Nafasi Ya Matangazo

December 02, 2015

Mwenyekiti wa kamati ya amani mkoa wa Arusha(APET) Petro Ahham akimkabidhi kikombe cha ushindi  wa bonanza la amani na utalii mkoa wa Arusha,nahodha wa timu ya Kitambi Noma, James Lugangira

Wanamichezo wa kitambinoma wakiwa wanashabikia ushindi mara baada ya kukabidhiwa kombe katika kiwanja cha General Tyre jijini Arusha

 Washindi wakiwa na kuku wao. KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Na Woinde Shizza,Arusha

Klabu ya Kitambi noma ya jijini Arusha, juzi ilitwaa ubingwa wa soka katika tamasha la kwanza la amani na utalii ambalo lilifanyika viwanja vya General Tyre jijini Arusha.



Timu hiyo ilitwaa ubingwa baada ya kuzishinda timu za Wazee Klabu na chuo cha Uandishi wa habari Arusha(AJTC) kwa kukusanya alama nyingi  kutokana na mashindano yaliyoendeshwa kwa mfumo wa Ligi.



Katika tamasha hilo, liliandaliwa na taasisi ya Arusha media jumla ya timu sita zilishiriki katika michezo mbali mbali na sambamba na kutolewa burudani ya  ngoma za asili kutoka kikundi cha Cultural Arts Center cha chuo kikuu cha Makumira



Hata hivyo kwa upande wa mpira wa pete, timu ya Wazee Qeen ilifanikiwa kutwaa ubingwa baada ya kuichapa katika mchezo wa fainali timu ya AJTC Qeen magoli 34-7.



Katika mchezo wa kukimbiza kuku, timu ya Kitambi noma ilishinda dhidi ya Wazee Klabu na kwa upande wa wasichana AJTC ilishinda dhidi ya Wazee Qeen.



Akikabidhi zawadi za washindi , Mwenyekiti wa kamati ya amani mkoa wa Arusha, Petro Ahham alipongeza timu zote zilizoshiriki kutokana kudumisha amani kwa vitendo.



"tamasha hili limekuja wakati muafaka kwani Arusha ni jiji la kitalii ambalo linahitaji amani wakati wote hivyo kufanya michezo kuhimiza amani na utalii ni jambo jema sana"alisema



Awali Katibu wa chama cha soka wilaya ya Arusha,Zakhayo Mjema alipongeza taasisi ya Arusha Media kwa kuandaa tamasha hilo la amani na utalii katika jiji la Arusha.



"matamasha kama haya yalipaswa kufanywa na chama cha soka lakini tumekwama hivyo, tunapongeza Arusha Media kwa kusaidia kuendeleza michezo katika jiji la Arusha"alisema.



Tamasha hilo, lilidhaminiwa na Shirika la hifadhi za taifa(TANAPA),kampuni ya vinywaji ya Cocacola, kampuni ya Sunny Safaris, kampuni ya Big Expedition na kampuni ya Marera Lodge &tours.
Posted by MROKI On Wednesday, December 02, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo