Nafasi Ya Matangazo

June 20, 2019

SHIRIKA la Maendeleo ya Mafuta Tanzania  (TPDC), limempa tuzo Waziri wa zamani wa Serikali ya Tanzania, Prof Mark Mwandosya kutokana na mchango wake mkubwa katika maendeleo ya shirika hilo.

Mwandosya amepata kuhudumu TPDC kwa nafasi ya  Kamishna wa kwanza wa Petroli  nchini na Mwenyekiti wa bodi  ya Shirika hilo.

Tuzo hiyo ilitolewa wakati shiruka hilo likiadhimisha miaka 50 tangu kuanzishwa kwake ambapo mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa Waziri Mkuu, Majaliwa Kassimu  Majaliwa,  ambaye aliwakilishwa na Waziri Ofisi ya Waziri Mkuuu- Uwekezaji Mh. Angela Jasmine  Kairuki.

TPDC  ilitumia maadhimisho hayo kutoa  TUZO kwa baadhi ya Wawstaafu waliokuwa na michango  mbalimbali  katika utumishi wao.

Pichani (juu) ni Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa TPDC, Marie Msellemuakimkabidhi tuzo Prof Mwandosya kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi wa TPDC

Posted by MROKI On Thursday, June 20, 2019 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo