Nafasi Ya Matangazo

March 08, 2014



Huyu ndiye Mama Mkubwa wa Mtoto Adolotea Nyavike bi. Salome Kiegu(35) ambaye ametoweka na mtoto huyo kusiko julikana huku wasamalia wema wakitaka kutoa misaada.
 ******
 Katika hali ya Kutatanisha na kushangaza mama mkubwa wa Mtoto aliye ungua kwa Moto na kusababisha Shingo yake kuungana na mwili ametoweka na mtoto huyo huku wasamalia wema waliokuwa wakiendelea kutoa michango yao kwa ajili ya kumsaidia akatibiwe wanaendelea kufanya hivyo.

Mama huyo alitoweka mapema alfajili jana huku asiseme ni sehemu gani alikuwa amekwenda bila hata kuaga kwa mtu yeyote yule, Kutokana na swala hili Tulikuwa tunaomba wale watu wote wanao endelea kumchangia mtoto huyo na wanaopanga kumchangia kupitia namba hii ya mama huyo  0752 986879 wasitishe kufanya hivyo, na mpaka sasa namba yake haipatikani na taratibu za kumsaka zinaendelea.
Tutaendelea kuwafahamisha..
MTOTO Adolotea Njavike(1.4) ambae Kichwa na Kiwiliwili vimeungana baada ya kupata na ajali ya Moto akiwa na mama yake Mzazi.

Na mbeya yetu
Posted by MROKI On Saturday, March 08, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo