Nafasi Ya Matangazo

April 23, 2024

Naibu Waziri wa Utumishi na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete akishiriki katika maandamano ya amani kuelekea uzinduzi wa Jukwaa la kuwawezesha wanawake kiuchumi Kata ya Kiwangwa, Tarafa ya Msata. 
Naibu Waziri wa Utumishi na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete akishiriki katika maandamano ya amani kuelekea uzinduzi wa Jukwaa la kuwawezesha wanawake kiuchumi Kata ya Kiwangwa, Tarafa ya Msata.
Naibu Waziri wa Utumishi na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete akizungumza wakati wa 25 uzinduzi wa Jukwaa la kuwawezesha wanawake kiuchumi Kata ya Kiwangwa, Tarafa ya Msata
Naibu Waziri wa Utumishi na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete amezindua Jukwaa la kuwezesha wanawake kiuchumi Kata ya Kiwangwa, Tarafa ya Msata. 

Sherehe hizo zilizopambwa na maandamano ya Amani yakifuatiwa na mjadala kuhusu uwezeshaji na fursa mbalimbali za kumkomboa na kumuwezesha Mwanamke katika jamii.

Kikwete alisema kupitia fursa mbalimbali zilizopo zikiwemo za ndani ya Halmashauri na zile zinazo simamiwa na Serikali kuu wanawake wana nafasi ya kusaidia ukuaji wa kipato ndani ya jamii na familia.

 "Kwa mujibu wa Taarifa za Sensa, ongezeko wa idadi ya Wanawake wanaotegemewa ndani ya Familia umeongezeka  kufikia asilimia 37.6. Idadi hii inatoa fursa za kuwezesha wanawake katika jamii," alisema Kikwete.  

Aidha alisema Serikali imeendelea kufanya jitihada mbalimbali ikiwemo kurudisha mikopo ya asilimia 10, mfuko kusaidia Wananchi kuendelea kutenga fedha kuwezesha wananchi kiuchumi na fursa nyenginezo. 

Kikwete ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Chalinze aliwaunga mkono kupitia ofisi ya Mbunge ambayo ilichangia Shilingi Milioni 4.6 kuwezesha vikundi kukopeshana.
Posted by MROKI On Tuesday, April 23, 2024 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo