Nafasi Ya Matangazo

September 18, 2026



Na Neema Mbuja
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe.Dennis Londo, amewataka wafanyabiashara wa Tanzania  kutumia fursa kubwa kupitia Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Soko Huru la Afrika, kuuza bidhaa  zao.

Mhe. Londo ameyasema hayo wakati alipokuwa akifunga hafla ya utoaji tuzo za jukwaa la 4 la biashara na uwekezaji kwa Watendaji Wakuu na Wakurugenzi wa makampuni 200 ambalo linawakutanisha wadau kujadili namna ya kufungua fursa kwa watanzania, wajasiriamali kufanya  biashara nje ya Tanzania.

Mhe Londo amesema kuwa uwepo wa jukwaa hili kunasaidia kuwakutanisha Wakurugenzi   Makampuni kubadilishana uzoefu  ma kuchangamkia fursa zilizopo.

Aliongeza kuwa Tanzania ni mwanachama wa EAC na SADC na sasa inaelekea kwenye Itifaki ya Soko Huru la Afrika, hivyo maandalizi ni sehemu muhimu ya kuhakikisha Watanzania wanashiriki na kunufaika na jumuiya hizo.

Amesema Wizara ya viwanda na Biashara itaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa ajili ya wafanyabiashara kufungua fursa zaidi kwa kushirikiana na sekta binafsi ili kukuza uchumi wa nchi.
Posted by MROKI On Friday, September 18, 2026 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo