Nafasi Ya Matangazo

July 23, 2019




Na mwandishi wetu,Arusha
 Taasisi za Chemchem Association imepanga kutumia  zaidi ya sh 100 milioni mwaka  mwaka 2019 kuchangia miradi ya Maendeleo katika eneo la Jumuiya ya  hifadhi ya jamii ya Wanyamapori( JUHIBU) .

JUHIBU, ilianzishwa mwaka 2003  inaundwa na vijiji vya Sangawe, Mwada,Ngoley, Vilimavitatu, Minjingu,K Olasiti,M Magala, na Maweni na ina ukubwa wa 283.

Afisa Maendeleo ya jamii ya Taasisi ya  Chemchem association,  Walter Palangyo alisema taasisi inachangia miradi hiyo kama sehemu ya wajibu wake kuchagia shughuli za Maendeleo ya jamii(SCR) mbali ya kodi na tozo nyingine zinazolipwa na Chemchem iliyowekeza shughuli za Utalii katika hifadhi hii.

Alisema  taasisi hiyo, imekamilisha  ukarabati wa majengo ya shule ya msingi vilima vitatu,ofisi mbili za walimu na sasa mradi wa ujenzi wa vyoo .

"katika shule hii, tumetumia kiasi cha sh 50 milioni, ili kuhakikisha wanafunzi katika shule hii wanapata elimu bora katika mazingira mazuri kwani tayari tumewapatia  madawati 100  kwa ili kumaliza tatizo katika shule hii"alisema

Alisema taasisi  hiyo pia imetoa kiasi cha sh 5 milioni ili kusaidia Vikoba katika baadhi ya vijiji katika eneo hilo, ikiwepo vikundi vya jamii ya wabarbeig ili kuweza kuwa na miradi ya maendeleo.

"kuna kikundi cha Wicheda na Datoga vya jamii ya kibarbeig  ambavyo tumepatia kiasi cha sh 2.5 milioni ili kukuza mitaji yao"alisema

Alisema katika jamii hiyo, pia kumeanzishwa mradi wa maboma ya asili ambayo watalii wataweza kuwatembelea .

"Mwaka huu pia tunaendelea na mradi wa kusomesha watoto katika jamii hii, katika chuo cha wanyamapori cha Mweka na chuo cha Ufundi (VETA) naa wengine tumewalipia ada za shule ya sekondari "alisema

Alisema  pia kuna miradi ya maji, michezo na afya  katika vijiji hivyo, hasa kutokana na fedha ambazo zinatokana na la ya utalii.
Posted by MROKI On Tuesday, July 23, 2019 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo