Nafasi Ya Matangazo

April 30, 2016

Watu kadhaa wamenusurika baada ya ndege ya Shirika la Ndege la Auric Air waliyokuwa wakisafiria kupata ajali katika Uwanja wa Ndege wa Manispaa Bukoba ilipokuwa ikitua na rubani kupoteza uelekeo  kama inavyo onekana pichani.

Ndege hiyo ilikuwa ikisafiri kutoka Jijini Mwanza ,tukio limetokea majira ya saa nne asuhuhi ya leo Jumamosi April 30,2016.

Chanzo cha ajali hiyo bado hakijajulikana mpaka sasa
Posted by MROKI On Saturday, April 30, 2016 1 comment

April 29, 2016

MKUU wa Wilaya ya Newala, mkoani Mtwara, Christopher Magala akizungumza wakati wa kuhitisha mafunzo ya utekelezaji wa Mradi wa Usimamizi wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) yanayofadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Misaada la Marekani (USAID) na kutekelezwa katika Halmashauri 97 katika mikoa 13 nchini. Uzinduzi wa mradi wa PS3 ngazi ya mkloa wa Mtwara ilifanyika juzi mjini humo.

Mkoani Mtwara mradi huo utatekelezwa kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza itahusisha Halamshauri ya Nanyamba na Halmashauri ya Wilaya Masasi.

Awamu ya pili ambayo itatekelezwa mkoani mtwara kwa halamashauri saba zilizobaki utafanyika mwezi Februari na Oktoba mwaka 2017 na utahusisha Halmashauri za Mjiwa Newala, Wilayaya Newala, Mji wa Masasi, Wilaya ya Nanyumbu, Manispaa ya Mtwara, Wilaya ya Mtwara na Wilaya yaTandahimba.

 Baadhi ya Maofisa wa Mradi wa PS3 pamoja na wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya Mkoani Mtwara wakifuatilia ufungaji wa mafunzo hayo.
 Washiriki wakifuatilia mada mbalimbali katika mafunzo hayo.
 Mshauri wa Mradi katika Masuala ya Rasilimali Fedha, Dk Daniel Ngowi akizungumza wakati wa mafunzo hayo.
 Mshauri wa Mradi katika Masuala ya Elimu, Dk Rest Laswai akifafanua jambo juu ya uimarishaji mifumo ya sekta za Umma katika nyanja ya elimu.
 Washiriki akifuatilia mada katika mafunzo hayo.BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.
Posted by MROKI On Friday, April 29, 2016 No comments
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania Seattle, WA, Bwn. Mutta (kushoto) akiwa na mkewe wakiangalia majina yao huku Bi. Asha Nyang'anyi (kulia) akijaribu kuwahudumia.
Salum kutoka California akikabidhiwa beji na kabrasha lenye jina lake mara tu alipowasili kwenye hotel ya Hyatt Regency Dallas kwenye kongamano la DICOTA 2016 ambalo mwaka huu linafanyika Dallas nchini Marekani.
Mke wa Balozi Bi. Marustela Masilingi akiwa katika picha ya pamoja na Muzo, mwanafuzi wake wa darasa la tano shule ya msingi ya Mapambano ya Kijitonyama jijini Dar es Salaam.
Mhe. Balozi Wilson Masilingi akibadilishana mawili matatu na wageni waliofika kwenye mchapalo
Balozi Wilson Masilingi na mkewe Marystela wakiongea na mgeni wao Balozi Anisa Mbega. BOFYA HAPA KWA PICHGA ZAIDI.
Posted by MROKI On Friday, April 29, 2016 No comments
Na Woinde Shizza, Kilimanjaro
Umoja wa vijana wa Chama cha mapinduzi umemtaka Waziri mstaafu Frederick Sumaye hana vigezo wala sifa zozote zinazoweza kumfanya awe na uwezo wa kumkosoa Rais Dk John Magufuli katika uendeshaji wa serikali na masuala ya utawala. 

Sumaye ametakiwa amuache Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk Magufuli ili atimize majukumu yake kwasababu alipewa dhamana ya kuwa Waziri mkuu lakini hajufikia  utendaji unaofanyika sasa.   

Msimamo huo umetolewa jana na Kaimu katibu mkuu wa uvccm shaka hamdu shaka alipokuwa akizungumza na wanachama wa ccm wa kata mbili za kwandele na mbichi jimbo Rombo mkoani kilimanjaro.

Shaka alisema anachokifajya sumaye na baadhi ya wanasiasa muflis wanaojaribu kukosoa utendaji katika utawala wa serikali ya awamu ya tano ni kutaka nao wasikike wakidhani yale walioyafanya wakati wakiwa madarakani wananchi wameyasahau. SOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Posted by MROKI On Friday, April 29, 2016 No comments
SGS01
Mkurugenzi wa Kampuni ya Ulinzi ya SGA Security Bw. Eric Sambu akikabidhi koti maalum la usalama barabarani Bw. Thobias Msua  mmoja wa waendesha Bodaboda wa Mbezi Tangibovu jijini Dar es salaam wakati kampuni hiyo ilipotoa msaada wenye thamani ya shilingi milioni 4 na wametoa msaada huo kwa waendesha  bodaboda zaidi ya 4000, makabidhiano hayo yamefanyika Mbezi Tangibovu jijini Dar es salaam.
SGS1Mkurugenzi wa Kampuni ya Ulinzi ya SGA Security Bw. Eric Sambu akikabidhi koti maalum la usalama barabarani kwa waendesha Bodaboda wa Mbezi Tangibovu jijini Dar es salaam wakati wakati kampuni hiyo ilipotoa msaada wenye thamani ya shilingi milioni 4
SGS2 SGS4Waendesha Bodaboda wakiwa wamejipanga mara baada ya kukabodhiwa msaada huo wa vifaa vya usalama barabarani.
SGS5Mkurugenzi wa Kampuni ya Ulinzi ya SGA Security Bw. Eric Sambu akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukabidhi  vikoti maalum vya usalama barabarani  kwa waendesha Bodaboda wa Mbezi Tangibovu jijini Dar es salaam wakati wakati kampuni hiyo ilipotoa msaada wenye thamani ya shilingi milioni 4


KAMPUNI ya Ulinzi ya SGA imetoa msaada wa vifaa kusaidia waendesha bodaboda  Mtaa Mbezi A, katika kujiepusha na ajali katika siku  ya usalama  duniani.

Akizungumza wakati wa kakabidhi vifaa hivyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo, Erick Sambu amesema kuwa vifaa walivyopewa vitasaidia katika kujiepusha na ajali kutokana na dereva wa gari kuona kifaa hicho.

Amesema kuwa vifaa hivyo vina thamani ya sh.milioni Nne na kuahidi kuendelea kutoa msaada katika makundi mbalimbali kutokana na kazi yao ya kuangalia usalama.

Sambu amesema kuwa SGA  katika kuadhimisha siku ya usalama duniani na kuwataka wadau wengine kuunga mkono katika kuwangalia watu bodaboda.

Naye Mwakilishi wa Mwanyekiti wa Serikali ya Mtaa Mbezi A, Carolyne Ngoda amesema kuwa SGA wameokoa maisha ya vijana wao wanaoshughuli na biashara ya kusafirisa watu kutoka sehemu moja kwenda nyingine.
Posted by MROKI On Friday, April 29, 2016 No comments

Posted by MROKI On Friday, April 29, 2016 No comments

April 28, 2016





Mkuu wa kitengo cha elimu kwa Umma kitengo cha Usalama barabarani makao makuu ya Polisi ASP,Abel Swai akitoa mada kwa wafanyakaziwa kampuni ya TBL jijini Dar es Salaam wakati wa semina ya masuala ya usalama wakati kuadhimisha  Siku ya Afya na Usalama Duniani.Semina hiyo ilifanyika kiwanda cha TBL cha Ilala.


Wafanyakazi wa Kampuni ya Bia Tanzania TBL wakisikiliza mada wakati wa semina ya usalama kazini wakati wa maadhimisho ya siku ya Afya na Usalama Duniani

 Mmoja wa wafanyakazi wa TBL akiuliza swali wakati wa semina ya usalama kazini wakati wa maadhimisho ya siku ya Afya na Usalama Duniani iliyofanyika kiwanda cha ilala jijini Dar es Salaam.
Mtaalamu wa masuala ya afya na jamii Lilian Msaki,akitoa elimu kwa wafanyakazi wa TBL wakati wa semina ya usalama kazini wakati wa maadhimisho ya siku ya Afya na Usalama Duniani iliyofanyika kiwanda cha ilala jijini Dar es Salaam. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.
Posted by MROKI On Thursday, April 28, 2016 No comments


THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
MINISTRY OF WORKS, TRANSPORT AND COMMUNICATION
APPOINTMENT TO THE CHAIRMAN, VICE CHAIRMAN AND  BOARD MEMBERS OF THE TANZANIA COMMUNICATION  REGULATORY AUTHORITY (TCRA)

The Chairman of the Nomination Committee, established under section 8(1) (a) of the TCRA Act. No. 12 of 2003, invites Tanzanians with relevant qualifications as spelt out herein to apply for appointment to fill the positions of the Chairman, Vice Chairman and  Board members of Tanzania Communication Regulator Authority.  Attention is hereby drawn that all applicants are required to observe the provisions of Sections 7(5) and 11 of the TCRA Act,  2003 as well as the TCRA Code of Conduct relating to conflict of interest.

Qualifications required:
As per the First Schedule of the TCRA Act 2003, the following are the minimum qualifications for appointment to the TCRA Board:

1.      Should be a graduate of a recognized university;
2.      Have at least 10 years experience in one or more of the fields of Management, Law, Economics, Finance, Engineering, Broadcasting, ICT or related fields;
3.      Have knowledge of the communication  industry;
4.      Should satisfy the Nomination Committee that he/she is unlikely to have a conflict of interest under Section11 of the Act;
5.      Be willing to serve as member to the board.

All applications including detailed Curriculum Vitae and names and addresses of three references (including current or last employer) should be sent to the address below so  as reach the Chairman of the TCRA Nomination Committee by 23rd May, 2016

The Chairman,
TCRA Nomination Committee,
Ministry of Works, Transport and Communication,
14 Jamhuri Street,
P.O.BOX 2645,
11470 DAR ES SALAAM
Posted by MROKI On Thursday, April 28, 2016 No comments


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mh. John Mongella, akitoa hotuba rasmi wakati wa uzinduzi wa mradi wa Uimarishaji mifumo ya sekta za Umma (PS3) mkoani Mwanza Aprili 27, 2016. Mradi huo unafadhiliwa na shirika la Misaada la Kimataifa la Marekani (USAID) ni wa miaka mitano, na utafanya kazi na Serikali Kuu pamoja na Halmashauri 97 katika mikoa 13 ya Tanzania bara.

PS3 inalenga kuunda ushirikiano na Serikali ya Tanzania kwa ajili ya kuimarisha mifumo ya sekta za umma yakiwemo masuala ya utawala bora, rasilimali watu, fedha, utoaji wa taarifa, na tafiti tendaji.  Ushirkiano huu wa PS3 katika ngazi ya Serikali kuu na  Halmashauri, una nia ya kukuza utoaji, ubora, na matumizi ya huduma za umma, hususan kwa jamii ambazo hazijanufaika vya kutosha. Pichani Kulia ni Kiongozi wa Utawala na Ushirikishwaji wa Raia wa PS3, Dk. Peter Kilima.

Kiongozi wa Utawala na Ushirikishwaji wa Raia wa PS3, Dk. Peter Kilima, akiwasilisha mada wakati wa uzinduzi wa mradi wa PS3 mkoani Mwanza

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, akizungumza katika uzinduzi huo.

Mwakilishi kutoka Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Bi. Beatice R. Kimoleta, akitoa neno wakati wa uzinduzi wa mradi wa PS3 mkoani Mwanza. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.
Posted by MROKI On Thursday, April 28, 2016 No comments

Posted by MROKI On Thursday, April 28, 2016 No comments
Kufuatia utekelezaji wa Mkakati wa Kitaifa wa kupanda miti kutunza Mazingira na Kuhifadhi Vyanzo vya Maji, Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano na Mazingira, imetekeleza ahadi yake ya kugawa miche ya miti ya matunda Mkoani Simiyu katika Majimbo ya ya Uchaguzi ya Busega, Bariadi, Itilima, Kisesa, Meatu, Maswa Mashariki na Maswa Magharibi.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Raisi Mhe. Luhaga Mpina, amechangia miti ya matunda ya maembe na machungwa ipatayo Elfu Kumi (10,000) huku, Halmashauri na Wabunge wa Mkoa huo ,wamechangia idadi ya miche inayozidi Elfu Kumi na Tatu (13,000).

Kwa kuanzia idadi ya miche ya miti ya matunda ipatayo Elfu Kumi na Tatu Mia Sita Sitini na Sita,(13,666) imeshapelekwa Mkoani simiyu ikiwa ni miti ya maembe Elfu Kumi na Tatu na Mia Tano Sitini na Sita (13,566) na Michungwa Mia Moja (100).

Awali, Mhe. Mpina akitoa ahadi hiyo alisema, Mkoa wa Simiyu hauna miti ya matunda ya kutosha hivyo Mkakati wa upandaji miti ya matunda utasaidia chakula kwa familia, fedha kwa kuuza matunda na malighafi kwa viwanda nchini na kusema kuwa miti ni Mali na miti ni uchumi. 

Aidha, Ofisi ya Makamu wa Rais inamshukuru Mhe. Daudi Njalu Silanga (Mb). wa Itilima, kwa kujitolea usafiri wa kusafirisha miche hiyo kutoka Chuo cha Kilimo cha Sokoine kilichopo Mkoani Morogoro.

Idadi ya miche elfu ishirini na saba (27,000) inatarajiwa kugawanywa katika majimbo hayo, ikiwa ni pamoja na michango ya wabunge wa majimbo hayo.
Kupitia Mkakati huo wa Kitaifa wa kupanda miti na kuhifadhi vyanzo vya Maji, Serikali pia imewataka wananchi kushiriki kikamilifu katika kutunza mazingira na hususan wananchi wa Simiyu kuitunza miti hiyo ya muda mfupi, ili kuiepusha nchi na hali ya jangwa na ukame.
IMETOLEWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
OFISI YA MAKAMU WA RAIS

Posted by MROKI On Thursday, April 28, 2016 No comments

April 27, 2016




Mwanaharakati kutoka mtandao wa kijinsia Tanzania (TGNP), Bi Gema Akilimali akizungumza na waandishi wa habari wakati akitoa shukrani fupi kwa uongozi wa DAWASCO kutokana na jitihada zilizofanyika katika kuboresha huduma ya Majisafi na Majitaka Jijini Dar es salaam hususani maeneo ya wananchi wenye kipato cha chini. Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Dawasco Mhandisi Cyprian Luhemeja.
************
WANAHARAKATI WA Mtandao wa kijinsia (TGNP) wamepongeza juhudi zinazofanywa na Shirika la Majisafi na Majitaka Dar es salaam (Dawasco), kutokana na Mabadiliko na jitihada zinazofanywa na Dawasco za kuboresha huduma ya Maji pamoja na kufanya kazi za kusaidia jamii inayoizunguka.


Akizungumza katika kikao cha pamoja na Dawasco, Mratibu wa kampeni ya Maji ya “MAMA TUA NDOO KICHWANI” kutoka Mtandao wa Kijinsia Bi. Martha Samwel. Ameitaka Dawasco kuhakikisha inapeleka huduma ya Majisafi na salama katika sehemu zote muhimu ikiwamo mashuleni na hospitalini ili kumpunguzia mwanamke adha ya kutafuta Maji kutoka umbali mrefu pamoja na kumuondolea mwanamke adha ya kubakwa na hata kupigwa kutokana na kuhangaika kutafuta Maji.

“Tunataka kutoa salamu za pongezi kwa DAWASCO kwa mabadiliko na  jitihada tunazoziona za kuboresha huduma ya Maji na kufanya kazi ya kusaidia jamii, tumefurahishwa na jitihada zenu,  tutafanya kazi pamoja ili kuhakikisha tunamuondolea mwanamke shida ya kupoteza muda mwingi kuhangaika kutafuta Maji  kwani kampeni yenu ya “MAMA TUA NDOO YA MAJI KICHWANI” ndio kampeni yetu” alisema Bi. Martha.

Aidha, Mwanaharakati wa mtandao wa kijinsia Bi. Gema Akilimali, amefurahishwa ya kampeni ya Mama tua ndoo kichwani kwani itamsaidia mwanamke kwa kiasi kikubwa kushiriki kikamilifu katika kujenga uchumi wa nchi, kitendo ambacho kwa sasa hatimizi ipasavyo kutokana na kutumia muda mwingi kutafuta maji, pia anaamini utaongeza ufaulu mashuleni kwani badala ya watoto wa kike kutumia muda mwingi kutafuta Maji sasa wataweza kuokoa muda na kuwa kushiriki masomo ipasavyo.

 “Wanawake wanatumia muda mwingi kutafuta Maji, hivi ni saa ngapi ataleta maendeleo ya nchi? Lazima tumkwamue mama katika janga hili ili na yeye aweze kujenga nchi yake” alisema Bi. Akilimali.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji mkuu wa Dawasco, Mhandisi Cyprian Luhemeja, amehaidi hadi kufikia Disemba 31 watahakikisha kampeni ya mama tua ndoo ya Maji kichwani itawafikia wakazi wengi wa Dar hususani wale walio katika tabaka la chini.

Aidha amehaidi kutoa huduma ya Majisafi na salama bure kwa wazee, walemavu na yatima wote ambao hawana uwezo wa kumudu gharama za kuunganisha huduma ya Maji, pamoja na kujenga pointi za ya kunywea Maji katika sehemu mbalimbali za Jiji ikiwa ni pamoja na maeneo ya  stendi ya Mabasi ya Ubungo, Buguruni chama, Magomeni Mapipa na Kisutu stendi ya zamani.

“Mimi pamoja na menejimenti yangu tunaenda kumtua mama ndoo ya Maji kichwani mpaka kufikia mwishoni wa mwaka huu, kwani Maji yatakuwa mengi katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam pamoja na Pwani” alimalizia Mhandisi Luhemeja
Posted by MROKI On Wednesday, April 27, 2016 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo