Nafasi Ya Matangazo

December 09, 2012

Amiri Jeshi mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania,Mh. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili katika Uwanja wa Uhuri akiwa kwenye gari maalum la Kijeshi na Sambamba na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama,Jenerali Davis Mwamunyange walipokuwa wakioa salamu kwa wananchi na wageni mbali mbali waliofika Uwanjani hapo kwa ajili ya maadhimisho ya miaka 51 Uhuru wa Tanzania Bara.Kauli Mbiu ya Maadhimisho ya Mwaka huu ni “Uwajibikaji, Uadilifu na Uzalendo ni nguzo ya Maendeleo ya Taifa letu”.
 
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mh. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride la vikosi vya Ulinzi na usalaama katika maadhimisho Miaka 51 ya Uhuru wa Tanzania Bara,leo katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam.
Kikosi cha Brass Band cha majeshi ya Ulinzi na usalama kikitumbuiza katika maadhimisho hayo.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mh. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na viongozi wengine wa Serikali wakipokea salamu za heshima kutoka kwa Vikosi mbali mbali vya Ulinzi la Usalama wakati wa maadhimisho ya miaka 51 ya uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika leo kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.
Viongozi mbalimbali wakiwa katika maadhimisha hayo,kutoka kulia ni Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo,Mh. Joseph Kabila,Mama Maria Nyerere, Rais wa Msumbiji,Mh. Armando Guebuza,Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania,Dkt. Mohamed Gharib Bilal na Rais Mstaafu wa awamu ya pili,Mzee Ali Hassan Mwinyi.
Makamu wa Rais Dkt.Mohamed Gharib Bilal akisalimiana na Mama Fatma Karume mara baada ya kuwasili uwanjani hapo.katikati ni Waziri Mkuu,Mh. Mizengo Pinda.
Vijana wa chipukizi wakionyesha michezo na ujumbe mbalimbali wakati wa maadhimisho hayo.
Kikosi cha wanaanga cha Jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ) kikitoa salamu za heshima kwa Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jakmhuri ya Muungano ya Tanzania,Mh. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.
Kikosi cha ardhini Jeshi la wananchi la Tanzania (JWTZ) kikitoa salamu za heshima kwa Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jakmhuri ya Muungano ya Tanzania,Mh. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.
Vikosi vya Ulinzi na Usalama vikiwa vimejipanga tayari kwa gwaride la utii na heshima mbele ya Amiri jeshi Mkuu na Rais Jamhuri ya muungano ya Tanzania,Mh. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.Picha kwa hisani kubwa ya Full Shangwe Blog.
Posted by MROKI On Sunday, December 09, 2012 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo