Nafasi Ya Matangazo

January 22, 2026

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi akizungumza kabla ya hafla ya makabidhiano kati ya Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) na Kituo cha Taifa cha Ufuatiaji Kaboni (NCMC) mjini Morogoro Januari 21,2026.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi akizungumza kabla ya hafla ya makabidhiano kati ya Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) na Kituo cha Taifa cha Ufuatiaji Kaboni (NCMC) mjini Morogoro Januari 21,2026.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi (mwenye tai) akiwa kwenye ziara ya kutembelea jengo la Kituo cha Taifa cha Ufuatiliaji wa Kaboni (NCMC) kabla ya hafla ya kukabidhi Ofisi kati ya Chuo Kikuu Kilimo cha Sokoine (SUA) na Kituo cha Taifa cha Ufuatiaji Kaboni (NCMC) mjini Morogoro Januari 21, 2026.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na watendaji wakati wa hafla ya makabidhiano ya Ofisi kati ya Chuo Kikuu Kilimo cha Sokoine (SUA) na Kituo cha Taifa cha Ufuatiaji Kaboni (NCMC) mjini Morogoro Januari 21, 2026.

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi amekitaka Kituo cha Taifa cha Kufuatilia Kaboni (NCMC) kuimarisha ushiriki wa Tanzania katika masoko ya kimataifa ya kaboni kwa kuimarisha miradi ya uhifadhi na utunzaji wa mazingira.

Hayo ameyasema Januari 21, 2026 wakati wa makabidhiano ya kituo hicho kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) kwenda Ofisi ya Makamu wa Rais, ambapo Dkt. Muyungi amefafanua kuwa kituo kitachangia kukua kwa uchumi wa Taifa na kujenga uwezo wa Tanzania kushiriki katika biashara hiyo.

“Katika Dira ya 2050 tumejiwekea malengo ya kukusanya mapato ya dola bilioni moja kwa mwaka kutoka katika biashara ya kaboni ya nchi kavu na dola bilioni moja kutoka uchumi wa bluu”

Kwa upande wake Naibu Makamu Mkuu wa SUA Prof. Raphael Chigunda amemhakikishia Katibu Mkuu kuwa chuo hicho kitaendelea kutoa ushirikiano wa kitaalamu katika masuala ya biashara ya kaboni ili kituo kiendelee kuibua na kuandaa miradi ya kaboni na hatimaye Taifa na wananchi waweze kunufaika.

Awali akaiongea katika hafla hiyo; aliyekuwa Afisa Mtendaji Mkuu wa NCMC Prof. Eliakimu Zahabu amesema ataendelea kutoa ushirikiano kwa wataalamu wa kituo hususan katika Kutafuta fursa za uwekezaji katika biashara ya kaboni.

Naye Afisa Mtendaji Mkuu wa Kituo hucho Bi. Kathryn Kigaraba, amebainisha kuwa Kituo hicho kitaendelea na usimamizi wa gesi joto; na biashara ya kaboni na masoko ya kaboni ili kuwa taaasisi muhimu katika mfumo wa kitaifa wa mabadiliko ya tabianchi na masoko ya kaboni. 

Kituo hicho kimeanzishwa kwa mujibu wa Kifungu cha 29 cha Sheria ya Usimamizi wa Mazingira, Sura ya 191 (Marekebisho ya 2025), Kituo hicho ni taasisi ya kimkakati ya kitaifa yenye jukumu la kuratibu shughuli zinazohusiana nausimamizi wa gesi joto pamooja na biashara ya kaboni na masoko ya kaboni. 

Biashara ya Kaboni ni mfumo wa kiuchumi unaoruhusu uuzaji na ununuzi wa Viwango vya Kaboni ambapo lengo lake ni kupunguza gesijoto angani.
 
Posted by MROKI On Thursday, January 22, 2026 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo