Na Mwandishi Maalum
Bodi ya Taasisi ya Miradi na Maendeleo ya Miundombinu iliyo chini ya Wizara ya Fedha (UTT-PID), pamoja na Menejimenti yake iliyozuru nchini China katika ziara maalum ya siku tano kwa ajili ya Mafunzo na kubadilishana uzoefu imefana na tayari bodi hiyo imerejea nchini.
Katika ziara hiyo, Bodi ya UTT-PID, ikiongozwa na mwenyekiti wake Mrs. Elipina Mlaki pamoja na Menejimenti nzima walieleza kuwa imeweza kuwa ya mafanikio makubwa huku wakiahidi kuyafanyia kazi yae yote waliojifunza nchini China.
Katika ziara hiyo, bodi na menejimenti ya UTT-PID walipata wasaha wa kutembelea maeneo mbalimbali ya miji ya nchi hiyo ikiwemo makampuni makubwa na kujifunza na kujenga na kudumisha ushirikiano wa utendaji wa kazi.
Mwenyekiti wa Bodi ya UTT-PID, Mrs. Elpina Mlaki (wa pili kulia) akilezea jambo katika moja ya mkutano wao waliofanya katika ziara hiyo nchini China. Anayemfuatia ni Mkurugenzi Mkuu wa UTT-PID, Dr. Gration Kamugisha pamoja na wajumbe wa bodi na Menejimenti ya UTT-PID, Wengine kushoto ni watendaji kutoka kampuni ya Chengdu Engineering Corperation ya nchini humo.
UTT-PID wakiwa katika picha ya pamoja na wenyeji wao katika baadhi ya miji ya nchini China walipotembelea kwa ziara ya mafunzo ya siku tano ya kujenga uzoefu na ufanisi wa utendaji wa kazi za Taasisi hiyo.
Mwenyekiti wa Bodi ya UTT-PID, Mrs. Elpina Mlaki (mwenye skafu nyekundu) wakisikiliza maelezo kwa umakini kutoka kwa wataalamu wa kampuni ya Chengdu Engineering Corporation walipotembelea katika nchi ya China kwa ziara ya mafunzo ya siku tano. (kulia kwake) ni mjumbe wa bodi hiyo, Mrs. Janeth Mmari.




0 comments:
Post a Comment