Nafasi Ya Matangazo

August 02, 2026

Maandalizi ya Kizimkazi Festival itakayofanyika Agosti 12 hadi 14, 2026, yamepamba moto. Tamasha hili linalofanyika kila mwaka linatayarajiwa kuwaleta pamoja wananchi, wadau wa utalii, biashara, burudani na uchumi wa buluu katika mandhari ya kipekee ya Kizimkazi visiwani Zanzibar.


Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa  Kamati ya Maandalizi ya Tamasha, Mahfoudh Said Omar, shamrashamra zitaanza Agosti 12 kwa matembezi ya pamoja, yakifuatiwa na maonyesho ya biashara, mdahalo wa uchumi wa buluu na mashindano ya ngalawa yatakayopamba mwambao wa Bahari ya Hindi.

Agosti 13 kutakuwa na uzinduzi wa miradi ya maendeleo na mdahalo wa Nishati Safi, na kisha usiku wake kutakua na tamasha kubnwa la muziki lijulikanalo kama ‘Usiku wa Kizimkazi’ litakalowakutanisha wasanii wakubwa nchini, na maelfu ya wananchi kwa burudani ya pamoja.

Kilele cha Tamasha hilo kitakua Agosti 14 kwa kusherehekewa urithi wa Kizimkazi, vivutio vya utalii na fursa mbalimbali za maendeleo zinazofungua milan
Posted by MROKI On Sunday, August 02, 2026 No comments


Na. WMA- DODOMA
Wakala wa Vipimo (WMA) imetoa elimu kwa wajasiriamali wanaoshiriki Maonesho ya Nane Nane Kitaifa yanayofanyika katika Viwanja vya Dkt. John Malecela Nzuguni  jijini Dodoma, kuhusu umuhimu wa ufungashaji na uwekaji wa taarifa sahihi kwenye bidhaa ili kuongeza ushindani katika soko.

Akizungumza wakati wa kutoa elimu hiyo Agosti 2, 2026, Meneja wa Wakala wa Vipimo Mkoa wa Singida, Willie Amosi, amesema kuwa wamefika katika banda la Halmashauri ya Wilaya ya Iramba kwa ajili ya kukagua bidhaa zinazozalishwa na wajasiriamali pamoja na kutoa maelekezo ya namna ya kuziboresha.

Amesema kuwa lengo la ukaguzi huo ni kuangalia namna bidhaa zilivyofungashwa na kuwashauri wajasiriamali kuhusu maboresho yanayoweza kufanyika ili bidhaa zao ziweze kupata soko ndani na nje ya nchi.

“Katika ukaguzi ambao tumeufanya hapa leo, tumebaini wajasiriamali wanazalisha bidhaa ambazo ni nzuri lakini zina baadhi ya mapungufu ambayo wakiyaboresha yataongeza soko na tija kwenye shughuli zao za uzalishaji,” amesema Amos.

Amebainisha kuwa baadhi ya bidhaa za asili walizoziona kama dengu zina muonekano mzuri lakini hazina taarifa muhimu zinazohitajika kwenye bidhaa, hivyo amewashauri wajasiriamali kuboresha eneo hilo ili kuongeza thamani ya bidhaa zao.

Aidha, amesema kuwa wameona bidhaa za sabuni zinazozalishwa na wajasiriamali hao ambazo zimeweka taarifa za mzalishaji, lakini bado kuna baadhi ya maeneo yanahitaji kuboreshwa ili ziweze kufikia viwango vinavyohitajika sokoni.

Pia ameongeza kuwa baadhi ya bidhaa nyingine hazina taarifa kabisa licha ya kuwa na ubora na mahitaji katika soko, akitolea mfano mahindi yaliyochemshwa ambayo hayajaoneshwa taarifa muhimu kama jina la bidhaa na kiwango kilichopo kwenye kifungashio.

Kwa upande wake, Husseini Maghembe Husseini kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, amesema kuwa wanashiriki Maonesho ya Nane Nane wakiwa na bidhaa mbalimbali ikiwemo mafuta ya alizeti, karanga, dengu, pamba pamoja na mahindi yaliyochemshwa na kukaushwa.

Amesema kuwa kupitia elimu waliyoipata kutoka Wakala wa Vipimo wameweza kutambua umuhimu wa kuweka nembo (logo), mawasiliano ya mzalishaji na taarifa nyingine muhimu kwenye bidhaa zao ili kurahisisha upatikanaji wa wateja.

“Bidhaa zetu zilikuwa zinakuja bila logo, kwa hiyo uuzaji wetu ulikuwa unakuwa tabu pale mtu anapotaka kututafuta tunapatikana kwa njia gani. Tumepata elimu namna ya kupima na kubrand bidhaa zetu,” amesema Husseini.

Ameongeza kuwa elimu hiyo imewasaidia na kuahidi kuwa katika maonesho yajayo watawasilisha bidhaa zilizokamilika zikiwa na taarifa zote muhimu pamoja na mawasiliano yao.

Naye Jackline Lishaberi, Msimamizi wa Manzuki kutoka Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) upande wa Manyoni, amesema wamepata msaada mkubwa kutoka Wakala wa Vipimo katika kuboresha bidhaa zao hasa kwenye eneo la uhifadhi wa asali na matumizi sahihi ya lebo.

Amesema kuwa wameelekezwa namna ya kuweka lebo kwa usahihi kulingana na ukubwa wa vifungashio pamoja na upangaji wa maandishi ili bidhaa zao ziweze kuvutia zaidi katika soko.

Amebainisha kuwa awali walikuwa na changamoto kwenye uwekaji wa lebo hasa kwenye bidhaa za nta na bidhaa nyingine walizokuwa wakiziweka kama maonesho, lakini baada ya kupata elimu wameweza kufahamu namna bora ya kuboresha.

“Watu wa vipimo wametuelekeza namna nzuri ya kuweka label kwa uwiano ulio sawa ili kuweza kuelimisha watu zaidi lakini kuvutia ile biashara, ile bidhaa iweze kwenda katika mfumo mzuri wa kibiashara,” amesema Jackline.
Posted by MROKI On Sunday, August 02, 2026 No comments







Na WMA - DODOMA
Katika siku ya pili ya Maonesho ya Nanenane kitaifa jijini Dodoma, wadau mbalimbali wameonekana kuvutiwa na elimu ya vipimo inayotolewa na Wakala wa Vipimo (WMA) hivyo kuitikia kwa wingi kutembelea Banda hilo.

Tangu mapema asubuhi banda la WMA limekuwa likizungukwa na wakulima, wafugaji, wavuvi na wafanyabiashara wanaotaka kujifunza jinsi ya kutumia na kuhakiki vifaa vya upimaji.

 Wataalamu wa WMA wamekuwa wakitoa elimu kuhusu madhara ya vipimo visivyo sahihi na faida ya kutumia vifaa vilivyohakikiwa katika uuzaji wa mbegu, mbolea, maziwa na mazao mengine.

Akizungumza wakati wa kutoa elimu hiyo, Meneja Mawasiliano wa WMA Bi. Veronica Simba alisema mwitikio ni mkubwa kwasababu wadau wameanza kuelewa kuwa kilimo chenye tija kinategemea vipimo sahihi. “Hii inaonyesha watu wanataka kujua na kujikinga na hasara,” alisema. 

WMA imesema elimu hii itaendelea kutolewa bure kwa siku zote za maonesho chini ya kaulimbiu "Usahihi wa Vipimo vya Mbegu, Pembejeo, Mazao na Bidhaa Sokoni ni Msingi wa Tija na Utekelezaji wa Dira 2050."
Posted by MROKI On Sunday, August 02, 2026 No comments








Na Neema Chalila Mbuja, Dodoma
NAIBU Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. James Milya leo Agosti 02, 2026, ametembelea Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii kwenye Maonesho ya Siku ya  Wakulima Duniani ( Nane Nane) yanayoendelea katika Viwanja vya John Malecela, Nzuguni  jijini Dodoma.

Baada ya kuwasili kwenye Banda la Wizara ya Maliasi na Utalii, Naibu Waziri Milya  alipata fursa ya kuzungumza na wadau mbalimbali wa Sekta ya Utalii sambamba na kujionea uwepo wa wanyamapori hai kwenye maonesho hayo kama kivutio ili kukuza utalii wa ndani.

Amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan amefanya kazi kubwa ya kuitangaza Sekta ya Utalii nje ya mipaka ya Tanzania na kumpongeza kwa kuwa kinara kwenye sekta hiyo.

“Niwapongeze sana Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kazi kubwa mnayoifanya kwenye Sekta ya Utalii, Wanyamapori, Misitu na Nyuki na Malikale kwani kazi hii inalenga kutunza rasilimali tulizonazo Kama nchi,” amesema Mhe. Milya.

Kwa upande wake Balozi wa Tanzania nchini Nigeria aliyeambatana na Naibu Waziri Milya,  Mhe. Hannafi Luqman amesema Tanzania na Nigeria zimekuwa na ushirikiano mzuri wa kidiplomasia na kuongeza kuwa Tanzania itaendelea kuwa mstari wa mbele  kutunza na kutangaza rasilimali ilizonazo. 

Awali kabla ya kupokea ugeni wa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Wizara ya Maliasili na Utalii ilipokea ujumbe wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agness Meena pamoja na Naibu Katibu Mkuu wake Dkt. Fabian Madele ambapo kwa pamoja walipata fursa ya kutembelea banda la Wizara na kuzungumza na wadau mbalimbali wa uhifadhi na wanyamamapori.

Wizara ya Maliasili na Utalii kwa  pamoja na taasisi zake 18 inashiriki Maonesho  ya Wakulima ya  Nane Nane yanayoendelea Viwanja vya John Malecela Nzuguni Dodoma ambapo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mwigulu Nchemba aliyafungua rasmi hapo jana.
Posted by MROKI On Sunday, August 02, 2026 No comments
 



Dodoma
Waziri wa Kilimo Mhe.Daniel Chongolo (Mb) leo tarehe 02 Agosti 2026,ameongoza mamia ya washiriki katika Marathon ya Maadhimisho ya Miaka 10 ya Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) Katika Viwanja vya Dkt.Samweli Malecela Nane Nane Nzuguni jijini Dodoma ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka kumi tangu kuanzishwa kwa taasisi hiyo.

Marathon hiyo imewakutanisha viongozi wa serikali, watafiti, wadau wa sekta ya kilimo, wanamichezo pamoja na wananchi kutoka maeneo mbalimbali nchini, kwa lengo la kuhamasisha Utafiti kwa usalama wa chakula DIRA 2050, kuboresha afya, mshikamano na kutambua mchango wa TARI katika kuendeleza tafiti na teknolojia zinazochochea maendeleo ya sekta ya kilimo nchini.

Akizungumza mara baada ya kukamilika kwa mbio hizo, Waziri wa Kilimo amesema katika kipindi cha miaka 10, TARI imeendelea kuwa nguzo muhimu katika kuibua ubunifu na kufanya tafiti zilizochangia kuongeza tija ya uzalishaji, kuimarisha usalama wa chakula na kuinua uchumi wa wakulima nchini.

Aidha, ametoa wito kwa wananchi kuendelea kuunga mkono tafiti za kilimo na matumizi ya teknolojia zinazozalishwa na TARI ili kuongeza uzalishaji na kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya kilimo.

Maadhimisho ya Miaka 10 ya TARI yanatarajiwa kuendelea kwa shughuli mbalimbali zikiwemo maonesho ya teknolojia za kilimo, elimu kwa wananchi na utoaji wa huduma za ushauri wa kitaalamu kwa wadau wa sekta hiyo.

TARI ilianzishwa kwa Sheria Na. 10 ya Mwaka 2016








Posted by MROKI On Sunday, August 02, 2026 No comments




Na Mwandishi Wetu, Pangani
Viongozi na watendaji wa matawi wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), wilaya ya Pangani mkoani Tanga, wamepatiwa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa masuala mbalimbali ya kichama, kiuongozi na kijamii ili kuboresha utendajikazi wao wa kila siku.

Mafunzo hayo yametolewa Agosti 2, 2026, katika Kata ya Kipumbwi wilayani humo.

Akizungumza katika mafunzo hayo, Mwenyekiti wa Seneti ya vyuo vya kati, vyuo na vyuo vikuu mkoa wa Tanga, Leila Mnaki, ambaye alikuwa miongozo mwa wakufunzi, amesema CCM ni Chama imara kwani misingi yake ipo ngazi za chini za mabalozi na matawi, hivyo ni wajibu wa Chama kutoa mafunzo ya mara kwa mara kwa viongozi wake ili kuboresha utendajikazi.

"Nguvu ya Chama ni wanachama na viongozi wake, ndiyo maana tupo hapa kupata mafunzo ya kutujengea uwezo ili utendajikazi wetu uwe wenye tija kwa manufaa ya Chama na wananchi tunaowahudumia," amesema Mnaki.

Aidha, Mnaki amesema, ni wajibu wa viongozi kuwahudumia wananchi kwa kufuata misingi ya Chama, ambayo imesisitiza kutanguliza maslahi ya wananchi ili kukuza maendeleo.

"Chama chetu hakiongozwi kwa utashi wa mtu, bali kanuni, miongozo na taratibu, ni matumaini yangu kuwa viongozi na watendaji mtazingatia hili katika Utumishi wenu wote," ameongeza.

Awali, mratibu wa mafunzo hayo, ambaye pia ni Katibu wa UVCCM wilaya, Nasri Mkalipa, aliwasisitiza viongozi hao kuzingatia yote na kuyatendea kazi.

"Niwasihi sana tuzingatie yote tutakayofundishwa hapa, kwani mafunzo haya ni mahsusi katika kuboresha utendajikazi wetu na kuonyesha utofauti wa kiuongozi," amesema Mkalipa.

Katika mafunzo hayo, mada mbalimbali zilifundishwa kwa viongozi hao. Miongoni mwa mada hizo ni pamoja na itikadi, kanuni na falsafa ya CCM, uandishi wa muhtasari na utunzaji kumbukumbu.

Pia, masuala ya uongozi wa kimkakati, ukatili wa kijinsia, afya ya akili, usalama barabarani na matumizi ya mitandao ya kijamii.

Ikumbukwe kuwa, mafunzo hayo maalum yamepewa jina la "Darasa la Ushindi" huku yakichagizwa na kaulimbiu ya "T3 - Tujifunze, Tuongoze na Tuwajibike".

Kimsingi, mkakati uliopo ni kufikisha mafunzo hayo katika kata zote 14 za wilaya hiyo, huku walengwa wa mafunzo hayo wakiwa ni wenyeviti, makatibu na makatibu hamasa wa UVCCM wa matawi yote wilayani humo.
Posted by MROKI On Sunday, August 02, 2026 No comments
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Ndugu Aggrey Mwanri akipokewa na kusalimiana kwa tabasamu na bashasha na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, Ndugu John Mongella, Jumamosi, tarehe 1 Agosti 2026, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar Es Salaam, wakati wa mapokezi ya Wajumbe wa Sekreterieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, walioteuliwa hivi karibuni.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro (katikati) akishuhudia makabidhiano ya ofisi na majukumu, kati ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, Komredi Aggrey Mwanri (kushoto pichani) na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, Komredi John Mongella (kulia pichani), yaliyofanyika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar Es Salaam,  Jumamosi, tarehe 1 Agosti 2026.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, akiongoza Kikao cha Sekreterieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, wakati wa kuwapokea na kuwatambulisha wajumbe walioteuliwa na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), hivi karibuni. Katika kikao hicho kilichofanyika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar Es Salaam, Jumamosi, tarehe 1 Agosti 2026, pia Balozi Dkt. Migiro alishuhudia makabidhiano ya ofisi na majukumu kati ya viongozi wapya na wanaoondoka.
Posted by MROKI On Sunday, August 02, 2026 No comments

August 01, 2026




Na WMA - DODOMA.
Wakala wa Vipimo (WMA) umeanza kutoa elimu ya vipimo kwa wakulima, wafugaji na wavuvi katika siku ya kwanza, (Agosti 1, 2026) ya Maonesho ya Wakulima Nane Nane yanayofanyika kitaifa katika Viwanja vya John Malecela, eneo la Nzuguni jijini Dodoma.

Kwenye banda lake lenye kaulimbiu 
"Usahihi wa Vipimo vya Mbegu, Pembejeo, Mazao  na Bidhaa Sokoni ni Msingi wa Tija na Utekelezaji wa Dira 2050," Maafisa Vipimo wa WMA wanatoa elimu ya vipimo na majukumu ya Wakala kwa ujumla katika kulinda haki za wakulima, wafugaji, wavuvi na wanunuzi.  

Akizungumza na waandishi wa habari, Meneja Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma wa WMA Bi. Veronica Simba alisema lengo ni kuhakikisha kila mkulima, mfugaji na mvuvi anaelewa umuhimu wa kutumia mizani na vipimo vingine vilivyohakikiwa na WMA. 

“Kama unauza mahindi, mbolea au maziwa, na kama unanunua pembejeo za mifugo au samaki, kipimo sahihi ndiyo msingi wa faida. Tunataka kila mtu atoke hapa Nane Nane akiwa na uelewa wa kutambua na kudai kipimo sahihi,” alisisitiza Bi. Veronica.

Bi. Veronica aliwataka wakulima, wafugaji, wavuvi na wananchi kwa ujumla kutembelea banda la WMA katika kipindi chote cha maonesho hayo. “Wataalamu wetu wapo hapa kutoa elimu bure. Njoo ujifunze, uulize maswali na hata kutoa maoni yako,” aliongeza.

WMA imesema itatumia kipindi chote cha maonesho hayo kuhamasisha matumizi ya vipimo sahihi kama njia moja ya kutekeleza Kauli Mbiu ya Taifa ya  NaneNane 2026 "Tambua Soko, Ongeza Tija, Kutekeleza Dira 2050" na kuhakikisha sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi inakuwa na ushindani na uhakika wa soko.
Posted by MROKI On Saturday, August 01, 2026 No comments



 

Posted by MROKI On Saturday, August 01, 2026 No comments

Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Taifa, Mary Chatanda, amesema Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa, ni muumini mzuri wa kutumia meza ya mazungumzo kujadili na kufikia muafaka wa masuala mbalimbali ya kimaendeleo.

Chatanda ameyasema hayo, kufuatia kumalizika kwa mazungumzo baina ya Rais Dk. Samia na viongozi wa vyama 18 vya siasa, Julai 30, 2026, Ikulu, Jijini Dar es Salaam.

Chatanda amesema, mazungumzo ya pamoja baina ya serikali na viongozi wa vyama vya siasa ni muhimu katika kuimarisha umoja na mshikamano.

"Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ni muumini mkubwa wa meza ya mazungumzo. Katika meza hiyo, mengi yanajadiliwa kuliko kutumia mitandao ya kijamii kulalamika. Kimsingi, serikali imepokea ushauri kutoka kwa viongozi wa vyama vya siasa, na hapa kama taifa tunapata mawazo chanya ya kujenga na hivyo tunaimarisha umoja na mshikamano wetu," amesema.

Katika hatua nyingine, Chatanda amesema, Rais Dk. Samia amejipambanua kuwa kinara wa kusikiliza hoja kutoka kwa wadau mbalimbali hata wenye itikadi tofauti za kisiasa ili tu kufikia azma ya kujenga taifa letu.

"Linapokuja suala la ujenzi wa taifa, Rais wetu Dk. Samia anasikilizia kila mtu kwani anaamini taifa hujengwa kwa mawazo jumuishi," amesisitiza.

Aidha, katika mazungumzo hayo na viongozi wa vyama vya siasa, Rais Dk. Samia alieleza namna serikali inavyohimiza maridhiano ya kisiasa ili kufanikisha mipango mingi ya kimaendeleo.

Sambamba na hilo, Rais alieleza mchakato ya maridhiano visiwani Zanzibar huku aliwajulisha viongozi hao maandalizi ya mchakato wa maridhiano kuelekea mapitio ya katiba.

Kwa upande wa viongozi wa vyama vya siasa, walitumia mkutano huo kushauri masuala mbalimbali ya kijamii, kiuchumi na kisiasa ambayo serikali inapaswa kufanyia kazi ili kukuza maendeleo na ustawi wa wananchi.
55th




Posted by MROKI On Saturday, August 01, 2026 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo