Nafasi Ya Matangazo

October 04, 2016



Meneja Masoko wa Tbl Group ,George Kavishe (kulia) na Kaimu Meneja Mkuu wa Kampuni ya Konyagi Tanzania (TDL) Devis Deogratius (kushoto) wakiteta jambo wakati walipokuwa wakiwaonyesha  waandishi wa habari( hawapo pichani)  moja ya  zawadi ya magari  wakati wa kutambulisha  wa zawadi za kampeni iliyoendeshwa kwa wasamabazaji wake  ya NUNUA,UZA,SHINDA NA KONYAGI iliyodumu kwa muda wa wiki 12 iliyoanza Julai mpaka Septemba 2016 hafla hiyo ilifanyika leo kwenye ofisi za Konyagi Chang’ombe jijini Dar es Salaam.

Moja ya zawadi ya magari ya Kampeni ya Nunua Uza ,Shinda na Konyagi kwa wasambazaji wake nchini yaliyotambulishwa  kwa waandishi wa habari kwenye ofisi za Tanzania Distilleries Limited(TDL) leo jijini Dar es Salaam.



Kaimu Meneja Mkuu wa Kampuni ya Konyagi Tanzania (TDL) Devis Deogratius (kushoto) akiongea na waandishi wahabari wakati wa kutambulisha  zawadi za kampeni iliyoendeshwa kwa wasamabazaji wake  ya NUNUA,UZA,SHINDA NA KONYAGI iliyodumu kwa muda wa wiki 12 iliyoanza Julai mpaka Septemba 2016.Katikati ni Kaimu meneja wa huduma za masoko wa Konyagi, George Kavishe. hafla hiyo ilifanyika leo jijini Dar es Salaam.

Kaimu Meneja wa huduma za masoko wa Konyagi George Kavishe (kulia) akiongea na waandishi wahabari wakati wa kutambulisha  zawadi za kampeni iliyoendeshwa kwa wasamabazaji wake  ya NUNUA,UZA,SHINDA NA KONYAGI iliyodumu kwa muda wa wiki 12 iliyoanza Julai mpaka Septemba 2016 hafla hiyo ilifanyika leo kwenye ofisi za Konyagi Chang’ombe jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Kaimu Meneja Mkuu wa Kampuni ya Konyagi Tanzania (TDL) Devis Deogratius

Meneja Masoko wa TBL Group, George Kavishe akijaribu kuendesha moja zawadi ya gari wakati wa kutambulisha kwa waandishi wahabari (hawapo pichani) zawadi za kampeni iliyoendeshwa kwa wasamabazaji wake  ya NUNUA,UZA,SHINDA NA KONYAGI iliyodumu kwa muda wa wiki 12 iliyoanza Julai na inakaribia kuika mwisho, hafla hiyo ilifanyika leo kwenye ofisi za Konyagi Chang’ombe jijini Dar es Salaam. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.

KAMPUNI ya Tanzania Distilleriers Limited (TDL) inayotengeneza na kusambaza kinywaji maarufu cha Konyagi na jamii zake, leo imezitambulisha zawadi za kampeni iliyoendeshwa kwa wasambazaji wake kwa kampeni iliyojulikana kama NUNUA, UZA, SHINDA NA KONYAGI  iliyodumu  kwa muda wa wiki 12. Toka Mwanzo wa Julai  mpaka Mwisho wa mwezi Septemba 2016.


Akizungumza katika hafla hiyo iliyofanyika katika Ofisi za Konyagi Changombe  - Dar es salaam, Kaimu Meneja Mkuu wa Kampuni ya TDL, Bwana Devis Deogatius  “Tunazitambulisha zawadi hizi kwa ili watu waamini kwamba tulichohaidi tumetekeleza, tunafahari kubwa kwa jinsi kampeni hii ilivyoongeza chachu ya manunuzi na wasambazaji wetu walifanya kazi nzuri .

Tutakabidhi magari haya katika hafla mbili, droo ya kwanza itafanyika Mbeya siku ya Ijumaa tarehe 07 Oktoba katika ukumbi wa Mbeya City Pub na itahusisha wasambazaji wa mikoa ya Kusini na Nyanda za juu Kusini.

 Droo ya pili itafanyika Mjini Moshi tarehe 13 Oktoba katika ukumbi wa Kili Home na itahusisha wasambazaji wa Kanda ya Kaskazini na Kanda ya Magharibi mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Dhumuni kuu la kampuni yetu ya TDL kuendesha kampeni hii ni kwanza kabisa kuwainua wasambazaji wa bidhaa zetu kwa kuwapa nafasi ya kushinda vitendea kazi. 

Tuliwapa malengo na waliofikia wataingizwa kwenye droo ili kujishindia  magari mapya mawili ya usambazaji (Eicher 3 Tonne Truck zenye thamani ya zaidi ya milioni 110). Tunaamini kwa magari haya wasambazaji wetu wataweza kurahisishwa utendaji wao ndani ya maeneo yao ya mauzo”

Pia, kupitia shindano hili tutaweza kuchangia maendeleo ya kichumi nchini pamoja na jamii kwa ujumla. Aliendelea kusema.

Naye Kaimu Meneja wa huduma za Masoko wa Konyagi Bwana George Kavishe “ ni faraja yetu kubwa tukiona huduma za bidhaa zetu zikiboreshwa kila mara na kuwafanya wasambazaji wetu wawe na motisha ya kuendelea kufanya kazi na sisi tunawashukuru sana kwa wale waliofanikisha programu hii. Maandalizi yote ya droo kwenye mikoa ya Mbeya na Kiimanjaro yamekamilia na tupo imara.
Posted by MROKI On Tuesday, October 04, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo