Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uhamisho na uteuzi wa viongozi mbalimbali. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, uhamisho na uteuzi huo ni kama ifuatavyo:
May 06, 2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uhamisho na uteuzi wa viongozi mbalimbali. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, uhamisho na uteuzi huo ni kama ifuatavyo:
Wakala wa Nishati Vijijini (REA), umepongezwa na Jeshi la Magereza kwa kuhamasisha, kuwezesha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa taasisi zinazohudumia watu zaidi ya 100 hapa nchini.
Nyamguma Mahamud, Mwandishi wa Habari kutoka Mlimani FM ameibuka kidedea katika Tuzo za Uandishi wa Habari za Samia Kalamu Awards 2025 kupitia kipengele cha habari za Nishati Safi ya Kupikia ambapo Wizara ya Nishati imetambua mchango wake kwa kumpa zawadi mbalimbali ili kuendelea kuhamasisha utoaji wa elimu ya Nishati Safi ya Kupikia.
May 05, 2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akiwa pamoja na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Mhe. Abdullah Bin Zayed Al Nahyan, wakishuhudia utiaji saini wa hati ya makubaliano kati ya Rais wa Chemba ya biashara,Viwanda na Kilimo(TCCIA) Vicent Minja na Waziri Msaidizi wa Masuala ya Uchumi na biashara UAE, Mh. Saeed Mubarak Al Hajeri wa Shirikisho la Vyama vya Biashara na Viwanda vya UAE na Chemba ya Biashara,Viwanda na Kilimo(TCCIA) kuhusu uanzishwaji wa Baraza la Pamoja la Biashara kati ya Umoja wa Falme za Kiarabu na Tanzania tarehe 05 Mei, 2025 Ikulu jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele (shati la drafti) akiwa katika kituo cha shule ya Msingi Mahela katika Halmashauri ya Mji wa Mbinga Mkoani Ruvuma wakati akitembelea vituo mbalimbali vya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura katika mkoa huo jana. Kulia walio simama ni Afisa Mwandikishaji wa Jimbo la Mbinga Mjini, Ndg. Amina Hamisi Seif. (Picha na INEC).
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele (kulia) akiwa katika kituo cha shule ya Msingi Mahela katika Halmashauri ya Mji wa Mbinga Mkoani Ruvuma wakati akitembelea vituo mbalimbali vya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura katika mkoa huo jana. Wapili Kulia ni Afisa Mwandikishaji wa Jimbo la Nyasa, Ndg. Khalid Khalifa. (Picha na INEC).
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele (Kushoto) akimkabidhi kadi ya Mpiga Kura Ndg. Acheni Maulid mkazi wa Mbamba Bay katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyasamkoani Ruvuma aliyefika katika kituo cha Shule ya msingi Mbamba bay kuboresha taarifa zake katika Daftari la Kudumu la Mpiga Kura. (Picha na INEC).
Mpiga Kura Ndg. Acheni Maulid mkazi wa Mbamba Bay katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa Mkoani Ruvuma akionesha aliyefika katika kituo cha Shule ya msingi Mbamba bay kuboresha taarifa zake katika Daftari la Kudumu la Mpiga Kura. (Picha na INEC).
Na Mwandishi Wetu, Ruvuma
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imewataka wananchi wa mikoa 15 inayotekeleza zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura katika mzunguko wa kwanza wa awamu ya pili kuzitumia siku chache zilizobaki katika mikoa yao kuhakikisha wanajitokeza kujiandikisha na kuhakiki taarifa zao ili wasijekosa haki yao ya msingi ya kupiga Kura katika uchaguzi ujao mwaka huu.
Zitto Zuberi Ruyagwa Kabwe Kiongozi mstaafu wa ACT Wazalendo, Ndg. Zitto Zuberi Ruyangwa Kabwe amejitosa kuwania kuteuliwa na chama chake kuwania Ubunge wa Jimbo la Kigoma Mjini katika uchaguzi Mkuu utakaofanyikia Mwezi Oktoba mwaka huu.
Waziri Mkuu na Mbunge wa Ruangwa , Kassim Majaliwa akizungumza na wananchi katika Uwanja wa Namango wilayani Ruangwa, Mei 4, 2025
Amesema Serikali imenunua mitambo 15 ya kisasa ya uchenjuaji ambayo itasambazwa kwenye maeneo ya wachimbaji wadogo hivyo ametoa wito kwa wachimbaji hao kujiunga katika vikundi ili waweze kunufaika na fursa hiyo.
Ameyasema hayo leo Jumapili (Mei 04,2025) wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kijiji cha Chingumbwa kitongoji cha Namungo Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi.
Kadhalika Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa Afisa Madini wa mkoa kuendelea na mpango wa kubaini maeneo yenye madini yatambulike na kisha kutoa leseni kwa wachimbaji wadogo ili waweze kufanya shughuli za uchimbaji.
“Pamoja na hili tumeamua maeneo yote ya madini yaliyochukuliwa leseni na hayajaendelezwa kwa muda mrefu, tutayachukua, tutayapima upya na kuyagawa kwa wachimbaji wadogo.”
"Serikali yenu inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia imenunua ndege maalum ambayo itasaidia kufanya tafiti ya kujua aina ya madini yaliyopo na kiwango chake na sisi huku Lindi itakuja kuruka, Ruangwa na maeneo ya Nachingwea”.
Akizungumzia sekta ya barabara, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Serikali inaendelea na mipango ya kuziboresha barabara mbalimbali katika wilaya ya Ruangwa ili kuziwezesha kupitika wakati wote na hivyo kuwafanya wakazi wa maeneo hayo kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi.
Naye Kaimu Meneja wa Tanesco Mkoa wa Lindi Emmanuel Sengwaji amesema kuwa Wataalam wa Idara ya Miradi mikubwa kutoka Tanesco wamefanya uhakiki wa mahitaji ya umeme katika mkoa wa Lindi kutokana na ongezeko la wawekezaji katika mkoa huo “Tuliomba tujengewe laini la gridi ya Taifa itakayotoa umeme kutoka Masasi hadi Ruangwa katika eneo la Kitandi ili umeme huo uweze kusambazwa maeneo ya uwekezaji ikiwemo kwenye migodi ya Namungo”.
May 04, 2025
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndg. Ramadhani Kailima, akimkabidhi kadi ya mpiga kura Mwanafunzi wa Kidato cha Sita wa Shule ya Sekondari ya Milambo, Maboto Wambura, wakati alipokitembelea Kituo cha Kuandikisha Wapiga Kura katika shule hiyo iliyopo Kata ya Chemchem, Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, Mei 4, 2025. Picha na INEC
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndg. Ramadhani Kailima, akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari ya wasichana Tabora, wakati alipotembelea Kituo cha Kujiandikisha Wapiga Kura kilichopo shuleni humo, Mei 04, 2025, ambapo pia aliwahamasisha wanafunzi wa shule hiyo na Sekondari ya Milambo zilizopo katika Hamlashauri ya Manispaa ya Tabora, wajitokeze kujiandikikisha kwa walio na sifa. Picha na INEC.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndg. Ramadhani Kailima (kulia), akizungumza na mwendesha kifaa cha ‘Bayometriki’ katika Kituo cha kuandikisha wapiga kura kilichopo Kata ya Isevya, Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, alipotembelea na kukagua vituo vya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya pili linalokwenda sambamba na uwekaji wazi wa Daftari la Awali la Wapiga Kura Mkoani Tabora, leo Mei 04, 2025. Katikati ni Mratibu wa Uandikishaji Mkoa wa Tabora, Elihuruma Nyella. Picha na INEC
MKURUGENZI wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi,Ndg Ramadhani Kailima amewataka wananchi wa Mkoa wa Tabora kujitokeza kuhakiki na kuboresha taarifa zao katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na uwekaji wazi wa Daftari la Awali la Wapiga Kura kwenye vituo walivyojiandikishia na kutazama daftari la awali lilolowekwa wazi na kutoa taarifa za wale waliokosa sifa kuwepo kwenye daftari hilo