Nafasi Ya Matangazo

August 01, 2026



 

Posted by MROKI On Saturday, August 01, 2026 No comments

Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Taifa, Mary Chatanda, amesema Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa, ni muumini mzuri wa kutumia meza ya mazungumzo kujadili na kufikia muafaka wa masuala mbalimbali ya kimaendeleo.

Chatanda ameyasema hayo, kufuatia kumalizika kwa mazungumzo baina ya Rais Dk. Samia na viongozi wa vyama 18 vya siasa, Julai 30, 2026, Ikulu, Jijini Dar es Salaam.

Chatanda amesema, mazungumzo ya pamoja baina ya serikali na viongozi wa vyama vya siasa ni muhimu katika kuimarisha umoja na mshikamano.

"Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ni muumini mkubwa wa meza ya mazungumzo. Katika meza hiyo, mengi yanajadiliwa kuliko kutumia mitandao ya kijamii kulalamika. Kimsingi, serikali imepokea ushauri kutoka kwa viongozi wa vyama vya siasa, na hapa kama taifa tunapata mawazo chanya ya kujenga na hivyo tunaimarisha umoja na mshikamano wetu," amesema.

Katika hatua nyingine, Chatanda amesema, Rais Dk. Samia amejipambanua kuwa kinara wa kusikiliza hoja kutoka kwa wadau mbalimbali hata wenye itikadi tofauti za kisiasa ili tu kufikia azma ya kujenga taifa letu.

"Linapokuja suala la ujenzi wa taifa, Rais wetu Dk. Samia anasikilizia kila mtu kwani anaamini taifa hujengwa kwa mawazo jumuishi," amesisitiza.

Aidha, katika mazungumzo hayo na viongozi wa vyama vya siasa, Rais Dk. Samia alieleza namna serikali inavyohimiza maridhiano ya kisiasa ili kufanikisha mipango mingi ya kimaendeleo.

Sambamba na hilo, Rais alieleza mchakato ya maridhiano visiwani Zanzibar huku aliwajulisha viongozi hao maandalizi ya mchakato wa maridhiano kuelekea mapitio ya katiba.

Kwa upande wa viongozi wa vyama vya siasa, walitumia mkutano huo kushauri masuala mbalimbali ya kijamii, kiuchumi na kisiasa ambayo serikali inapaswa kufanyia kazi ili kukuza maendeleo na ustawi wa wananchi.
55th




Posted by MROKI On Saturday, August 01, 2026 No comments





Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam
Kufuatia mabadiliko ya sheria za kodi kwa mwaka wa fedha 2026/2027, Mamkala ya Mapato Tanzania (TRA), imetoa elimu na mafunzo ya kuwajengea uwezo wafanyabiashara na walipakodi ili kuwa na uelewa wa pamoja wa masuala ya kodi.

Mafunzo hayo yameratibiwa na TRA mkoa wa kikodi wa Kariakoo, Julai 30, 2026, Jijini Dar es Salaam.

Katika mafunzo hayo, Meneja wa Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, CPA Paul Walalaze, amesema miongoni mwa mabadiliko ya sheria za kodi ni pamoja kutoa msamaha wa kodi kwa muda wa miezi 12 (mwaka mmoja) kwa mfanyabiashara mpya ambaye mauzo yake kwa mwaka hayazidi shilingi milioni 200.

"Serikali imesikia kilio cha wafanyabiashara wapya ambao wanaanza bishara zao. Katika mabadiliko haya, mfanyabiashara mdogo anayeanza biashara ambaye mauzo yake kwa mwaka hayazidi shilingi millioni 200, atapata msamaha wa kodi katika kipindi cha miezi 12 tangu aliposajiliwa," amesema Walalaze.

Aidha, amesema mfanyabiashara anapoanza kufanya shughuli zake za biashara, anahitaji kujijenga kabla ya kuanza kulipa kodi, hivyo, wafanyabiashara na wajasiriamali wanapaswa kuchangamkia fursa hii kwa kuanzisha biashara kwani wana kipindi cha neema (grace period) cha kujijenga kibiashara kabla ya kuanza kulipa kodi.

Katika hatua nyingine, Walalaze amekumbusha umuhimu wa kufanya miamala ya malipo kwa njia ya kieletroniki ili kuwezesha malipo hayo kufika panapohusika na hivyo kuchangia makusanyo ya kodi.

"Sheria ya Miamala ya Kieletroniki inahimiza malipo yote kama vile ya ununuzi wa mashamba, nyumba, magari, ada za shule, huduma za migahawa na mengineyo, kufanyika kwa njia ya kieletroniki," amesema.

Halikadhalika, Walalaze amewajuza wafanyabiashara hao kuwa, Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) inamtaka wakala wa kodi ya zuio kuwasilisha na kufanya malipo ya VAT alizozuia ndani ya siku kumi ya mwezi unaofuata.

Kimsingi, serikali kupitia TRA, katika utekelezaji wa bajeti kwa mwaka wa fedha 2026/2027, imefanya mabadiliko ya sheria nyingi za kodi ambapo sasa wanao wajibu wa kutoa elimu kuhusiana na mabadiliko hayo kwa wafanyabiashara, walipakodi na wananchi kwa ujumla.

Awali, akizungumza kuhusiana na mafunzo hayo, Kaimu Meneja Msaidizi wa Huduma kwa Walipakodi, Khalid Mchuma, amesema wafanyabiashara wayatumie mafunzo hayo katika utendajikazi wao wa kila siku ili kuendelea kujenga nchi kupitia ulipaji kodi wa hiari na kwa moyo wa uzalendo.
Posted by MROKI On Saturday, August 01, 2026 No comments

July 28, 2026

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, akiongoza Kikao cha Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kilichofanyika katika Afisi Kuu ya CCM, Kisiwandui, Zanzibar, leo Jumanne, tarehe 28 Julai 2026.






Posted by MROKI On Tuesday, July 28, 2026 No comments




Wananchi zaidi ya 500 kutoka Kata za Chanji, Msua, Kantalamba na Kizwite zilizopo Manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa wamenufaika na huduma mbalimbali za afya zilizotolewa bure na Jeshi la Polisi Mkoa wa Rukwa kupitia Zahanati ya Polisi Mkoa wa Rukwa, ikiwa ni sehemu ya kusogeza huduma za afya karibu na wananchi na kuimarisha ustawi wa jamii.


Huduma hizo zilitolewa Julai 28, 2026 katika Zahanati ya Serikali Kizwite, ambapo wananchi walipatiwa vipimo vya kisasa vya Ultrasound, uchunguzi wa magonjwa mbalimbali, ushauri wa kitaalamu pamoja na dawa bila malipo. Huduma hizo ni miongoni mwa huduma ambazo kwa kawaida hazipatikani katika zahanati hiyo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa zoezi hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Shadrack Masija, alisema Jeshi la Polisi linaendelea kutekeleza dhana ya Polisi Jamii kwa vitendo kupitia ushiriki wake katika shughuli za maendeleo na utoaji wa huduma zinazogusa maisha ya wananchi.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Manispaa ya Sumbawanga, Dkt. Robert Lwebangila, aliipongeza Zahanati ya Polisi Mkoa wa Rukwa kwa kushirikiana na Halmashauri ya Manispaa katika kusogeza huduma za afya karibu na wananchi, akisema ushirikiano huo unaimarisha upatikanaji wa huduma bora za afya.

Naye Mkuu wa Kikosi cha Afya Polisi Mkoa wa Rukwa, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Edgar Ullaya, alisema lengo la zoezi hilo ni kuwapatia wananchi huduma za uchunguzi na matibabu bila gharama pamoja na kugundua mapema changamoto za kiafya ili kutoa tiba stahiki.

Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Serikali Kizwite, Dkt. Simon Mjema, alisema huduma za Ultrasound zimeongeza uwezo wa zahanati hiyo kuwahudumia wananchi waliokuwa wakilazimika kusafiri umbali mrefu kufuata huduma hizo katika vituo vingine vya afya.

Kwa upande wake, Kaimu Mtendaji wa Kata ya Chanji, Dominica Mwaipopo, aliishukuru Serikali na Jeshi la Polisi kwa kuandaa huduma hiyo, akisema imepunguza gharama na muda ambao wananchi walikuwa wakitumia kutafuta matibabu.

Baadhi ya wananchi waliopata huduma hizo walieleza kufurahishwa na hatua ya Jeshi la Polisi kusogeza huduma za afya karibu na makazi yao na kuomba zoezi hilo liendelee ili wananchi wengi zaidi wanufaike.

Zoezi hilo ni sehemu ya juhudi za Jeshi la Polisi Mkoa wa Rukwa za kuimarisha ushirikiano na jamii kupitia utoaji wa huduma za kijamii zinazogusa maisha ya wananchi moja kwa moja.
Posted by MROKI On Tuesday, July 28, 2026 No comments
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa ufunguzi wa Semina Elekezi kwa Mawaziri, Naibu Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuhusu Umuhimu wa Mawasiliano Serikalini, tarehe 28 Julai, 2026, Ikulu ya Tunguu, Zanzibar.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amefungua Semina Elekezi ya Mawaziri, Naibu Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuhusu Umuhimu wa Mawasiliano Serikalini, katika Ikulu ya Tunguu, Zanzibar.

Semina hiyo ya siku mbili imewakutanisha, kwa mara ya kwanza, viongozi waandamizi wa Serikali kutoka pande zote mbili za Muungano, kwa lengo la kujenga uelewa na msimamo wa pamoja kuhusu mawasiliano ya Serikali na umma.

Akizungumza wakati wa ufunguzi, Rais Dkt. Samia amesema mawasiliano ya Serikali yanahitaji uratibu, weledi na mwelekeo wa kimkakati ili kujenga imani ya wananchi kwa Serikali na kulinda maslahi ya Taifa. 

“Mawasiliano ni sehemu ya uongozi na nyenzo ya kimkakati ya kulinda maslahi ya Taifa,” amesema Rais Dkt. Samia.

Ameeleza kuwa mawasiliano yanapotumika vizuri hujenga ushirikishwaji na imani ya wananchi kwa Serikali, huku taarifa sahihi zikiwawezesha kuelewa na kushiriki katika mipango ya maendeleo.

“Taarifa za Serikali zinapaswa kutolewa kwa wakati, kwa lugha inayoeleweka na kwa takwimu zilizothibitishwa,” amesema.

Rais Dkt. Samia amesema Serikali zote mbili zimepata mafanikio katika sekta za elimu, afya, miundombinu, nishati na maeneo mengine ya maendeleo, ambayo yanapaswa kuelezwa kwa wananchi kwa ufasaha.

Kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, amesema Serikali zote mbili zimeanza kutekeleza mageuzi makubwa ya uchumi na huduma zinazowagusa wananchi moja kwa moja. 

Amesema takribani asilimia 70 ya utekelezaji wa Dira 2050 inategemea ushiriki wa sekta binafsi, hivyo mafanikio yake yanahitaji mawasiliano na ushirikiano wa karibu kati ya Serikali na sekta hiyo.

Awali, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Mpogole Kusiluka, amesema semina hiyo ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais Dkt. Samia ya kuwajengea viongozi uwezo katika mawasiliano ya Serikali na umma.

Amesema mafunzo hayo yatahusu utoaji wa taarifa kwa ufasaha na kwa wakati, pamoja na matumizi sahihi ya vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.
Viongozi mbalimbali wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa Semina Elekezi kwa Mawaziri, Naibu Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuhusu Umuhimu wa Mawasiliano Serikalini, tarehe 28 Julai, 2026, Ikulu ya Tunguu, Zanzibar
Viongozi mbalimbali wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa Semina Elekezi kwa Mawaziri, Naibu Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuhusu Umuhimu wa Mawasiliano Serikalini, tarehe 28 Julai, 2026, Ikulu ya Tunguu, Zanzibar
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera Bunge Uratibu na Wenye Ulemavu Prof. Palamagamba A. Kabudi akitoa mada inayohusu Muungano na Mawasiliano; Msingi, Muundo na Umuhimu wake wakati wa ufunguzi wa Semina Elekezi kwa Mawaziri, Naibu Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuhusu Umuhimu wa Mawasiliano Serikalini, tarehe 28 Julai, 2026, Ikulu ya Tunguu, Zanzibar.

Viongozi mbalimbali wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa Semina Elekezi kwa Mawaziri, Naibu Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuhusu Umuhimu wa Mawasiliano Serikalini, tarehe 28 Julai, 2026, Ikulu ya Tunguu, Zanzibar

Viongozi mbalimbali wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa Semina Elekezi kwa Mawaziri, Naibu Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuhusu Umuhimu wa Mawasiliano Serikalini, tarehe 28 Julai, 2026, Ikulu ya Tunguu, Zanzibar

Viongozi mbalimbali wakifuatilia mada wakati wa Semina Elekezi kwa Mawaziri, Naibu Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuhusu Umuhimu wa Mawasiliano Serikalini, tarehe 28 Julai, 2026, Ikulu ya Tunguu, Zanzibar
Viongozi mbalimbali wakifuatilia mada wakati wa Semina Elekezi kwa Mawaziri, Naibu Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuhusu Umuhimu wa Mawasiliano Serikalini, tarehe 28 Julai, 2026, Ikulu ya Tunguu, Zanzibar



Posted by MROKI On Tuesday, July 28, 2026 No comments

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Salaam Maalum kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Mhe Xi Jinping iliyokabidhiwa kwake na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Tanzania ni Mhe. Chen Mingjian, Ikulu ya Tunguu, Zanzibar tarehe 28 Julai, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Tanzania ni Mhe. Chen Mingjian, Ikulu ya Tunguu, Zanzibar tarehe 28 Julai, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Tanzania ni Mhe. Chen Mingjian mara baada ya kumaliza mazungumzo yaliyofanyika Ikulu ya Tunguu, Zanzibar tarehe 28 Julai, 2026.

Posted by MROKI On Tuesday, July 28, 2026 No comments
Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Elias Magosi, akizungumza wakati wa ufunguzi wa Wiki ya Tisa ya Viwanda ya SADC (SADC Industrialisation Week 2026), inayoadhimishwa katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (ICC), jijini Durban, Afrika Kusini. Mkutano huo unawakutanisha viongozi wa serikali, sekta binafsi na wadau wa maendeleo kujadili mikakati ya kuharakisha maendeleo ya viwanda na biashara ya kikanda.
Washiriki wa Wiki ya Tisa ya Viwanda kutoka nchi wanachama wa SADC wakifuatilia hotuba ya Mgeni Rasmi, Katibu Mtendaji wa SADC, Elias Magosi, wakati wa ufunguzi wa mkutano huo uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (ICC), Durban, Afrika Kusini.
Meneja wa Utafiti na Biashara Dkt.Hilderbrand Shayo na Meneja wa Mawasiliano, Masoko na Mahusiano Bw. Allan Chonjo, kutoka Benki ya Maendeleo - TIB wakitoa maelezo kuhusu bidhaa na huduma zinazotolewa na Benki hiyo kwa mdau aliyetembelea banda la Tanzania, pembezoni mwa Mkutano wa Wiki ya Viwanda ya SADC (SADC Industrialisation Week 2026) unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (ICC), jijini Durban, Afrika Kusini.
Meneja wa Mawasiliano, Masoko na Mahusiano wa Benki ya Maendeleo - TIB, Bw. Allan Chonjo akitoa maelezo kuhusu bidhaa na huduma zinazotolewa na Benki hiyo kwa baadhi ya wadau waliotembelea Banda la Tanzania, pembezoni mwa Mkutano wa Wiki ya Viwanda ya SADC (SADC Industrialisation Week 2026) unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (ICC), jijini Durban, Afrika Kusini.
********************
 Na Ramadhani Kissimba, Durban
Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) imezitaka nchi wanachama kuongeza kasi ya utekelezaji wa ajenda ya maendeleo ya viwanda kwa kuwekeza katika kuongeza thamani ya malighafi na kuimarisha miundombinu ili kukuza biashara, ajira na ustawi wa wananchi wa Jumuiya ya hiyo.

Wito huo umetolewa na Katibu Mtendaji wa SADC, Bw. Elias Magosi, wakati akifungua rasmi Wiki ya Tisa (9) ya Viwanda ya SADC (SADC Industrialisation Week 2026) inayofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Durban, Afrika Kusini.

Alisema kuwa ukanda wa SADC una rasilimali nyingi za kilimo, madini na nishati ambazo zinapaswa kutumika kama msingi wa kujenga uchumi wa viwanda badala ya kuendelea kuuza malighafi bila kuziongezea thamani.

Alisisitiza kuwa maendeleo ya viwanda hayawezi kufikiwa bila ushirikiano wa karibu kati ya serikali, sekta binafsi, taasisi za fedha na wadau wa maendeleo. 

“Ushirikiano utasaidia kuvutia uwekezaji, kuongeza ushindani wa bidhaa za ukanda na kuimarisha biashara ndani ya SADC, hatua itakayochochea ukuaji wa uchumi jumuishi na wenye manufaa kwa wananchi wote” alisema Bw. Magosi.

Aidha, alizihimiza nchi wanachama kuwekeza katika miundombinu ya nishati, usafirishaji, TEHAMA na ubunifu, pamoja na kuwawezesha wanawake na vijana kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji na ujasiriamali wa viwanda.

Wiki ya Viwanda ya SADC imebeba kaulimbiu isemayo: "Kukuza Viwanda Imara, Endelevu na Jumuishi kupitia Maendeleo ya Miundombinu, Mageuzi ya Kilimo na Madini kwa Ajili ya Dunia Yenye Haki." Ikihimiza matumizi ya rasilimali zilizopo katika nchi wanachama katika kujenga uchumi wenye ushindani, unaostahimili changamoto za kiuchumi na mabadiliko ya tabianchi. 

Mkutano huo wa siku tano unaowakutanisha Viongozi wa Serikali, sekta binafsi, wawekezaji, wataalamu na wadau wa maendeleo kutoka nchi wanachama wa SADC unatarajiwa kutoa mapendekezo yatakayosaidia kuimarisha ushindani wa viwanda kwa nchi za SADC, kuvutia uwekezaji mpya na kuongeza thamani ya mazao ya kilimo pamoja na madini, ukiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea Mkutano wa 46 wa kawaida wa  Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC utakaofanyika tarehe 17 Agosti, 2026 Jijini Durban, Afrika ya Kusini. 
Meneja wa Utafiti na Biashara kutoka Benki ya Maendeleo - TIB, Dkt.Hilderbrand Shayo akimkabidhi zawadi Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani Tanzania (FCC), Bi. Khadija Juma Ngasongwa alipotembelea Banda la Tanzania katika maonesho yanayofanyika sambamba na Wiki ya Tisa ya Viwanda ya SADC (SADC Industrialisation Week 2026) katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (ICC), Durban, Afrika Kusini.
Posted by MROKI On Tuesday, July 28, 2026 No comments

Dar es Salaam,
Kufuatia kuimarishwa kwa mfumo wa udhibiti wa biashara haramu ya madini unaofanywa na Wizara ya Madini kupitia Kikosi Kazi (Taskforce), madini aina ya dhahabu Gramu 4,402.20 yenye thamani ya 1,238,458,594.42 yamekatwa yakitoroshwa.

Hayo yamesemwa tarehe 27 Julai, 2026 na Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde  Jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari.

Serikali kupitia Wizara ya Madini iliunda Kikosi kazi ambacho kinahusisha vyombo vya dola ili kudhibiti biashara haramu ya madini na utoroshaji. Hii ni sehemu tu ya kazi ambazo zimeendelea kufanywa na Kikosi kazi hicho katika kuimarisha mfumo wa ufanyaji biashara ya madini.

"Ndugu zangu, dhahabu hii yenye zaidi ya thamani ya bilioni 1.2 haikupitia katika mfumo rasmi wa ufanyaji biashara ya madini na hivyo kupelekea Serikali kukosa mapato ambayo yangeisaidia kuimarisha utoaji wa huduma mbalimbali kwa wananchi," amesisitiza  Mhe. Mavunde.

Aidha, Waziri Mavunde amebainisha kuwa dhahabu hiyo iliyokamatwa imetaifishwa kwa mujibu wa taratibu za Sheria na imehifadhiwa Benki Kuu ya Tanzania.

Vilevile, Mhe. Mavunde amekielekeza Kikosi Kazi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya dola kumhoji vizuri mtuhumiwa aliyekamatwa na dhahabu hizo kufahamu alikotoka na alikuwa anapeleka wapi, ili kuweza kutibu kabisa mzizi wa vitendo hivyo na kuvunja mnyororo wa wote wa utoroshaji.

Mhe. Mavunde amesisitiza kuwa, iwapo mtuhumiwa aliyekamatwa alikuwa na leseni ya ufanyaji biashara ya madini kufutiwa leseni hiyo mara moja na kuingizwa kwenye orodha maalum ya wenye makosa (blacklisted) ili asiruhusiwe tena kufanya biashara ya madini nchini.

Katika hatua nyingine, Waziri Mavunde ametoa rai kwa wananchi wote kuzingatia na kufuata sheria na mifumo ya ufanyaji biashara ya madini ambayo tumejiwekea kupitia masoko ya madini na vituo vya ununuzi ambavyo vimesambaa Nchi nzima.
Posted by MROKI On Tuesday, July 28, 2026 No comments









Na Neema Chalila Mbuja
NAIBU Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii Bw. Nkoba Mabula leo Julai 27, 2026 amefungua rasmi Kikao Kazi cha Wadau wa Sekta ya Utalii kujadili Rasimu ya Mpango Mkakati wa Miaka Mitano wa wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2026/2030, wenye lengo la kutoa mwelekeo  wa utekelezaji wa pamoja wa malengo yaliyowekwa na vipaumbele vyake.

Akizungumza kwenye kikao hicho kilichojumuisha wadau wa Sekta ya Utalii wakiwemo Wakurugenzi wa Idara za Wanyamapori, Utalii na Malikale, Bw. Mabula amesema mchango wa wadau wa sekta hiyo ni muhimu kwani wao ndio watekelezaji wa mipango, mikakati na vipaumbele mbalimbali vilivyowekwa na Wizara na ndio maana wamealikwa ili kutoa maoni yao juu ya Mpango Mkakati huo ili kufikia malengo yaliyowekwa.

“Kuelekea lengo la kufikia watalii milioni 8 ifikapo mwaka 2030 niwaombe wadau kushirikiana na Wizara ili kuhakikisha malengo yanafikiwa na kuongeza pato la Taifa,” amesema Bw. Mabula.

Akiwasilisha Rasimu ya Mpango Mkakati huo wa Wizara,   Mkurugenzi wa Sera na Mipango kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii,  Bw. Abdullah Mvungi amesema Rasimu ya Mpango Mkakati huo wa Wizara imeainisha ni nini Wizara inataka kufanya, ni vipaumbele gani vya utekelezaji na ni malengo yapi yanapimika sambamba na viashiria vya utekelezaji ili kufikia malengo mahususi. 

Amesema Rasimu ya Mpango Mkakati wa Wizara imeandaliwa kwa kuangalia vipaumbele vya utekelezaji kwa upande wa Serikali ikiwemo mapambano dhidi ya rushwa na Ukimwi, uelekeo wa Dira 2050 ambayo inaitaka Wizara kuhakikisha idadi ya watalii na mapato yatokanayo na utalii vinaongezeka, sambamba na Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya Mwaka 2025.

Kwa upande wa wadau waliotoa maoni ya utekelezaji wa Mpango Mkakati huo wameipongeza wizara kwa kuandaa rasimu iliyogusa maeneo yote ya utekelezaji na kuahidi kushirikiana bega kwa bega na Wizara ili malengo mahususi hayo yaweze kufikiwa.

Miongoni kwa maeneo yaliyopewa kipaumbele ni pamoja na kuongeza nguvu ya kutangaza vivutio vya utalii, kutunza urithi wa malikale na kushirikisha zaidi jamii kwenye shughuli za uhifadhi.
Posted by MROKI On Tuesday, July 28, 2026 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo