Nafasi Ya Matangazo

May 29, 2025

Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi imetangaza vipaumbele saba ambavyo itaavitekeleza katika Bajeti ya mwaka 2025/2026.

Vipaumbele hivyo vimetanagazwa Mei 29, 2025 na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Deogratoius Ndejembi wakati wa kusoma hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ardhi ya Wizara hiyo Bungeni jijini Dodoma.

“Maeneo ya kipaumbele yatakayotiliwa mkazo na Wizara katika mwaka 2025/26 ili kufikia malengo yaliyowekwa ni kuongeza kasi ya upangaji, upimaji, umilikishaji na usajili wa ardhi mijini, vijijini na katika maeneo ya kimkakati’’ amesema Waziri Ndejembi.

Maeneo mengine ya kipaumbele ni kuimarisha mifumo ya TEHAMA katika utunzaji wa kumbukumbu, utoaji wa huduma, ukusanyaji wa maduhuli na upatikanaji wa taarifa za ardhi na uthamini na kuimarisha mifumo ya utatuzi wa migogoro ya ardhi kiutawala na kwenye Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya.

Kwa mujibu wa Mhe. Ndejembi vipaumbele vingine ni kuhakikisha uwepo wa nyumba bora, ukuaji wa sekta ya milki na maendeleo ya makazi kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii; kuimarisha mipaka ya kimataifa na kuendeleza miji ya mipakani, kuimarisha upatikanaji wa ramani ili kuwezesha uandaaji wa mipango mbalimbali ya kitaifa na matumizi mengine na kuimarisha mifumo ya usimamizi na ufuatiliaji wa utekelezaji wa vipaumbele.



Posted by MROKI On Thursday, May 29, 2025 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo