Nafasi Ya Matangazo

June 06, 2013

Kila mwaka Benki ya Barclays inaandaa matembezi ya kuchangisha fedha yaliyobatizwa kwa jina la Step Ahead Walk. Mchakato huu umekuwa ukiendelea toka mwaka 2006 na Tanzania walifanya Step Ahead yao ya kwanza mwaka 2008 ambapo  fedha zilichangishwa na zilitumika kusaidia matibabu ya kansa kwa watoto kwenye kituo cha kansa cha Ocean Road.

Tunu Kavishe, Meneja Mawasiliano na Huduma kwa jamii wa Benki ya Barclays Tanzania amesema tukio hili rasmi itafanyika tarehe 8 juni, 2013 katika hoteli ya Golden Tulip kuanzia saa kumi na mbili ya asubuhi na litahusisha matemebzi ya hisani ya kilomita tano (5) na kila mtu katika jamii anakaribishwa kushiriki. Pia mtu yeyote anaweza kuchangia pesa kwa kutumia namba ya Mpesa au tigo pesa 133133.

Mgeni wetu rasmi atakuwa Mheshimiwa Dr Asha Rose Migiro, Naibu Katibu Mkuu mstaafu wa Umoja wa Mataifa.

Naye Erwin Telemans, Mkurugenzi Mtendaji wa CCBRT amesema “msaada huu ambao  CCBRT wanaupokea kutoka Benki ya Barclays ni wa thamani sana ambapo tunafanya  kazi ili kufikia malengo ya Tanzania ambapo jamii itajiwezesha kupaha huduma bora na salama hasa kwa walemavu wa viungo na pia itawafikia wakinamama wote na kuhakikishia usalama wao kwenye  huduma ya  afya ya uzazi na watoto wachanga inafanikiwa. 

Mkakati huu wa benki ya Barclays Step Ahead utasaidia pia katika kukinga mapungufu ya mtindio wa ubongo na fistula hapa Tanzania, na vile vile kuhakikisha kwamba wale waliopata mapungufu wakati wa kuzaliwa wanapata matibabu  katika sehemu za viungo vyao haraka iwezekanavyo.

Naye Dr, Festus Ilako Mkurugenzi wa AMREF Tanzania amesema “Msaada na mkakati huu wa benki ya Barclays Tanzania kwa AMREF ni wa kila wakati, na kwa pamoja tunaweza tukaibadilisha jamii kutoka ilipo katika masuala ya afya kwa wakina mama na watoto, hivyo kuitengenezea jamii uelewa na ustadi katika kusimamia afya njema na kuvunja marudio rudio  ya ufukara katika afya na umaskini. Kampeni hii kutoka benki ya Barclays ijulikanayo kama Step Ahead itasaidia kuelimisha wakunga na wazalishaji katika wilaya ya Kilindi mkoani Tanga na kuwawezesha wakina mama wajawazito kujifungua katika mikono ya salama ya wafanyakazi waliofuzu katika Nyanja ya afya hivyo kupunguza uchangiaji wa vifo visivyo lazima na ulemavu wa viungo kwa mama na watoto chini ya miaka mitano.  Ushirika huu baina ya Barclays na AMREF ni mfumo mpya  ambayo utawezesha jamii kupata ubora na unafuu katika masuala ya kiafya.

Mwaka 2011, Benki ya Barclays na washiriki wake walifanikiwa kuchangisha shilingi za kitanzania milioni 150 kutokana na  mauzo ya tiketi na matoleo mengine kutoka kwa wafadhili. Mwaka huu lengo ni kuchangisha zaidi ya marambili ya shilingi milioni 150 kutoka kwenye matoleo ya washirika muhimu na washiriki wengine katika jamii.

Fedha zitakazochangishwa mwaka huu zitakwenda kusaidia katika masuala ya uzazi na afya ya watoto kama ifuatavyo:-

1. Mafunzo kwa wakunga wa uzazi
2. Matibabu ya Fistula
3.Upasuaji kwa watoto waliozaliwa na ulemavu unaosababishwa na uzazi
Step Ahead Walk 2013 itaweza kufanikiwa tu kama itawezeshwa na kila mshiriki na jamii nzima ya kitanzania kwa ujumla. Kwa sababu hiyo basi tujiunge wote ili tuweze kufanya badiliko katika masuala ya afya kwa ujumla hapa Tanzania hususani masuala ya uzazi na afya ya watoto.

Matembezi haya yamedhaminiwa na Montage Ltd, ITV/Radio One Ltd, Clouds Media group, Mwananchi Communications, Cocacola, NSSF, African Medical Investments, Home Shopping Centre, Golden Tulip Hotels, Grand Malt na Serena Hotels.
Posted by MROKI On Thursday, June 06, 2013 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo