Nafasi Ya Matangazo

March 12, 2019

SEHEMU ya Wanawake wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU) wakishiki maandamano katika siku ya maadhimisho ya siku ya wanawake duniani. Maandamano yalianzia Chuoni hapo na kuhitimishwa eneo la Mlimani City jijini Dar es Salaam. (Imeandaliwa na Robert Okanda) 
SEHEMU ya Wanawake wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU) wakishiki maandamano katika siku ya maadhimisho ya siku ya wanawake duniani. Maandamano yalianzia Chuoni hapo na kumalizikia eneo la Mlimani City jijini Dar es Salaam. 
BAADHI ya Wanawake wa Tawi la Chama cha wafanyakazi wa Elimu ya juu wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU) wakiwa wakipita mbele ya jukwaa wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyohitimishwa katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Sarah Msafiri na viongozi mbalimbali. 
SEHEMU ya Wanawake wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU) wakifuatilia matukio mbalimbali katika ukumbi wa Mlimani City wakati wa maadhimisho hayo jijini Dar es Salaam. 
BAADHI ya Wanawake wa Tawi la Chama cha wafanyakazi wa Elimu ya juu wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU) wakiwa wamebeba dawa na mahitaji muhimu ya kibinadamu walipowasili katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kutoa msaada kwa watoto wenye saratani jijini Dar es Salaam Machi 9 2019. 
MWENYEKITI wa Kamati ya Wanawake wa Tawi la Chama cha wafanyakazi wa Elimu ya juu wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU), Dkt. Kerbina Moyo (wa pili kushoto) na Mhazini Grace Nakoba (kushoto) wakimkabidhi Peter Massawe, Mwakilishi wa wagonjwa wanaotibiwa kwenye wodi ya watoto wenye saratani katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), sehemu ya msaada wa dawa na mahitaji muhimu ya kibinadamu jijini Dar es Salaam Machi 9 2019. Pamoja nao (wa pili kulia) ni Kaimu Msimamizi mkuu wa Wodi hiyo, Ephraim Kiswaga.




Posted by MROKI On Tuesday, March 12, 2019 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo