January 28, 2026
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limefanya ukaguzi wa kitaalamu wa mita za umeme kwa baadhi ya wateja waliowasilisha malalamiko hayo kwa njia za mitandao katika maeneo ya Tabata Kimanga na Kimara Suka jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Kaspar Mmuya amesema atahakikisha anasimamia kila mwananchi mwenye uhalali wa kupata hati milki ya eneo lake analomiliki anapata hati.
Halmashauri ya Mji Ifakara Januari 27,2026 imetoa mikopo ya asilimia 10 yenye thamani ya Shilingi milioni 600 ikiwa ni Mikopo ya Asilimia 10 inayotokana na Mapato ya ndani kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, ikiwa ni utekelezaji wa sera ya kuwawezesha wananchi kiuchumi.
Akizungumza wakati wa hafla ya utoaji wa mikopo hiyo iliyofanyika katika Viwanja vya Stendi ya mabasi kibaoni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Felista Mdemu, ameipongeza Halmashauri hiyo kwa kuendelea kutekeleza kwa vitendo azma ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia mikopo isiyo na riba.
Mdemu amevitaka vikundi vilivyonufaika kutumia mikopo hiyo kwa malengo yaliyokusudiwa, kuzingatia masharti ya mikataba, pamoja na kurejesha mikopo kwa wakati ili kutoa fursa kwa wananchi wengine kunufaika.
Shilingi 404,787,300 tayari imekwishatolewa kwa vikundi 41, vikiwemo vikundi 20 vya wanawake, 17 vya vijana na 4 vya watu wenye ulemavu na Shilingi 195,212,700 zitatolewa kwa vikundi 17 vilivyosalia mara baada ya kukamilisha maboresho yaliyoelekezwa.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Ifakara, Pilly Kitwana amewasihi wananchi wa Halmashauri ya Mji Ifakara kuendelea kuunda Vikundi kwani pesa bado zipo ambazo zitasaidia kuwainua pia ameahidi kuendelea kufanya tathimini na ufuatiliaji kwa vikundi vilivyonufaika ili kuhakikisha mikopo hiyo inaleta tija na kuchangia maendeleo ya kiuchumi kwa wanufaika na jamii kwa ujumla.
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mohamed Aloyce akimuonesha namna uwiano wa uzito na urefu unavyatakiwa kuwa Mfanyakazi wa Bohari Kuu ya Dawa (MSD) Christopher Komba wakati wa kambi maalumu ya siku mbili ya uchunguzi wa afya inayofanywa na wataalamu kutoka JKCI katika ofisi za MSD zilizopo jijini Dar es Salaam.
27/01/2026 Wafanyakazi wanaotumia muda mwingi maofisini wametakiwa kujenga utamaduni wa kufanya uchunguzi wa afya mara kwa mara ili kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo shinikizo la juu la damu na magonjwa ya moyo.
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Daktari bingwa wa watoto kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Theophilly Mushi wakati akitoa mafunzo maalumu kuhusu namna ya kuzuia magonjwa ya moyo na shinikizo la juu la damu katika kambi maalumu ya siku mbili ya upimaji wa afya kwa wafanyakazi wa Bohari Kuu ya Dawa (MSD).
Akizungumzia hali ya afya nchini, Dkt. Theophilly alisema takwimu za Wizara ya Afya zinaonesha kuwa asilimia 20 ya vijana nchini wanakabiliwa na ugonjwa wa shinikizo la juu la damu, huku upande wa watu wazima tatizo hilo likichukua asilimia 35%.
“Mazingira ya kazi za mijini, kushindwa kupata nafasi ya kufika katika vituo vya afya ili kufanya uchunguzi wa afya, kazi za kukaa muda mrefu ofisini bila mazoezi, vimechangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la magonjwa ya moyo miongoni mwa wafanyakazi wanaotumia muda mwingi ofisini”, alisema Dkt. Theophilly
“Magonjwa ya moyo na shikinizo la juu la damu yameendelea kuwa tishio kubwa kwa jamii hususani wafanyakazi wa mijini ndio maana leo tumefika MSD ili kutoa elimu ya afya bora mahali pa kazi, kufanya upimaji wa afya, kuwapa elumu kuhusu umuhimu wa kufanya mazoezi, kuzingatia uzito wenu wa mwili na kuzingatia lishe bora,” alisema Dkt. Theophilly.
Kwa upande wake Mtaalamu wa tiba viungo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Jackline Mariki alisema ni muhimu wafanyakazi wakazingatia afya mahali pa kazi ili kuepuka maumivu ya shingo mabega na mgongo yanayotokana na kukaa kwa muda mrefu na kutokukaa kama inavyotakiwa.
“Tumeona ni muhimu tukawaelimisha wafanyakazi kuhusu afya mahali pa kazi ili waweze kufahamu namna sahihi ya kukaa, aina ya viti vitakavyowaepusha kupata shida za mgongo, namna nzuri ya kunyanyua vitu na kupanga vifaa ili waweze kujikinga na magonjwa ya viungo vya mwili,” alisema Jackline.
Nao wafanyakazi wa MSD walisema mafunzo waliyoyapata yamewapa uelewa mpana kuhusu umuhimu wa kujali afya zao hivyo kuepuka kupata maradhi yanayoweza kuzuilika endapo hatua za kinga zitazingatiwa ipasavyo.
“Nawashukuru sana wataalamu wa JKCI kwa kutufiika na kutupa elimu ambayo itanisaidia kujikinga na magonjwa ya moyo, kinga ni bora kuliko tiba nitatumia elimu niliyoipata kufanya mazoezi yatakayoniepusha na magonjwa hayo,” alisema Emanuel Kiunga, Afisa Tehama Mwandamizi kutoka Bohari Kuu ya Dawa (MSD).
“Kama mfanyakazi ninayetumia muda mwingi kukaa ofisini nimejifunza kupangilia muda wangu ili niweze kupata na muda wa kuchunguza afya yangu na kujilinda na magonjwa yasiyoambukiza, pia nitazingatia ushauri tuliopewa na wataalamu ili afya yangu iwe imara wakati wote,” alisema Dorothy Mtatifikolo.
January 27, 2026
WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kufanya mageuzi ya sera zinazogusa moja kwa moja maslahi na ustawi wa maisha ya wananchi.
Amesisitiza kuwa Serikali haitavumilia watendaji wa Serikali wanaotoa visingizio, wasiowajibika na wenye hulka ya kufanya kazi kwa mazoea, ujanja ujanja na kutoa taarifa za michakato badala ya majibu yanayotakiwa.
Amesema hayo Bungeni leo (Jumanne, Januari 27, 2026) wakati akitoa hoja ya kujadili hotuba ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoitoa jijini Dodoma wakati akizindua Bunge la 13 Novemba 14, 2025.
“Tunapozungumzia utendaji Serikalini, msisitizo ni uadilifu na uwajibikaji wa Serikali kwa wananchi waliotuchagua ili kuhakikisha wananchi wananufaika na rasilimali za nchi pamoja na kupata huduma wanazostahili.”
Dkt. Mwigulu amesema kuwa hotuba aliyoitoa Rais Dkt. Samia ilitoa mwelekeo na dira ya Serikali ya Awamu ya Sita kwa kipindi cha pili. “Hotuba ya Mheshimiwa Rais ilitoa maelekezo na kubainisha changamoto pamoja na majukumu yanayotupasa kuyatekeleza kwa kushirikiana na wananchi na wadau wengine wa maendeleo.”
Katibu Mkuu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. John Jingu akipata mti nje ya jengo la Wizara leo tarehe 26 Januari, 2026 ikiwa zoezi la kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uamuzi wake wa kizalendo wa kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa kwa vitendo vya kulinda mazingira.

Naibu Katibu Mkuu (Muungano) Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Abdallah Hassan Mitawi akipanda mti katika eneo la Mji wa Serikali Mtumba kwa ajili kuadhimisha Kumbukizi ya Siku ya Kuzaliwa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Januari 27, 2026 jijini Dodoma.
pamoja na mambo mbalimbali lengo la kufanya zoezi la upandaji wa miti katika eneo hilo ni kurejesha hali nzuri ya mazingira kwa ajili ya kupumzikia.
Dk Bungwa aliongeza kuwa hadi sasa Tanzania ina jumla ya misitu 465 ambayo inamilikiwa na Serikali Kuu, Serikali za Mitaa, Vijijini na mamlaka zingine na kati ya hiyo, 26 ni hifadhi za misitu ya asili.
Mfuko wa kimataifa wa uwekezaji Sino American Global Fund (SinoAm LLC) umeonesha nia ya kuwekeza hadi Dola za Marekani bilioni 5 nchini Tanzania katika miradi mikubwa ya kimkakati, hususan katika sekta za miundombinu, usafirishaji, nishati, teknolojia, huduma za kifedha na maendeleo ya viwanda.




















.jpeg)
.jpeg)
























