Nafasi Ya Matangazo

December 18, 2018


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) Mhe. Benjamin William Mkapa (Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu) kufuatia kifo cha Makamu Mkuu wa chuo hicho Prof. Egid Beatus Mubofu kilichotokea leo tarehe 18 Desemba, 2018 huko Pretoria, Afrika Kusini.

Prof. Mubofu alipelekwa Jijini Pretoria kwa matibabu zaidi akitokea Taasisi ya Tiba ya Mifupa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MOI) alikokuwa akipatiwa matibabu ya kiharusi.

Mhe. Rais Magufuli amemuomba Mhe. Mkapa kufikisha salamu zake za pole kwa familia ya Marehemu Prof. Mubofu, Wahadhiri na wafanyakazi wa UDOM, Wanafunzi wote wa UDOM, Jumuiya na taasisi zote ambazo Prof.

Mubofu alifanya kazi na wote walioguswa na msiba huu. “Nimesikitishwa sana na kifo cha Prof. Mubofu, nitamkumbuka kwa uchapakazi wake, ubunifu, uadilifu na uaminifu mkubwa aliouonesha katika utumishi wake kwa Taifa ikiwemo kazi nzuri aliyoifanya katika Shirika la Viwango la Taifa (TBS) akiwa Mkurugenzi Mkuu, kabla ya kuteuliwa kuwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha UDOM” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli ameiombea familia ya Marehemu Prof. Mubofu kuwa na moyo wa subira na uvumilivu na amemuombea kwa Mwenyezi Mungu aipumzishe roho yake mahali pema peponi, Amina.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
18 Desemba, 2018

Posted by MROKI On Tuesday, December 18, 2018 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo