichocheo muhimu cha ukuaji wa uchumi wa Mkoa wa Manyara kwa kuongeza mapato ya Serikali, kutoa ajira na kuimarisha maendeleo ya jamii,” amesema Mkupe.

Aidha, amewahimiza Watanzania kuchangamkia fursa za uwekezaji zilizopo mkoani humo, akibainisha kuwa pamoja na madini ya phosphate, Mkoa wa Manyara una rasilimali nyingine zikiwemo dhahabu, moonstone, green tourmaline, amethyst, green aventurine, limestone, azurite, chumvi, muscovite mica, feldspar na quartz crystal.
Posted by MROKI On Thursday, February 26, 2026 No comments
   

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe mkoani Pwani, Selemani Jafo, ameonesha kuridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mradi wa maji katika Kijiji cha Nyani, Kata ya Mafizi, akieleza kuwa hatua iliyofikiwa inaleta matumaini mapya kwa wananchi.

Mradi huo unaotekelezwa na kampuni ya BROADWAYS ENGINEERING CO LTD una thamani ya shilingi milioni 402.8 na hadi sasa umefikia asilimia 70 ya utekelezaji, jambo linaloashiria kuwa upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wakazi wa eneo hilo si wa muda mrefu tena.

Kwa mujibu wa taarifa ya utekelezaji, mradi unahusisha ujenzi wa mnara wa tanki la maji lenye urefu wa mita 12 na uwezo wa kuhifadhi lita 50,000, pamoja na ujenzi wa vituo vitano vya kuchotea maji na ulazaji wa mtandao wa mabomba wenye urefu wa kilometa 16.167.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa mradi huo, Dkt. Jafo alimpongeza mkandarasi kwa kufanya kazi kwa kasi na weledi mkubwa, akibainisha kuwa kampuni hiyo imeendelea na kazi hata kabla ya kupokea malipo yoyote, jambo alilolitaja kuwa ni uzalendo na kujitolea kwa maendeleo ya wananchi.

Kutokana na kasi hiyo, Jafo ameiiomba Wizara ya Maji kulipa kiasi cha shilingi milioni 279.1 kwa kazi zilizokamilika ili kumwezesha mkandarasi huyo kuendelea na hatua zilizobaki na kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati.

Mbali na mkandarasi, mbunge huyo pia amempongeza Meneja wa RUWASA Wilaya ya Kisarawe, Mhandisi Evangelista Kahwili, kwa usimamizi makini wa miradi ya maji ndani ya jimbo hilo, akisema nidhamu na ufuatiliaji wa karibu umechangia mafanikio yanayoonekana.

Wananchi wa Nyani na maeneo ya jirani wanatarajia kunufaika na mradi huo mara utakapokamilika, huku wakieleza kuwa utapunguza adha ya kutembea umbali mrefu kutafuta maji na kuboresha afya pamoja na shughuli za kiuchumi katika eneo hilo. 

Posted by MROKI On Thursday, February 26, 2026 No comments




Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimetoa salamu za rambirambi kwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Jude Thaddeus Ruwa’ichi OFMCap, kufuatia kifo cha Askofu Mkuu mstaafu wa Jimbo hilo, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo, aliyefariki dunia Februari 19, 2026, katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) alipokuwa akipatiwa matibabu.

Akizungumza Februari 26, 2026 baada ya kusaini kitabu cha maombolezo katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu, Dar es Salaam, Katibu Mkuu CCM, Dkt. Asha-Rose Migiro, alisema amewasilisha salamu za rambirambi kwa niaba ya Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Dkt. Migiro alisema marehemu Kadinali Pengo atakumbukwa kama mchungaji wa faraja na tumaini, kiongozi wa kiroho mwenye hekima, unyenyekevu na msimamo thabiti wa maadili. 

Alijipambanua si tu kwa huduma ya Kanisa, bali pia kwa mchango wake katika kuimarisha mshikamano wa kitaifa, maadili ya jamii, malezi ya vijana na uwajibikaji wa viongozi.

“Kadinali Pengo ameacha alama inayodumu ya utumishi wa Mungu, utumishi wa Taifa na utumishi wa jamii. Maisha na mafundisho yake yataendelea kuwa dira kwa vizazi vijavyo,” alisema Dkt. Migiro.

CCM imesema inaliombea Kanisa Katoliki na waumini wote wapate faraja katika kipindi hiki cha maombolezo na  Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.

Kwa mujibu wa ratiba ya mazishi, mwili wa marehemu utawasili Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu Februari 27, 2026 kwa ajili ya waumini kutoa heshima zao za mwisho, na Ibada ya Misa ya Mazishi itafanyika Februari 28, 2026 katika Kituo cha Hija Pugu, Dar es Salaam.
Posted by MROKI On Thursday, February 26, 2026 No comments

February 25, 2026




Na Heri Shaaban ,Dar es Salaam
Mkuu wa Wilaya ya Ilala Edward Mpogolo, amewasilisha Taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya chama cha Mapinduzi CCM ya Desemba 2025 mpaka FEBRUARY 2026 kwa wajumbe wa Halmashauri Kuu ya ccm wilaya ya Ilala. 


Akiwasilisha taarifa hiyo Mkuu wa Wilaya Edward Mpogolo, amesema Halmashauri hiyo imejipanga kujenga vyumba vya madarasa kwa ajili ya kupokea wanafunzi  65000 ambapo Halmashauri hiyo imeweka fedha nyingi sekta ya Elimu. 

Alisema miradi yote Ilala imekamilika kwa asilimia 89 changamoto ilikuwa katika vyumba vya madarasa kwa sasa wanaenda kuitatua changamoto ndani ya wilaya Ilala. 

"Leo nimewasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani katika taarifa hii tumeelekeza shilingi bilioni 80 kuelekezwa katika miradi mbalimbali ya maendeleo katika fedha  shilingi bilioni  347 zilizotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan ambapo natumia fursa hii kumpongeza Rais kwa kushusha Neema Ilala inaenda kuwa ya kisasa" amesema Mpogolo .

Katika hatua nyingine aliagiza viongozi wa ngazi ya kata kusimamia vikundi vya mikopo ya Serikali ya asilimia kumi ambayo inatolewa ngazi ya Halmashauri wakishirikiana Umoja wanawake UWT Wilaya ya Ilala katika kuratibu vikundi hivyo .

Akizungumzia migogoro ya ardhi ndani ya wilaya Ilala  ameagiza viongozi wa chama na Serikali kushirikiana pamoja katika kutatua changamoto hizo.

Alitumia fursa hiyo kuwapongeza Wajumbe wa Halmashauri Kuu wilaya ya Ilala wakiongozwa na Madiwani na Wabunge kwa kufanya kazi kwa kushirikiana 

Wakati huohuo Mkuu wa Wilaya Edward Mpogolo amesema Wenyeviti wa Serikali za mitaa 159 wa Wilaya ya Ilala hivi karibuni wanatarajia kukabidhiwa Vitamburisho vyao vya kazi  hivyo aliwataka wavute subira taratibu zote zimekamilika 

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Ilala Said Sidde alitumia fursa hiyo kumpongeza mkuu wa Wilaya Edward Mpogolo pamoja na Katibu Tawala Wilaya Charangwa Selemani na Watendaji wote kwa kuleta maendeleo makubwa Ilala. 

Mwenyekiti Side alisema Ilala wana mahusiano mazuri kati ya chama na Serikali katika utendaji wao wa kazi kila jambo wanashirikiana pamoja kujenga Serikali. 


Meya wa Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam Nurudini sheta ameomba Wajumbe wa Halmashauri Kuu wilaya waweze kupatiwa mafunzo kwa ajili ya kuwajengea uwelewa kila mjumbe aweze kufanya kazi kwa Weledi. 
Posted by MROKI On Wednesday, February 25, 2026 No comments






Na Mwandishi Wetu, Dodoma
Serikali kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeyapatia ufumbuzi malalamiko ya muda mrefu ya viwanja mbadala kwa wananchi wa jiji la Dodoma.

Suluhisho hilo linafuatia malalamiko ya takriban wananchi 4000 wa jiji la Dodoma wanaodai viwanja na halmashauri ya jiji la Dodoma kuwapa ahadi bila kutekeleza mpaka sasa.

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 25 Februari 2026 na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo wakati akizungumza na wananchi wenye migogoro ya ardhi katika eneo la Mahomanyika lilopo kata ya Nzuguni jijini Dodoma.

Dkt Akwilapo amesema, eneo la Mahomanyika ni eneo la serikali hivyo lipangwe na kupimwa kwa ajili ya utatuzi wa migogoro ya meneo mbalimbali ya jiji la Dodoma pamoja na matumizi ya serikali.

"Eneo hili lenye mgogoro hapa Mahomanyika ni eneo la serikali hivyo lipangwe na kupimwa kwa ajili ya utatuzi wa migogoro na siyo ya hapa tu na mingine ya jiji la Dodoma na matumizi ya serikali" amesema.

Amesisitiza kuwa katika upangaji wa eneo hilo kipaumbele kiwe kutatua changamoto za wananchi wa jiji la Dodoma ambao kwa muda mrefu wamedai viwanja na jiji kuwaahidi bila ya kuwapatia.

Katika kufanikisha zoezi hilo, zimeundwa timu mbili kwa ajili ya upangaji na upimaji na pamoja na ile ya kushughulika na uhakiki wa wananchi wenye migogoro na kustahili kupatiwa  viwanja mbadala.

"Timu hizi zitaanza kazi mara moja na kazi hiyo itafanyika kwa muda wa siku sitini, miezi miwili kazi iwe imekamilika kila mtu kujua amepata nini na anaenda wapi" amesema.

Akigeukia uuzwaji viwanja 1,037 vilivyoingizwa kwenye mfumo wa TAUSI ili wananchi wapate viwanja vilivyopimwa katika eneo la Mahomanyika, Dkt. Akwilapo amuagiza Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kuendelea na uuzaji viwanja kwa waombaji 352 pekee walioanza kulipa huku wale ambao hawajaanza kulipa maombi yao yasitishwe.

Eneo la Mahomanyika limekuwa na changamoto ya malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa wananchi wakidai ni wamiliki wa asili wa maeneo hayo jambo lililosababisha kuundwa kwa Timu (Timu ya DC) ambayo ilishirikisha wananchi, Vyombo vya Usalama na Wataalam ambapo timu hiyo ilibaini eneo husika ni eneo la Serikali.
Posted by MROKI On Wednesday, February 25, 2026 No comments

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila leo Feb 25,2026 amekutana na Gavana wa Jimbo la Maniema-Congo DRC Mhe Mussa Kabwankubi Moise akiwa ameambatana na ujumbe wake alipomtembelea Ilala Boma Jijini Dar es Salaam.

Katika mazungumzo yao wamekubaliana mashirikiano katika nyanja mbalimbali ikiwemo Uchumi na Masuala ya Kiusalama kati ya Mkoa wa Dar es Salaam na Jimbo la Maniema.

Aidha RC Chalamila amesema Congo na Tanzania ni majirani na ni marafiki wa muda mrefu ndiyo maana katika Mkoa wa Dar es Salaam wakongo ni wengi na wanajishughulisha na shughuli mbalimbali ikiwemo biashara

"Ukiangalia  kupitia Bandari ya Dar es Salaam mzigo unaokwenda Congo kitakwimu ni kiasi kikubwa kwa mwaka hivyo Mkoa unathamini sana wacongo" Alisema Chalamila










Posted by MROKI On Wednesday, February 25, 2026 No comments
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imetoa Tuzo za ubunifu kwa washindi 9 waliotoa mawazo bora zaidi yatakayosaidia kuendelea kuboresha huduma za kodi na kuongeza wigo wa kodi. 

Akikabidhi tuzo hizo, vyeti pamoja na hundi kwa washindi hao Februari 25.2026, Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar ameipongeza TRA kwa kuja na Tuzo hizo ambazo zitaongeza ukaribu na ushirikishwaji wa wananchi katika masuala ya ukusanyaji wa kodi. 

Mshindi wa jumla katika tuzo hizo ni Gabriel Mashenene ambaye amepatiwa hundi ya Sh. Milioni 50, washindi watatu wamepatiwa Sh. Milioni 30 kila mmoja huku washindi 5 wakipatiwa Sh. Milioni 20  kwa kila mmoja.










Posted by MROKI On Wednesday, February 25, 2026 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo