Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi amesema kuwa Serikali inatambua jitihada za wabunifu wa nyenzo mbalimbali zinazosaidia kupunguza gesijoto inayotokana na matumizi ya mafuta kwenye vyombo vya moto.February 10, 2026
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi amesema kuwa Serikali inatambua jitihada za wabunifu wa nyenzo mbalimbali zinazosaidia kupunguza gesijoto inayotokana na matumizi ya mafuta kwenye vyombo vya moto.Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Paul Makonda akizungumza katika kikao cha Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2027), Katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ndogo ya Waziri Mkuu Magogoni jijini Dar es Salaam. Kikao hicho kimeongozwa na Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba.
Dar es Salaam, Februari 10, 2026: Katika hatua inayoonesha mwelekeo mpya wa michezo ya kubahatisha nchini, PigaBet imezindua kampeni ya “SHINDA BODA” inayolenga si burudani pekee, bali pia kuwawezesha wachezaji—hasa vijana—kujipatia mtaji wa kujiajiri na kujiongezea kipato kupitia ushindi wa pikipiki mpya kila wiki.
Kampeni hiyo inawapa wachezaji wawili kila wiki fursa ya kushinda boda boda, zawadi ambayo kwa wengi imekuwa nyenzo muhimu ya kujiajiri au kuongeza kipato cha kila siku. Kupitia mfumo wa PigaPoints, kila mchezaji anayeshiriki michezo ya PigaBet ikiwemo Sports Betting, Casino na Aviator hujikusanyia pointi kwa kila bet au raundi, hali inayoongeza nafasi yake ya kuingia kwenye droo ya ushindi.
Akizungumza kuhusu dira ya kampeni hiyo, Meneja Masoko wa PigaBet, Arthur Kazora, alisema kampeni ya Shinda Boda inalenga kuwafanya wachezaji waone thamani ya muda na ushiriki wao.
“Tumelenga kumwezesha mchezaji kubadili ushindi kuwa fursa ya maisha. Boda si zawadi tu, ni chombo cha ajira, ni mtaji na ni mwanzo wa safari ya kujitegemea kiuchumi,” alisema Kazola.
Tofauti na kampeni nyingi za awali, Shinda Boda imebuniwa kuunganisha burudani, ushindi na uwezeshaji wa kiuchumi. Wachezaji hawazuiliwi na mchezo mmoja pekee, bali wanaruhusiwa kucheza michezo mbalimbali ndani ya jukwaa la PigaBet, jambo linalowawezesha kukusanya pointi zaidi na kuongeza nafasi ya ushindi.
PigaBet pia imeendelea kuvutia wachezaji kwa promosheni zinazolinda na kuongeza thamani ya mchezaji, ikiwemo 10% Cashback kila Jumatatu kwa bet zilizopotea, Win Boost hadi 1000%, pamoja na huduma ya 2UP na Cashout, vinavyompa mchezaji udhibiti zaidi wa michezo yake.
Kwa kutambua nguvu ya mitandao ya kijamii, kampeni hiyo pia imefungua milango kwa content creators kupitia PigaBet Content Creator Challenge, itakayoratibiwa na mshirika wao WAKA.WIN. Kupitia mpango huo, wabunifu wa maudhui watapata nafasi ya kunufaika kifedha kwa kushiriki kikamilifu katika kuhamasisha kampeni.
Wadau wa michezo ya kubahatisha na vijana kwa ujumla wamehimizwa kujisajili kupitia www.pigabet.co.tz na kushiriki kampeni hiyo, huku PigaBet ikisisitiza umuhimu wa kucheza kwa uwajibikaji kwa watu wenye umri wa miaka 18 na kuendelea.
Kwa mtazamo mpya unaoangazia ajira na uwezeshaji, Shinda Boda imejipambanua kama kampeni inayotazama mbali zaidi ya ushindi wa muda mfupi, na kuweka msingi wa matumaini mapya kwa vijana wanaotafuta fursa za kujikwamua kiuchumi.
February 09, 2026
Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Bw.Frederic Van de vyver Mkuu wa Jeune Afrique Media Group, kampuni inayoongoza ya habari ya ki-panafrika yenye makao yake makuu jijini Paris, Ufaransa.
February 06, 2026
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Februari 6, 2026 ameahirisha Mkutano wa Pili wa Bunge la 13 jijini Dodoma na kutumia fursa hiyo kuwaasa Watanzania wote kuwa na matumizi chanya ya mitandao ya kijamii na kuifanya kuwa nyenzo muhimu ya kujielimisha, kuendeleza biashara na kueneza ujumbe wa mshikamano.
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema kuwa ahadi za Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan zimeendelea kutekelezwa kikamilifu ikiwemo ya kugharimia kwa asilimia 100 matibabu ya vipimo vya kibingwa kwa magonjwa sugu yasiyoambukiza kama saratani, figo, moyo, sukari, mifupa na mishipa ya fahamu.
WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema mipango inayoandaliwa na Serikali inalenga kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha usafiri na usafirishaji wa bidhaa, viwanda na biashara katika ukanda wa Afrika.
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group imetoa huduma za upimaji na matibabu ya magonjwa mbalimbali kwa watu 138,699 kwa mwaka 2025.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Hospitali ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Dkt. Tulizo Shemu alisema watu wazima 124,959 na watoto 13,740 walipatiwa matibabu mwaka 2025 huku wagonjwa 4,144 kulazwa katika hospitali hiyo kwaajili ya matibabu.
Dkt. Shemu alisema ukilinganisha na mwaka 2024 Hospitali hiyo ilitoa huduma kwa wagonjwa 133,756 kati yao watu wazima walikuwa 109,931 na watoto 23,825 hivyo kuwa na ongezeko la wagonjwa 4,943 huku idadi ya watoto ikipungua na idadi ya watu wazima ikiongezeka.
“Huduma nyingine zilikuwa ni kliniki ya mfumo wa mkojo, kliniki ya magonjwa ya tumbo na ini, kliniki ya magonjwa ya figo, upasuaji mkubwa na mdogo, huduma za fiziotherapia (mazoezi tiba) na huduma za maabara”, alisema Dkt. Shemu.
Aidha Dkt. Shemu alisema kwa mwaka 2025 JKCI Hospitali ya Dar Group ilitoa huduma mpya ambazo hapo awali zilikuwa hazitolewi ikiwemo kuangalia shinikizo la damu kwa masaa 24 (ambulatory blood pressure monitoring), matibabu ya kuangalia umeme wa moyo kwa masaa 24 (ECG Halter Monitoring) na kipimo cha kuchunguza mishipa ya damu ya moyo na mfumo wa umeme wa moyo katika hali ya mazoezi kwa kutumia mashine ya treadmill (Treadmill stress test).
Kwa upande mwingine Dkt. Shemu alisema watu 251 walifanyiwa uchunguzi na matibabu ya magonjwa mbalimbali yakiwemo magonjwa ya moyo, ngiri, vidonda sugu, matatizo ya mifupa na mgongo pamoja na tiba ya kinywa na meno kupitia huduma za tiba mkoba zijulikanazo kwa jina la Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach Services zilizofanyika katika viwanja vya Mbagala wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam.
“Kupitia kambi hiyo jumla ya watu 198 walikutwa na magonjwa mbalimbali na hivyo kupewa rufaa ya kufika JKCI Hospitali ya Dar Group kwaajili ya vipimo zaidi na kuanzishiwa matibabu”, alisema Dkt. Shemu.
Dkt. Shemu alisema mwaka 2025 JKCI Hospitali ya Dar Group ilifanya upasuaji kwa wagonjwa 1,874 ikiwemo upasuaji wa mfumo wa mkojo, upasuaji wa mifupa, Upasuaji wa uzazi, Upasuaji wa pua, masikio na koo, Upasuaji wa matatizo mbalimbali ya wanawake na upasuaji wa jumla.
Upande wa ajira Dkt. Shemu alisema Serikali kupitia Tume ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa mwaka 2025 ilitoa ajira mpya kwa wafanyakazi 149 katika kada mbalimbali zikiwemo za afya, utawala, uhasibu, ugavi, ICT, na nyinginezo.
SERIKALI imewahimiza wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuwekeza katika viwanda vya uchenjuaji na uchakataji wa madini ya dhahabu mkoani Geita ili kuongeza thamani ya madini, kuimarisha ajira, kulinda mazingira na kukuza mapato ya Taifa.
Wito huo umetolewa na Mjiolojia kutoka Ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Geita, John Maganga, wakati wa ziara ya kutembelea masoko ya madini mkoani humo, ambapo amesema Geita ina fursa kubwa ya uwekezaji kutokana na uzalishaji mkubwa wa dhahabu unaofanywa na wachimbaji wadogo na wa kati.
Amesema licha ya uzalishaji huo, bado kuna upungufu wa viwanda vya uchenjuaji na uchakataji wa dhahabu, hali inayosababisha madini mengi kuuzwa yakiwa ghafi bila kuongeza thamani, jambo linalonyima wananchi na Serikali mapato makubwa.
“Ni wakati sasa kwa wawekezaji kuchangamkia fursa zilizopo Geita kwa kujenga viwanda vya uchenjuaji na uchakataji wa dhahabu, hatua itakayopunguza matumizi ya zebaki, kulinda afya za wananchi na mazingira, pamoja na kuongeza mapato ya Serikali,” amesema.
Ameeleza kuwa uanzishwaji wa viwanda hivyo utaenda sambamba na uwepo wa masoko rasmi ya madini, ambayo yameimarisha uwazi, usalama na ufanisi katika biashara ya dhahabu, na kudhibiti vitendo vya magendo vilivyokuwa vikisababisha upotevu wa mapato ya Serikali.
Ameongeza kuwa masoko ya dhahabu yamekuwa kichocheo cha ukuaji wa uchumi wa mkoa wa Geita kwa kuongeza ajira, biashara na mzunguko wa fedha, huku wachimbaji wakinufaika kwa kuuza madini yao kwa bei ya soko na kwa mifumo rasmi ya Serikali.
Kwa upande wake, Afisa Mthaminishaji wa Madini, Peter Jamhuri, amesema mifumo ya kidigitali inayotumika katika masoko ya madini imeongeza uwazi na ufanisi kwa kuwezesha ukusanyaji wa takwimu sahihi za mauzo, jambo linalosaidia wafanyabiashara kupata mikopo kutoka taasisi za fedha.
Amesema mifumo hiyo imeimarisha uwazi na kuondoa magendo, huku akimpongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kusimamia sera na mifumo bora inayochochea maendeleo ya sekta ya madini na uchumi wa Taifa kwa ujumla.
Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, imesaini Hati ya Makubaliano (MoU) na Benki ya CRDB kupitia CRDB Bank Foundation kwa ajili ya uendeshaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Vijana, hatua inayolenga kuimarisha uwezeshaji wa vijana kiuchumi, kijamii na kitaaluma nchini.February 05, 2026
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amekabidhi hundi ya shilingi bilioni 200 kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana, Joel Nanauka ikiwa ni utekelezaji wa vitendo wa ahadi ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoitoa wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, ya kutenga na kutoa mitaji kwa ajili ya kuwawezesha vijana na wanawake.
Pia, Waziri Mkuu amesema uwezeshaji wananchi kiuchumi ni mhimili wa kukuza uzalishaji, biashara, uwekezaji na ustawi wa maisha ya wananchi, hasa vijana na wanawake ambapo amezitaka wizara, taasisi na mamlaka za kisekta zinazoendelea kutekeleza mpango huo kuhakikisha fedha hizo zinawafikia walengwa wote na program zilizokusudiwa na kutoa tija tarajiwa.
“Utoaji wa Hundi ya Shilingi Bilioni 200 unaonesha kwa vitendo kwamba Serikali ya Awamu ya Sita inatekeleza ahadi zake kwa vitendo, si kwa maneno. Tukio hili linaweka msingi mpya wa kuimarisha ushiriki wa vijana na wanawake katika uchumi wa Taifa na kuharakisha safari ya Tanzania kuelekea uchumi jumuishi na endelevu.”
Amekabidhi hundi hiyo leo Alhamisi, Februari 5, 2026 katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma, ambapo pamoja na mambo mengine amesisitiza kuwa mafanikio hayo hayatapimwa kwa kiasi cha fedha kilichotolewa, bali kwa mabadiliko halisi ya maisha ya wananchi, hususan vijana na wanawake.
“Wizara, Taasisi na Mamlaka zote zinazoshiriki katika utekelezaji wa uwezeshaji kiuchumi lazima zibadilishe mtazamo kutoka katika kutoa fedha kwenda katika kusimamia matokeo na kwamba kila taasisi ijiwekee malengo yanayopimika, viashiria vya utendaji na ratiba za utekelezaji, ili kuhakikisha mitaji hiyo inazalisha ajira, kipato na biashara endelevu.”
Waziri Mkuu amesisitiza kwamba uwezeshaji huo usiwe zoezi la kawaida la kiofisi bali uwe chombo cha mageuzi ya kiuchumi, hivyo utekelezaji wa Shilingi Bilioni 200 lazima uendeshwe kwa uwazi na uwajibikaji. “Taarifa za maendeleo zitolewe mara kwa mara, na hatua zichukuliwe dhidi ya matumizi mabaya. Serikali haitasita kuchukua hatua kwa yeyote atakayekiuka dhamira ya uwezeshaji huu.”
Kadhalika, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema katika kipindi kifupi cha Novemba 2024 hadi Januari 2025, Serikali kupitia mifuko na programu za kuwawezesha wananchi kuichumi imetoa mikopo na dhamana zenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 66.9 kwa wanufaika zaidi ya 13,000, wakiwemo vijana na wanawake katika sekta mbalimbali.
Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu); William Lukuvi amemshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwa kinara katika kukuza uwezeshaji kiuchumi pamoja na jitihada mbalimbali anazofanya katika kuhakikisha vijana na wanawake wanashiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi ikiwa ni pamoja na kuwawezesha mitaji.
Waziri Lukuvi amesema hata hivyo, changamoto ya upatikanaji wa mitaji ikiwemo mikopo, vifaa, mashine na mitambo bado imekuwa kikwazo kikubwa cha ukuaji wa shughuli za kiuchumi zinazotekelezwa na vijana na wanawake. ”Kutokana na changamoto hiyo, Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongeza fedha shilingi bilioni 200 kwa ajili ya kuwawezesha vijana na wanawake.
Amesema uwezeshaji huo wa shilingi bilioni 200 ni uthibitisho wa maono na dhamira aliyonayo Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inayolenga kupanua wigo wa upatikanaji wa mitaji ya gharama nafuu kwa vijana na wanawake ili waweze kuwa shindani kitaifa, kikanda na kimataifa.




.jpeg)

.jpeg)
.jpg)






































