July 28, 2026
Semina hiyo ya siku mbili imewakutanisha, kwa mara ya kwanza, viongozi waandamizi wa Serikali kutoka pande zote mbili za Muungano, kwa lengo la kujenga uelewa na msimamo wa pamoja kuhusu mawasiliano ya Serikali na umma.
Akizungumza wakati wa ufunguzi, Rais Dkt. Samia amesema mawasiliano ya Serikali yanahitaji uratibu, weledi na mwelekeo wa kimkakati ili kujenga imani ya wananchi kwa Serikali na kulinda maslahi ya Taifa.
“Mawasiliano ni sehemu ya uongozi na nyenzo ya kimkakati ya kulinda maslahi ya Taifa,” amesema Rais Dkt. Samia.
Ameeleza kuwa mawasiliano yanapotumika vizuri hujenga ushirikishwaji na imani ya wananchi kwa Serikali, huku taarifa sahihi zikiwawezesha kuelewa na kushiriki katika mipango ya maendeleo.
“Taarifa za Serikali zinapaswa kutolewa kwa wakati, kwa lugha inayoeleweka na kwa takwimu zilizothibitishwa,” amesema.
Rais Dkt. Samia amesema Serikali zote mbili zimepata mafanikio katika sekta za elimu, afya, miundombinu, nishati na maeneo mengine ya maendeleo, ambayo yanapaswa kuelezwa kwa wananchi kwa ufasaha.
Kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, amesema Serikali zote mbili zimeanza kutekeleza mageuzi makubwa ya uchumi na huduma zinazowagusa wananchi moja kwa moja.
Amesema takribani asilimia 70 ya utekelezaji wa Dira 2050 inategemea ushiriki wa sekta binafsi, hivyo mafanikio yake yanahitaji mawasiliano na ushirikiano wa karibu kati ya Serikali na sekta hiyo.
Awali, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Mpogole Kusiluka, amesema semina hiyo ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais Dkt. Samia ya kuwajengea viongozi uwezo katika mawasiliano ya Serikali na umma.
Amesema mafunzo hayo yatahusu utoaji wa taarifa kwa ufasaha na kwa wakati, pamoja na matumizi sahihi ya vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.
Viongozi mbalimbali wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa Semina Elekezi kwa Mawaziri, Naibu Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuhusu Umuhimu wa Mawasiliano Serikalini, tarehe 28 Julai, 2026, Ikulu ya Tunguu, Zanzibar
Viongozi mbalimbali wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa Semina Elekezi kwa Mawaziri, Naibu Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuhusu Umuhimu wa Mawasiliano Serikalini, tarehe 28 Julai, 2026, Ikulu ya Tunguu, Zanzibar
Viongozi mbalimbali wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa Semina Elekezi kwa Mawaziri, Naibu Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuhusu Umuhimu wa Mawasiliano Serikalini, tarehe 28 Julai, 2026, Ikulu ya Tunguu, Zanzibar
Viongozi mbalimbali wakifuatilia mada wakati wa Semina Elekezi kwa Mawaziri, Naibu Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuhusu Umuhimu wa Mawasiliano Serikalini, tarehe 28 Julai, 2026, Ikulu ya Tunguu, Zanzibar
Viongozi mbalimbali wakifuatilia mada wakati wa Semina Elekezi kwa Mawaziri, Naibu Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuhusu Umuhimu wa Mawasiliano Serikalini, tarehe 28 Julai, 2026, Ikulu ya Tunguu, Zanzibar
Washiriki wa Wiki ya Tisa ya Viwanda kutoka nchi wanachama wa SADC wakifuatilia hotuba ya Mgeni Rasmi, Katibu Mtendaji wa SADC, Elias Magosi, wakati wa ufunguzi wa mkutano huo uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (ICC), Durban, Afrika Kusini.
Meneja wa Utafiti na Biashara Dkt.Hilderbrand Shayo na Meneja wa Mawasiliano, Masoko na Mahusiano Bw. Allan Chonjo, kutoka Benki ya Maendeleo - TIB wakitoa maelezo kuhusu bidhaa na huduma zinazotolewa na Benki hiyo kwa mdau aliyetembelea banda la Tanzania, pembezoni mwa Mkutano wa Wiki ya Viwanda ya SADC (SADC Industrialisation Week 2026) unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (ICC), jijini Durban, Afrika Kusini.
Meneja wa Mawasiliano, Masoko na Mahusiano wa Benki ya Maendeleo - TIB, Bw. Allan Chonjo akitoa maelezo kuhusu bidhaa na huduma zinazotolewa na Benki hiyo kwa baadhi ya wadau waliotembelea Banda la Tanzania, pembezoni mwa Mkutano wa Wiki ya Viwanda ya SADC (SADC Industrialisation Week 2026) unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (ICC), jijini Durban, Afrika Kusini.
Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) imezitaka nchi wanachama kuongeza kasi ya utekelezaji wa ajenda ya maendeleo ya viwanda kwa kuwekeza katika kuongeza thamani ya malighafi na kuimarisha miundombinu ili kukuza biashara, ajira na ustawi wa wananchi wa Jumuiya ya hiyo.
Wito huo umetolewa na Katibu Mtendaji wa SADC, Bw. Elias Magosi, wakati akifungua rasmi Wiki ya Tisa (9) ya Viwanda ya SADC (SADC Industrialisation Week 2026) inayofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Durban, Afrika Kusini.
Alisema kuwa ukanda wa SADC una rasilimali nyingi za kilimo, madini na nishati ambazo zinapaswa kutumika kama msingi wa kujenga uchumi wa viwanda badala ya kuendelea kuuza malighafi bila kuziongezea thamani.
Alisisitiza kuwa maendeleo ya viwanda hayawezi kufikiwa bila ushirikiano wa karibu kati ya serikali, sekta binafsi, taasisi za fedha na wadau wa maendeleo.
“Ushirikiano utasaidia kuvutia uwekezaji, kuongeza ushindani wa bidhaa za ukanda na kuimarisha biashara ndani ya SADC, hatua itakayochochea ukuaji wa uchumi jumuishi na wenye manufaa kwa wananchi wote” alisema Bw. Magosi.
Aidha, alizihimiza nchi wanachama kuwekeza katika miundombinu ya nishati, usafirishaji, TEHAMA na ubunifu, pamoja na kuwawezesha wanawake na vijana kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji na ujasiriamali wa viwanda.
Wiki ya Viwanda ya SADC imebeba kaulimbiu isemayo: "Kukuza Viwanda Imara, Endelevu na Jumuishi kupitia Maendeleo ya Miundombinu, Mageuzi ya Kilimo na Madini kwa Ajili ya Dunia Yenye Haki." Ikihimiza matumizi ya rasilimali zilizopo katika nchi wanachama katika kujenga uchumi wenye ushindani, unaostahimili changamoto za kiuchumi na mabadiliko ya tabianchi.
Mkutano huo wa siku tano unaowakutanisha Viongozi wa Serikali, sekta binafsi, wawekezaji, wataalamu na wadau wa maendeleo kutoka nchi wanachama wa SADC unatarajiwa kutoa mapendekezo yatakayosaidia kuimarisha ushindani wa viwanda kwa nchi za SADC, kuvutia uwekezaji mpya na kuongeza thamani ya mazao ya kilimo pamoja na madini, ukiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea Mkutano wa 46 wa kawaida wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC utakaofanyika tarehe 17 Agosti, 2026 Jijini Durban, Afrika ya Kusini.
July 27, 2026
Rais Dkt. Samia pia ameiagiza Ofisi ya Makamu wa Rais kuimarisha usimamizi wa masuala ya Muungano na kuhakikisha changamoto zinazojitokeza zinatatuliwa kwa ushirikiano ili kuendelea kuulinda na kuuimarisha Muungano. Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuimarisha usimamizi wa mazingira kwa kushirikiana katika utekelezaji wa programu za uhifadhi na kukabiliana na changamoto zinazotishia mazingira na ustawi wa Taifa.
Katika kuimarisha utendaji wa Serikali, Rais ameitaka Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kuweka mazingira bora yatakayowawezesha watumishi wa umma kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi. Kwa upande wa sekta ya uchukuzi, ameelekeza kuongeza kasi ya ujenzi na usimamizi wa miradi ya reli, barabara, bandari na meli, sambamba na kutathmini fursa za kupanua biashara ya anga ya Shirika la Ndege la Tanzania.
Vilevile, Rais Dkt. Samia ameitaka Wizara ya Katiba na Sheria kuendelea kuimarisha upatikanaji wa haki nchini kwa kuongeza kasi ya utekelezaji wa kampeni za msaada wa kisheria ili huduma hizo ziwafikie wananchi wengi zaidi na kuwawezesha kupata haki zao kwa wakati. Aidha, ameitaka Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) kuimarisha ukuzaji wa biashara pamoja na usimamizi wa maonesho ya biashara nchini.
Kwa upande wa uhifadhi wa maliasili, Rais ameliagiza Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kuimarisha usimamizi na ulinzi wa hifadhi za wanyamapori na rasilimali za utalii, akisisitiza kuwa taasisi hiyo ina nafasi muhimu katika kulinda na kukuza sekta ya utalii nchini. Pia amelitaka Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kuendelea kuimarisha nafasi yake kama chombo cha Serikali na sauti ya Taifa kwa kuboresha maudhui, kuongeza ufanisi wa utendaji na kuendeleza weledi wa watumishi wake.
Walioapishwa ni Dkt. Latifa Mohammed Khamis, aliyeteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia masuala ya Muungano, na Bi. Prisca Burton Lwangili, aliyeteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
Viongozi wengine walioapa Kiapo cha Uadilifu kwa Viongozi wa Umma ni Bw. Ephraim Balozi Mafuru, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE); Bw. Salum Nassor Mnuna, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA); Bw. Massana Gibril Mwishawa, Kamishna wa Uhifadhi wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA); na Bi. Asha Dachi Mbaruk, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).












.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)







































