Nafasi Ya Matangazo

March 15, 2016

Bomba la Maji lilounganishiwa kiholela ambalo halina mita linalopeleka huduma ya Maji kwenye jengo kubwa la ghorofa ambalo linamilikiwa na Chuo cha Biashara (CBE) eneo la Oysterbay mtaa wa Msasani Rd Jijini Dar es Salaam.
Maofisa wa Dawasco Kinondoni waking’oa laini ya Bomba la Maji lilounganishiwa kiholela lisilo na Mita kwenye jengo kubwa la ghorofa linalomilikiwa na Chuo cha Biashara (CBE) eneo la Oysterbay mtaa wa Msasani Rd Jijini Dar es Salaam.
****************
Shirika la maji safi na maji taka Dar es Salaam (Dawasco) limeendeledea na msako wake wa kubaini wezi wa maji na waharibifu wa miundombinu yake jijini Dar es Salaam na safari hii limeingia Oysterbay Wilayani Kinondoni na kubaini wizi wa maji kwenye majengo makubwa.

Katika msako uliofanyika Oysterbay Mtaa wa Msasani, jijini Dar es salaam na kuongozwa na Meneja wa Dawasco Kinondoni, Judith Singinika walibaini kuwepo kwa wizi wa maji katika jingo la ghorofa mali ya Chuo cha Biashara (CBE) katika jingo lake lenye makazi 25.

Singinika alisema kuwa operesheni hiyo maalum inayoendelea ni utekelezaji wa agizo la waziri wa Maji na Umwagiliaji, Gerson Lwenge la kuwataka Dawasco kukagua majengo yote makubwa na viwanda juu ya matumizi yao ya maji.

“Tunaendelea na utekelezaji wa agizo la Waziri la  kukagua majengo yote makubwa pamoja na viwanda Jijini Dar es Salaam ilikubaini vyanzo vyake vya  Maji ,ndipo tulipobaini wizi mkubwa wa maji mtaa wa Msasani Road kwenye jengo hilo la ghorofa lenye nyumba ndogo(apartments) 25  linalomilikiwa na CBE ambapo kulikutwa na laini mbili  zinazoleta Maji na laini moja ikiwa haina mita na ndiyo ilikuwa inafanyiwa atumizi makubwa,”alisema Singinika.

Singinika alisema wamechukua hatua za kisheria kwa kukitoza chuo hicho faini ya Shilingi milioni 100 ambapo inatakiwakulipwa ndani ya miezi 24 hivyo kila mwezi wanatakiwa kulipa kiasi kisichopungua shilingi milioni 4,160,000.


Dawasco inaendelea kuwasihi wamiliki wote wa Majengo makubwa ya ghorofa pamoja na viwanda waliojiunganishia huduma ya Maji kiholela kijisalimisha kwani operesheni hiyo ni endelevu na hatu kali za kisheria zitachukuliwa kwa yoyote atakaye kamatwa.
Posted by MROKI On Tuesday, March 15, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo