Nafasi Ya Matangazo

April 23, 2024

Mkuu wa mkoa wa Singida Halima Dendego akishiriki zoezi la usafi katika Soko Kuu la Mji wa Singida akiwa na Wananchi wa Singida.
Mkuu wa mkoa wa Singida Halima Dendego akizungumza na Wakazi wa Mji wa Singida mara baada ya kumaliza shughuli za usafi katika Soko Kuu la Singida ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Mkuu wa wilaya ya Singida Godwin Gondwe  akifanya usafi na wananchi katika soko kuu la Singida.
Mkuu wa wilaya ya Singida Godwin Gondwe akizungumza na wakazi wa mji wa Singida kabla ya kumkaribisha Mkuu wa mkoa Kuzungumza na Wakazi wa Mji wa Singida walioshiriki zoezi la Usafi.


Mkuu wa mkoa wa Singida Halima Dendego akishiriki zoezi la usafi katika Soko Kuu la Mji wa Singida akiwa na Wananchi wa Singida.

Mkuu wa mkoa wa Singida Halima Dendego ameonya kuwa atawachukulia hatua kali watu au kikundi cha watu wanaotaka kuvuruga au kuvunja amani na utulivu kwa wananchi wa mkoa wa Singida.

Mkuu wa mkoa wa Singida ametoa kauli hiyo (leo 23/Apr/24 ) mjini Singida, katika uzinduzi wa wiki ya maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa kufanya usafi katika maeneo mbalimbali ya Soko Kuu la Singida.

Mkuu huyo wa mkoa wa Singida amewasisitiza wananchi wa mkoa wa Singida kuwakataa watu au mtu yeyote anayetaka kumdhalilisha Rais au Watanzania kwani wakiwaruhusu kufanya hivyo watakuwa wamedhalilisha Taifa na Watanzania wote hivyo ni lazima wananchi wote waungane kukataa watu hao wenye nia mbaya na Taifa la Tanzania.

“Tuungane wote katika kupambana na yeyote anayetaka kuleta ujinga ujinga katika Taifa letu tuwabaini ili tuwawajibishe “ Amesisitiza Halima Dendego.

Halima Dendego amesema yeye ni rafiki wa wote Vijana,Wazee na Wanawake hivyo Ofisi yake ipo wazi muda wote kwa anayetaka kusaidiwa kwa shida yeyote aende ili asaidiwe nia ni kuona wananchi Singida wanaishi maisha mazuri na yenye staha bila kero. 

Kwa upande wake, Mkuu wa wilaya ya Singida Godwin Gondwe amemhakikishia Mkuu wa mkoa wa Singida kuwa atasimamia maelekezo yake yote aliyotoa hasa ya kuhakikisha Manispaa ya Singida inakuwa safi katika maeneo yote ya Masoko na maeneo yenye watu wengi kama hatua ya kudhibiti magonjwa ya maambukizi ikiwemo kipindupindu.

Godwin Gondwe amesema kuwa hivi karibuni watazindua kampeni kubwa ya usafi katika Manispaa ya Singida ambayo itasaidia kuboresha usafi katika maeneo yote ya mji wa Singida ikilinganishwa na hali ilivyo sasa.

Naye, Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida Edward Mboya amebainisha kuwa kupitia mapato ya ndani wanaendelea na mchakato wa kununua gari nyingine mpya ya kubebea taka na vifaa vya kuhifadhi taka lengo ikiwa ni kuifanya Manispaa ya Singida kuwa bora nchini hasa katika masuala ya Usafi.


 Mkuu wa wilaya ya Singida Godwin Gondwe akizungumza na wakazi wa mji wa Singida kabla ya kumkaribisha Mkuu wa mkoa Kuzungumza na Wakazi wa Mji wa Singida walioshiriki zoezi la Usafi.
Posted by MROKI On Tuesday, April 23, 2024 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo