Nafasi Ya Matangazo

June 30, 2013

Posted by MROKI On Sunday, June 30, 2013 No comments
 Mkurugenzi wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Steve Gannon (kushoto) akisalimiana na moja ya wachezaji wa timu ya kampuni hiyo  Erick Salvatory(kulia)wakati wa ukaguzi kabla ya kuanza kwa mechi ya ujirani mwema kati ya SBL na vijana kutoka Chang`ombe B iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya DUCE jijini Dar es Salaam. 
Posted by MROKI On Sunday, June 30, 2013 No comments
Mafundi wa DAWASCO wakizibua chemba ya maji taka iliyokuwa imeziba na kumwaga maji katika mzunguko wa Bandari Klabu jijini Dar es Salaam leo. Chemba hiyo ilikuwa ikitema maji hayo kwa siku kadhaa bila marekebisho.
Posted by MROKI On Sunday, June 30, 2013 No comments
 Umeonaa! Hivi ni kazi yangu nikimaliza najiajiri. Ndivyo anavyoelekea kusema mwanafunzi Paulina Emmanuel anayejifunza masuala ya ubunifu wa mavazi na mitindo katika chuo cha VETA Chang’ombe Dar es Salaam, akitoa maelezo kwa Mkurugenzi wa soko la ajira, mipango na maendeleo wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) Bw. Enock Kibendela alipotembelea banda a VETA kwenye maonyesho ya SabaSaba, Dar es Salaam.
Posted by MROKI On Sunday, June 30, 2013 No comments

June 28, 2013

 Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu (aliyevaa miwani katikati), akifuatwa na wananchi baada ya kumaliza mkutano wa kuelezea utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika Kata ya Temeke, Dar es Salaam hivi karibuni.
 Mbunge wa Jimbo la Temeke, Dar es Salaam, Abbas Mtemvu akihutubia katika mkutano wa hadhara wa kuelezea utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika Kata ya Temeke, Dar es Salaam hivi karibuni.
Posted by MROKI On Friday, June 28, 2013 No comments

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda (wapili kushkto) akizungumza na Wabunge kutoka kulia, John Cheyo Bariadi Mashariki (UDP), James Mbatia wa kuteuliwa  (NCCR Mageuzi) na Mansoor Shanif Hiran  mbunge wa Kwimba (CCM) nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma jana.Kushoto ni Mkurugenzi wa Msama Promotion, Alex Msama.

 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, (kulia) akizungumza na Mkurugenzi wa Msama Promotion, Alex Msama nje ya Ukumbi wa Bunge mjini DodomaJuni 27,2013.
Posted by MROKI On Friday, June 28, 2013 No comments

June 27, 2013

Warembo wanao wania Taji la Redd's Miss Temeke 2013, kutoka kushoto walio simamaMargreth Olotu, Narietha Boniface, Latifa Mohamed, Mutesa George, Naima Ramadhan, Margreth Gerald, Mey Karume, Esther Muswa, Aksaritha Vedustus na Svtlona Nyameyo CHINI, Irenej Rajab, Darlin Mmary, Stella Mngazija na Hyness Oscar. Wakipiga picha ya pamoja baada ya mazoezi yao jijini Dar es Salaam leo.
Posted by MROKI On Thursday, June 27, 2013 No comments
 Meneja Chapa wa Tigo Tanzania Bw. William Mpinga akiongea na waandishi wa habari kuhusu tamasha kubwa la Tigo Mini Kabaang litakalofanyika siku ya jumapili hii bure kabisa katika viwanja vya  CCM Kirumba jijini Mwanza, kushoto msanii Diamond Platnumz na kulia msanii Madee ambao watatoa shoo siku hiyo na wasanii wengine. 
Posted by MROKI On Thursday, June 27, 2013 No comments
Rais Wa Sri Lanka Me.Mahinda Rajapaksa akikagua gwaride la heshima liliandaliwa na Jeshi la ulinzi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo asubuhi kwa ziara ya kikazi nchini.
 Mtoto Faith Warioba nayesoma katika shule ya awali ya Montessori jijini Dar es Salaam akimlaki kwa maua Rais Mahinda Rajapaksa wa Srilanka muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere kwa ziara ya kikazi nchini huku Rais Dkt.Jakaya Kikwete akishuhudia.
Posted by MROKI On Thursday, June 27, 2013 No comments
WADAU WA MTANDAO WETU WA FULLSHANGWE TUNAWAOMBA RADHI KWA USUMBUFU ULIOJITOKEZA KUANZIA LEO KUTOKANA NA MTANDAO WETU KUTOKUWA HEWANI KUTOKANA NA SABABU ZILIZO NJE YA UWEZO WETU HATA HIVYO WATAAAMU WETU WANAFANYA KILA LIWEZEKANALO ILI TUWEZE KUREJEA WAKATI WOWOTE
TUNATUMIA NAFASI HII PIA KUWAOMBA RADHI WADHAMINI WETU NMB, NBC SBL, NHIF NA WILNA INTERNATIONAL TUNAOMBA MTUVUMILIE WAKATI TUNASHUGHULIKIA TATIZO HILO.
Posted by MROKI On Thursday, June 27, 2013 No comments
 
 Meneja wa bia ya Serengeti Allan Chonjo (wa pili kulia) akiongea kwa njia ya simu na mshindi wa droo ya pili ya Winda na Ushinde  Mwl.Michael Valerian Mbuya katika mkutano na wana habari uliofanyika jana katika ofisi za Kampuni ya Bia ya Serengeti jijini Dar es Salaam, kushoto kwake ni Meneja mauzo  wa Push Mobile Rugambo Rodney, kulia kwake ni Afisa mwandamizi kutoka PWC Daniel Nnko na Mkaguzi kutoka Bodi ya Michezo ya Bahati Humudi Abdul Hussen(wa kwanza kushoto).
 Meneja wa bia ya Serengeti Allan Chonjo(katikati) akiongea na wana habari wakati wa kumtangaza mshindi wa droo ya pili ya Winda na Ushinde katika mkutano uliofanyikajana katika ofisi za Kampuni ya Bia ya Serengeti jijini Dar es Salaam. 
Posted by MROKI On Thursday, June 27, 2013 No comments
 Mbunge wa Jimbo la Ilala, jijini Dar es Salaam, na mmoja wa Wenyeviti wa Bunge, Mussa Zungu Azzan akiongoza kikao cha Bunge
 Mbunge wa Viti Maalum (CCM) kutoka Mkoani Arusha, Catherine Magige akiwa Bungeni mjini Dodoma Juni 26,2013.
 Mbunge wa Nzega, Dk. Hamisi Kingwangalla (kulia) akizungumza na Mwenyekiti wa CCM nchi za SADC, Kelvin Nyamori (katikati) na Mbunge wa Kisesa, Luhanga Mpina, nje ya Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma jana.
Posted by MROKI On Thursday, June 27, 2013 No comments
DSC03460 
Dr. Mary Mwanjelwa mbunge wa Mbeya (viti maalum) mgeni rasmi katika wa mkutano wa Je Nifanyeje ulioandaliwa na VOA kwa ushirikiano na USAID akifungua rasmi mkutano huo wa vijana katika ukumbi wa African Dreamer Dodoma Jumatano.
Posted by MROKI On Thursday, June 27, 2013 No comments
 Mapema wiki hii Wanachama wa Chama cha Washereheshaji na watoa Huduma katika Shughuli mbalimbali nchini hasa Sherehe walifika Mjini Dodoma na kutembelea Bungeni na kujionea shughuli mbalimbali za Bunge. Father Kidevu Blog kupitia Kampuni yake ya MD Digital Company ambayo pia ni mtoa huduma ya Picha katika sherehe mbalimbali ilinasa taswira mbalimbali za wakali hao wa Kuongoza Shere na Misosi wakiwa Mjengoni.
Posted by MROKI On Thursday, June 27, 2013 No comments

June 25, 2013

FAMILIA YA ZAINABU ABEID ALLY (BABY SHANGAZI HOTELI) YA MBEYA INAPENDA KUCHUKUA FURSA HII KUMKUMBUKA MAMA YAO MPENDWA ALIYEFARIKI USIKU WA TAREHE 5-06-2013 KATIKA HOSPITALI YA RUFAA JIJINI MBEYA NA KUZIKWA SIKU YA ALHAMISI TAREHE 6.06.2013.

WATOTO WAKO POSTER, MABRUCK, ASHA, HAWA, HUSSEIN, HASIRA NA ABEID WANAUNGANA NA NDUGU NA JAMAA WALIOJITOLEA KWA HALI NA MALI KUHAKIKISHA MAMA YAO MPENDWA ANAPATA KILA AINA YA MSAADA ULIOKUWA UNAHITAJI MPAKA PALE MWENYEZI MUNGU ALIPOCHUKUA ROHO YAKE.

KUMBUKUMBU YA KUTIMIZA SIKU YA 40 BAADA YA KIFO CHA MAMA YETU INATARAJIWA KUFANYIKA NYUMBANI KWAKE MAREHEMU MBEYA SIKU YA JUMAMOSI TAREHE 6.07.2013 WOTE MNAKARIBISHWA.

MUNGU AILAZE ROHO YAKE MAHALA PEMA PEPONI.
AHSANTENI SANA
Posted by MROKI On Tuesday, June 25, 2013 No comments
Shirika la Utangazaji la Sauti ya Amerika Idhaa ya Kiswahili (VOA) ikishirikiana na USAID limeandaa mkutano mkubwa wa Vijana utakao fanyika kesho mjini Dodoma maarufu kama Je Nifanyeje?.


Washiriki wa mkutano huo ni vijana mbalimbali kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) pamoja na Vijana wengine wa mtaani Dodoma wamealikwa kuhudhuria.

Mtangazaji Mashuhuri  aliyejiunga na idhaa hiyo mwaka 2008 akitokea kituocha ITV na Redio One Sanday Shomari ndiye atakuwa akiongoza mkutano huo.


Wakizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Habari wa Bunge mjini Dodoma, Sande Shomari pamoja na Bi. Rose Mwakitwange (pichani juu) wamesema maandalizi  ya mkutano huo yamekamilika na mjadala wake utarushwa moja kwa moja na redio Mshirika ABM FM ya mjini Dodoma.
Posted by MROKI On Tuesday, June 25, 2013 No comments
Mbunge wa Monduli, ambaye pia ni waziri mkuu mstaafu, Edward Lowasa, akisalimiana na wanafunzi wa chuo kikuu cha UDOM waliotoka shule za sekondari za kata, wakati walipofika nyumbani kwake mkoani Dodoma kutoa shukrani zao kwa hatua waliyofikia kielimu
Posted by MROKI On Tuesday, June 25, 2013 No comments

Direcotor Credit Bureau Expansion- Creditino Group Mr.Hakon Stafansson speaking at the press conference today at Serena Hotel (left) is Mr.Davith Kahwa,Director-Creditino Tanzania.
 Creditinfo Tanzania Limited (CIT) received the licence to conduct credit reference business after satisfactorily met the conditions stipulated in the provisional licence that was granted by the Bank of Tanzania on October 2012 and demonstrated its readiness to commence business. This means that Creditinfo Tanzania, is the first company to receive a licence to operate a credit reference bureau in Tanzania issued under Section 48 of the Bank of Tanzania Act, 2006.

Subsequently, on 12th June 2013, Creditinfo Tanzania started to provide services to public and various categories of business that are denominated under the Act as being eligible to provide credit information to a Credit Reference Databank. These include banks and non-bank financial institutions, savings and credit schemes, micro-finance companies, any other finance company that are licensed and supervised by the Bank of Tanzania. Similar services are available for subscriptions to all other credit providers, he added.
Posted by MROKI On Tuesday, June 25, 2013 No comments
 Skauti Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania mteule Mhe. Mwantumu Mahiza akisubiri kuapishwa Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 23, 2013
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akijiandaa kuvishwa skafu na skauti kabla ya kumuapisha Skauti Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Mhe. Mwantumu Mahiza akisubiri kuapishwa Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 23, 2013
Posted by MROKI On Tuesday, June 25, 2013 No comments
 Mabalozi wa kinywaji cha Johnnie Walker kutoka Kampuni ya Bia ya Serengeti  wakionesha wageni waalikwa moja ya aina ya Johnnie Walker.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Steve Gannon(kulia) na mdau Mr. Paul(kushoto) wakiwa washika chupa ya Johnnie Walker blue label
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Steve Gannon (wa pili kushoto) katika picha ya pamoja na Afisa mawasiliano wa SBL Bi. Hawa (wa pili kulia) wakiwa na wadau  Paul(kulia) na Mac(kushoto) waliohudhuria katika hafla ya ‘Johnnie Walker Mentorship’ iliyoandaliwa na Kampuni ya Bia ya Serengeti jijini Dar es Salaam.
Posted by MROKI On Tuesday, June 25, 2013 No comments

June 24, 2013

IMG_2565
Mgeni rasmi katika uzinduzi wa Tamko la Mount Meru la kuwalinda waandishi wa habari wakiwa kazini Afrika Mashariki, Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika Bw. Francis Stolla akizungumza machache wakati wa uzinduzi huo ambapo alisisitiza umuhimu wa uhuru wa vyombo vya habari katika kujenga Demokrasia na Utawala Bora katika Ukanda wa Afrika Mashariki na kati. Wengine katika picha ni Mwenyekiti wa Misa-Tan Bw. Mohammed Tibanyendera (wa tatu kushoto), Mjumbe wa MCT Bw. Allan Lawa (kulia), Mkurugenzi Mtendaji wa Umoja wa Vilabu vya waandishi wa habari Tanzania (UTPC) Bw. Abubakar Karsan ( wa pili kushoto) na Mkurugenzi wa MISA-TAN Bw. Tumaini Mwailenge (kushoto). (Picha na Zainul Mzige wa Dewji Blog).
IMG_2504
Mtangazaji wa Radio Clouds Fm Regina Mwalekwa akisoma Tamko rasmi la Mount Meru lililoandaliwa siku ya maadhimisho ya Uhuru wa vyombo vya habari Duniani yaliyofanyika Mei 3-4 mwaka huu jijini Arusha yaliyohudhuriwa na washiriki mbalimbali toka vyombo vya habari, redio za jamii, jumuiya mbalimbali za Kimataifa, Taasisi za mafunzo ya tasnia ya habari na mifuko ya Maendeleo ya Tasnia ya habari kutoka Tanzania, Kenya, Uganda na Rwanda.
Posted by MROKI On Monday, June 24, 2013 No comments
 
 Makamu wa pili wa Rais wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar Balozi Seif Ally Iddy akipokea vifaa mbalimbali vya michezo kwa timu za baraza la wawakilishi za mpira wa miguu na pete toka kwa Meneja masoko wa kinywaji cha Grandmalt  Fimbo Mohamed Butallah kwenye makabidhiano yaliyofanyika kwenye ukumbi la baraza la wawakilishi Zanzibar, kushoto kwake ni mwenyekiti wa timu ya Baraza la wawakilishi mheshimiwa Hamza Hassan Juma.
Posted by MROKI On Monday, June 24, 2013 No comments
RAMBIRAMBI MSIBA WA MATHIAS KISSA
Shrikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha mchezaji wa zamani wa timu za Cosmopolitan na Taifa Stars, Mathias Kissa (84) kilichotokea leo alfajiri (Juni 24 mwaka huu) kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam.

Msiba huo ni mkubwa kwa wadau wa mpira wa miguu kwani enzi zake, Kissa akiwa na timu ya Tabora alitamba katika michuano ya Kombe la Taifa wakati huo ikiitwa Sunlight Cup. Alikuwa akicheza katika nafasi ya ulinzi.

Baadaye alijiunga na Cosmoplitan ya Dar es Salaam, na pia kuwa mchezaji wa timu ya Taifa ambapo enzi zake akiwa na wachezaji kama Yunge Mwanansali wakiiwakilisha Tanganyika na baadaye Tanzania Bara walitamba katika michuano ya Kombe la Chalenji wakati huo ikiitwa Gossage, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.
Posted by MROKI On Monday, June 24, 2013 No comments
   Mchezaji chipukizi wa timu ya soka ya Sifa United ya Manzese Abuu Mohamed (kushoto) akichuana na mchezaji wa Makumbusho United Shabani Idd wakati wa mechi ya ufunguzi wa mashindano ya vijana chini ya umriwa miaka 17 ya Airtel Rising Stars, Mkoa wa Kinondoni, iliyofanyikauwanja wa mpira wa shule ya msingi Mwanamanyala jijini Dar es Salaam Juni 23, 2013. Makumbusho United walishinda 3-1
 Ofisa Uhusiano wa Airtel TanzaniaJane Matinde akipiga penati kuashiria
uzinduzi rasmi ya Airtel Rising Stars Mkoa wa Kinondoni.
 Ofisa Uhusiana wa Airtel Tanzania akikagua timu kabla ya mechi kuanza.

Mchezaji wa timu ya soka ya Sifa United ya Manzese Yassin Saleh (kulia) akichuanana na Shaban Idd wa Makumbusho United wakati wa mechi ya ufunguzi wa mashindano ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars, Mkoa wa Kinondoni, iliyofanyika uwanja wa mpira wa shule ya msingi Mwanamanyala jijini Dar es Salaam Juni 23, 2013. Makumbusho United walishinda 3-1
Posted by MROKI On Monday, June 24, 2013 No comments
MBUNGE WA Kigoma Kaskazini, Ndugu Zitto Z. Kabwe amealikwa  kuhudhuria tamasha la tisa la Aspen la mwaka huu huko Marekani. Tamasha hilo linawaleta pamoja watu mashuhuri kutoka nyanja mbalimbali duniani.

Lengo kubwa la tamasha ni kuwawezesha washiriki kubadilishana mawazo kuhusiana na masuala mbalimbali ambayo wana uzoefu nayo.
Posted by MROKI On Monday, June 24, 2013 No comments
 Katibu wa Wabunge wa Tanzania Katika Bunge la Afrika Mashariki, Shy-Rose Bhanji akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu miswada mbalimbali iliyojadiliwa na bunge hilo kwa kipindi cha  mwaka mmoja. Kushoto ni mbunge wa bunge hilo, Abdullah Mwinyi.
 Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Abdullah Mwinyi akizungumza na waandishi wa habari leo. Kulia ni Katibu wa wabunge wa Tanzania katika bunge hilo, Shy-Rose Bhanji.
Posted by MROKI On Monday, June 24, 2013 No comments
 Mmoja wa washiriki wa shindano la Bibi Bomba awamu ya pili Bi.Anna Nicholaus akikabidhiwa fulana yenye jina lake na mmoja wa Waratibu wa shindano hilo,AJ Jonathan,wakati wa utambulisho rasmi wa washiriki hao mapema jana jioni mbele ya Wanahabari (hawapo pichani),uliofanyika kwenye ukumbi wa alliance française,jijini Dar.Aidha pia washiriki hao wapatao ishirini walipata nafasi ya kusaini mikataba yao na pia kuelezwa utaratibu mzima wa mchakato wa Bibi Bomba 2013.
Posted by MROKI On Monday, June 24, 2013 No comments

June 22, 2013

JUMLA ya timu nane zimethibitisha kushriki katika bonaza la soka klabu ya Break Point lililopangwa kufanyika Jumapili Juni 23 kwenye viwanja vya Survey (Chuo Kikuu cha Ardhi).
Mkurugenzi wa Breake Point Outdoor Distributors, Daudi Machumu alizitaja timu ambazo ambazo zitashiriki katika bonanza hilo lililodhaminiwa na kampuni ya bia ya Seregeti (SBL) kuwa ni, Rose Garden, Survey, Mbezi Beach na Boko Veterans.
Machumu alisema kuwa timu nyingine ni Clouds Media Group, Magogoni, Umoja na waaandaaji, Break Point ambayo itakuwa chini ya Rodrick “Neymar” Mwambene. Alisema kuwa bonanza hilo  limepangwa kuanza saa 2.30 asubuhi na madhumuni yake ni kuwakutanisha wadau wa michezo na kubadilishana mawazo.
Posted by MROKI On Saturday, June 22, 2013 No comments


 Wakili Froldius Mugisha Mutungi (wapili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Wakili Emmanuel Tamila Makene (wapilikushoto) pamoja na Mkewe mama Mutungi na kijana kutoka Ofisi ya Kings Low Chember, Daudi. 
*********


Ama kweli penye nia njia hupatikana….
Msemo huu wa wahenga umekamilika tarehe 21 Juni 2013 ambapo Ndugu Froldius Mugisha Mutungi ameapishwa kuwa wakili wa kujitegea.

Muuguzi huyu anamshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kumpa afya ya mwili, roho na akili pia. Na anawashukuru sana familia yake hasa mke wake ,wafanyakazi wenzake, ndugu jamaa na marafiki ambao wamemsaidia kwa njia moja au nyingine hata kupatikana mafanikio haya.
Posted by MROKI On Saturday, June 22, 2013 No comments
Washindi wa Redds Miss Kinondoni Talent 2013 wakiwa katika sura za furaha mara baada ya kuwagalagaza wenzao na kujikuta wanapatikana wao Kutoka Kulia ni Sophia Yusuf, Phillious Lemi na Linda Joseph.
Posted by MROKI On Saturday, June 22, 2013 No comments

June 21, 2013

Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Bw.Matina Nkurlu akimpigia mmoja wa washindi miongoni ya watano waliojishindia shilingi milioni mbili  kila mmoja kwenye droo kubwa ya Promosheni ya Cheka Nao,inayowezesha  wateja kuongea na mitandao yote bila mipaka kwa bei nafuu. Ili kujiunga mteja anatakiwa kupiga *149*01#.wanaoshuhudia   ni Meneja wa Idara ya Malipo ya Kabla wa kampuni hiyo, Yvonne Maruma (kati kati)pamoja na  Ofisa wa bodi ya michezo ya kubahatisha Tanzania Bi.Chiku Saleh.

     HAWA NDIYO WASHINDI WA PROMOSHENI YA CHEKA NAO - 21/06/2013
WAMEJINYAKULIA KITITA CHA  MILIONI TSH 2,000,000 KILA MMOJA
  



JINA
UMRI
ANAKOISHI
KAZI YAKE
Majija Amos Kidara
24
Shinyanga - Kahama
Peasant
Mkude Idd
30
Msamvu - Morogoro
Peasant
Isaya Edward Sengo
35
Mbeya
Petty Trader
Alexander Vinson
33
Mbinga - Ruvuma
Peasant
Derick Charles Cosmas
25
Karagwe - Bukoba
Peasant







Posted by MROKI On Friday, June 21, 2013 No comments
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwahutubia wakazi wa jijini Tanga, wakati alipofika eneo la Pongwe jijini Tanga leo Juni 21, 2013 kwa ajili ya kuweka Jiwe la Msingi la ujenzi wa Viwanda katika eneo hilo maalum la Uwekezaji la Tanga Economic Corridor Sez, linalosimamiwa na Wawekezaji kutoka nchini Korea Kusini.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Viwanda, katika eneo maalum la Uwekezaji la Tanga Economic Corridor Sez, wakati wa sherehe hizo zilizofanyika leo Juni 21, 2013 jijini Tanga. Kushoto kwa Makamu ni Mwenyekiti wa Bodi ya Tanga Economic Corridor Ltd, Chris Incheul Chae.
Posted by MROKI On Friday, June 21, 2013 No comments
 Michelle Jeng (right) With some of the guest at the Launch.
Dr Mwele Malecela officiating michelle Jeng Foundation.
Fashion Show during the LAunch of the Michelle Jeng Foundation.
 Guest Of honour Dr Mwele Malecela giving a speech.
 Michelle Jeng Speaking at the LAunch of her Foundation.
The MICHELLE JENG FOUNDATION was launched in Stockholm, Sweden by Tanzanian Model Michelle Jeng who aims to provide educational support to young girls living in her home country, United Republic of Tanzania.

At the launch she said, “Through my foundation, I look forward to providing hope to young girls who shall be the leaders of tomorrow and provide for their education that shall be the catalyst to the change in their lives”
Posted by MROKI On Friday, June 21, 2013 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo