Nafasi Ya Matangazo

February 25, 2026

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imetoa Tuzo za ubunifu kwa washindi 9 waliotoa mawazo bora zaidi yatakayosaidia kuendelea kuboresha huduma za kodi na kuongeza wigo wa kodi. 

Akikabidhi tuzo hizo, vyeti pamoja na hundi kwa washindi hao Februari 25.2026, Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar ameipongeza TRA kwa kuja na Tuzo hizo ambazo zitaongeza ukaribu na ushirikishwaji wa wananchi katika masuala ya ukusanyaji wa kodi. 

Mshindi wa jumla katika tuzo hizo ni Gabriel Mashenene ambaye amepatiwa hundi ya Sh. Milioni 50, washindi watatu wamepatiwa Sh. Milioni 30 kila mmoja huku washindi 5 wakipatiwa Sh. Milioni 20  kwa kila mmoja.










Posted by MROKI On Wednesday, February 25, 2026 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo