Nafasi Ya Matangazo

March 02, 2012

 Hii  ni  nguzo  ya  tatu nayo  ipo  katikati  ya  barabara  hivyo  magari  yanapata  shida  kupita
Hii  ndio  nguzo  iliyowekwa  katikati  ya  barabara   mita  100  baada  ya nguzo  ya  kwanza  niliyoonesha
 Nguzo  ambayo  imefuata  mpaka  wa  barabara  na  ipo  sahihi

Kwako  Meneja  wa Tanesco  Kisarawe

Jamani  mwaka  jana  mwezi  wa  kumi  na  moja  nilitoa  pongezi   kwa viongozi  wa Tanesco  kisarawe  kwa   kufanya  juhudi  ya kuweka  nguzo za  umeme   maeneo  ya Pugu  kinyamwezi  na  viunga  vyake. 
Lakini shughuli  hiyo  imeishia  kwa  kuweka  nguzo  tu  na  kuziacha  kama zilivyo.  na mwaka  huu  mwezi  wa  pili  wamerudi  na  kuanza kubadilisha  nguzo  na  kuziweka barabarani  kwa  shinikizo   la  wenye pesa  ili  maeneo  yao  yawe  makubwa  wakati mawe  ya  mipaka   ya barabara  yanajulikana.  

Angalia nguzo  ya  kwanza  ilipo  , ya  pili na ya  tatu  utajionea   mwenyewe.  yaani  hata  mtoto   wa  chekecheaanauliza  mbona nguzo   ipo   barabarani.  pamoja  na  hayo  bado suala  la umeme  ni  kitendawili    kwa wakati  hawa  wa  kinyamwezi  na viwege.   Naomba  wahusika   wawe  makini wasipende  kurubuniwa  na bahasha  au  kusikiliza   maneno  ya  viongozi  uchwara.Naomba  mnipe  mawazo  itabidi  na  sisi  tufungue  kesi  kama Nyaronyo  ichere  anavyowaburuza  kwenye  mita  za luku  ambazo walichukua  two years.


Regards


XAVERY   LANGA  KAPECHA  NJOVU
0783  662681
MKAZI  WA  PUGU KINYAMWEZI  DAR ES  SALAAM
Posted by MROKI On Friday, March 02, 2012 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo