Nafasi Ya Matangazo

February 18, 2016

Baada ya kufanya semina ya ujasiriamali na kutoa elimu ya kuboresha mtaji kwa vijana takribani vijana 300 mkoani Morogoro, Kampuni ya Simu za mkononi ya Airtel kupitia Mpango wa Airtel Fursa  imeendeleza na dhamira yake ya kuboresha maisha ya watanzania na kuwawezesha kuzifikia ndoto zao.

Kwa kuthibitisha dhamira  Airtel FURSA imemkabidhi mjasiliamali  wa bucha la nyama  wa  mji mdogo wa Ngerengere, wilayani Morogoro, Hashim Mikidadi , vifaa vya kisasa vinavyotumika katika kazi yake, jokofu,  pamoja nakukarabati bucha,  vyenye jumla ya thamani ya shilingi  milioni tisa.

Hashim Mikidadi ni kijana mwenye umri wa miaka 23 aliyejikita katika shughuli za ujasiliama wakati akiendelea na elimu ya Sekondari ili kukidhi mahitaji ya shule na chakula pamoja na kusaidia wazazi wake ambao ni wazee. Akiwa Katika umri wa miaka 17 alianza kuweka akiba ya Ths. 300,000 iliyopatikana kutokana na kazi ya kufyatua na kuuza matofali.  Aliamua kuzitumia pesa hizo na kuwekeza katika kilimo cha Ufuta ambapo baada ya  misimu miwili ya kilimo , Hashimu alifanikiwa kupata shilingi laki Tsh 800,000 ambazo alianzisha biashara ya bucha ambayo anaendelea nayo hadi sasa.

Akiongea kwa furaha mara baada ya kukabithiwa vifaa hivyo Mjasiriamali  Mikidadi , aliishukuru mungu kwa kupata msaada huu kupitia  Airtel Fursa na kusema “ nilianza biashara nikiwa na mtaji mdogo ambao haukidhi mahitaji ya biashara yangu. Sikuwa na vifaa vya kuniwezesha kufanya biashara yangu kwa ufanisi lakini leo Airtel kupitia Airtel FURSA imeniwezesha na sasa naamini ntawawezesha kuendesha biashara hii na kuisadia familia yangu pamoja na jamii inayonizunguka”

“Napenda kutoa shukrani pia  kwa wafanyakazi wa Airtel kwa kushiriki katika  ukarabati mkubwa wa bucha langu kwani uwepo wa vifaa hivi  vya kisasa katika bucha yangu ni  kuhamasisha wateja wangu na wale ambao si  wateja wangu wavutiwe kupata huduma  kutoka katika hii” alisema Mikidadi.

Akiongea wakati wa kumkabithi vifaa hivyo, Meneja wa Huduma za Jamii wa  Airtel Tanzania, Hawa Bayumi alisema Airtel inaijali jamii inayowazunguka na kuzielewa changamoto nyingi ambazo vijana wamekuwa wakikutana zao ikiwa ni pamoja na ukosefu wa ajira na ukosefu wa mitaji wa kuanzisha biashara zao  na mpango wa Airtel Fursa ni njia moja wapo  ya kubadirisha maisha yao.

Leo unayofuraha kumpatia msaada wenye thamani ya shilingi milioni 9 ikiwa vifaa, ni pamoja  na gharama za ukarabati mkubwa uliofanyika kwenye  bucha hiyo  ambayo  kwa sasa imekuwani ya viwango vya juu katika mji wa Ngeregere .

 “Airtel FURSA”  ni mradi endelevu unaowalenga vijana nchi nzima kwa kuwapatia vifaa  ,mafunzo ya biashara na mafunzo mbalimbali kupitia mtandao ili kufikia malengo yao.

Kutuma maombi tuma ujumbe mfupi kwenda namba 15626 ikiwa na taarifa zifatazo Jina, umri, aina ya biashara unayoifanya, mahali na namba za simu. Unaweza pia kutuma maombi yako kwa kupitia barua pepe ya airtelfursa@tz.airtel.com. Or tembelea tovuti yetu ya  www.airtel.com  na ujaze fomu yako ya maombi
Posted by MROKI On Thursday, February 18, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo