Nafasi Ya Matangazo

February 24, 2016

Hivi karibuni Mkurugenzi wa Doris Mollel Foundation, Bi. Doris Mollel alitembelea ofisi za mchora vibonzo nchini Nathan Mpangala na kufanya nae mazungumzo kuhusu namna vibonzo vinavyoweza kutumika kuelimisha umma kuhusu watoto wanaozaliwa kabla ya wakati maarufu kwa jina la Njiti.

Bi. Doris alisema baadhi ya sababu zinazosababisha watoto njiti ni pamoja na pombe, dawa za kulevya, upungufu wa damu mwilini, uzito mkubwa kwa mama mjamzito, uvutaji sigara/bangi, magonjwa ya kisukari, presha, maambukizi, kifafa cha uzazi, matatizo kwenye cervix inashindwa kujifunga na kujikaza kubeba mtoto, kondo (placenta) inapokuwa na tatizo, kushika mimba haraka baada ya kujifungua mtoto mwingine, mimba ya mapacha, chupa kupasuka kabla ya wakati, msongo wa mawazo, kazi ngumu, vipigo, mimba za utotoni, mimba za uzeeni, kutopata vipimo sahihi na kwa wakati, kutotumia vitamins/foilic acid, lishe nk.
Posted by MROKI On Wednesday, February 24, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo