Nafasi Ya Matangazo

October 06, 2016

Kamanda Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohammed Mpinga akipokea moja ya stika zilitolewa na TPB kutoka kwa Meneja Masoko na Uendeshaji wa TPB, Deo Kwiyukwa



Kamanda Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohammed Mpinga, Meneja Masoko na Uendeshaji wa TPB, Deo Kwiyukwa pamoja na Afisa Uhusiano na Mawasiliano ya TPB, Timotheo Mwakifulefule wakionyesha stika hizo kwa vyombo vya habari.



Kamanda Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohammed Mpinga akibandika stika hizo katika moja ya gari la abiria katika stendi ya mabasi yaendayo mikoani, Ubungo. Kulia niMeneja Masoko na Uendeshaji wa TPB, Deo Kwiyukwa



Meneja Masokona Uendeshaji wa TPB, Deo Kwiyukwa akiongea na vyombo vya habari, baada ya kutoa stika za kwenda kwa usalama barabarani



Kamanda Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohammed Mpinga akiishukuru TPB wakati akiongea na vyombo vya habari.



Kamanda Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohammed Mpinga akitoa maelekezo juu ya matumizi sahihi ya stika hizo kwa viongozi wa Kikosi cha usalama barabarani pamoja na wakuu wa Chama cha Kutetea Abiria (CHAKUA) BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.




Kamanda Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohammed Mpinga akipokea zawadi ya TPB kutoka kwa Meneja Masoko na Uendeshaji wa TPB, Deo Kwiyukwa.
*****************
BENKI ya Posta Nchini (TPB) imetoa msaada wa stika zaidi ya 2,000 zenye namba za Wakuu wa Usalama Barabarani wa Mikoa yote nchini zitakazobandikwa kwenye mabasi yaendayo mikoani.Huu ni mwaka wa nne mfululizo benki hiyo anatoa stika hizo kwa lengo la kupunguza ajali katika kipindi hiki cha kuelekea mwishoni mwa mwaka.


Akizungumza wakati wa kubandika stika walizozipokea katika mabasi hayo, Kamanda Mkuu wa Usalama Barabarani Mohammed Mpinga, aliwataka madereva  kuendelea kuzingatia Sheria na kanuni za usalama barabarani ili kutokomeza ajali zinazoendelea kupoteza maisha ya watu wengi.Alisema ofisi yake ilikuwa inapokea maombi mengi kutoka kwa wananchi ili kupata namba zitakazowawesha kutoa taarifa za madereva wanaofanya makosa wakiwa safarini.

Alisema kuwa stika hizo zitabandikwa katika mabasi yote yaendayo mikoani pamoja na yae madogo maarufu kama Coastal. "Tunaishukuru benki ya Posta kwa msaada huu kwani wametupa muda muafaka wa kuelekea mwishoni mwa mwaka ambapo kumekuwa na ajali nyingi sana zinazopoteza maisha ya watu wengi na kuwaacha wengine na ulemavu wa kudumu", alisema Kamanda Mpinga.

Aliongeza kuwa Kitengo chake kitaendelea kushirikiana na TPB na wadau wengine kuhakikisha wanaendesha kampeni hii na kutokomeza kabisa ajali za barabarani.

Akikabidhi msaada huo Meneja Masoko na Uendeshaji wa TPB, Deo Kwiyukwa alisema kuwa lengo la kutoa stika hizo ni kupunguza ajali na kupoteza nguvu kazi ya Taifa katika kipindi hiki cha kuelekea mwishoni mwa mwaka.

Alisema kwa kipindi cha miaka minne iliyopita toka waanze kampeni hiyo ajali nimeweza kupungua kwa kiasi kikubwa kutokana na madereva kuhofia kuripototiwa na abiria katika vyombo vya Usalama ambapo itapelekea kusimamishwa, faini kali au kifungo.

Deo aliwataka abiria kutumia vema namba hizo za simu kwa lengo lakudhibiti mwendo mkali na kutokomeza kabisa ajali hizo."TPB napenda kuwaasa watumiaji wa mabasi ambao wengi ni wateja wetu kutoa taarifa katika vyombo vya Usalama pale madereva wanaofanya makosa hasa.

Naye Afisa elimu kutoka Chama cha Kutetea Abiria (CHAKUA), Gervas Rutagunziga alisema kuwa viashiria vya ajari ni vingi sana lakini wananchi hawapo katika sehemu sahihi ya kulisemea jambo hilo, hivyo basi TPB inawapa nafasi kwa abiria kuokoa maisha yao kwa kupiga simu pale ambapo wanakuwa hawaridhishwi na mwendo kasi wa dereva au hali ya dereva kama amelewa au hajalewa.

"Mara nyingi abiria wamekuwa na uwezo wa kuzuia ajali lakini wanashindwa kufanya hivyo kutokana na kutojua watafikisha vipi taarifa katika vyombo husika, hivyo tunaamini kupitia stika hizi zenye namba za simu abiria sasa watakuwa na uwezo mkubwa zaidi wa kulinda maisha yao" alisema Rutagunziga.

Posted by MROKI On Thursday, October 06, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo