Meneja Masoko wa Kampuni
ya Bia ya Serengeti Bw. Allan Chonjo akiwaongoza washindi wa tiketi ya
Winda SAFARI YA Brazil na Serengeti mara baada ya kuwasili katika
kiwanja cha ndege cha Mwalimu Nyerere. Nyuma ni Bi Juliana Joseph
Masawe(mshindi)
Menrad Faustin Shayo
kutoka Arusha akihojiwa na waandishi mara baada ya kurejea nchini. Bw.
Shayo alielekea nchini Brazil baada ya kushinda tiketi kupitia kampuni
ya bia ya Serengeti. Shayo aliambatana na washindi wawili katika ziara
ya utembelea vivutio mbalimbali.
Pilikapilika za washindi
mara baada ya kuwasili nchini kutokea Brazil kula bata baada ya ushindi
kupitia kampeni ya Winda Tiketi ya Brazil na Serengeti iliyokuwa
ikichezeshwa na kampuni ya bia ya Serengeti kupitia bia yake ya
Serengeti Lager. Kulia ni Deusdedit Kahwa kutoka Dar es Salaam, Bi
Juliana Joseph Masawe kutoka Kilimanjaro (katikati) pamoja na kushoto ni
mwenyeji wa washindi hao Bw. Allan Chonjo Meneja Masoko wa kampuni ya
Serengeti.
***********
Washindi wa promosheni ya
Winda Safari ya Brazil na Serengeti waliokwea pipa wiki iliyopita kuelekea nchini
Brazil kutembelea vivutio mbalimbali wamerejea kwa shangwe kubwa baada ya
kuyaona maisha mapya ya bara jingine. Ziara yao ilichukua siku tano nchini
Brazil huku washindi hao wakila bata katika vivutio mbalimbali nchini Brazil.
Washindi wa tiketi hizo Bi
Juliana Joseph Masawe kutoka Kilimanjaro, Deusdedit Kahwa kutoka Dar es Salaam
pamoja na Menrad Faustin Shayo kutoka Arusha wamerejea nchini wakiwa na
mwenyeji wao Bw Allan Chonjo ambaye ni Meneja Masoko wa Kampuni ya Bia ya
Serengeti. Washindi hao walijishindia tiketi hizo baada ya kutumia bia ya
Serengeti na kufungua chini ya kizibo ili kushinda na hivyo walijipatia tiketi
za kwenda nchini Brazil kutembelea vivutio mbalimbali.
Juliana Joseph Masawe amewapongeza
Kampuni ya Bia ya Serengeti kwa kuwa wakweli na kuwajali wateja wao. “Sitasahau
starehe nilizoziona nchini Brazil. Siku tano zimakuwa kama siku mbili.
Nilitamani kukaa mwezi. Najivunia kutumia bia ya Serengeti kwani imenionjesha
maisha tofauti kabisa. Mwanzo nilijihisi uoga kwani sikuwahi kupanda ndege
lakini kupitia bia ya Serengeti nimepanda ndege, nimetembelea vivutio
mbalimbali, nimeona makanisa makubwa mno sijawahi kuona, mashamba makubwa ya
mpunga na mihogo pia nimekutana na watu wapya kabisa katika maisha yangu”.
Nae Menrad Faustin Shayo
kutoka Arusha alishindwa kujizuia kwa
furaha wakati akihojiwa katika uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere “Sio siri
najiona mpya kabisa sikutegemea kufika nchini Brazil katika maisha yangu, kila
promosheni itakayotolewa na Kampuni ya bia ya Serengeti lazima nitashiriki kwa sababu hawana
upendeleo kabisa kama ni mshindi basi utapewa kile unachostahili. Kampuni ya
bia ya Serengeti imenifanya niwe na kitu cha kuhadidhia maisha yangu yote,
naamini familia yangu itafurahi zaidi nikiwapa habari za nchini Brazil.
Mwenyeji wa washindi hao Meneja
Masoko wa Kampuni ya Bia ya Serengeti
Bw. Allan Chonjo amewashukuru sana washinidi kwa kuichagua bia ya
Seregeti na kushiriki katika promosheni ya Winda Safari ya Brazil na Serengeti.
“Ninaamini mmefurahia ushindi wenu. Bila shaka mtakuwa mabalozi wa bia ya
Serengeti kila mtakapokuwa. Promosheni hii ililenga kawashukuru wateja wetu kwa
kuichagua bia ya Serengeti kuwa kinywaji chao. Tumerudisha fadhida kwa wateja
wetu kama shukrani kwao kwani bila wao sisi tusingeweza kusonga mbele”.
0 comments:
Post a Comment