WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa akishuhudia mchezo kati ya Timu ya Taifa ya Tanzania ya Mpira wa Miguu (Taifa Stars) na Timu ya Taifa ya Congo wa kuwania nafasi ya kufuzu michuano ya AFCON 2025.
October 15, 2024
Rais Dkt. Samia amewapongeza vijana walioshiriki mbio za Mwenge wa Uhuru za mwaka 2024 kwa kuzunguka nchi nzima kuhamasisha shughuli za maendeleo na kuwahimiza wananchi kufanya kazi kwa bidii, kuwajibika na kuwa wazalendo kwa Taifa lao.
Vilevile, ameeleza kuwa Serikali itafanyia kazi taarifa na mapendekezo yaliyowasilishwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge, Ndugu Godfrey Eliakim Mzava inayojumuisha changamoto, maombi na ushauri uliotolewa na wananchi kupokelewa na Mwenge wakati wa mbio hizo.
Kwa upande mwingine, Rais Dkt. Samia ametoa rai kwa vijana kuendelea kulinda Mwenge wa Uhuru ambayo ni Tunu ya Taifa na kuuenzi kwa kuendelea kufanya kazi kwa bidii.
Akizungumzia Maonesho ya Wiki ya Vijana, Rais Dkt Samia ametoa pongezi kwa vijana kwa ubunifu, ujuzi, uthubutu na utayari wao walioonesha kupitia kazi zao na amewahakikishia kuwa Serikali itaendelea kutatua changamoto zinazowakabili.
Katika kuchochea zaidi ubunifu wa vijana, Rais Dkt. Samia ameelekeza Halmashauri zote nchini kununua vifaa vinavyotumika kwenye vituo vya kutolea huduma za afya na kufundishia wanafunzi ambavyo vinazalishwa kwa ubora na vijana wabunifu hapahapa nchini.
Rais Dkt. Samia pia amerejea wito wake kwa wananchi kujiandikisha ili waweze kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ikiwa ni kuendana na dhamira ya Uhuru ya kuwawezesha wananchi kujiamulia mambo yao wenyewe, ikiwemo kwa kuwachagua viongozi wao.
October 13, 2024
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, ametoa wito kwa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) pamoja na jumuiya nyingine za chama hicho kuendelea kushindana kwa hoja na kuwa mfano bora wanapojadili masuala mbalimbali ya kitaifa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia S. Hassan kwa usimamizi madhubuti wa sekta unaopelekea ukuaji wa haraka wa mchango wa sekta ya madini katika pato la Taifa.
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema Serikali inaendelea na jitihada za kufanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya hali ya hewa nchini ambapo ifikapo mwishoni mwa mwaka huu, Tanzania itakuwa na Rada saba ikiwa ni kiwango kikubwa cha Rada katika nchi za Afrika Mashariki na Kati.
Amesema kuwa hatua hiyo ni mwendelezo Serikali za kufanya uwekezaji katika sekta ya hali ya hewa nchini kwa kufunga miundombinu ya kisasa ya hali hewa ili kuimarisha mifumo ya ufuatiliaji wa taarifa za hali ya hewa.
Amesema hayo leo (Jumapili, Oktoba 13, 2024) wakati alipotoa tamko la kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kupunguza Madhara ya Maafa, Jijini Mwanza.
“Nitumie fursa hii kumshukuru Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa uwekezaji mkubwa katika eneo hili lakini pia kuendelea kutoa kipaumbele kwa makundi maalumu na kuweka mikakati thabiti inayolenga kuwawezesha vijana kiuchumi na kijamii. ”
Amesema kuwa maadhimisho ya mwaka huu yanatoa fursa ya kuimarisha ushirikiano wa kitaifa na kimataifa ili kuunganisha juhudi za kuwalinda watoto na vijana dhidi ya athari za majanga.
“Ili kuifikia adhma hiyo, katika ngazi ya Taifa tunapaswa, pamoja na mambo mengine, kuhakikisha kuwa tunatumia fursa hii kutoa mafunzo kwa jamii kuhusu mikakati ya kujikinga na maafa, hasa elimu ya hali ya hewa na jinsi ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi; kuandaa mikutano ya kujadili changamoto za maafa na kupanga mikakati ya pamoja. ”
Ameongeza kuwa mamlaka husika zinapaswa kuendesha kampeni za uhamasishaji kuhusu umuhimu wa elimu na mawasiliano ya hatari, pamoja na ushiriki wa jamii, kuandaa matukio ya utamaduni na michezo ili kuhamasisha jamii na kutoa elimu kwa njia ya burudani, kuendeleza tafiti kuhusu madhara ya maafa pamoja na kutoa taarifa kwa umma ili kuongeza uelewa.
Aidha, Waziri Mkuu ameielekeza wizara yenye dhamana ya elimu na taasisi zake kuhakikisha wanaendelea kuimarisha mitaala ya elimu ili ijumuishe masuala ya usalama shuleni, kupunguza hatari, na uelewa wa majanga. “Vilevile, kuhakikisha mafunzo kwa walimu kuhusu mbinu za kufundisha masuala haya kwa wanafunzi yanaendelea kuimarisha. ”
Pia, Mheshimiwa Majaliwa amezitaka mamlaka husika ziendelee kuhamasisha na kuwezesha matumizi ya mbegu zinazokomaa kwa muda mfupi pamoja na utunzaji wa chakula cha binadamu na malisho ya mifumo. “Imarisheni utoaji taaluma ya matumizi ya mbinu za kilimo cha kisasa kinazohitaji maji kidogo. ”
Awali, akipokea taarifa kuhusu maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru na Kumbukizi ya Miaka 25 ya Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius K. Nyerere, Mheshimiwa Majaliwa amesema ameridhishwa na hatua za maandalizi ya maadhimisho hayo.
Mgeni Rasmi katika maadhimisho hayo yatakayofanyika katika uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza, Oktoba 14, 2024 atakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Kwa upande wake, Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Ridhiwani Kikwete amesema kuwa maandalizi yamekamilika ambapo pamoja na mambo mengine Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajia kushiriki katika ibada maalum ya kumuombea Baba wa Taifa itakayofanyika katika Kanisa Katoliki la Parokia ya Mtakatifu Fransisco Xavery Jijini Mwanza.
Mkurugenzi wa Bodi ya Bima ya Amana, Isack Kihwili, alibainisha hayo leo, Oktoba 12, 2024, katika Maonesho ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika katika viwanja vya EPZ, Bombambili, Geita. Kihwili alisema bodi hiyo inatoa elimu kwa wananchi ili kuwafahamisha namna wanavyoweza kunufaika na ulinzi wa amana zao kupitia bodi hiyo.
"Utaratibu ni kwamba hatulipi asilimia 100 ya fidia, lakini kiwango kilichowekwa ni milioni 7 na laki 5. Iwapo mteja alikuwa na kiasi chochote kinachozidi kiwango hicho, atarudishiwa fedha zake hadi kufikia milioni 7.5 bila kujali hali ya benki husika," aliongeza Kihwili.
Alieleza kuwa endapo mteja alikuwa na kiasi cha chini ya milioni 7.5, atalipwa fedha zote kwa utaratibu uliowekwa. Kihwili alifafanua zaidi kuwa utaratibu huu unazingatia ridhaa ya serikali pamoja na uwezo wa mfuko wa Bima ya Amana katika kufidia wateja.
Akijibu swali la mmiliki wa Full Shangwe Blog, John Bukuku, kuhusu vigezo vilivyotumika kuweka kiwango hicho cha fidia, Kihwili alieleza kuwa kiwango hicho kimewekwa kwa kuzingatia uwezo wa mfuko na hali ya uchumi wa nchi.
"Kuanzia mwaka 2010 hadi mwaka 2022, kiwango cha fidia kilikuwa milioni 1.5, lakini kutokana na ukuaji wa uchumi na mfuko kuwa na uwezo wa kifedha zaidi, tumeongeza kiwango hicho mara tano hadi milioni 7.5," alisema Kihwili.
Pia alisisitiza kuwa si jambo jema kulipa fidia kwa asilimia 100 hata kama mfuko unaruhusu, kwani kuna hofu ya kuibuka kwa tatizo linaloitwa 'moral hazard,' ambapo watu hawatakuwa makini katika kufuatilia hali ya benki wanazoweka fedha zao.
Kihwili alihitimisha kwa kutoa wito kwa wananchi kufuatilia maendeleo ya benki wanazoweka fedha zao kila robo mwaka ili wawe na uhakika wa usalama wa amana zao.