Nafasi Ya Matangazo

January 20, 2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amepokea kwa masikitiko makubwa, taarifa za kifo cha Mzee Edwin Isaac Mbiliewi Mtei, kilichotokea usiku wa tarehe 19 Januari, 2026, jijini Arusha.
 
"Kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwa niaba yangu binafsi, natuma salamu za rambirambi kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki, na wote walioguswa na msiba huu," alisema Rais Dkt. Samia.
 
Rais Dkt. Samia alimkumbuka Marehemu Mtei kama mmoja wa watumishi na viongozi wenye mchango mkubwa katika ujenzi wa Taifa kwenye eneo la fedha, mipango na uchumi, aliyehudumu katika nafasi mbalimbali ikiwemo Gavana wa kwanza wa Benki Kuu ya Tanzania (1966 - 1974), na kushiriki kuimarisha misingi ya uendeshaji wa Benki Kuu na uthabiti wa mfumo wa fedha nchini.
 
Aidha, Rais Dkt. Samia alisema Mzee Mtei ataenziwa katika historia ya siasa za vyama vingi kama miongoni mwa waasisi wa demokrasia ya ushindani wa vyama, akitajwa kuwa ni miongoni mwa waanzilishi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
 
Aliongeza kuwa, mchango wa Marehemu utaendelea kukumbukwa na kuenziwa na vizazi vya sasa na vijavyo, hususan kupitia maandiko yake binafsi (autobigraphy) yanayoeleza safari yake ya maisha na utumishi wake wa uongozi katika kuijenga Tanzania.
 
Rais Dkt. Samia anawaombea faraja, nguvu na amani; familia, ndugu na wafiwa wote, na kumuomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali pema peponi, Amina.
Posted by MROKI On Tuesday, January 20, 2026 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo