Nafasi Ya Matangazo

March 13, 2014

 Baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba wakimpongeza Makamu Mwenyekiti wa Bunge hilo, Samia Suluhu Hassan baada ya kuibuka mshindi dhidi ya mpinzani wake Amina Abdallah Amour. Samia ni Waziri wa Muungano katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Samia Suluhu  Hassan ameshinda kwa - 390  sawa na asilimia 74.6 na mpinzani wake  Amina Abdalla Amour - alipata kura 126 sawa na asilimia 24 huku kura zilizoharibika ni  7 swa na asilimia 1.3.

Kwa Muji wa taarifa ya Mwenyekiti wa Muda wa Bunge la Katiba, Pandu Amir Kificho, Viongozi hao wataapishwa Machi 14 2014 saa 10:00 jioni baada ya kuapishwa kwa Makatibu wa Bunge hilo saa nne asubuhi na Rais Jakaya  Kikwete.
Sehemu ya wajumbe wanawake wa Bunge Maalum la Katiba wakishangilia wakati wa kumpongeza Mgombea wao Mshindi wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Samia Suluhu Hassan.
Posted by MROKI On Thursday, March 13, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo