Kikwete ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Chalinze ameyasema hayo wakati akihutubia wahitimu wa kidato cha Sita katika mahafali shuleni hapo leo.
Kikwete aliwaasa wahitimu hao kuhakikisha wanafaulu ili waache deni la kufuatwa na wadogo zao wanaowafuata kwa upande mmoja, wawape heshima Walimu na wazazi pia kwa kufaulu vizuri.
Akizungumza kabla ya kumkaribisha Mbunge kuzungumza na Wahitimu, Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Mwalimu Sakasa aliishukuru serikali kwa kuendelea kupeleka pesa za Elimu bure , vifaa na kuongezeka kwa madarasa na walimu shuleni hapo huku akimuomba Mgeni rasmi kuendelea kuikumbuka shule hiyo kwa kuisaidia vifaa na kuongeza mabweni ya wanafunzi.
0 comments:
Post a Comment