March 29, 2024
March 28, 2024
BALOZI wa Misri nchini Tanzania, Sherif Abdelhamid amevutiwa na miradi itayojengwa kwa ubia wa kati ya sekta binafsi na umma (PPP) itakayokuwa chini ya Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS), imeelezwa.
March 27, 2024
Juma la wadau wa Elimu Mkoa wa Dodoma limetamatika Kwa viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Dodoma kuzungumza na kushiriki Chakula Cha Mchana na wanafunzi wa Shule za kidato Cha Sita za Mkoa huo.
MBUNGE MAVUNDE AANZA UJENZI WA KIWANJA CHA MICHEZO SHULE YA SEKONDARI KIWANJA CHA NDEGE DODOMA JIJI.
Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mh. Anthony Mavunde ameanza ujenzi wa viwanja vya michezo ya mpira wa kikapu(_basketball_),mpira wa pete(_netball_) na mpira wa wavu(_volleyball_) katika eneo la shule ya Sekondar Kiwanja cha Ndege Jijini Dodoma.
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amekagua mradi wa ujenzi wa Kituo cha Kupoza umeme cha Uhuru kilichopo wilayani Urambo mkoani Tabora na kueleza kutoridhishwa kwake na kazi ya ujenzi wa laini ya msongo wa kV 132 kutoka Tabora hadi Urambo ambayo inatekelezwa na kampuni tanzu ya TANESCO (ETDCO).
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Patrobas Katambi akizungumza na viongozi wa Mkoa wa Kilimanjaro na Kamati ya Mkoa wakati akikagua maandalizi ya uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa Mwaka 2024 zitakazofanyika katika Uwanja wa michezo wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), Mkoani Kilimanjaro.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Patrobas Katambi akikagua baadhi ya maeneo alipotembelea Uwanja wa michezo wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), ambapo uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa Mwaka 2024 zitakazofanyika Mkoani Kilimanjaro.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Patrobas Katambi (katikati) akifuatilia vijana wa halaiki wakati akikagua maandalizi ya uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa Mwaka 2024 zitakazofanyika katika Uwanja wa michezo wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), Mkoani Kilimanjaro. Wa tatu kutoka kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Fatma Rajab.
Vijana wa Halaiki wakiwa katika mazoezi kwenye uwanja wa shule ya msingi Mwereni, uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa Mwaka 2024 zitakazofanyika katika Uwanja wa michezo wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), Mkoani Kilimanjaro.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Patrobas Katambi ameeleza hadi sasa maandalizi ya uzinduzi wa mbio za mwenge wa uhuru yamefikia zaidi ya asilimia 90 huku akihimiza Mkoa wa Kilimanjaro kuhakikisha unahamasisha wananchi kushiriki kwa wingi katika tukio hilo la kihistoria.
Amesema hayo wakati akikagua maandalizi ya uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru katika uwanja wa michezo wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), Mkoani Kilimanjaro.
Aidha, Naibu Waziri Katambi amesema kuwa Mbio hizo za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka huu 2024 zinaadhimisha miaka 60 tangu kuanzishwa rasmi mwaka 1964 zikienda sanjari na Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na Miaka 60 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Vile vile, Mhe. Katambi ameupongeza mkoa huo kwa utayari na maandalizi mazuri ya tukio hilo la kitaifa na kuongeza kuwa mwenge huo ni alama ya umoja, hivyo utakimbizwa katika halmashuri 195 kwa lengo la kuunganisha wananchi sambamba na kukagua viwango vya utekelezaji wa miradi ya serikali katika kuwahudumia wananchi.
Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Fatma Rajab amesema kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Wizara hiyo wamekua wakishirikiana kwa karibu na ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo wa Kilimanjaro katika kuhakikisha maandalizi yanakamilika ndani ya muda uliopangwa.
Kwa upande wake, Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Kilimanjaro, Mhandisi Jackson Masaka amesema kuwa viongozi wa mkoa wamekua na utaratibu wa kukutana na makundi mbalimbali ya wananchi ikiwemo Bodaboda, Wazee, Wafanyabiashara, Wanawake kwa lengo la kuwahamasisha kujitokeza kwa wingi katika uzinduzi huo.
Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa kwa mwaka 2024 zinaogozwa na kauli mbiu isemayo “Tunza Mazingira na Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Ujenzi wa Taifa Endelevu”.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Akiba Commercial Bank (ACB) ametoa salaamu kwa Waislamu wote nchini na wateja wa benki hiyo popote walipo katika hafla ya Futari iliyoandaliwa kwa Wateja, Wafanyakazi pamoja na Wadau mbalimbali wa benki hiyo katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhan.
Akizungumza Katika hafla hiyo iliyofanyika Machi 25, 2024 katika Hoteli ya Serena Bw. Silvest Arumasi ametumia fursa hiyo kuwapongeza Waislamu wote kwa mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhan, na amewashukuru wadau wote kwa kutenga muda wao na kujumuika pamoja katika Futari hiyo kwani kwa kitendo hicho kimeleta faraja na heshima kubwa sana.
Aidha, alisema kuwa, ACB imekuwa na utamaduni wa kufanya hafla ya kufuturisha kwa kila mwaka kwa ajili ya kuunga mkono ndugu zetu Waislam katika funga yao na pia ni njia nzuri ya kuboresha mahusiano ya benki na wateja wake.
Akiba Commercial Bank inatambua na kuheshimu sana Imani za wateja, Wafanyakazi na wadau wake na kuupa umuhimu wa kipekee mwezi Mtukufu wa Ramadhan.
Bw. Silvest Arumasi amesema kuwa ACB inaendelea kuboresha na kupanua wigo wa huduma zake ili kuendana na soko kwa lengo ya kukidhi matarajio ya wateja, amewaomba wateja na umma kwa ujumla kuendelea kuiamini Benki hiyo ambayo imeweza kuwahudumia Watanzania wengi na kuleta maendeleo makubwa kwa wajasiriamali na Jamii nzima kwa ujumla.
Akiba Commercial Bank Benki kwa maendeleo yako
March 26, 2024
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amezindua Kiwanda cha kuwekea mifumo ya kupasha na kutunza joto katika mabomba yatakayosafirisha mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani Tanga nchini Tanzania kupitia Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP).
MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi akijumuika na Wananchi wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja katika kuitikia dua ikisomwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh.Saleh Omar Kabi (hayupo pichani ) baada ya kumalizika kwa hafla ya Iftaar Maalum iliyoandaliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Mwinyi katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Wilaya ya Mjini Unguja Jijini Zanzibar jana 25-3-2024.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza wakati wa hafla ua Iftaar maalum aliyowaandalia Wananchi wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, iliyofanyika katika ukumbi wa Sheikh.Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Wilaya ya Mjini Unguja Jijini Zanzibar jana 25-3-2024.
WANANCHI wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja wakijumuika na Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi katika Iftaar maalum iliyoandaliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi , katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakal Kikwajuni Wilaya ya Mjini Unguja jana 25-3-2024.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akimkaribisha Tende Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh.Saleh Omar Kabi, wakati wa hafla ya Iftaar maalum kwa Wananchi wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja iliyofanyika katika ukumbi wa Sheikh.Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Wilaya ya Mjini Unguja jana 25-3-2024.
WANANCHI wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja wakijumuika na Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi katika Iftaar maalum iliyoandaliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi , katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakal Kikwajuni Wilaya ya Mjini Unguja jana 25-3-2024.
WANANCHI wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja wakijumuika na Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi katika Iftaar maalum iliyoandaliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi , katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakal Kikwajuni Wilaya ya Mjini Unguja jana 25-3-2024.