Nafasi Ya Matangazo

December 03, 2015

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick (kushoto) akimkabidhi msaada wa madawa ya kusafishia maji yaliyotolewa na Benki ya DCB kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Musa Natty, Dar es Salaam jana. Katikati ni Meneja Mwandamizi ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya DCB, Gray Ndandika. DCB walikabidhi madwa yenye thamani ya shilingi milioni tano kwaajili ya kukabiliana na ugonjwa wa kindupindu. Kulia ni  Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa DCB, Balozi Paul Rupia. Benki ya DCB ilikabidhi katoni 58 za dawa  zenye thamani ya shilingi Milioni 5.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick (kushoto) akimkabidhi msaada wa madawa ya kusafishia maji yaliyotolewa na Benki ya DCB kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Musa Natty, Dar es Salaam jana. Katikati ni Meneja Mwandamizi ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya DCB, Gray Ndandika. DCB walikabidhi madwa yenye thamani ya shilingi milioni tano kwaajili ya kukabiliana na ugonjwa wa kindupindu.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa DCB, Balozi Paul Rupia akizungumza katika makabidhiano hayo ambapo alisema Benki hiyo imetoa msaada huo kwa kuguswa  na tatizo la mlipuko wa kipindupindu unaoikabili wilaya ya Kinondoni na hivyo kuitikia wito na ombi la  Mkurugenzi wa Manispaa kutoa madawa ya kusafisha maji ili kukabiliana na ugonjwa huo. Wengine pichani ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Musa Natty (kushoto), Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadicky (wapili kulia) na Meneja Mwandamizi ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya DCB, Gray Ndandika.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadicky akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano hayo Dar es salaam leo ambapo aliwashukuru Benki ya DCB kwa msaada huo na kuzitaka taasisi zingimne kuiga mfano huo. Aidha aliwataka watendaji wa Kata kuwa makini na kazi zao na kuhakikisha ugonjwa huo unatokomezwa katika maeneo hayo na watu wakaidi wa kufuata kanuni za usafi kuchukuliwa hatua.
Baadhi ya watendaji wa Kata mbalimbali za Manispaa ya Kinondoni wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa na viongozi wengine wakati wa makabidhiano hayo.
Posted by MROKI On Thursday, December 03, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo