Nafasi Ya Matangazo

September 10, 2024

Na Mwandishi Wetu, WHMTH, Arusha.
Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH) kwa kushirikiana na Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania-TANAPA, kupitia mradi wa Anwani za Makazi (NaPA) imefanikiwa kusajili anwani za makazi za vivutio vya utalii 187 na barabara zaidi ya 60 zinazopatikana ndani ya Hifadhi tatu zilizofanyiwa kazi.

Katika zoezi hilo lililoendeshwa katika Hifadhi za Taifa za Arusha, Ziwa Manyara na Tarangire, WHMTH imefanikiwa pia kusajili huduma 221 na kujenga uelewa wa Mfumo wa NaPA na umuhimu wake kwa Menejimenti zote za Hifadhi husika.

Hayo yamebainishwa tarehe 10 Septemba, 2024 na Mratibu wa kitaifa wa Mradi huo kutoka WHMTH, Mhandisi Jampyon Mbugi kwenye kikao cha majumuisho ya zoezi la usajili wa Vivutio vya Utalii katika Mfumo wa NaPA kwenye Hifadhi za Taifa.


Viongozi na Wataalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH), Wizara ya Maliasili na Utalii (WMU) na Wahifadhi na Viongozi wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania-TANAPA, wakiwa kwenye kikao cha majumuisho ya zoezi la ukusanyaji wa taarifa za Anwani za Makazi lililofanyika awamu ya kwanza katika Hifadhi za Arusha, Ziwa Manyara na Tarangire tarehe 10 Septemba, 2024 mkoani Arusha.

Viongozi na Wataalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH), Wizara ya Maliasili na Utalii (WMU) na Wahifadhi na Viongozi wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania-TANAPA, wakifuatilia wasilisho kwenye kikao cha majumuisho ya zoezi la ukusanyaji wa taarifa za Anwani za Makazi lililofanyika awamu ya kwanza katika Hifadhi za Arusha, Ziwa Manyara na Tarangire tarehe 10 Septemba, 2024 mkoani Arusha.



Viongozi na Wataalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH), Wizara ya Maliasili na Utalii (WMU) na Wahifadhi na Viongozi wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania-TANAPA, wakifuatilia wasilisho kwenye kikao cha majumuisho ya zoezi la ukusanyaji wa taarifa za Anwani za Makazi lililofanyika awamu ya kwanza katika Hifadhi za Arusha, Ziwa Manyara na Tarangire tarehe 10 Septemba, 2024 mkoani Arusha.





Katika kikao hicho kilichohudhuriwa na wataalamu wa Mfumo wa NaPA, baadhi ya Wahifadhi, Viongozi wa TANAPA na Wawakilishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Mhandisi Mbugi amesema, ukamilishaji wa zoezi hilo utawezesha kuwa na taarifa nyingi za vivutio hivyo na kuzidi kuvitangaza ili kuwavutia watalii kufika na kuvitembelea.

Kuhusu uwekaji wa miundombinu katika maeneo ya Hifadhi, Mhandisi Mbugi amesema, kwa kuwa NaPA una sehemu mbili, yaani kidijitali (digital part) na miundombinu (Physical infrastructure), ni muhimu sehemu ya miundombinu ikafanyiwa kazi kwa kuweka kulingana na taarifa zilivyoingizwa kwenye Mfumo wa NaPA, kwani kwa sasa taarifa zimekusanywa kwenye mfumo wa kidigitali pekee.

Amesema, kuweka mfumo wa miundombinu kutamrahisishia mtalii au askari kutambua na kuona kwa urahisi eneo alilohitaji kulitembelea au kulifanyia kazi.

Aidha Mhandisi Mbugi amesema, ili kuhamasisha matumizi ya Mfumo wa NaPA kwa watalii, ni muhimu TANAPA ikashiriki kikamilifu kutangaza na kuhamasisha matumizi yake katika masuala ya utalii kuwezesha kufikiwa kwa malengo na kupata manufaa yanayokusudiwa.

Ameshauri picha za vivutio ziwekwe kwenye Mfumo wa NaPA ili kumvutia Mtalii anapotafuta taarifa za Hifadhi husika kama picha hizo zinavyowekwa kwenye Mitandao (Website) za Hifadhi, na kusisitiza kuwa, uwekaji wa Miundombinu ya Anwani za Makazi katika majengo ya Ofisi, mageti na hoteli, uzingatie Mwongozo wa Anwani za Makazi wa Mwaka 2016, isipokuwa kwa maeneo mengine, uzingatie Sheria, Kanuni na Miongozo ya uhifadhi.

Kwa upande wake Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi, Bw, Ignace Gara ameipongeza Wizara kwa utekezaji wa zoezi hilo na kwamba siyo tu ni msaada katika kutangaza utalii bali pia una faida katika ulinzi na uhifadhi wa wanyama adimu.
Posted by MROKI On Tuesday, September 10, 2024 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo