Nafasi Ya Matangazo

December 31, 2015

Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako (kushoto), akisisitiza jambo, alipokuwa akizungumza na wafanykazi wa Baraza la Taifa la Elimu na Ufundi (NACTE) jana alipotembelea makao makuu ya baraza hilo lililopo jijini Dar es Salaam jana,wapili toka kushoto ni na Katibu Mtendaji wa Baraza hilo Dk.Primus Nkwera.
Waziri wa Elimu,Sayansi,Teknolojia na Ufundi Profesa Joyce Ndalichako,akimsikiliza kwa makini Vincent Jacob, mtalamu wa mtandao wa udhibiti wa utoajia wa vyeti vya satifiketi na Diploma wa Baraza la Taifa la  Elimu na ufundi (NACTE). Waziri alifanya ziara ya kutembelea makao makuu ya baraza hilo jijini Dar es Salaam jana,Watatu kushoto ni Katibu Mtendaji wa Baraza hilo Dk.Primus Nkwera.
 Waziri wa Elimu Sayansi,Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako, akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumaliza kuzungumza na wafanyakazi wa Baraza la Taifa la  Elimu na ufundi (NACTE) jijini Dar es salaam jana.
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Profesa. Joyce Ndalichako, akitembezwa katika maeneo ya ofisi za Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) jijini Dar es salaam jana na Katibu Mtendaji wa Baraza hilo Dk.Primus Nkwera. Waziri huyo alikuwa katika ziara ya kutembelea taasisi za elimu zilizochini ya wizara yake.
Posted by MROKI On Thursday, December 31, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo