Nafasi Ya Matangazo

September 01, 2026


Balozi wa Uingereza nchini Tanzania Mh.  Marianne Young amekutana na Waziri wa Madini, Mh. Anthony Mavunde, kwa na kufanya  mazungumzo kuhusu sekta ya madini nchini Tanzania na fursa za kuimarisha ushirikiano kati ya Uingereza na Tanzania.

Mkutano huo ulijadili kuhusu uwekezaji, uongezaji wa thamani, na kuhakikisha sekta hiyo inachangia katika ukuaji wa uchumi unaoshirikisha wote ulifanyika jijini Dodoma leo Septemba 1, 2026.





Tanzania na Uingereza zitaendelea kushirikiana katika maeneo yenye manufaa kwa pande zote mbili ili kudumisha ustawi wa mataifa yote mawili.
Posted by MROKI On Tuesday, September 01, 2026 No comments

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema jukumu kuu la Wizara ya Nishati ni kuhakikisha wananchi wanapata umeme wa uhakika na wanapatiwa taarifa kwa wakati pindi changamoto zinapojitokeza.

Mhe. Makamba ameyasema hayo leo, tarehe 01 Septemba 2026, wakati akijibu Swali lanMhe. Exaud Silaoneka Kigahe, Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kaskazini, aliyetaka kufahamu lini Serikali itabadilisha mkataba wa usambazaji wa umeme kwa wananchi kutoka Mwenga Power kwenda TANESCO, ili Mwenga Power ibaki kuwa mzalishaji wa umeme.

Akijibu swali hilo, Mhe. Makamba amesema utoaji na usimamizi wa leseni za uzalishaji na usambazaji wa umeme nchini ni jukumu la kisheria la Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA), kwa mujibu wa Sheria ya Umeme ya mwaka 2008 na taratibu za utoaji wa leseni hizo.

“Jukumu namba moja la Wizara ya Nishati ni kuhakikisha wananchi wanapata umeme wa uhakika na wanapata taarifa kwa wakati kunapotokea changamoto,” amesema Mhe. Makamba.

Ameeleza kuwa uamuzi wowote wa kubadili muundo wa leseni ya usambazaji umeme katika eneo hilo unapaswa kuzingatia matakwa ya sheria na taratibu zilizowekwa.

Hata hivyo, Mhe. Makamba amesema Serikali, kwa kutambua kuwa kumekuwa na malalamiko kuhusu ubora wa huduma inayotolewa na Mwenga Power, tayari taasisi zake za EWURA, TANESCO na REA zimeanza kufanya tathmini ya kina ili kubaini uwezekano wa kufanya mabadiliko hayo bila kuathiri uwekezaji uliopo.

Amesema tathmini hiyo itafanyika kwa haraka ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya umeme yenye uhakika na inayokidhi mahitaji yao.

Aidha, akihitimisha, Mhe. Makamba amesema yupo tayari, pindi Vikao vya Bunge vitakapokamilika, kuongozana na Mhe. Exaud Silaoneka Kigahe, Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kaskazini, kwenda kusikiliza na kufahamu kwa kina changamoto zinazowakabili wananchi katika eneo hilo.
Posted by MROKI On Tuesday, September 01, 2026 No comments


Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SJMT) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) zimekubaliana kuondoa jambo la 15 la Maliasili ya mafuta, pamoja na mafuta yasiyochujwa ya motokaa na mafuta ya aina ya petroli na aina nyinginezo za mafuta au bidhaa, na gesi asilia katika orodha ya mambo ya Muungano.
 
Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa wakati akijibu swali la Mbunge wa Mtambwe Mhe. Rashid Habib Ali Rashid aliyeuliza Serikali ina mpango gani wa kuondoa suala la Mafuta na Gesi kwenye orodha ya Masuala ya Muungano.
 
Akiendelea kujibu swali hilo, Mhe. Kwagilwa alisema kwa sasa, suala la Mafuta na Gesi Asilia linasimamiwa na kila upande ambapo SJMT imetunga Sheria ya Mafuta na Gesi Asilia ya Mwaka 2015 ambayo chini ya kifungu cha 11 imeanzisha Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA - Petroleum Upstream Regulatory Authority).

Aliongeza kuwa kwa upande wa Zanzibar, SMZ imetunga Sheria ya Utafutaji na Uchimbaji wa Mafuta na Gesi Asilia, Namba 6 ya Mwaka 2016 iliyoanzisha Mamlaka ya Udhibiti, Utafutaji na Uendelezaji wa Mafuta na Gesi Asilia (ZPRA – Zanzibar Petroleum Regulatory Authority) na Kampuni ya Maendeleo ya Mafuta na Gesi Asilia Zanzibar (ZPDC – Zanzibar Petroleum Development Corporation).

“Mheshimiwa Naibu Spika Kwanza niungane na Mheshimiwa mbunge ambaye amesema kwamba Baraza la Wawakilishi lilisharidhia na lilishawasilisha kutaka suala hili liondolewe na ndio maana Baraza la Wawakilishi limetunga sheria ya kuanzisha Mamlaka ya Udhibiti na hivyo linashughulikiwa katika kila upande hivyo halina hoja kinzani,” alifafanua Kwagilwa.

Pamoja na hayo, kila ongezeko au kuondolewa kwa masuala ya Muungano hupata nafasi ya kujadiliwa na kupata ridhaa ya Serikali zote mbili ya SJMT na SMZ na kupitia mchakato mahususi wa kikatiba.

Mabadiliko husika hupitia katika Baraza la Wawakilishi na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ibara ya 98(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 inaruhusu Bunge kutunga sheria kwa ajili ya kubadilisha masharti yoyote ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lakini kwa utaratibu maalumu ufuatao ulioainishwa na Katiba.
 
Posted by MROKI On Tuesday, September 01, 2026 No comments
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi akizungumza na Wananchi wa Mbuyuni, Moshi Mjini, waliojitokeza kumlaki akiwa katika ziara binafsi mkoani Kilimanjaro, leo tarehe 01 Septemba 2026.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi, amewasalimu Wananchi wa Mbuyuni, Wilayani Moshi waliokusanyika kumlaki akiwa katika ziara binafsi mkoani Kilimanjaro leo tarehe 01 Septemba 2026.
 
Akiwasalimu wananchi hao, Makamu wa Rais amewasihi kuendelea kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na yeye binafsi ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi. Amesema kwa imani ya maombi ataweza kumsaidia kwa hekima na utii Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Makamu wa Rais amesema ataendelea kutekeleza wajibu wake kwa uadilifu, umakini na kujituma, akisisitiza utayari wake wa kushirikiana na viongozi pamoja na wananchi.
 
Akizungumza kwa msisitizo, Makamu wa Rais amesema: “Hatawazingua Wana wala hatamzingua Mama,” kauli ambayo aliitoa pia mkoani Dodoma, kwa wananchi wa Chamwino, mara baada ya kuapishwa.
 
Awali, Makamu wa Rais aliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) ambapo alipokelewa na viongozi mbalimbali wa Serikali, Viongozi wa Dini na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Kilimanjaro.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi akisalimiana na Viongozi mbalimbali wakati alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro, leo tarehe 01 Septemba 2026.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi akisalimiana na Viongozi mbalimbali wakati alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro, leo tarehe 01 Septemba 2026.

Posted by MROKI On Tuesday, September 01, 2026 No comments


Kwa mara ya kwanza watalamu wa upasuaji wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na mwenzao kutoka Mradi wa Little Heart wa Shirika la Muntada lililopo nchini Uingereza Dkt. Ahmet Sasmazel wamemfanyia upasuaji wa moyo mtoto aliyezaliwa na mishipa miwili mikubwa ya damu inayotoka kwenye moyo kupishana (Nikaidoh Operation).


Upasuaji huo umefanyika kwa njia ya kufungua kifua kwa mtoto mwenye umri wa miaka miwili na mwezi mmoja kwa mafanikio makubwa.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii leo jijini Dar es Salaam Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Thabit Ramadhani alisema upasuaji huu ni wa kwanza kufanyika JKCI na Afrika Mashariki na Kati.

“Tumefanya upasuaji huu kwa umakini mkubwa, na sasa mtoto anaendelea vizuri, ameshatolewa katika chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU) na kupelekwa katika chumba cha ungalizi wa watoto (PICU)”, alisema Dkt. Thabit.

Dkt Thabit alisema mtoto huyo mbali na kuwa na mishipa mikubwa ya damu inayotoka kwenye moyo kupishana pia alikuwa na tundu kwenye moyo pamoja na uvimbe uliosababisha mshipa wa damu kusinyaa hivyo kuzuia damu kutoka kwenye moyo kwenda kwenye mwili na mapafu kwa mtiririko unaostahili.

 “Tatizo hili la mshipa wa damu unaopeleka damu kwenye mapafu kusinyaa ulisababishwa na kukandamizwa na uvimbe aliokuwa nao mtoto hivyo kutoruhusu damu kupita kwa urahisi, tumemuwekea mtoto mrija wa damu bandia ili kuwezesha damu kwenda kwenye mapafu”, alisema dkt. Thabit.

Kwa upande wake Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka Mradi wa Little Heart wa Shirika la Muntada lililopo nchini Uingereza Dkt. Ahmet Sasmazel alisema mafanikio ya upasuaji huo yametokana na ushirikiano wa karibu uliokuwa ukifanywa na watalaamu wa JKCI.

“Tumepata matokeo mazuri ya upasuaji huu kwasababu ya uwepo wa vifaa tiba vya kisasa na watalaamu waliobobea ambao wana moyo wakuhudumia watoto kama hao na kujikita katika kuokoa maisha yao, waendelee kujifunza kwaajili ya matokeo mazuri zaidi ya baadaye”, alisema Ahmet.

Naye mama wa mtoto aliyefanyiwa upasuaji huo Witness Kibuga alisema mtoto wake aligundulika kuwa na tatizo la moyo akiwa na umri wa miezi saba na kuanza kuudhuria kliniki ya matibabu ya moyo hadi sasa alipofanyiwa upasuaji huo.

 “Namshukuru Mungu na watalaamu wote wa JKCI kwa kumfanyia upasuaji mtoto wangu ambaye kwa sasa anaendelea vizuri naomba waendelee na moyo wa kuwahuduma watoto wetu na kuokoa maisha yao kwani tunawategemea sana”, alisema Witness.
- Mwisho -

CAPTION

PICHA 2

Wataalamu wa upasuaji wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimfanyia upasuaji wa moyo mtoto wa miaka miwili (Nikaidoh Operation) kwa kushirikiana na daktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka Uturuki Ahmet Sasmazel wa Mradi wa Liitle Aid wa Shirika la Muntada Aid jijini Dar es Salaam.

 

PICHA 2.

Mama wa mtoto Deus Mgonzo, Witness Kibuga akiwa na Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Idd Kimaro katika chumba cha ungalizi wa watoto (PICU) alipolazwa mtoto huyo jijini Dar es Salaam

Posted by MROKI On Tuesday, September 01, 2026 No comments

August 31, 2026

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano) Mhe. Deus Sangu akiteta jambo na  Sheikh Mkuu wa Jumuiya ya Waithna’ashariyyah Tanzania (TIC) Sheikh Hemed Jalala (Kushoto) Pamoja na Mwenyekiti wa Taifa wa Jumuiyah ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT) Sheikh Alhad Mussa Salum (Kulia) katika hafla ya kumbukizi ya mazazi ya Mtume Muhammad (Sallallahu Alayhi Wasallam) iliyofanyika Agosti 30,2026 katika uwanja wa Kigogo Posti, Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano) Mhe. Deus Sangu akiteta jambo na  Sheikh Mkuu wa Jumuiya ya Waithna’ashariyyah Tanzania (TIC) Sheikh Hemed Jalala (Kushoto) Pamoja na Mbunge wa Jimbo la Kinondoni Mhe. Abbas Tarimba (Kulia) katika hafla ya kumbukizi ya mazazi ya Mtume Muhammad (Sallallahu Alayhi Wasallam) iliyofanyika Agosti 30,2026 katika uwanja wa Kigogo Posti, Jijini Dar es Salaam.
**************
Na: OWM (KAM), Dar es Salaam
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu ametoa wito kwa wananchi na Taasisi za dini kuendelee kushirikiana na Serikali katika kudumisha amani, upendo, umoja na mshikamano, akisisitiza kuwa misingi hiyo ni nguzo muhimu katika kujenga Taifa imara.

Aidha, pia amewasihi kuhusu suala la malezi bora na uadilifu kwa watoto na vijana ili kuepuka athari za mmomonyoko wa maadili pamoja na kutokomeza ukatili dhidi ya watoto, kwa lengo la kujenga kizazi kijacho chenye maadili na upendo.
 
Mhe. Sangu ametoa wito huo (Jumapili, Agosti 30, 2026) alipomwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba katika hafla ya kumbukizi ya mazazi ya Mtume Muhammad (Sallallahu Alayhi Wasallam) iliyofanyika katika uwanja wa Kigogo Posti, Jijini Dar es Salaam.

Amesema Serikali inatambua mchango wa Taasisi za Dini katika kuimarisha mshikamano wa kijamii; kukuza maadili ya uadilifu, uwajibikaji na upendo; kutoa huduma za kijamii kama vile elimu, afya na msaada wa kijamii pamoja na kuelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa amani na mshikamano wa kitaifa.

“Serikali inatambua nafasi ya Jumuiya ya Waithna’ashariyyah Tanzania (TIC), ikiongozwa na Sheikh Mkuu wa TIC Maulana Sheikh Hemed Jalala na taasisi zote za dini katika kuimarisha mahusiano mema, amani na utuivu,” amesema

Kadhalika, ametoa wito kwa waumini wa dini ya kiislamu kuyashika na kuyaishi kwa vitendo mafundisho na Maisha ya Mtume Mohammad (S.A.W) dini hususan katika kuimarisha maadili, upendo, amani na mshikamano katika jamii ili kujenga Taifa lente maadili mema na uwajibikaji.

Kwa upande mwengine, Waziri Sangu amewasilisha salamu za Sikukuu ya Maulid kutoka kwa Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba na pia kuwapongeza kwa kuendelea kushirikiana na Serikali katika kudumisha Amani, mshikamano na umoja wa kitaifa.

Pia, Sheikh Mkuu wa Jumuiya ya Waithna’ashariyyah Tanzania (TIC) Sheikh Hemed Jalala,ameishukuru Ofisi ya Waziri Mkuu kwa nia njema ya kushiriki katika Sherehe za Maulid, akisema ushiriki huo ni ishara ya ushirikiano mzuri kati ya Serikali na jamii. Aidha, upendo na Huruma ndo Mafunzo ya Mtume Muhammad (S.W.W) ampapo amezitaka taasisi zote za dini kuendeleza juhudi za kuwaleta pamoja waumini na wasiokuwa waumini kupitia mihadhara na shughuli mbalimbali za kidini zinazolenga kumuenzi na kumsifia Mtume Muhammad (S.W.W), huku akisisitiza umuhimu wa mshikamano na umoja katika jamii.
Posted by MROKI On Monday, August 31, 2026 No comments
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi, pamoja na familia yake wameungana na waumini mbalimbali katika kushiriki Ibada ya Misa Takatifu ya Jumapili, katika Kanisa Katoliki, Parokia ya Paulo wa Msalaba Jimbo Kuu Katoliki Dodoma. Tarehe 30 Agosti 2026.











Posted by MROKI On Monday, August 31, 2026 No comments
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akimpongeza Askofu Jimbo la Mpanda Eusebius Nzigilwa baada ya kuzungumza katika Ibada ya Misa ya Jubilei ya miaka 25 ya Jimbo hilo leo tarehe 30 Agosti, 2026. 
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akizungumza katika Jubilee ya miaka 25 ya Jimbo Katoliki la Mpanda zilizofanyika kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Saint Mary’s  mjini Mpanda, Agosti 30, 2026.
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akizungumza katika Jubilee ya miaka 25 ya Jimbo Katoliki la Mpanda zilizofanyika kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Saint Mary’s  mjini Mpanda, Agosti 30, 2026.
******************
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema Serikali itaendelea kushirikiana kwa karibu taasisi za dini likiwemo kanisa Katoliki katika kuimarisha huduma za kijamii, maendeleo na ustawi wa wananchi, akisisitiza kuwa mchango wa taasisi za dini ni sehemu muhimu ya safari ya maendeleo ya Tanzania.

Dkt. Mwigulu ameyasema hayo leo Jumapili, Agosti 30, 2026, katika maadhimisho ya Jubilee ya Miaka 25 ya Jimbo Katoliki la Mpanda, yaliyofanyika mkoani Katavi, ambapo amesema Serikali inatambua mchango wa Kanisa Katoliki katika maendeleo ya nchi, hususan katika sekta za elimu, afya na huduma za kiroho.

 “Serikali inatambua mchango wa Kanisa na baba Askofu. Kila tunapotaja maendeleo ya nchi yetu, kuanzia mwanzo mpaka hapa tulipofika, hatuwezi kuyataja kwa kina maendeleo hayo bila kutaja mchango wa Kanisa.”

Amesema ushirikiano kati ya Serikali na Kanisa umeendelea kuwa muhimu katika kuhakikisha huduma za kijamii na shughuli za maendeleo zinaimarika, akisisitiza kuwa milango ya Serikali itaendelea kuwa wazi kwa Kanisa na taasisi nyingine za dini katika masuala yanayolenga ustawi wa wananchi.

 “Niwahakikishie Serikali itaendelea kushirikiana na Kanisa na popote pale mlipo na jambo msisite, milango yetu iko wazi ili tuweze kuhakikisha kwamba tufanye jambo lolote linalotufurahisha.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ametoa maelekezo kwa viongozi wa Mkoa wa Katavi na mamlaka husika kuharakisha utekelezaji wa miradi ya barabara, maji na umeme, akisisitiza kuwa wananchi wanapaswa kupata huduma hizo kwa wakati.

Amesema maandalizi ya kukabiliana na uwezekano wa kutokea kwa El Niño yanapaswa kwenda sambamba na hatua za vitendo, ikiwemo ujenzi na uboreshaji wa mifereji na madaraja ili kupunguza athari za mafuriko.

Kuhusu huduma za maji, Waziri Mkuu ameitaka Wizara ya Maji na wahusika wa mradi wa maji Mpanda kuhakikisha wananchi wanapata huduma hiyo ifikapo Desemba 2026, huku akisisitiza pia kuharakishwa kwa miradi ya barabara inayounganisha Katavi na mikoa jirani.

Aidha, Waziri Mkuu amesema Serikali inaendelea kuchukua hatua za kuboresha mazingira ya haki kwa wananchi, akitangaza kuwa Serikali inaelekea kufuta sheria inayohusu utaifishaji wa mifugo, akieleza kuwa hatua hiyo inalenga kuondoa changamoto za wananchi kunyang’anywa mifugo yao.

 “Katika Bunge hili linaloendelea tunakwenda kufuta sheria ya utaifishaji wa mifugo... kumekuwepo na majeraha makubwa ya watu kunyang’anywa katika baadhi ya maeneo. Tunataka tuondoe hayo ili kuhakikisha kwamba wananchi wetu wanaepukana na hayo.”

Pia ametoa maelekezo kwa wasimamizi wa sheria kuacha kukamata vitendea kazi vya wananchi kama pikipiki, bajaji na magari katika utekelezaji wa sheria za makosa mbalimbali, akisisitiza umuhimu wa kutumia utaratibu wa kisheria wa adhabu na faini.

Kwa upande wake, Askofu wa Jimbo Katoliki la Mpanda, Mhashamu Baba Askofu Eusebius Nzigilwa, amemshukuru Waziri Mkuu kwa kutenga muda na kushiriki katika maadhimisho hayo, akisema uwepo wake umeonesha heshima na kuthaminiwa kwa Jimbo la Mpanda na Kanisa Katoliki Tanzania.

 “Ninakushukuru sana. Tunaona hiyo ni heshima kwa Jimbo letu na kwa Kanisa Katoliki Tanzania, na hivyo tunaomba Mwenyezi Mungu azidi kuwaongoza na kuwajalia neema na hekima katika kutuongoza sisi raia na wananchi wenu.”

Naye Balozi wa Baba Mtakatifu nchini Tanzania anayemaliza muda wake, Mhashamu Askofu Mkuu Angelo Accattino, amesisitiza umuhimu wa kuendeleza ushirikiano kati ya Serikali na Kanisa Katoliki, akisema ushiriki wa viongozi wa Serikali na viongozi wa dini mbalimbali katika maadhimisho hayo ni ishara ya mahusiano mema kwa ajili ya ustawi wa jamii.

Maadhimisho hayo yamefanyika katika kuadhimisha miaka 25 tangu kuanzishwa kwa Jimbo Katoliki la Mpanda mwaka 2001, huku viongozi wa Kanisa wakieleza kuwa katika kipindi hicho Jimbo limepiga hatua katika huduma za kichungaji, elimu, afya na ujenzi wa miundombinu kwa ajili ya jamii.

Waziri Mkuu amewapongeza viongozi wa Kanisa, waamini na wananchi wa Jimbo Katoliki la Mpanda kwa kufanikisha Jubilee hiyo, akiwataka kuendelea kushirikiana na Serikali katika kujenga jamii yenye amani, mshikamano na maendeleo.

Watoto wa Shirika la Mtakatifu PMS Jimbo Katoliki Mpanda wakiimba katika Ibada ya Misa ya Jubilee ya miaka 25 ya Jimbo hilo kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari ST.  Mary’s mjini Mpanda, Agosti 30, 2026. 
 Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akimtuza mtoto Ritha Msangama aliyekuwa akiimba pamoja na Watoto wa Shirika la Mtakatifu PMS jimbo la Mpanda ikiwa ni moja ya shamrashamra za Jubilee ya miaka 25 ya Jimbo Katoliki Mpanda kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari  ST. Mary’s mjini Mpanda, agosti  30, 2026.



Posted by MROKI On Monday, August 31, 2026 No comments

August 30, 2026





Na WMA  -  Mwanza
Banda la Wakala wa Vipimo (WMA) limeendelea kuvutia makundi mbalimbali ya wananchi katika Maonesho ya Biashara ya Afrika Mashariki yanayoendelea katika Viwanja vya Furahisha jijini Mwanza, ikiwa ni siku ya tatu, Agosti 30, 2026.

Makundi hayo yameonesha kuvutiwa na elimu ya vipimo tofauti tofauti.

Wakiwa bandani hapo, wengi wa wanafunzi na vijana wameonesha kuvutiwa zaidi na elimu ya matumizi  ya mizani za kielektroniki na pampu za kupimia mafuta.

 Wamesema elimu hiyo inawapa uelewa wa kuwa mabalozi wa vipimo shuleni na majumbani mwao huku wengine wakidai ndoto yao ni kuwa Maafisa Vipimo wa baadae.

Kwa upande wa akina mama wajasiriamali, wengi  wamejikita kujifunza kuhusu matumizi sahihi ya mizani  inayotumika masokoni na waliuliza maswali mengi kuhusu namna ya kutambua ujazo wa mtungi wa gesi ya kupikia wanapoenda kununua.

 Wengi wameipongeza WMA kwa kuwaelimisha jinsi ya kuepuka hasara na kuhakikisha mteja anapata haki yake.

Askari na wazee waliotembelea Banda la WMA wameonesha kuvutiwa na elimu ya vipimo katika sekta ya mafuta ya petroli, saruji na bidhaa nyingine za ujenzi. Askari wamesema elimu hiyo itawasaidia katika doria za kuhakikisha biashara inafanyika kwa haki, wakati wazee wamesema wamepata uelewa mpya wa kulinda familia zao dhidi ya udanganyifu.

Wananchi wote waliotembelea banda hilo wamepongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kuwa na Wakala wa Vipimo nchini. Wamesema uwepo wa WMA umesaidia kulinda haki za walaji na kuweka mazingira bora ya biashara yanayosadifu kaulimbiu ya maonesho isemayo “Usalama na  Amani ni Kichocheo cha Biashara na Uwekezaji".
Posted by MROKI On Sunday, August 30, 2026 No comments

August 28, 2026

Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali inaendelea kutoa elimu kuhusu majukumu mbalimbali yanayotekelezwa na Mamlaka hiyo hususan katika uchunguzi wa kimaabara wa Dawa Asili kwa wadau wa Tiba Asili katika maadhimisho ya wiki ya Tiba Asili ya Mwafrika yanayofanyika katika viwanja vya Uhindini mkoani Mbeya.








Posted by MROKI On Friday, August 28, 2026 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo