Nafasi Ya Matangazo

August 08, 2026

Na: Mwandishi Wetu
Mpango wa serikali wa kutoa mikopo isiyo na riba ya asilimia kumi kwa wanawake, vijana na wenye mahitaji maalum, imeonyesha kuzaa matunda kwa wananchi wa Mbalizi mkoani Mbeya.

Hii ni kutokana wa wanufaika wa mikopo hiyo kuitumia kwa malengo ya kujikwamua kiuchumi na kubadili hali za maisha yao.

Matokeo chanya hayo yameonekana katika ziara ya Wajumbe wa Baraza la Utekelezaji la Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Taifa, wakiongozwa na Mwenyekiti wake, Mary Chatanda, Agosti 6, 2026.

Akiwa katika ziara hiyo, Chatanda ametembelea kikundi cha wauzaji wa nafaka ambacho kimenufaika na mkopo wa shilingi milioni 56. Kikundi hicho kimefanikiwa kurejesha robotatu ya mkopo huo. Kutokana na uaminifu huo, Chatamda ameeleza wakimaliza mkopo huo, wakopeshwe tena kwa kuwa wamefanya vizuri katika marejesho ya mkopo wao.

"Mmefanya vizuri kukopa ili mjikwamue kiuchumi, na kwa kuwa mmefanikiwa kurejesha robotatu ya mkopo wenu, nitoe wito kwa uongozi wa Halmashauri kuwakopesha tena pindi mtakapomaliza mkopo wenu wote, na mimi nawachangia 1,200,000 ili mlipe pango kwa kipindi cha mwaka mzima," amesema Chatanda.

Vilevile, ujumbe wa UWT Taifa, ulitembelea kikundi cha mamalishe cha stendi ya Mbalizi ambacho kimekopeshwa milioni 50. Kikundi hicho kimeendelea kurejesha vizuri mkopo wao na kufanikisha kuzalisha biashara nyingine.

Halikadhalika, wamewatembelea wanawake wauzaji wa matunda katika stendi hiyo, ambapo Chatanda aliwapa elimu ya ujasiriamali na kuwachangia 300,000 ili iongeze mtaji katika biashara yao.





 

Posted by MROKI On Saturday, August 08, 2026 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo