Nafasi Ya Matangazo

June 19, 2025






Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Ridhiwani Jakaya Kikwete amefungua 
Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama Cha Waajiri (ATE) mjini Dar Es Salaam.

Mkutano huo ulifunguliwa Juni 18,2025 ambao ulitanguliwa na taarifa za kiutendaji za mwaka na kongamano kujadili mabadiliko ya sheria za kazi na athari yake kwa Waajiri na Waajiriwa katika kuleta Tija. 

Waziri Kikwete alipata nafasi ya kushiriki na kusikia mafanikio na changamoto zilizomaliza na haswa hali ilivyokuwa kabla na baada ya mabadiliko ya sheria. 

Aidha, alitumia mkutano huo kueleza  nafasi ya serikali katika utatu wa mashirikiano baina ya wadau wakuu watatu wa Kazi ambapo katika hotuba yake ameeleza nia ya mabadiliko hayo na kuwashukuru sana ATE kwa ushiriki wao katika kuhakikisha tunakuwa na sheria nzuri za kazi na kusimamia utekelezaji wa mikataba mbalimbali ya Kimataifa ya Wafanyakazi ambayo Tanzania ni Mwanachama wa Mikataba hiyo.

Pia nilitumia nafasi hiyo kuwashukuru sana wadau wetu wa maendeleo shirika la Kazi Duniani (ILO) kwa kuendelea kushirikiana nasi na pia kuwapa salamu za hongera toka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa ILO Cde. Gilbert F. Houngbo.
Posted by MROKI On Thursday, June 19, 2025 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo