Nafasi Ya Matangazo

August 11, 2014

Mjumbe wa bunge maalum la katiba kutoka kundi la 201,Thomas Magnus Mgoli amelazwa katika hospital ya mkoa Dodoma baada ya kupigwa na vijana anaodai kuwa ni washabiki wa Chadema.Akizungumza kitandani kwake Mgoli amesema alishambuliwa na vijana hao jana usiku majira ya saa moja eneo la area D anakoishi.Amesema vijana hao hukutana nao mara kwa mara anapokwenda dukani na huzungumzia masuala ya bunge hilo, lakini hiyo jana walimshambulia kwa kumuambia kuwa yeye ni CCM.Pichani waziri mkuu mstaafu na mbunge wa Monduli Mh Edward Lowassa akimjulia hali Mh Mgoli hospitalini hapo, wote wako kamati namba 12.
Posted by MROKI On Monday, August 11, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo