Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja akijibu maswali ya wabunge Bungeni Novemba 2,2022 wakati wa kikao cha pili cha mkutano wa tisa wa Bunge unaoendelea jijini Dodoma.
Serikali imesema
haioni haja ya kupunguza eneo la hifadhi ya msitu wa Mbiwe ili litumike kwa
matumizi ya Wananchi na shughuli za Kiuchumi.
Hayo
yamesemwa leo Bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,
Mhe. Mary Masanja (Mb) , alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Lupa,
Mhe. Masache Njelu aliyetaka kujua endapo Serikali inaona haja ya kupunguza
eneo la hifadhi ya msitu huo kwa wananchi.
“Lengo la
kuanzishwa hifadhi hiyo ni kulinda bioanuai zilizomo ndani ya hifadhi ikiwemo;
vyanzo vya maji vinavyotumika kwa matumizi ya binadamu na wanyamapori,”alisema
Naibu Waziri Masanja.
Aidha Masanja
amesema, Sheria ya misitu inaruhusu uchimbaji wa madini ndani ya hifadhi kwa
kuzingatia kanuni na taratibu zilizopo kwa njia endelevu.
Hifadhi ya
Msitu wa Mbiwe ipo Halmashauri ya Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya.
0 comments:
Post a Comment