Nafasi Ya Matangazo

April 22, 2024

Na Joseph Mahumi, WF, Washington
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia anayesimamia Kundi la Kwanza la nchi za Kanda ya Afrika (Africa Group 1 Constituency), Dkt. Floribert Ngaruko, wakati wa mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) jijini Washington D.C, Nchini Marekani, ambapo wamejadiliana masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Benki hiyo na Tanzania.

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb) (kushoto), na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia anayesimamia Kundi la Kwanza la nchi za Kanda ya Afrika (Africa Group 1 Constituency), Dkt. Floribert Ngaruko, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumalizika kwa kikao chao kilichofanyika Makao Makuu ya Benki hiyo, jijini Washington D.C, nchini Marekani, wakati wa mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), ambapo wamejadiliana masuala mbalimbali yanayohusu ushirikiano kati ya Benki ya Dunia na Tanzania.

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), akizungumza jambo wakati wa kikao chake na  Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia anayesimamia Kundi la Kwanza la nchi za Kanda ya Afrika (Africa Group 1 Constituency), Dkt. Floribert Ngaruko (hayupo pichani) Makao Makuu ya Benki hiyo jijini Washington D.C, nchini Marekani,  wakati wa mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), ambapo wamejadiliana masuala mbalimbali yanayohusu ushirikiano kati ya Benki ya Dunia na Tanzania.

Ujumbe wa Tanzania (kushoto) ukiongozwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), ukiwa katika kikao na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia anayesimamia Kundi la Kwanza la nchi za Kanda ya Afrika (Africa Group 1 Constituency), Dkt. Floribert Ngaruko, Makao Makuu ya Benki hiyo jijini Washington D.C, nchini Marekani, wakati wa mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), ambapo wamejadiliana masuala mbalimbali yanayohusu ushirikiano kati ya Benki ya Dunia na Tanzania.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia anayesimamia Kundi la Kwanza la nchi za Kanda ya Afrika (Africa Group 1 Constituency), Dkt. Floribert Ngaruko (Katikati), akizungumza wakati wa kikao na ujumbe wa Tanzania ulioongozwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), kilichofanyika Makao Makuu ya Benki hiyo jijini Washington D.C, nchini Marekani, wakati wa mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), ambapo wamejadiliana masuala mbalimbali yanayohusu ushirikiano kati ya Benki ya Dunia na Tanzania. Wengine katika picha ni Mkurugenzi Mtendaji Mbadala wa Benki ya Dunia, anayewakilisha Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika (Africa Group 1 Constituency (AfG1), Dkt. Zarau Kibwe (kushoto), Mshauri wa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia, anayewakilisha Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika (Africa Group 1 Constituency (AfG1), Bw. Venuste Ndikumwenayo (kulia).

 

Posted by MROKI On Monday, April 22, 2024 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo