Nafasi Ya Matangazo

August 18, 2014

Mkurugenzi wa Kampuni ya S & D Collection, Devota Kijogoo Mtambo akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo wakati akitangaza udhamini wake katika Shindano la Miss Tanzania 2014. Pamoja nae ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Lino International Agency, Hashim Lundenga ambao ndio waandaaji wa shindano la Miss Tanzania.
 Mkurugenzi wa Kampuni ya Lino International Agency, Hashim Lundenga ambao ndio waandaaji wa shindano la Miss Tanzania akifafanua jambo juu ya udhamini huo wa S & D Collection.Kulia ni  Mkurugenzi wa Kampuni ya S & D Collection, Devota Kijogoo Mtamb. 
Mkurugenzi wa Kampuni ya S & D Collection, Devota Kijogoo Mtambo akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo wakati akitangaza udhamini wake katika Shindano la Miss Tanzania 2014. 

Kijogoo amesema kuwa kampuni yake imeamua kuingia katika udhamini  wa mashindano hayo makubwa ya urembo nchini kwa lengo la kujitangaza, kutangaza biahara ya mavazi ambapo bidhaa zao zinatoka nchi za Marekani, Uturuki, Ghana na Ethiopia.

Aidha amesema kuwa kampuni ya S & D Collection itatoa mavazi ya aina mbalimbali kwa washiriki wa Miss Tanzania ambapo ni kuanzia mavazi ya kwaajili ya show ya ufunguzi, Mavazi ya ubunifu, kwaajili ya washiriki kujitambulisha, mavazi ya ufukweni, pamoja na vazi la kutokea jioni.

Kijogoo amesema kampuni yake pia itatoa mavazi ya jioni mrembo atakaeshinda taji la Miss Tanzania 2014.

Kampuni hiyo iliyo na duka lake Shoppers Plaza Mikocheni gorofa ya pili imeungana na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia kinywaji chake cha Redd's na Marie Stop Tanzania katika udhamini huo.  
Posted by MROKI On Monday, August 18, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo