Nafasi Ya Matangazo

December 03, 2012



  • Kocha Afurahishwa na Mwinyi Kazimoto kurejea uwanjani 
Wakati timu ya Tanzania bara, Kilimanjaro Stars, ikishuka dimbani leo dhidi ya Rwanda katika michuano ya Tusker Cecafa Challenge Cup inayoendelea Jijini Kampala, kocha wa timu hiyo, Kim Poulsen amesema wanaiheshimu Rwanda lakini watakufa nayo katika hatua hii ya robo fainali.



Aliyasema hayo jana baada ya mazoezi kika uwanja wa Chuo Kikuu cha Kyambogo ili kujiandaa na mechi hii ya robo fainali.



“Rwanda ina timu nzuri na tunaiheshimu sana lakini tuko tayari kupambana nao katika mechi ya kesho na ninaamini vijana wataendelea kufunga mabao kama ilivyofanyika katika mechi dhidi ya Somalia,” alisema.



Kocha huyo alisema wachezaji wote wako katika hali nzuri na wana ari ya kushinda mechi hii ili watinge katika hatua ya nusu fainali.



Alisema amefurahishwa kuona mchezaji Mwinyi Kazimoto akirejea uwanjani jeruhiwa wakati wa mechi na Burundi Jumatano iliyopita “Kwa sasa yuko katika hali nzuri na atacheza mechi ya kesho.



“Vijana wana morali na wamejiandaa vizuri na mechi hii ya kesho na tuna imani watatupa raha tena kama Jumamosi.


Katika hatua nyingine, Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager George Kaishe ambaye Bia ya kampuni yake  inaidhamini Kilimanjaro Stars, alitoa pongezi kwa Stars kwa kutinga hatua ya robo fainali.



“Tumekuwa tukifuatilia mashindano haya kwa njia ya runinga na kwa kweli yameleta hamasa kubwa sana hasa mchezo wa Jumamosi tulipoifunga Somaliake kwa vya 7-0,” alisema katika taarifa yake kwa vyombo vya habari.



Bw Kavishe alisema Stars ina uwezo mkubwa wa kutinga fainali na kurejea nyumbani na kombe hili la Cecafa.


“Watanzania wote lazima wawe na imani na waiombee dua njema timu yetu ili ishinde…sisi tukiwa wadhamini tutaendelea kuipa nguvu timu wao watuletee kombe tu,” alisema.



Timu nyingine zinazoshuka dimbani leo katika Uwanja wa KCC Lugogo Jijini Kampala ni Zanzibar Heroes na Burundi mechi ambayo itachezwa saa kumi alasiri baada ya ile ya Stars na Rwanda.



Mechi za Jumanne ni Kenya dhidi ya Malawi saa Kumi alasiri na baadaye mwenyeji Uganda atashuka dimbani na Ethiopia katika Uwanja wa Mandela eneo la Nambole.



Fainali za mashindano haya zitapigwa JUmamosi ijayo Disemba 8 katika uwanja wa Mandela.
Posted by MROKI On Monday, December 03, 2012 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo