Nafasi Ya Matangazo

March 10, 2024












gahaha
Kamanda Mkuu wa Idara Maalum za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amewahimiza Maafisa, Askari na Wapiganaji wa Vikosi vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuendelea kudumisha nidhamu, uzalendo , uwajibikaji na uadilifu.

Rais Dk Mwinyi amesema hayo akizungumza na Maafisa , Askari na Wapiganaji alipotembelea Kikosi cha Kuzuia Magendo Zanzibar(KMKM) Kibweni na Kikosi  cha KVZ Mtoni Mkoa wa Mjini Magharibi ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kutembelea Vikosi vya SMZ  na kuhitimisha leo tarehe: 10 Machi 2024. 

Aidha Rais Dk.Mwinyi amewapongeza Kikosi cha Kuzuia Magendo (KMKM) na Kikosi cha KVZ kwa utekelezaji wa kazi nzuri za ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayofanywa na Serikali.

Kwa upande mwingine Rais Dk.Mwinyi amesema Serikali itaendelea kuboresha miundombinu mbalimbali ya Vikosi hivyo.
Posted by MROKI On Sunday, March 10, 2024 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo