Nafasi Ya Matangazo

January 18, 2016

MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya ndege nchini (TAA), Suleiman Suleiman  amefariki dunia akiwa katika mazoezi ya kuogelea  katika Bahari ya Hindi,  eneo la Kigamboni jijini Dar es Salaam.

Taarifa kutoka kwa Mkurugenzi wa Sheria na Mahusiano wa TAA, Ramadhan Maleta, alisema Mhandisi Suleiman alifikwa na mauti leo asubuhi kwa  kukosa nguvu wakati akiwa anaogelea .

Maleta,  amesema ni kawaida ya Suleiman kufanya mazoezi ya mwili kila siku kabla ya kwenda kazini na miongoni mwa mazoezi hayo ni kuogelea ambapo leo kati ya saa 12:00 na saa 1:00 asubuhi ,akiwa anaogelea, mmoja wa aliokuwa ameongozana nao, alibaini kuwa amekosa nguvu akiwa majini.

Baada ya kuomba msaada wa kumtoa majini na kumpa huduma ya kwanza walimkimbiza Hospitali ya Aghakan kwa ajili ya matibabu lakini kabla ya kufika walibaini amesha poteza maisha.

Mwili wa Marehemu Suleiman ambaye aliwahi pia kuwa Katibu wa Klabu ya Simba ulitaraji kuzikwa leo jioni katika Makaburi ya Kisutu Dar es Salaam.

Wakatihuohuo Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetuma salamu za rambirambi kwa klabu ya Simba SC, kufuatia kifo cha aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa klabu hiyo miaka ya 1998-2000 Seleman Said ‘Yeltisn’ kilichotokea leo jijini Dar es salaam.
Katika salamu hizo TFF imesikitishwa na kifo cha kiongozi huyo, ambaye alingoza klabu ya Simba SC na kupelekea kupewa jina la utani la ‘Yelstin” kutokana na ufanisi wake katika kazi na misimamo akifananishwa na aliyekua Rais wa kwanza Urusi wakati huo Boris Yeltsin.
TFF kwa niaba ya familia ya mpira wa miguu nchini inawapa pole familia ya Seleman Said ‘Yelstin’ ndugu jamaa, marafiki, uongozi na wanachama wa klabu ya Simba kufuatia kifo hicho, na kusema wako pamoja katika kipindi hiki cha maombelezo.
Mazishi ya marehemu Selaman Said ‘Yelstin’ yanafanyika leo saa 10 kamili jioni katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam.
Marehemu Suleiman ameacha  mke na watoto watatu.


MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI-AMEN
Posted by MROKI On Monday, January 18, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo