Nafasi Ya Matangazo

August 07, 2026


Na Neema Chalila Mbuja
WIZARA ya Maliasili na Utalii imevunja rekodi ya kupokea  wageni zaidi ya 17,000  kwa siku kwenye  Maonesho ya mwaka huu ya Wakulima, Wafugaji  na Wavuvi maarufu  lama NANE NANE yanayoendelea kitaifa kwenye Viwanja vya John Malecela, Nzuguni Jijini Dodoma.

Makundi makubwa ya wananchi, wanafunzi na wadau mbalimbali wa uhifadhi na wanyamapori wamefurika kwenye banda l Wizara ya Maliasili na Utalii kwa ajili ya kuona wanyama aina mbalimbali waliopo kwenye bustani ya wanyamapori kwa lengo la kutangaza utalii wa ndani. 

Idadi hiyo inafanya banda la Wizara ya Maliasili na Utalii kuvunja  rekodi ya kutembelewa na wananchi wengi ambapo Bi. Amina Saleh  mmoja wa wananchi waliotembelea bustani ya wanyama anasema wamefurahishwa sana na ujio wa wanyamapori hao kwani hajawahi kuwaona wanyama ana kwa ana zaidi ya kwenye picha.

Tembo Mary aliyekuwa kwenye bustani hiyo ya Maonesho ya wanyamapori amekuwa kivutio kwa wanafunzi wengi na wananchi kwa ujumla kutokana na historia yake na usikivu alionao ambapo mwanafunzi Collins Msemwa wa Kato Victoria Academy anasema kuwa ziara hiyo ya shule imehamasisha wanafunzi wengi kupenda wanyamapori na kujifunza kwa kina tabia za wanyamapori hao.

Mamlaka ya Usimamizi wa  Wanyamapori Tanzania (TAWA) ambayo ndiyo msimamizi wa wanyamapori imefanikiwa kuleta wanyama Kama  Tembo, Simba, Nyumbu, Pofu, Ngiri maarufu Kama Kasongoyeye, Duma, Chatu, ndege Karani, Mbuni, ndege Korongo (Crane) ambaye ni alama ya nchi ya Uganda, na ndege Mwali (White Perican bird) mbalimbali waliopo kwenye bustani ya NANE NANE.






Posted by MROKI On Friday, August 07, 2026 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo