Nafasi Ya Matangazo

July 22, 2026

Na.Mwandishi wetu - Dar es Salaam
Kamati ya Kitaifa ya Wataalamu ya Usimamizi wa Maafa imeidhinisha Mpango wa Taifa wa Dharura wa Kukabiliana na Madhara ya El Niño na kuzielekeza Wizara, Idara, Taasisi, Mikoa na Halmashauri kuongeza kasi ya maandalizi ili kupunguza madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na mvua za El Niño zinazotabiriwa kudumu hadi mwisho wa mwaka 2026.

Akizungumza katika kikao hicho, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, ambaye pia ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Dkt. Jim Yonazi, ameelekeza kila sekta kutenga rasilimali zitakazowezesha hatua za kuzuia, kujiandaa, kukabili na kurejesha hali katika eneo lake na pia kuandaa mipango ya dharura ya manunuzi. Pia amesisitiza umuhimu wa kutambua mapema maeneo hatarishi, kufanya tathmini za vihatarishi na kuwahamasisha wananchi wanaoishi katika maeneo hayo kuhamia maeneo salama.

Aidha, Dkt. Yonazi ameelekeza wananchi kupewa elimu kuhusu namna ya kupunguza madhara ya mvua hizo kwa kuweka akiba ya chakula, kulima mazao yanayostahimili mvua nyingi na kutumia fursa zitokanazo na mvua katika kilimo, uvunaji wa maji, ufugaji na uvuvi. Vilevile, amezitaka taasisi husika kuandaa mipango ya kuzuia milipuko ya magonjwa kwa binadamu, mifugo na mimea.

Kamati hiyo pia imeagiza ukaguzi na uboreshaji wa miundombinu muhimu ikiwemo barabara, maji na umeme, kuimarisha usimamizi wa mazingira, kuhakikisha vifaa vya uokoaji, huduma za dharura na mifumo ya mawasiliano vinakuwa tayari wakati wote, pamoja na kuhuisha mipango ya utekelezaji katika maeneo hatarishi. 

Aidha, Wizara, Taasisi, Mikoa na Halmashauri zimeelekezwa kufuatilia kwa karibu utabiri na maelekezo ya kitaalamu kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) ili hatua zote za maandalizi na kukabiliana na athari za El Niño zichukuliwe kwa wakati.











Posted by MROKI On Wednesday, July 22, 2026 No comments






Na Mwandishi Wetu, Kisarawe
Kamati ya Utekelezaji ya Baraza Kuu la Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), imefaya ziara ya mafunzo katika Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Julai 21, 2026, wilayani Kisarawe mkoani Pwani.

Ujumbe huo uliongozwa na Mwenyekiti wa UWT Taifa, Mary Chatanda. Katika ziara hiyo, Wajumbe wa Kamati hiyo, walitembelea kiwanda cha Rafiki Briquettes, kinachochakata makaa ya mawe kuwa nishati safi ya kupikia ambayo ni rafiki wa afya na utunzaji mazingira.

Katika ziara hiyo, Chatanda amesema, wanawake wana mchango mkubwa katika kufanikisha kampeni ya nishati safi ya kupikia kutokana na ukweli kuwa kazi hiyo inafanywa kwa kiwango kikubwa na wanawake.

"Tunamuunga mkono Rais wetu, Dk. Samia Suluhu Hassan, katika kampeni ya kuhimiza matumizi ya nishati safi ya kupikia ili kutunza afya na mazingira. Sisi UWT tunahimiza jamii itumie nishati safi," amesema Chatanda.

Aidha, amesema UWT wapo tayari kuwa mabalozi na kushirikiana na STAMICO katika kutoa elimu kwa wanawake na jamii kwa ujumla ili kuongeza idadi ya watumiaji wa nishati safi nchini.

"UWT tuna vikao na mikutano mingi inayotukutanisha na wanawake na wananchi, hivyo niwaombe wenzetu wa STAMICO watupe wataalamu wa kuja kutoa elimu katika mikusanyiko yetu, ili elimu hiyo iwafikie wananchi wengi zaidi," ameongeza.

Kwa upande wake, Mjumbe wa Kamati hiyo na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Subira Mgallu, ameipongeza STAMICO kwa kusimamia kikamilifu sera ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ambayo ni muhimu katika dunia ya sasa ya maendeleo ya sayansi na teknolojia.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Petro Magoti, aliwashukuru Wajumbe wa Baraza hilo, kufanya ziara ya mafunzo kwani agenda ya nishati safi ni ya kitaifa na kimataifa, hivyo wakawe mabalozi wa kuelimisha wengine watumie nishati hiyo.
Posted by MROKI On Wednesday, July 22, 2026 No comments

July 20, 2026








Chato, Geita
Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, ameanza ziara rasmi ya kikazi mkoani Geita kwa lengo la kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo, kuhamasisha shughuli za kiuchumi na kufuatilia utekelezaji wa maagizo ya Serikali yanayolenga kuboresha maisha ya wananchi.

Mhe. Mavunde, ambaye pia ni Mlezi wa shughuli za maendeleo mkoani Geita, anatarajiwa kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya kimkakati inayotekelezwa katika halmashauri na wilaya za mkoa huo, sambamba na kuzungumza na wananchi kuhusu fursa za maendeleo na mchango wa sekta ya madini katika kukuza uchumi wa Taifa.

Katika siku ya kwanza ya ziara hiyo, Waziri Mavunde amekagua mradi mkubwa wa maji wenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 40, unaotarajiwa kunufaisha zaidi ya wananchi 185,000 kwa kuwapatia huduma ya maji safi na salama. Ameeleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuwekeza katika miradi ya maji ili kuboresha afya, ustawi wa jamii na kuongeza tija katika shughuli za uzalishaji.

Akizungumza baada ya kukagua mradi huo, Mhe. Mavunde amesema upatikanaji wa maji ni msingi muhimu wa maendeleo ya kijamii na kiuchumi, huku akiwataka wakandarasi kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyokidhi thamani ya fedha za umma.

Katika kuendelea kuhamasisha maendeleo ya sekta ya madini, Waziri Mavunde pia ametembelea mradi wa vijana wa ujenzi wa kiwanda cha kuchenjua madini, akisisitiza kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki yatakayowawezesha vijana kushiriki kikamilifu katika shughuli za uchimbaji na uongezaji thamani wa madini.

Amesema uwekezaji katika viwanda vya uchakataji na uchenjuaji wa madini utaongeza thamani ya rasilimali za madini nchini, kufungua ajira kwa vijana na kuongeza mchango wa sekta hiyo katika ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Aidha, Waziri Mavunde ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa Daraja la Rwantaba, mradi unaotarajiwa kuboresha miundombinu ya usafiri na usafirishaji, kurahisisha shughuli za biashara, kuunganisha maeneo ya uzalishaji na masoko pamoja na kuchochea maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi wa Mkoa wa Geita.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mh. Martin Shigela amesema utekelezaji wa shughuli za maendeleo mkoani Geita unajibu changamoto za wa wananchi kivitendo na kwamba serikali ya mkoa imejipanga kuhakikisha miradi yote ya maendeleo inakamilika kwa wakati.
Posted by MROKI On Monday, July 20, 2026 No comments

July 18, 2026



📍Bagamoyo - PWANI
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Pwani inaendelea kutekeleza majukumu yake ya kusimamia sheria za Forodha kwa lengo la kuhakikisha kunakuwepo ushindani wa haki katika biashara na kulinda mapato ya Serikali.

Katika operesheni iliyofanyika tarehe 16 Julai 2026 wilayani Bagamoyo, TRA imekamata Jahazi likiwa na katoni 50 za sabuni aina ya Malaika Brown Soap, zilizoingizwa nchini kinyume na taratibu za Forodha. Hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa sheria unaolenga kuimarisha biashara halali.

TRA Mkoa wa Pwani inaendelea kuwahimiza wafanyabiashara kuzingatia sheria na taratibu za Forodha, huku ikiahidi kuendelea kutoa huduma kwa weledi, kulinda ushindani wa haki na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.
Posted by MROKI On Saturday, July 18, 2026 No comments

July 16, 2026

Katibu Mkuu Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Dkt. Asha-Rose Migiro, amefanya mazungumzo na Balozi wa Norway nchini Tanzania, Mhe. Tone Tinnes, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam.

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika Julai 15,2026, viongozi hao walijadiliana kuhusu uhusiano na ushirikiano mzuri uliopo kati ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na Ufalme wa Norway, pamoja na maeneo ya ushirikiano yanayohusu maendeleo ya kidemokrasia, utawala bora, ujenzi wa taasisi na maendeleo endelevu.





Posted by MROKI On Thursday, July 16, 2026 No comments

July 15, 2026





Dodoma
Kufuatia utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa maabara ya kisasa ya Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), hatua hiyo inakwenda kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha utoaji wa huduma za maabara ya madini kusini mwa Jangwa la Sahara.

Hayo yamesemwa leo tarehe 15 Julai, 2026 na Waziri wa Madini, *Mh.Anthony Mavunde (Mb)* alipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa maabara ya GST uliopo Kizota, Jijini Dodoma.

"Tunamshukuru Rais wetu Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kukubali kutoa fedha za utekelezaji wa mradi huu wa kisasa, unaokwenda kuifanya Nchi yetu kuwa kinara na mahiri katika utoaji wa huduma za maabara za madini"

"Mradi huu pia unakwenda kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha utoaji wa huduma za maabara kwa Nchi za Afrika ya Mashariki na Kati, kutokana na ubora wa huduma hizo kuwa za kimataifa" alieleza Waziri Mavunde.

Aidha, Waziri Mavunde alibainisha kuwa kwa muda mrefu wachimbaji wadogo wamekuwa wakipata changamoto ya upimaji wa sampuli zao kwenye maabara, hali iliyopelekea kushindwa kufanya shughuli zao kiufanisi.

Mavunde alisisitiza kuwa ujio wa maabara hiyo ya kisasa unakwenda kuwa mwarobaini wa changamoto za wachimbaji ikiwa ni pamoja na kuhudumia wachimbaji wengi zaidi kwa ubora wa kimataifa.

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Madini Tanzania, *Mhandisi Ally Samaje* alieleza kuwa ujenzi wa mradi huo wa maabara unagharimu shilingi bilioni 14.3 na upo katika hatua mbalimbali za utekelezaji ambapo unataraji kukamilika ifikapo Mwezi Septemba, 2027. 

Aidha, aliongeza kuwa maabara hiyo ikikamilika itakuwa ni ya kisasa na inakwenda kuhudumia wateja wengi wa ndani na nje ya Nchi.
Posted by MROKI On Wednesday, July 15, 2026 No comments
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imekuletea mashindano ya Wazo Bunifu yanayolenga kupata suluhisho za kibunifu zitakazochangia kuboresha mfumo wa kodi nchini. Hii ni fursa yako ya kuwasilisha wazo lenye tija na kushindania zawadi ya hadi Shilingi Milioni 50.

Mawazo yatakayowasilishwa yanapaswa kulenga eneo moja au zaidi kati ya yafuatayo ; kupanua wigo wa kodi, kurahisisha ukadiriaji na ulipaji wa kodi kwa biashara ndogo ndogo, kuimarisha huduma za kodi za kidijitali, kupunguza gharama za ukusanyaji wa mapato, kutumia teknolojia za kisasa kama AI, Big Data na Blockchain katika usimamizi wa kodi, pamoja na kuboresha utatuzi wa migogoro ya kodi ili kuwa wa haraka, wazi na wenye kuaminika zaidi.

Kutuma Wazo lako ingia tovuti ya TRA, Bonyeza kitufe cha innovation portal fuata hatua zinazofuata, Mwisho wa kutuma wazo lako bunifu ni julai 31, 2026.  

@tratanzania #WazobunifuTRA2026 #Buniwazoushinde
Posted by MROKI On Wednesday, July 15, 2026 No comments

July 13, 2026

Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Thabit Ramadhani akumueleza Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Mhe. Fatma Almasi Nyangasa namna moyo unavyofanya kazi alipotembelea banda la Taasisi hiyo lililopo katika maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.
Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Idd Kimario akimpima Shinikizo la damu Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Mhe. Fatma Almasi Nyangasa alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Mhe. Fatma Almasi Nyangasa akitazama mfano wa saani ya makundi ya chakula alipotembelea banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) lililopo katika maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Mhe. Fatma Almasi Nyangasa akipokea zawadi kutoka kwa daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mohamed Aloyce alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Mhe. Fatma Almasi Nyangasa akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) mara baada ya kutembelea banda la Taasisi hiyo lililopo katika maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini.
*************
Mwandishi Maalumu – Dar es Salaam
Wananchi wametakiwa kutumia fursa ya Maonesh ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA) kutembelea banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ili kupima afya zao na kutambua mapema vihatarishi vya magonjwa ya moyo na magonjwa mengine yasiyoambukiza kupitia kampeni ya Jua Namba Zako.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Mhe. Fatma Almasi Nyangasa alipotembelea banda la  Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) lililopo katika maonesho hayo na kuweza kujua namba zake.

Mhe. Fatma alisema JKCI imewaletea wananchi huduma muhimu zinazowawezesha kufanya uchunguzi wa afya, lakini pia kupata elimu ya kujikinga na magonjwa ya moyo.

“Kuna vitu vingi vya faida katika banda hili kuna huduma zote za msingi zinazohusiana na masuala ya moyo, lakini pia huduma nyingine muhimu za afya zinazopatikana kwa urahisi”, alisema Mhe. Fatma

Aidha Mhe. Fatma alisema kampeni ya Jua Namba Zako ni ya muhimu kwa kuwa inawahamasisha wananchi kujenga utamaduni wa kupima afya mara kwa mara badala ya kusubiri hadi wanapoumwa.

“Mimi tayari nimezijua namba zangu, fika kwenye banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete upime urefu, uzito, shinikizo la damu na vipimo vingine muhimu ili ujue hali yako ya afya”, alisema Mhe. Fatma

Vile vile Mhe. Fatma aliipongeza Serikali kwa uwekezaji mkubwa uliofanywa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na kuifanya  Taasisi hiyo kuwa miongoni mwa vituo vinavyotoa huduma za kisasa za matibabu ya moyo.

Mbali na kampeni ya Jua Namba Zako, Mhe. Fatma aliwahamasisha wananchi kuendelea kushiriki katika kampeni ya Kutoa ni Moyo inayolenga kuchangisha fedha za kuwasaidia watoto wenye matatizo ya moyo kupata matibabu katika Taasisi hiyo.
Posted by MROKI On Monday, July 13, 2026 No comments
 
Na Mwandishi Wetu
Rai imetolewa kwa wadau mbalimbali kujitoa kwa hali na mali kuchangia fedha kwa ajili ya mfuko unaohudumia wagonjwa wa figo na upandikizaji uloto kwa watoto wenye selimundu (sickle cell) wanaopatiwa matibabu katika Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) ya jijini Dodoma.

Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti Taifa wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Mary Chatanda, Julai 13, 2026, jijini Dodoma.

Chatanda amesema, kutokana na gharama kubwa za matibabu ya magonjwa hayo, viongozi, taasisi binafsi, asasi za kiraia na wananchi kwa ujumla hawana budi kuunganisha nguvu ya pamoja, kuwezesha upatikanaji wa shilingi bilioni saba, ili wagonjwa wasio na uwezo, waweze kunufaika na mfuko huo na hatimaye kuokoa maisha yao.

"Wenzetu Hospitali ya Benjamin Mkapa, wamekuja na mpango kabambe wa kukusanya shilingi bilioni saba za kugharamia wagonjwa wa figo na selimundu, na UWT tuliposhirikishwa tuliona ni jambo jema kwani linagusa uhai wa watu, hivyo basi, niwaombe wadau na wananchi kwa ujumla kuchangia kuwezesha kuokoa maisha ya wagonjwa hao," amesema Chatanda.

Aidha, amesema upatikanaji wa fedha hizo utawezesha kuleta matumaini ya wagonjwa hao kuishi tena na ndiyo maana hafla hiyo imepewa jina la "Okoa Maisha Gala".

"Hata jina la tukio hili linajieleza wazi, yaani Okoa Maisha Gala, na sisi UWT tuko sambamba na serikali yetu ambayo imewekeza fedha nyingi katika uboreshaji wa sekta ya afya ili kuokoa maisha ya wananchi kwani wananchi wanapokuwa na afya njema, wanakuwa na uwezo wa kufanya shughuli zao za kujiingizia kipato na kujenga uchumi wa nchi," ameongeza.

Katika kuadhimisha miaka kumi ya utoaji huduma, BMH wameratibu hafla ya uchangiaji ili kupata fedha za kutibu wagonjwa wa figo na selimundu. Hafla hiyo inatarajiwa kuongozwa na Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba, Julai 16, 2026, katika Ukumbi wa Mabeyo wa jijini Dodoma.
Posted by MROKI On Monday, July 13, 2026 No comments

July 12, 2026



 

Posted by MROKI On Sunday, July 12, 2026 No comments

Na Mwandishi Wetu.
Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa Kisheria wa Utoaji wa Ithibati ya Maisha kwa Waandishi wa Habari Wakongwe, hatua inayolenga kutambua na kuthamini mchango wa waandishi wa habari waliolitumikia Taifa kwa muda mrefu na kwa utumishi uliotukuka katika maendeleo ya sekta ya habari nchini.

Uzinduzi huo umefanyika leo, Julai 11, 2026, wakati wa maadhimisho ya JAB Day yaliyofanyika katika Banda la Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwenye Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba).

Kupitia hotuba yake iliyosomwa na Dkt. Egbert Mkoko, Mwenyekiti wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari, Bw. Tido Mhando, alisema mwongozo huo umeandaliwa kwa kuzingatia mamlaka iliyopewa Bodi chini ya Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229 pamoja na Kanuni zake, ili kuweka utaratibu wa utoaji wa Ithibati ya Maisha kwa waandishi wa habari wakongwe waliotoa mchango wa kipekee katika maendeleo ya taaluma hiyo.

Alisema mwongozo huo unawahusu waandishi wa habari ambao wakati Sheria ya Huduma za Habari ilipoanza kutumika mwaka 2016 walikuwa na umri wa miaka 50 au zaidi na walikuwa tayari wametoa mchango mkubwa katika sekta ya habari, lakini hawakupata fursa ya kujiendeleza hadi kufikia sifa za kitaaluma zinazohitajika kwa mujibu wa sheria.

"Mwongozo huu unalenga kuhifadhi historia ya tasnia ya habari, kuthamini mchango wa waandishi wa habari wakongwe na kuhakikisha uzoefu wao unaendelea kuwa sehemu ya urithi wa taaluma ya uandishi wa habari nchini," ilieleza sehemu ya hotuba ya Mwenyekiti.

Bw. Mhando alisisitiza kuwa mwongozo huo hauondoi wala haupunguzi masharti ya msingi yaliyowekwa na Sheria ya Huduma za Habari kuhusu sifa za kupata ithibati kwa waandishi wa habari, bali unaweka utaratibu wa kutekeleza mamlaka ambayo sheria imeipa Bodi kuhusu utoaji wa Ithibati ya Maisha kwa watu wenye utumishi uliotukuka na waliotoa mchango wa kipekee katika maendeleo ya sekta ya habari.

Aidha, aliipongeza Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kuendelea kuiwezesha Bodi kutekeleza majukumu yake na kuimarisha ushirikiano unaolenga kukuza weledi, uwajibikaji na maadili katika taaluma ya uandishi wa habari.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari, Wakili Patrick Kipangula, alisema uzinduzi wa mwongozo huo ni hatua muhimu katika utekelezaji wa Sheria ya Huduma za Habari na unaonesha dhamira ya Bodi ya kuimarisha viwango vya taaluma huku ikitambua na kuthamini mchango wa waandishi wa habari wakongwe waliolitumikia Taifa kwa uaminifu, uzalendo na weledi.

Sambamba na uzinduzi huo, JAB iliendesha mdahalo uliowakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya habari kujadili maendeleo ya sekta ya habari nchini, utekelezaji wa Sheria ya Huduma za Habari pamoja na mafanikio na changamoto zilizojitokeza katika mwaka mmoja wa utekelezaji wa mfumo wa utoaji wa ithibati kwa waandishi wa habari waliokidhi vigezo vya sheria.

Posted by MROKI On Sunday, July 12, 2026 No comments

July 11, 2026

Mkurugenzi wa Sera na Mipango kutoka Wizara ya Nishati,Petro Lyatuu ametembelea banda la Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA ) katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba)leo  Julai 11 2026.



Posted by MROKI On Saturday, July 11, 2026 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo