Nafasi Ya Matangazo

June 09, 2014

Mwenyekiti wa wabunge wa Tanzania katika bunge la Afrika Mashariki(EALA) Mh. Adam Kimbisa akitoa tamko la wabunge wa Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki kwa waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu sakata la kumvua madaraka spika wa bunge hilo wakati wa Mkutano uliofanyika katikamukumbi wa Idara ya Habari(MAELEZO).Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari(MAELEZO) Bw. Assah Mwambene.
 Katibu wa wabunge wa Tanzania katika bunge la Afrika Mashariki(EALA) Mh. Shy-rose Bhanji akieleza kwa waandishi wa habari juu ya uamuzi wake wa kutoiunga mkono hoja kwa kutoa sahihi zao kama inavyoelezwa katika kanuni ya 9(2) ya kanuni na utaratibu wa uendeshaji wa bunge.Kulia ni Mbunge wa Bunge hilo Mh. Twaha Taslima
 Mbunge wa Tanzania katika bunge la Afrika Mashariki(EALA) Mh. Twaha Taslima akieleza jambo kwa waandishi wa Habari(Hawapo pichani)wakati wa Mkutano uliofanyika katikamukumbi wa Idara ya Habari(MAELEZO). Kushoto ni Katibu wa wabunge wa Tanzania katika bunge hilo Mh. Shy-rose Bhanji.Picha na Hassan Silayo-MAELEZO.
********
BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI KANDA YA TANZANIA (EALA-TZ)
______________________________________________

TAMKO LA PAMOJA LA WABUNGE WA TANZANIA WANAOWAKILISHA BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI (EALA) JUU YA SAKATA LA KUTAKA KUMVUA MADARAKA SPIKA WA BUNGE HILO 0/06/2014

Sisi, Wabunge saba wa Bunge la Afrika Mashariki kutoka Tanzania (EALA-TZ), tunapenda kusisitiza msimamo wetu wa kutounga mkono jaribio la kutaka kumuondoa madarakani Spika wa EALA, Mh. Margaret Nantongo Zziwa.

Baada ya kutafakari kwa uangalifu na kwa umakini mkubwa kuhusu chanzo halisi cha hoja yenyewe ya kutaka kumuondoa Spika wa EALA madarakani, tuligundua mambo yafuatavyo:
1. Hoja hii haina maslahi ya Tanzania na iko kinyume na malengo ya ushirikiano ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC). Tumebaini kuwa hoja yenyewe ni sehemu ya "mchezo mchafu" wa ajenda ya siri ya kujaribu kuweka mbele maslahi ya baadhi ya wanachama wachache wa jumuiya badala ya kuzingatia maslahi mapana ya EAC.

2. Tuhuma mbalimbali zilizotajwa dhidi ya Spika wa EALA kuhusu yeye kuonesha upendeleaji, ujeuri na mapungufu mengine ya uongozi zimegundulika kuwa hazina mashiko na wala mantiki .

3. Kitendo ambacho kimetushtua ni kuwa kumekuwa na majaribio kadhaa ya baadhi ya Wabunge wa EALA kutoka nje ya Tanzania na viongozi wa Sekretarieti ya EAC kutaka kulazimisha sahihi za baadhi ya Wabunge wa Tanzania zitumike kinyume na utaratibu kuunga mkongo Azimio tajwa (kitu ambacho tunakipinga kwa nguvu zote). Hii inadhihirisha kuwepo kwa ajenda ya siri katika sakata hilo dhidi ya maslahi ya Tanzania na jumuiya kwa ujumla.

4. Kufuatia malumbano yaliyoibuka katika kikao cha Bunge cha mwezi Machi huko Arusha, sisi Wabunge wa Tanzania tulipokea maoni na masikitiko mengi kutoka kwa wana Afrika Mashariki na viongozi kwa ujumla wakitusihi kumaliza tatizo hili kwa njia ya amani na utulivu, lakini jitihada zetu ziligonga ukuta. Hatua hii ilizidi kutudhihirisha kuwepo kwa ajenda ya siri.
Posted by MROKI On Monday, June 09, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo