Nafasi Ya Matangazo

August 14, 2016

 Wakulima wakipalilia mashamba yao ya mizabibu mkoani Dodoma
 Mche wa mzabibu shambani kabla ya mavuno
“Kwa muda mrefu wakulima wa zabibu mkoani Dodoma tumekuwa tukikabiliwa na changamoto mbalimbali kiasi kwamba licha ya kufanya kazi za kilimo hususani cha mazao ya biashara tumekuwa tukiendelea kukabiliwa na tatizo la kutopata faida na kubaki katika hali duni za kutuwezesha kupata mahitaji muhimu ya kukidhi mahitaji yetu ikiwemo kujenga nyumba bora na kusomesha watoto wetu”Anasema Yarendi Makuya ,mkulima wa zabibu  kijiji cha Handala mkoani Dodoma.
 Anasema kuwa katika miaka ya karibuni kutokana na kuongezeka kwa wawekezaji katika sekta ya viwanda wakulima wa zabibu wameanza kupata ahueni ya maisha kutokana na wateja wanaowatembelea vijijini wakihitaji kununua zao  la zabibu wamekuwa wakiongezeka siku hadi siku hali inayotia matumaini kuwa kilimo cha zao hilo kina fursa ya kuchangia uchumi na kuinua maisha ya wakulima iwapo watawezeshwa ipasavyo.
Yarendi aliyekuwa akiongea kwa niaba ya wenzake alieleza kuwa hivi sasa baadhi ya makampuni yaliyowekeza kwenye viwanda  yameanza kujenga ukaribu na kushirikiana na wakulima ili yaweze kupata malighafi kwa ajili ya viwanda vyao na kuhakikisha uzalishaji wa zao hili unaongezeka.
 Moja ya kampuni aliyoitaja kuwa  hivi sasa imejikita katika kilimo shirikishi na wakulima wa zabibu na ushirikiano huo umeanza kuonyesha mafanikio ni kampuni ya Tanzania Distilleries Limited (TDL) maarufu kama Konyagi iliyopo chini ya TBL Group ambayo hivi sasa inashirikiana na wakulima kwa lengo la kuwawezesha  kuongeza uzalishaji wa zabibu kupitia mpango wa Go Farming na  wakati wa msimu inanunua zao hilo kwa bei nzuri na malipo kufanyika bila urasimu kama ilivyokuwa hapo awali walipokuwa wanauza zabibu kupitia vituo vya Ushirika na walanguzi wa mazao ambao kwa kiasi kikubwa walikuwa wakiwapunja  katika bei ya kuuzia. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.
  “Katika miaka  ya karibuni tangu tuanze kufanya kilimo kwa kushirikiana na TDL tumeanza kupata mafanikio hasa ya uwezeshwaji katika kilimo kwa kupatiwa pembejeo,mbegu,madawa ya kuua wadudu,ushauri wa kitaalamu,uhakika wa soko na kitu kingine tunachokiona kama muujiza ni kampuni kusaidia kusomesha watoto wa wakulima kupitia mfuko unaojulikana kama Zabibu Kwanza”.Alisema kwa furaha na kuongeza kuwa mtoto wake anayeitwa Paschal amewezeshwa kusoma hadi amemaliza kidato cha nne mwaka jana.
 
Mkulima mwingine Yohana Petro kutoka kijiji cha Mpunguzi alisema anachofurahia kupitia ushirikiano na kampuni hii ya TDL ni kusaidia watoto  wao kwa kuwapatia mahitaji ya elimu “Watoto wamekuwa wakisaidiwa kulipiwa ada,pia kampuni imekuwa ikitoa misaada ya vitabu,madaftari,sare za shule na kuwapunguzia makali ya maisha  wakulima wengi kwa kuwa hali zetu za maisha ni ngumu”.Alisema
Hata hivyo alisema pamoja na changamoto nyingi wanazoendelea kukabiliana nazo kukuza uzalishaji wa zao la zabibu wanajivunia kuona zabibu wanaozalisha ni bora na inatengeneza Mvinyo wa kiwango cha juu cha kimataifa. “Mara nyingi tuonapo Mvinyo uliotokana na zabibu tunazolima tunafurahi sana na kujivunia zao letu japokuwa wengi wetu hatuna uwezo wa kumudu kutumia vinywaji hivyo kutokana na kutomudu bei zake”.Alisema.
 Kwa upande wake Mtafiti wa Mazao kutoka kituo cha utafiti wa   Kilimo cha  Makutupora Viticulture Training and Research Center (MVTRC)    ,Reon Mrosso amesema kuwa  kituo hicho kinaendelea kufanya kazi na wakulima wa zao la zabibu ili kuwezesha uzalishaji  wa zao hilo kuongezeka.
 Mrosso amepongeza makampuni yanayofanya kazi na wakulima kwa kuwawezesha hususani kwa kuwapatia  mbegu na pembejeo za kilimo ikiwemo kampuni ya TDL ambayo inawezesha wakulima wengi  “Changamoto kubwa kwa wakulima wetu ni vipato duni hivyo wakipatikana wawekezaji wengi kama TDL na kuwezesha wakulima wengi uzalishaji wa zao hili utaongezeka na maisha ya wakulima kubadilika kuwa bora zaidi”.Alisema.
Alitoa wito kwa wawekezaji wenye nia ya kusaidia kuunga mkono jitihada za serikali za kukuza sekta ya kilimo wajitokeza kwa kuwa sekta ya kilimo bado inazo fursa nyingi za kukuza uchumi wa taifa na kuboresha maisha ya watanzania na kuongeza kuwa kwenye kilimo cha zabibu bado kuna fursa kubwa ya kuchangia pato la taifa na kukwamua maisha ya wakulima.
 Naye Meneja wa ubora wa Vinywaji vya Mvinyo wa kampuni  ya TDL ,Jackob Mwavika amesema katika kilimo cha zabibu mkoani Dodoma nchini bado kuna fursa kubwa ya kuzalisha zao hili kwa kuwa japo kuna ardhi ya kutosha na hali ya hewa na ardhi inaofaa kwa kilimo chake  japo uzalishaji bado ni mdogo kukidhi soko lililopo nchini.
Mwavika alisema kampuni TBL Group tayari imeanza mkakati wa kushirikiana na wakulima na wadau mbalimbali kuendeleza zao ili na tayari imeanza kutekeleza mpango wa kilimo shirikishi mkoani humo na wakulima wameanza kuchangamkia fursa hii ambapo hivi kampuni mbali na kuwapatia wakulima pembejeo,mbegu na ushauri wa kisasa wa kilimo hivi sasa iko mbioni kuingiza mbegu bora na za aina mbalimbali za zabibu kutoka nchini ya Afrika ya Kusini ili kuwawezesha wakulima kuzalisha aina zaidi ya moja za zao hili kama ilivo kwa sasa.
“Ongezeko la matumizi ya mbegu bora ni moja  kati ya vitu vinavyohitajika kuwezesha kufikia uzalishaji na kukua kwa uchumi,kupunguza umaskini na kufikia lengo la kuwa na mazao ya kutosha na kuwezesha wakulima kupata mapato mazuri ya kuwawezesha kukidhi mahitaji yao na familia zao za kupanua shughuli zao za kilimo”.Alisema Mwavika.
Alisema katika kutekeleza suala hili kampuni inaendelea kukamilisha mchakato wa kupata vibali vya kuingiza mbegu kwa mujibu wa utaratibu unaotakiwa kufuatwa na ukikamilika katika siku chache zitaletwa mbegu za aina mbalimbali zitakazowezesha kupatikana zabibu za aina mbalimbali zinatakazotumika kutengeneza mvinyo na kwa matumizi ya chakula.
Mwavika alisema zaidi ya wakulima  700 wa zao la zabibu mkoani Dodoma wananufaika na  mpango wa kilimo shirikishi unaoendeshwa na kampuni ya TDL kwa  kuwawezesha  kuongeza uzalishaji  katika mashamba yao ya zabibu. “Tumeanza kutekeleza mpango huu katika vijiji vya Bihawana, Mpunguzi, Mvumi, Hombolo, Mbabala, Veyula, Makang’wa, Mzakwe na Mbalawala na tunashirikiana na taasisi ya Makutupora Viticulture Training and Research Center (MVTRC)”,Alisema.
Alisema kuwa Chini ya mpango huo wakulima wanawezeshwa kupatiwa utaalamu wa kilimo kwa kushirikiana na taasisi ya Makutupora Viticulture Training and Research Center (MVTRC) ambapo mafanikio ya mpango huo yameanza kuleta mafanikio kwa wakulima kupatiwa elimu ya kilimo cha kisasa cha zao la zabibu na kuanza kufanya utekelezaji kwa kutumia ushauri wa wataalamu wa kilimo.
Katika kuwapatia wakulima motisha wakulima ili wajiunge na  waweze kuboresha maisha yao kupitia kilimo cha zao la zabibu chini ya mpango huu watoto wa wakulima wa  zabibu wamekuwa wakisaidiwa kielimu kupitia  mfuko unaojulikana kama Zabibu na Shule Kwanza.
Posted by MROKI On Sunday, August 14, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo