Nafasi Ya Matangazo

March 17, 2018


Mkuu wa Idara ya Utalii,Mhifadhi Theodora Aloyce akitoa maelezo kwa Maafisa Habari,Mawasiliano na Uhusino Serikalini walipotembelea Hifadhi ya Taifa ya Tarangire iliyopo mkoani Manyara kwa lengo la kutangaza Utalii wa ndani.
Lango Kuu la Kuingia Hifadhi ya Taifa ya Tarangire iliyopo mkoani Manyara .
Baadhi ya Maafisa Habari,Mawasiliano na Uhusiano Serikalini wakiwa katika gari wakati wa kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Tarangire kujionea vivutio mbalimbali vilivyoko katika Hifadhi hiyo wakiwemo Wanyama mbalimbali.
Miti Mikubwa ya Mibuyu ni sehemu ya Vivutio vilivyoko katika Hifadhi ya Taifa ya Tarangire.
Digi Digi ni mmoja kati ya Wanyama wanaopatikana katika Hifadhi ya Taifa ya Tarangire ambaye Maafisa Habari wa Taasisi za Serikali walipata fursa kumuona.
Mnyama Simba akiwa katika muinuko ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Tarangire ili kumrahisishia kuweza kuona maeneo ya mbali.
Twiga ni miongoni mwa wanyama ambao pia walionekana kwa uzuri zaidi katika Hifadhi ya Taifa ya Tarangire.
Baadhi ya Maafisa Habari wa Taasisi za Serikali wakifurahia ziara ya kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Tarangire ikiwa ni pamoja Stori walizokuwa wakipatiwa na waongoza watalii .
Kundi la Swala wakipata malisho ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Tarangire.
Tumbili ni miongoni mwa wanyama walioko katika Hifadhi ya Tarangire.
Maafisa Habari wa Taasisi mbalimbali za Serikali wakichukua Taswira katika eneo la Picnic ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Tarangire.
Makundi Makubwa ya Tembo ni kivutio kikubwa zaidi katika Hifadhi ya Taifa ya Tarangire.
Baada ya Ziara ya kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Tarangire iliyopo mkoani Manyara ,Maafisa Habari wa Taasisi za Serikali wakachukua Taswira  na Mkuu wa Idara ya Utalii katia Hifadhi ya Taifa ya Tarangire Theodora Aloyce.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazini.
Posted by MROKI On Saturday, March 17, 2018 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo