Nafasi Ya Matangazo

February 11, 2025

Meneja wa EWURA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Mha. Karim Ally (kushoto), akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mhe. Kanali Ahmed Abbas Ahmed, mara alipo wasili ofisini kwa Mkuu wa Mkoa huyo leo Februari 11,2025  Ruvuma.
********
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mhe. Kanali. Ahmed Abbas Ahmed, ameipongeza EWURA, kwa kuwadhibiti wafanyabiashara wajanja waliokua wakitishia kuficha mafuta kwa kisingizio cha kusubiri bei mpya ya mafuta itangazwe.

Ameyasema leo Februari 11,2025 wakati alipotembelewa na Meneja wa EWURA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Mha. Karim Ally, kwa lengo la kuzungumzia shughuli mbalimbali zinazofanywa na ofisi hiyo ya kanda.

“Hongereni sana EWURA, kuweza kuwadhibiti wafanya biashara wa mafuta wasio waaminifu. Huduma zimekua nzuri wakati wote, pia nawapongeza kwa huu mfumo wenu wa NPGIS, ambao unawasaidia kujua kiasi cha mafuta kilichopo katika vituo vya mafuta” alisema

Pia Kanali Ahmed alitoa rai kwa EWURA kutoa elimu zaidi ya matumizi ya gesi ya kupikia majumbani na gesi asilia kwenye magari ili wananchi wengi wachangamkie fursa hizo mara moja.

Mhandisi Ally alisema ni jukumu la EWURA ni pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa huduma za nishati na maji kwa wakati na kwa gharama sahihi.

Ofisi ya EWURA nyanda za Juu Kusini ina ofisi zake katika jengo la NHIF, Ghorofa ya 6 Mbeya na inasimamia mikoa mitano ukiwepo mkoa wa Ruvuma, Mbeya, Njombe, Songwe na Rukwa.
Posted by MROKI On Tuesday, February 11, 2025 No comments
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akihutubia wakati wa ufunguzi wa Kikao Kazi cha Tano cha Serikali Mtandao kinachofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC). Tarehe 11 Februari 2025.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akihutubia wakati wa ufunguzi wa Kikao Kazi cha Tano cha Serikali Mtandao kinachofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC). Tarehe 11 Februari 2025.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akihutubia wakati wa ufunguzi wa Kikao Kazi cha Tano cha Serikali Mtandao kinachofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC). Tarehe 11 Februari 2025.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akipokea tuzo iliyotolewa na Mamlaka ya Serikali Mtandao kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa ufunguzi wa Kikao Kazi cha Tano cha Serikali Mtandao kinachofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC) leo tarehe 11 Februari 2025. Kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene na kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) Mhandisi Benedict Ndomba.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Ikulu Bw. Mululi Mahendeka, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) Mhandisi Benedict Ndomba, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Makonda pamoja na viongozi mbalimbali wakishiriki Kikao Kazi cha Tano cha Serikali Mtandao kinachofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC). Tarehe 11 Februari 2025.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akisikiliza maelezo kutoka Meneja wa Tafiti, Mafunzo na Ubunifu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) Dkt. Jaha Mvula wakati akikagua mabanda ya maonesho katika Kikao Kazi cha Tano cha Serikali Mtandao kinachofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC). Tarehe 11 Februari 2025.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Ikulu Bw. Mululi Mahendeka, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) Mhandisi Benedict Ndomba, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Makonda katika picha ya pamoja na wajumbe wa bodi ya Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) mara baada ya ufunguzi wa Kikao Kazi cha Tano cha Serikali Mtandao kinachofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC) leo tarehe 11 Februari 2025.
*******************
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ametoa rai kwa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) kukamilisha mchakato wa kusanifu na kujenga Mfumo Mkuu wa Ubadilishanaji Taarifa Serikalini na kuhakikisha Taasisi zote za umma zinajumuishwa katika mfumo huo.
 
Makamu wa Rais ametoa rai hiyo wakati wa Ufunguzi wa Kikao Kazi cha Tano cha Mamlaka ya Serikali Mtandao kinachofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC). Amesema Jambo hilo ni muhimu ili kurahisisha utendaji kazi katika taasisi na kurahisisha utoaji huduma kwa wananchi kama ilivyoelekezwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Taasisi za Umma kuhakikisha kuwa mifumo yao inasomana na kubadilishana taarifa.
 
Aidha Makamu wa Rais amesema Taasisi zote za umma zinapaswa kushirikiana na Mamlaka ya Serikali Mtandao katika hatua zote za ujenzi au ununuzi, usimamizi na uendeshaji wa  Miradi ya TEHAMA pamoja na kuwataka kuwaelekeza Wakuu wote wa taasisi za umma kuzingatia Sheria, Kanuni na Miongozo inayotolewa na Mamlaka husika katika utekelezaji wa shughuli za Serikali Mtandao.
 
Hali kadhalika, Makamu wa Rais ameagiza mikoa ambayo bado haijaanza kutumia utaratibu wa Ofisi ya Kielektroniki (e-office) kuhakikisha wanaaanza kutumia mfumo huo ifikapo tarehe 30 mwezi juni. Aidha ameagiza kituo cha utafiti kiweze kuimarishwa pamoja na kuongezewa eneo la ufanyaji kazi.
 
Makamu wa Rais amesema Serikali itaendelea kuwekeza katika kuwajengea uwezo wataalamu wa TEHAMA na kada nyingine, kwa kuweka mazingira wezeshi ya ufundishaji katika Vyuo Vikuu na Taasisi za elimu ya juu ili viendelee kuzalisha wataalam wa kutosha.
 
Makamu wa Rais amewasihi washiriki wa kikao kazi hicho pamoja na Watanzania wote kwa ujumla, ambao wana sifa za kupiga kura , kushiriki katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 kwa kuhakikisha wanajiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, kugombea nafasi mbalimbali za uongozi na kushiriki kupiga kura ili kuchagua viongozi wenye sifa na uwezo stahiki wa kusimamia na kuratibu shughuli za maendeleo katika ngazi husika.
 
Kwa upande wake Waziri Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene amesema lengo la kikao hicho ni kuwakutanisha wadau mbalimbali wa serikali mtandao kutoka katika Taasisi na Mashirika ya Umma na Sekta binafsi ili kuwapa fursa ya kujadili hatua iliyofikiwa katika jitihada ya serikali mtandao. Amesema kikao hicho kitaangazia mafanikio yaliyopatikana na changamoto zinazojitokeza wakati wa utekelezaji wa jitihada hizo na namna ya kukabiliana nazo.
 
Aidha ameongeza kwamba Tanzania imepiga hatua na kupata mafanikio katika utoaji huduma ambapo ilipata ushindi wa nafasi ya pili barani Afrika katika Ripoti ya utafiti ya Benki ya Dunia (2022) katika nchi 198 duniani, kuhusu Ukomavu wa Matumizi ya Teknolojia Duniani katika Utoaji wa Huduma za Serikali na Ushirikishwaji wa Wananchi (GovTech Maturity Index).
 
Awali akitoa taarifa ya kikao hicho Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) Mhandisi Benedict Ndomba amesema kuanzishwa kwa mamlaka hiyo kumeiwezesha serikali kuwa na udhibiti wa moja kwa moja wa mifumo na miundombinu ya TEHAMA inayotumika serikalini pamoja na kulinda usalama wa taarifa za serikali. Amesema Mamlaka ya Serikali Mtandao hutoa msaada wa kiufundi na ushauri kuhusu usalama wa TEHAMA na viashiria vya matishio ya kiusalama mtandaoni kwa Taasisi za Umma pamoja na kukabiliana na mashambulio ya kimtandao pindi yanapojitokeza.
 
Kikao hicho kinashirikisha zaidi ya washiriki 1300 ambapo Kauli mbiu ya kikao kazi hicho ni “Jitihada na ubunifu wa Serikali Mtandao kwa utoaji wa huduma za umma kwa ufanisi”.
Posted by MROKI On Tuesday, February 11, 2025 No comments
 Na Mwandishi wetu, Tanga
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imewataka waandishi wasaidizi na waendesha vifaa vya Bayometriki kutoa huduma bora kwa wananchi watakaojitokeza katika zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura linalotaraji kuanza Februari 13 hadi 19, 2025 katika mikoa ya Tanga na Pwani.
 
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taiofa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele wakati alipotembelea mafunzo ya siku mbili ya waandishi wasaidizi na waendesha vifaa vya Bayometriki katika Halmashauri za Jiji la Tanga, Mji wa Korogwe pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe vijijini.
 
“Ninawasihi muwahudumie wateja wenu kwa umahiri na unyenyekevu, msiwe na hasira kwani miongoni mwa wateja mtakao kuwa mnawashughulikia wengine ni wavijijini na wengine ni wamjini hivyo kila mtu anauelewa wake,” alisema Jaji Mwambegele.
 
Jaji wa Rufaa Mwambegele amesema ni jukumulao kuwaelishisha juu ya nini cha kufanya na wakawaeleze kwa upole na si kuwawakali bali kuwasaidia kuwaelekeza kwa unyenyekevu ili zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura liweze kufanikiwa vyema kama ilivyo kusudiwa.
 
Aidha, akizungumza na washiriki hao akiwa Jijini Tanga, Jaji Mwambegele amewataka washiriki hao kuwa waadilifu na kufanya kazi hiyo muhumu kwa taifa kwa moyo na kujituma.
 
Amewataka pia kutunza vifaa vyote watakavyo kabidhiwa wakati wa utekelezaji wa zoezi hilo ili vifaa hivyo vilivyonunuliwa kwa gharama kubwa vikaweze kutumika katika maeneo mengine pindi vikitunzwa vyema.
 
Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura utafanyika mkoani Tanga na Pwani kwa siku saba kuanzia tarehe 13 hadi 19 Februari, 2025 ambapo wapiga kura wapya 431,016 wanatarajiwa kuandikishwa na zoezi hilo litakapokamilika mikoa hiyo itakuwa na wapiga kura 2,727,318 sawa na ongezeko la asilimia 18.7 ya wapiga kura 2,296,302 waliopo kwenye daftari katika mikoa hiyo.
 
Mkoa wa Tanga zoezi la Uboreshaji litafanyika kwenye Halmashauri ya Jiji la Tanga, Halmashauri za Miji ya Handeni na Korogwe na Halmashauri za Wilaya ya Kilindi, Lushoto na Muheza na vituo vitafunguliwa saa 2:00 asubuhi na kufungwa Saa 12:00 jioni kila siku kwa siku saba.
 
Tume imeshakamilisha zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura  kwenye mikoa 27  ya Kigoma, Tabora, Katavi, Geita, Kagera, Mwanza, Shinyanga, Mara, Simiyu, Manyara, Dodoma, Singida, Mjini Magharibi, Kusini Unguja, Kaskazini Unguja, Kusini Pemba, Kaskazini Pemba, Arusha, Kilimanjaro, Mbeya, Iringa, Rukwa, Songwe, Njombe, Ruvuma, Lindi na Mtwara. 
Mwenyekiti wa Tume, Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambege akiteta jambo na afisa Mwandikishaji Msaidizi Jimbo la Tanga mjini Bi. Mwanaidi Nondo. 


Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele leo Februari 11,2025 ametembelea na kuzungumza na washiriki wa mafunzo ya siku mbili ya waandishi wasaidizi na waendesha  vifaa vya bayometriki katika Halmashauri ya jiji la Tanga Mkoani Tanga. Zoezi la Uboreshaji Mkoani humo linataraji kuanza Februari 13 hadi 19 mwaka huu. 




Washiriki wa mafunzo wakisikiliza neno kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume.

Washiriki wa mafunzo kutoka Halmashauri ya Mji wa Korogwe  wakisikiliza neno kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume

Watoa mada wakati wa mafunzo Halmashauri ya Mji wa Korogwe wakiendelea na utoaji mada.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele leo Februari 11,2025 ametembelea na kuzungumza na washiriki wa mafunzo ya siku mbili ya waandishi wasaidizi na waendesha  vifaa vya bayometriki katika Halmashauri ya Mji wa Korogwe na Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe vijijini Mkoani Tanga. Zoezi la Uboreshaji Mkoani humo linataraji kuanza Februari 13 hadi 19 mwaka huu. 


Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele leo Februari 11,2025 ametembelea na kuzungumza na washiriki wa mafunzo ya siku mbili ya waandishi wasaidizi na waendesha  vifaa vya bayometriki katika Halmashauri ya Mji wa Korogwe na Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe vijijini Mkoani Tanga. Zoezi la Uboreshaji Mkoani humo linataraji kuanza Februari 13 hadi 19 mwaka huu. 


Posted by MROKI On Tuesday, February 11, 2025 No comments
Na: Dk. Reubeni Lumbagala, Tanga.
Moja ya changamoto kubwa inayoikabili dunia kwa sasa na Tanzania ikiwepo ni tatizo la ajira hasa kwa vijana. Nchini Tanzania, changamoto hii imekuwa ikiongezeka kutokana na mifumo ya elimu iliyokuwepo ambapo vijana walipokuwa wakihitimu ngazi mbalimbali za elimu kuanzia elimu ya msingi, sekondari, vyuo vya kati na vyuo vikuu, walikuwa wakikosa ujuzi stahiki unaohitajika katika soko la ajira, na hivyo kubaki wakiwa hawana njia za kujiingizia kipato na kuendesha maisha yao. Hii ikapelekea ugumu wa maisha.

Kwa kutambua umuhimu wa stadi na ujuzi kwa vijana, serikali imekuja na mabadiliko ya mtaala wa elimu nchini ambapo sasa mwanafunzi atajifunza elimu ya mkondo wa kawaida pamoja na mkondo wa mafunzo ya amali (elimu ya ufundi), ili pindi atakapohitimu awe na uwanja mpana wa kuajiriwa au kujiajiri kutokana na kuwa na maarifa pamoja na ujuzi wa kutosha ambao ni muhimu sana katika ulimwengu wa sasa wa ushindani wa kazi, ajira na maendeleo.

Akizungumza na vyombo vya habari kabla ya uzinduzi wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014, toleo la 2023, Msemaji Mkuu wa Serikali na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa alisema "Rais Samia alitangaza na kutoa maelezo akitaka Wizara ya Elimu ifanye kazi kubwa ya kupitia sera na lengo lilikuwa ni kuwa na sera ambayo itawaandaa wanafunzi kuwa mahiri katika kujibu mahitaji ya dunia ya sasa".

Aidha, Kwa kuzingatia umuhimu wa mabadiliko ya mtaala nchini, Februari 01, 2025, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan alizindua rasmi Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014, toleo la 2023, katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma. Mabadiliko ya mtaala wa elimu na mafunzo umeambatana na mageuzi katika kufundishwa kwa somo la Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama), Mafunzo ya ufundi stadi kuanzia elimu ya msingi na Matumizi ya akili unde (AI).
Lengo la mageuzi haya ni kuendana na mahitaji ya raslimaliwatu wenye tija yaani wenye ujuzi na ustadi yaliyopo kitaifa na kimataifa. Vilevile, ni kuwafanya wanafunzi na vijana kuwa mahiri na wenye maarifa, stadi, ujuzi na mitazamo chanya katika kuchagiza maendeleo ya taifa.

Katika uzinduzi huo, Rais Samia alisema " Ninachokiona mbele kinahitajika tuwe na maandalizi ya kutosha kwa kuzingatia ubora wa elimu yetu kwa kutoa elimu bora zaidi na kuandaa vizuri zaidi vijana wetu kumudu stadi muhimu zitakazowawezesha kuajiriwa na kujiajiri. Wataalamu wetu wamechambua vizuri mwenendo wa uchumi wetu, mwelekeo wa dunia, kasi ya maendeleo ya dunia na kujifunza kutoka kwa wenzetu, dhamira yetu ni kumwandaa kijana anayejiamini na mwenye nyenzo stahiki kukabiliana na ushindani na anufaike kiuchumi". 

Kipekee, niipongeze Ofisi  ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu chini ya uongozi wa Waziri mwenye dhamana Ridhiwani Kikwete kwa kuitafsiri vyema Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014, toleo la  2023 na kufanyia kazi wajibu wa Wizara hiyo ya kuongeza fursa za ajira kwa vijana kuandaa mafunzo stadi kwa vijana 8,000 wenye umri kati ya miaka 15-35 katika fani mbalimbali huku serikali ikigharamia ada yote ya mafunzo kwa asilimia 100 huku wazazi na walezi wakigharimia mahitaji madogo madogo ya watoto wao. 

Mafunzo yatakayotolewa yanahusisha fani za uashi, ufundi wa vyuma, useremala, ukataji wa madini, ubunifu wa mitindo na ushonaji, umeme wa majumbani. Fani nyingine ni ufundi bomba na magari, uchomeleaji na uungaji vyuma, utengenezaji wa vipuli vya mitambo, upakaji rangi na maandishi ya alama, umeme wa majumbani na viwandani, huduma za hoteli na utalii. 

Mafunzo haya yanatolewa katika vyuo mbalimbali vya ufundi  vilivyopo katika wilaya na mikoa mbalimbali nchini. Muda wa kuomba ni kuanzia Januari 30 hadi Februari 12, 2025. Niwasihi vijana kuchangamkia mafunzo haya ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kupata kipato kwa kuajiriwa na kujiajiri. Hii ni neema na fursa ambayo si ya kuichezea bali kuichangamkia ili kuharakisha maendeleo  yao wenyewe na taifa lao pia. 
Maoni: 0620 800 462.
Posted by MROKI On Tuesday, February 11, 2025 No comments


Na Happiness Shayo- Dar es Salaam
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Chana (Mb) amefungua rasmi Onesho la Wiki ya Wabunifu wa Italia linaloonesha picha za wabunifu mbalimbali wakubwa wa zamani kutoka nchini Italia na  kuipongeza nchi hiyo kwa ushirikiano kati yake na Tanzania kwenye sekta ya utalii.

Ufunguzi huo umefanyika usiku wa Februari 10,2025 katika Kituo cha Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Jijini Dar es Salaam ambapo onesho hilo linatarajiwa  kumalizika Februari 20,2025 likiwa na lengo la kukuza ushirikiano katika masuala ya utalii, historia na uchumi.

 “Italia imejitolea katika juhudi zetu za kukuza utalii endelevu na kuhifadhi urithi wetu wa asili na kiutamaduni .Mfano mmoja mzuri wa ushirikiano huu ni mradi wa Kisiwa cha Bawe, ambao ni mwanzo mzuri unaoonyesha utalii endelevu. Mradi huu hauangazii tu uzuri wa visiwa vya Tanzania bali pia unaonesha matokeo chanya ya uwekezaji wa kigeni katika uchumi wetu.” amesisitiza Mhe. Chana.

Aidha, amesema katika kuendeleza mahusiano hayo Tanzania na Italia zinatarajiwa kuwa na Kongamano la Biashara na Uwekezaji katika siku mbili zijazo, jijini Dar es Salaam ambalo ni jukwaa la mazungumzo, ushirikiano,  na  litatoa matokeo yenye manufaa kwa mataifa yetu yote mawili.
Mhe. Chana amewasihi washiriki wote kutumia tukio hilo kutafiti  njia mpya za ushirikiano, hasa katika nyanja za teknolojia ya kilimo, uchumi wa bluu, uchumi wa kijani, afya na dawa na viwanda vya ubunifu. 

Katika hatua nyingine Mhe. Chana ameiomba Italia kuwekeza kwa vijana wa  Kitanzania kwa kuunga mkono juhudi zao za ubunifu ili kutengeneza mustakabali wao ambapo Tanzania na Italia zinasherehekewa katika soko la kimataifa.

“ Nchi yetu sio tu kitovu cha utalii bali pia ni shamba la uvumbuzi na ubunifu. Vijana wa Kitanzania wamejaa vipaji, na kwa usaidizi na uwekezaji unaofaa, wanaweza kuchukua nafasi yao miongoni mwa wabunifu na wavumbuzi wakuu duniani.” amesisitiza.

Naye, Balozi wa Italia nchini Tanzania, Mhe. Giuseppe Coppola ameweka bayana kuwa onesho hilo ni moja ya fursa ya mashirikiano kati ya Tanzania na Italia na litasaidia pamoja na mambo mengine kufungua fursa za ajira kwa watu pamoja na kuimarisha uhusiano kati ya  taasisi za nchini Italia na Tanzania.

Kwa upande wake, Kamishna wa Biashara wa Shirika la Biashara la Italia kutoka jijini Nairobi, Bw. Giuseppe Manenti amesema kuwa  ni onyesho la kihistoria la heshima lenye umaridadi, ubunifu wa hali ya juu, kwa kuonyesha picha 44 za wabunifu mbalimbali wakubwa wa nchini Italia.
“Onesho hili linaadhimisha washindi wa Tuzo la Compasso d'Oro, lililotafsiriwa upya kupitia lenzi za wapiga picha wa Italia, wa kihistoria na wa kisasa. Mpango huu unalenga kuangazia upigaji picha sio tu kama zana ya hali halisi lakini pia kama njia ya ubunifu ambayo imechangia usambazaji na mafanikio ya ubunifu wa Italia” amesema Bw. Manenti.

Hafla hiyo imehudhuriwa na  Viongozi mbalimbali kutoka Ubalozi wa Italia,  Watendaji kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, Makumbusho ya Taifa la Tanzania pamoja na baadhi ya  wadau wa sekta ya utalii nchini.
Posted by MROKI On Tuesday, February 11, 2025 No comments
Na. Mwandishi wetu,
TASINIA YA Walimu wana jukumu kubwa katika jamii kwa kuhakikisha kuwa watoto wanapata elimu bora, malezi, na ujuzi muhimu kwa maisha yao ya baadaye. Kazi yao ni nguzo muhimu katika kujenga kizazi kilichoelimika na jamii yenye maendeleo.

Hata hivyo, walimu wanakutana na changamoto nyingi zinazohusiana na mazingira ya kazi, maisha ya kijamii, na hali yao binafsi.

Changamoto hizi zinaweza kuathiri ufanisi wao kazini na kuwazuia kufikia malengo yao ya kuwasaidia wanafunzi kwa njia bora.

Kwabkulitambua hilo Chama Cha Walimu (CWT) Kimeanzisha Programu Maalumu ya Samia Teacher's Mobile Clinic ambayo kazi yake ni kutatua changamoto binafsi za walimu, Lengo kuu likiwa ni kuwafikia walimu katika maeneo mbalimbali nchini ili kusikiliza na kutatua changamoto zao .

Licha ya zoezi hili kufanyika katika ngazi za makao makuu ya mikoa, Walimu wengi wamejitokeza wakiwa na changamoto za kiutumishi. Takwimu zinaonesha kuwa katika mikoa 13 ambayo zoezi hili limefanyika Jumla ya Walimu 11,714 wamejitokeza mbele ya timu hiyo kuwasilisha changamoto zao ,

Kikosi kazi cha kusikiliza matatizo ya walimu kilianza kazi kikiwa na lengo la kuifikia mikoa yote ishirini na sita ya Tanzania Bara.

Kazi hii lipangwa kutekelezeka katika awamu 5 kama ifuatavyo:

Awamu ya Kwanza ambayo ilitekelezeka mwezi Novemba 2024 ikihusisha mikoa minne ya Kagera, Kigoma, Katavi na Rukwa.

Awamu ya pili ilitekelezeka mwezi wa Disemba 2024 ikihusisha Mikoa ya Dar Es Salaam na Pwani.

Awamu ya tatu ambayo inahitimishwa leo hapa Mkoani Mbeya, imehusisha Mikoa saba ya Lindi, Mtwara, Ruvuma, Njombe, Iringa, Songwe na Mbeya.

Aidha Awamu ya nne na tano zizatekelezeka mwezi Februari na Machi 2025 kwa kuhusisha mikoa 13 iliyobaki yaani Dodoma, Tabora, Shinyanga, Geita, Mwanza, Mara, Simiyu, Singida, Manyara, Arusha, Kilimanjaro, Tanga na Morogoro. 
Posted by MROKI On Tuesday, February 11, 2025 No comments

February 10, 2025

Na Mwandishi Wetu.
BUNGE limeelezwa mikakati mitano inayofanywa na serikali katika kukabiliana na tatizo la ajira kwa vijana nchini na namna kumudu ushindani kwenye soko la ajira.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema hayo leo Februari 10, 2025 bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mpendae (CCM), Mhe. Toufiq Turky aliyehoji kuna mpango gani wa kuwandaa vyema vijana waweze kushindana katika soko la ajira ndani na nje ya Tanzania ili kukabiliana na upungufu wa ajira nchini.

Akijibu swali hilo, Waziri Kikwete ametaja mipango ya serikali katika kuwaandaa vijana ili kumudu ushindani katika soko la ajira ndani na nje ya nchi.

Mhe. Kikwete amesema, mipango hiyo ni pamoja na kubuni na kutekeleza programu maalum zinazowawezesha vijana kujifunza kwa vitendo kupitia sekta zinazozalisha ajira kwa wingi kama vile sekta ya kilimo kupitia programu ya Jenga Kesho iliyobora (BBT), ujasiriamali, na madini kupitia Programu ya Mining for a better Tommorrow (MBT).

Pia, amesema kufanya maboresho ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 Tolea la Mwaka 2023 ambayo yanasisitiza mafunzo kwa kuandaa wataalamu.

“Kupitia ujenzi wa miundombinu ya Kimkakati muhimu inayochochea uchumi, vijana wameajiriwa na kunufaika na urithishwaji ujuzi kutoka kwa wataalamu wa nje mfano ujenzi wa Bwawa la umeme la Mwalimu Nyerere na barabara za mwendokasi (BRT),” amesema Mhe. Kikwete

Kadhalika, amesema Serikali itaendelea kubuni na kutekeleza programu ya kukuza ujuzi ambayo inalenga kukuza ujuzi kwa nguvu kazi ili kuwezesha vijana kushindana katika soko la ajira mfano mafunzo ya kuongeza ujuzi kwa wafanyakazi waliopo kazini na kwa wajasiriamali.

Waziri Kikwete amesema mkakati mwingine ni kuweka msisitizo kwenye matumizi ya TEHAMA katika kuzalisha fursa nyingi za ajira kwa vijana.

“Napenda kulihakikishia Bunge lako Tukufu kwamba serikali itaendelea kusimamia na kuhakikisha vijana wanaandaliwa ili wapate ujuzi unaohitajika katika soko la ajira na hivyo kumudu ushindani wa ajira,” amesema.
Posted by MROKI On Monday, February 10, 2025 No comments
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe Judith Kapinga akijibu maswali Bungeni Mjini Dodoma leo. 
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe Judith Kapinga amesema Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatoa kipaumbele katika kufikisha umeme kwenye taasisi zinazotoa huduma kwa jamii zikiwemo Taasisi za Elimu. 

Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Februari 10, 2025 bungeni jijini Dodoma  wakati akijibu swali la la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Neema Rugangira aliyeuliza iwapo Serikali haioni haja kupitia upya Mkataba wa REA kuhakikisha umeme unafikishwa Mashuleni ili Shule ziunganishwe na huduma za TEHAMA.

"Hadi kufikia mwezi Januari, 2025 taasisi za elimu zilizopatiwa umeme kupitia REA ni 18,597. Serikali kupitia REA itaendela kupeleka umeme kwenye vituo vya huduma nchini kulingana na upatikanaji wa fedha". Amesema Mhe. Kapinga

Ameongeza kuwa, Serikali inatekeleza miradi mbalimbali ikiwemo mradi wa COVID ambapo Serikali imepeleka umeme kwenye vituo vya afya 111.

Ameongeza kuwa  upo mradi mwingine ambao unapeleka umeme kwenye pampu za maji takribani 411 na kwenye maeneo ya kilimo na maeneo ya migodi 605.

Akijibu swali Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Kabula Shitobela aliyeuliza ni lini Serikali itatoa ruzuku katika nishati safi ya kupikia ili kuwasaidia akina Mama wasifanyiwe ukatili na kuuwawa kutokana na imani potofu, Mhe. Kapinga amesema Serikali inaendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 2024-2034. 

Amesema kupitia mkakati huo, Serikali imeanza kutoa ruzuku ya  asilimia 20 hadi 50 ya bei ya mitungi ya gesi ya LPG kwa watumiaji wa mwisho.

Aneongeza kuwa  Serikali inaendelea na hatua mbalimbali za kusambaza majiko banifu 200,000 pamoja na kusambaza umeme ili kuhamasisha matumizi ya majiko ya umeme. Amesisitiza hatua hiyo itasaidia wananchi wengi zaidi kutumia majiko hayo kupikia na mwisho kupunguza matumizi ya kuni.

Akijibu swali la Mbunge wa Mbulu Mjini, Mhe. Issaay Zacharia aliyeuliza kutokana na mahitaji ya wananchi kuhitaji huduma ya umeme ni makubwa, Serikali haioni haja ya kuongeza idadi ya vitongoji, Mhe. Kapinga amesema Serikali inaona umuhimu wa jambo hilo ndio maana Serikali inaanza mradi mwingine wa kupeleka umeme kwenye vitongoji 8000.

Akijibu swali la Mbunge wa Ludewa, Mhe. Joseph Kamomga aliyetaka kufahamu mkakati wa Serikali kutenga bajeti ya kutosha ili kuweza kurekebisha miundombinu ya wazalishaji binafsi ili iendane na standard za TANESCO,  Mhe. Kapinga amesema tayari uhakiki umeshafanyika ili kupata gharama halisi kwa ajili ya kufanya ukarabati kurekebisha miundombinu hiyo.
Posted by MROKI On Monday, February 10, 2025 No comments





WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Deogratius Ndejembi amemuagiza Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Mandeleo ya Makazi, Mhanidis Anthony Sanga kuunda kamati mara moja kwa ajili ya kushughulikia mgogoro wa ardhi wa kiwanja namba 01, Kitalu R kilichopo barabara ya Nyerere jijini Mwanza.

Mhe. Ndejembi ametoa agizo hilo Februari 10, 2025 baada ya kutembelea kiwanja hicho jijini Mwanza alipofanya ziara mahususi kushuhudia na kusikiliza pande mbili za malalamiko baina ya mmiliki Z.E.K Ladhan Ltd na Halmashauri ya jiji la Mwanza.

Waziri Ndejembi ameagiza hadi kufikia Ijumaa Februari 14. 2025 kamati hiyo iwe tayari imepatikana ikihusisha wajumbe kutoka Wizara Ardhi na Mkoa wa Mwanza.

Kamati hiyo inapaswa kufanya kazi ya kupitia nyaraka kwa siku saba kuanzia Februari 17, 2025 na itoe mapendekezo ya nani mmiliki halali na nini kifanyike ili kumaliza mgogoro huo.

Aidha, Waziri Ndejembi ametoa wito kwa jamii kuendelea kufuata sheria wakati wanapotaka kumiliki ardhi ili kujiepusha na migogoro na kuwahimiza watumishi wa Sekta ya Ardhi kuendelea kufanya kazi kwa kufuata maadili ya utumishi umma kwa mujibu wa sheria, kanuni, taratibu na miongozo inayotolewa na Serikali.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema serikali ya mkoa anauongoza upo mstari wa mbele kuhakikisha migogoro ya ardhi mkoani humo namalizika ili wananchi waendelee kufanya shughuli za maendeleo.a
Posted by MROKI On Monday, February 10, 2025 No comments
Lwamgasa na Katente
Wanufaika wa Vituo vya Mfano vinavyotoa mafunzo ya uchimbaji na uchenjuaji bora wa  madini vya Lwamgasa- Geita na Katente-Bukombe wameonesha kuridhishwa na jitihada za Serikali katika kuboresha mazingira ya uchimbaji mdogo, ikiwemo kuhamasisha matumizi ya  teknolojia bora za uchenjuaji  madini  ambazo  zimesaidia kuongeza ufanisi wa shughuli za uchimbaji mdogo  na uzalishaji.

Wazikungumza na Maafisa Habari kutoka Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Madini, waliotaka kufahamu ni kwa namna gani vituo hivyo vimewasaidia kuongeza tija katika shughuli zao.
Fortunatus Luhemeja, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Hexad na mchimbaji mdogo,

Luhemeja amesema baada ya kupata taarifa za uwepo wa Kituo cha Mfano cha Lwamgasa alianza kutumia huduma kutoka kituoni hapo na hivyo kupelekea kupata uzalishaji mkubwa ukilinganisha na uzalishaji waliokuwa wakiupata awali.

Luhemeja ameongeza kwamba, baada ya kuanza kutumia Kituo cha Lwamgasa, kiliwaletea tija ndani ya muda mfupi kitu ambacho kiliwapelekea kuanza kutumia pia Kituo cha Katente na kuzidi kuona mafanikio na hivyo kupelekea kuwa na ujasili wa kuongeza uzalishaji na kuwekeza zaidi ambapo kwa sasa mafanikio ya uwepo wa Vituo hivyo kwenye uwekezaji wao yanayonekana.

‘’Tuliona mafanikio makubwa ndani ya muda mfupi, na tukaongeza ujasiri wa kuongeza uzalishaji na kuwekeza zaidi," anasema Luhemeja, akipongeza ushirikiano wa STAMICO na wataalamu waliopo katika vituo hivyo kutoa miongozo ya kitaalamu.

Aidha, Luhemeja amesema, mbali na kupeleka mawe kwa ajili ya kuchakatwa katika Vituo hivyo, Wizara ya Madini kupitia Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) ilipeleka  wataalamu kwa ajili ya ushauri na miongozo mbalimbali na kutokana na hali hiyo wakajikuta wakiupenda mfumo huo na kupelekea kuajiri wataalamu wao wakiwemo wahandisi, wanamazingira, wahasibu, maafisa  Rasilimaliwatu, wajiolojia na wataalamu wengine ambapo kwa sasa mafanikio na ufanisi wa kampuni hiyo unaonekana.

Pamoja na mambo mengine, Luhemeja amesema marekebisho ya Sheria ya Madini ya mwaka 2017 yalimpelekea kuzipenda shughuli za Sekta ya Madini ambapo masuala mengi yamewekwa wazi huku upatikanaji wa masoko ya bidhaa zitokanazo na madini ukawa katika utaratibu mzuri kuliko ilivyo kuwa awali hivyo kupelekea kuhamasisha na kuingia katika shughuli za madini.

Luhemaja anamaliza kwa kunukuu maandiko kutoka kwenye Biblia akisema yanasema "watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa", na hivyo anatumia nafasi hiyo amewasihi watanzania wenye nia ya kufanya shughuli za uchimbaji akisema ‘’wasiogope kwasababu katika kipindi hiki maarifa yapo, masoko yapo,miongozo ipo, utaratibu upo na miundombinu ipo’’.





Christopher Kadeo –Mwenyekiti Mstaafu wa Wachimbaji Wadogo wa Madini wa Mkoa wa Geita

Kwa upande wake, Christopher Kadeo anasimulia kwamba yeye binafsi ana uzoefu wa zaidi ya miaka 40 katika uchimbaji wa madini na ana zaidi ya miaka 35 ya uchimbaji katika Kijiji cha Lwamgasa ambapo amesema ujio wa Kituo cha Mfano cha Lwamgasa kimemfanya afanikiwe katika shughuli zake za uchimbaji.

"Tunaishukuru Serikali yetu ambayo ni sikivu, tuliomba masoko tukaletewa, tukaomba tusogezewe ofisi ya upimaji madini tukaletewa GST, Serikali haikuishia hapo ikatuletea Vituo vya Mfano, imetuletea mashine ya uchorongaji (Drilling Rig) na imeendelea kuboresha mazingira na sasa tunapata mikopo katika taasisi za kifedha", anasema Kadeo.
 
Kadeo pia anasisitiza kuwa uchimbaji wa madini ni Sayansi, na siyo jambo la kishirikina kama wengi wanavyodhani. Amewashauri wachimbaji wengine kufika katika Vituo vya Mfano kujifunza teknolojia bora na mbinu sahihi za uchimbaji ili kufanikiwa zaidi na kuachana na mila potofu za kwenda kupiga ramli

Masunga Mashauri – Mchimbaji Mdogo wa Madini, Kijiji cha Lwamgasa
Naye, Masunga Mashauri ambaye ni Mchimbaji mdogo katika Kijiji cha Lwamgasa ameishukuru Serikali kwa kuwafungulia Kituo cha Mfano cha Uchenjuaji Lwamgasa ambacho kimemsaidia kwa kiasi kikubwa kupata mafanikio katika shughuli zake za uchimbaji.

Mashauri anasema gharama za uchenjuaji katika  vituo hivyo ni nafuu na  ameiomba Serikali kupitia STAMICO kukiongeza uwezo kituo hicho ili kiweze kuchakata mbale kwa wingi na kwa muda mfupi kuliko ilivyo sasa  kutokana na foleni ya mizigo inayongoja kuchakatwa.
Posted by MROKI On Monday, February 10, 2025 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo