Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Luteni Mstaafu Mheshimiwa Chiku Gallawa
atakuwa mgeni rasmi katika shindano la kumsaka mrembo wa mkoa huo, Nice
& Lovely Miss Tanga 2014 siku ya jumamosi tarehe 21/06/2014,
shindano ambalo litafanyika Mkonge Hotel.
Mkurugenzi wa kampuni ya Mac D Promotions ambao ndio
waandaaji wa shindano hilo, Irene Rweyunga amesema kuwa, Mkuu wa Mkoa
wa Tanga amekubali kuwa mgeni rasmi, napia amepongeza maandalizi makubwa
yaliyofanyika katika kuliandaa shindano hilo ambalo limekuwa gumzo
katika jiji la Tanga.
"Tumedhamiria kulifanya shindano hili kuwa na
msisimko wa kipekee, na maandalizi yote yamekamilika kwa asilimia mia
moja nasasa tunasubiria siku ifike ili kumpata mshindi, alisema Irene.
Warembo wote 13 hivi sasa wapo kambini katika Hoteli ya
Tanga Beach Resort chini ya mwalimu wao Mariam Bandawe na wanaendelea
vizuri na mazoezi yao. Mshindi wa kwanza wa shindano hilo atazawadiwa
zawadi ya gari dogo aina ya Toyota Vitz ambalo tayari limeshapelekwa
mkoani Tanga karibu wiki tatu sasa.
Shindano hilo ambalo liedhaminiwa na Nice &
Lovely, EATV, Tanga Beach Resort, Breeze Fm, CXC Africa, Rweyunga Blog
na Mwambao Fm, burudani kabambe itaporomoshwa na Malkia wa mipasho
Afrika Mashariki, Bi Khadija Omary Kopa.
0 comments:
Post a Comment