Nafasi Ya Matangazo

July 19, 2016

Mwezeshaji kutoka Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3), Magdalena Katunzi akiwasilisha mada ya uzimamizina Udhibiti wa fedha katika Mamlaka za serikali za mitaa. Mada hiyo ilitolewa kwa madiwani wa Halmashauri za Wilaya za Kyerwa na Biharamuo Mkoani Kagera leo.
Lengo kuu la mada hiyo kwa Madiwani ahao ambao halmashauri zao zimechaguiwa kuanza utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za umma ni pamoja na kumuwezesha Diwani kupata taarifa na uweewa juu ya taratibu za usimamizi na udhibitiwa fedha katika Mamlaka za Serikali za mitaa.

Aidha Katunzi alianisha mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na vyanzo vya mapato vya Mamlaka za serikali za Mitaa, ikiwa ni mapato ya ndani, ruzuku kutoka serikali kuu na Mikopo. 

Madiwani walifundishwa mbinu za kuongeza mapato ya Hamashauri ambapo walifundishwa namna ya kubuni na kuanzisha vyanzo vipya vya mapato, kuboresha viwango vya tozo, kuboresha mbinu za ukusanyaji mapato, kusimamia matumizi ya fedha za serikali ya mitaa na udhibiti wa fedha za Halmashauri. 
 Madiwani kutoka Hamashauri za Wilaya ya Kyerwa na Biharamulo wakifuatilia mada hiyo ya Usimamizi na Udhibiti wa fedha za Mamlaka ya Serikali za mitaa.
 Wakuu wa Wiaya za Kyerwa na Biharamulo mkoani Kagera, Kanali Mstaafu, Shaabn Lissu (kushoto) wa Kyerwa na Saada Malunde wa Biharamulo wakiwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo, Wende Ng'ahala (kulia) wakifuatilia mada hiyo.
Madiwani kutoka Hamashauri za Wilaya ya Kyerwa na Biharamulo wakifuatilia mada hiyo ya Usimamizi na Udhibiti wa fedha za Mamlaka ya Serikali za mitaa.BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.

 Ofisa Mipango wa Wilaya ya Biharamulo, Andambike Kyomo akifafanua jambo kuhusu namna ya ugawaji wa fedha za Halmashauri kwa makundi ya Vijana, Wanawake na matumizi mengine.
 Mratibu wa Mradi wa PS3 kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Bertha Swai akifafanua jambo kuhusu mada hiyo na maswali yaliyoulizwa na washiriki.
Madiwani kutoka Hamashauri za Wilaya ya Kyerwa na Biharamulo wakifuatilia mada hiyo ya Usimamizi na Udhibiti wa fedha za Mamlaka ya Serikali za mitaa.
 Ili kuondoa uchovu kwa washiriki kunakosababisha kusinzia wakati wa mafunzo, washiriki walifanya mazoezi kuchangamsha mwili na kuimarisha usikuvu.
Mkuu wa Wilaya ya Biharamulo, Saada Malunde (kulia) akifurahia kuonana na Mkurugenzi Mpya wa Hlamashauri ya Wilaya ya Biharamulo, Wende Israel Ng'ahala. Watendaji hao ndio walioonana kwa mara ya kwanza na wote ni wapya katika Wilaya hiyo.
Posted by MROKI On Tuesday, July 19, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo